Natumai Nyote Hamjambo Huku Tukizidi Kuliendeleza LIBENEKE Letu.
Jamani Mimi Nimejikuta Nikipenda Sana Kusoma Yale Maneno Ambayo Huandikwa ktk Eiether Mabasi Yetu Haya ( Dala Dala ) Or ktk Malori Ya Mchanga Pamoja Na Magari Ya Kubeba Taka.
Kwa Mfano Leo Nimekutana Na Magari Ya Aina Hiyo Mawili Moja Likiwa Dala Dala ( MKANGAFU ) Nikimaanisha Yale Ma DCM Likiwa Limeandikwa " KAMA SHIDA INGEKUWA SUMU WOTE TUNGEKUFA " Na Gari La Taka Nalo Likiwa Limeandikwa " MGANGA HAOMBI DAGAA " Siyo Siri Nilijikuta Nikivunja Mbavu Na Kujiuliza Ni Wapi Watu Hutoa Maneno Hayo Kwani Japo Yanachekesha Na Hata Kustaajabisha Lakini Yanachoma Sana Hadi Kumoyo na Hugusa Mno Hisia Za Mtu.
Hebu Kama Na Wewe Unayajua Mengine Hebu Tupia Hapa Nizidi Kuongeza Siku Za Kuishi Kwa Kuvunja Mbavu Lakini Pia Nipate Ujumbe................... Karibuni Wadau na Wakuu Wangu Wana JF.