Misemo inayoandikwa kwenye vyombo vya usafiri, we acha tu!

Chacha Isare Nyakyegi amemaliza kidato cha nne, anataka kwenda jeshini lakini hajui ajiunge jeshi lipi. Akamfuata Balozi wa mtaa Mhe. Nyamohanga Makere Ngocho amshauri jeshi la kujiunga nalo. Balozi Ngocho akamwambia faida anazoweza kupata Mkurya jeshini kama ifuatavyo:-
  • Ukiwa Polisi – hutapeleka Wakurya wenzako wa tuhuma za bangi na ukeketaji Mahakamani ili tudumishe mila zetu.
  • Ukiwa Jeshi – utazuia wavamizi wa ardhi ya Wakurya toka nchi jirani. Pia utalinda na kuhifadhi muungano.
  • Ukiwa Magereza – utawasaidia Mangariba waliofungwa wasifanye kazi ngumu.
  • Ukiwa Uhamiaji – utawasaidia Wakurya wenzako kuvusha bangi mpakani.
  • Ukiwa Mgambo – hapa Tarime hutakamata Buchoti wa Kikurya, tena hutatenganishwa na panga maana bunduki mgambo haruhusiwi na katiba.
  • Ukiwa Wanyamapori – hutawapiga Wakurya wanaodhaniwa kuvamia maeneo ya hifadhi ya Serengeti.
  • Ukiwa TAKUKURU – hakutakuwa na rushwa ya uchaguzi Tarime kwa sababu utawatia ndani Wajumbe wote watakaopokea rushwa.
  • Ukiwa Zimamoto – utazuia Waanchari, Warenchoka na Wasweta kuchomeana majumba. Pia utaokoa mashamba ya bangi kuchomwa moto na dola.

    NB: Chacha Isare Nyakyegi
    – mbona kothe kuthamu nichague ripi…?!​
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…