Misemo kutokana na Vichwa vya Treni

Naye Mkuu Wa makuhani akapata kunena yapaswa mjiulize ktk vichwa vyenu inawezekana vp mtu alete mzigo ndani ya nyumba na wewe usijue basi wale vijakazi wakabaki kutazamana usoni;3;07;2017

Basi zilipita sikumbili baadhi ya vijakazi wakasimamishwa kazi ili kupisha miujiza ya mkuu wa makuhani ifanye kazi 5;07;2017
 
Reactions: 314
Naye mmoja wa makuhani aitwaye mwijage akalia na kugaragara akisema, mniepushe na kikombe hiki, nina familia inanitegemea na kazi yangu ninaipenda... Akiomboleza kuikwepa hasira ya sizonje Viwonder 3:7-9
Hahahahahahahahahaaaaaaaa JF
 
Ndipo bwana akauliza tena,ni nani ajuaye asili ya vichwa hivi,kuhani mwenye dhamana akajibu mimi si mjuzi sana juu ya jambo hili labda askali mmoja aliyekuwa zamu.akaitwa na kusogea kwa upole akijibu bwana lilikuja wimbi zito kutoka pwani ya koromije.na kuacha vumbi zito likitanda baharini.ndipo vichwa taratibu vikajongea.kutumbuliwa:6:3-7
 
Hata zilipofika siku za mavuno,wadanganyika wakiwa wamejaza magala yao huku chakula kingine kikiharibika mashambani,akainuka yule aliyemkubwa wa wale wateuliwa naye akanena kwa ghadhabu kuu "in marafuku kwa mkulima kuuza mazao yake nchi jirani,atakayebainika basi atafilisiwa na hasira ya mteuliwa mkuu itawaka juu yake"
Nkowe 3:7-9

Bless I
 
"Basi Mfalme akaagiza aletewe mwanapunda ili aende katika soko(saba saba) kuu lilikuwa likiwakutanisha Wayahudi, waajemi na watu wa mataifa.Ndipo kama kawaida yake akaenda kumuaga mwanae (DAB).Basi mwanamfalme alimshangaa mfalme kuamua kupanda punda badala ya farasi ndipo akamuuliza...." Imekuwaje Leo upande mwanapunda badala ya farasi?. Na je huko uendako watajuaje kwamba we u mfalme wa nchi hii?" Ndipo mfalme akauliza "Mwanangu mpendwa wataka niendeje ili kudhihilisha utukufu wangu?" Ndipo mwana wa mfalme akamwambia panda farasi huku ukiongizana na walinzi wako waliokwisha yaondoa mapanga yao kwenye ala tayari kukata shingo ya yeyote aendaye kinyume na wewe" Ndipo mfalme akafanya kama alivyoambiwa na mwanae na tazama alipokwisha kufika huko wakutanapo wachuuzi ndipo wayahudi wakaanza kuulizana "amakuwaje mfalme wetu au kuna watu wa mataifa wametuvamia?" Na walipokwisha kujua mfalme amefanya hayo ili kuonesha ukuu wake uliotukuka ndipo wakaanza kusemezana " hakika hii divai imemlevya sana huyu mtawala maana kila siku amekuwa mtu wa kujionesha kuwa yu mkuu" (saba tano 1:3_12)
 
Tangu nijiunge jf huu Uzi ni wa kwanza kunifanya nsilale bila kuupitia.
 
Tazama sauti kuu yalia kutoka nyikani nilichukua form mwenyewe nikarudisha sikusindikizwa na mtu pia nilijipigia kura mwenyewe wadanganyika waka staajabu nabii akasema enyikizazi cha nyoka mtastaajabu jambo hili mpaka lini hakika nitawanyoosha maana mimi ndie nachagua huyu akae hekaluni yule alinde lango nao walipo sikia maneno yale kwakua walipewa tende na harua wakaruka ruka huyu hakika ndie tuliekua tunamsubiri basi wale makutano wakajibu na atawale milele
Usinipangie 1:20-20
 
Ha...ha...ha...toka nimejiunga Jamiiforum, uzi huu ni wakwanza kunifanya nitabasamu kwa furaha.
Kweli wanadamu wanamambo mengi mazuri.
Uzi huu ni mzuri na wa kufurahisha kuliko zote nilizowahi kuzisoma.
Asanteni wakuu kwa ubunifu mzuri.
Ingawa naona wachangiaji wengi wanashambulia upande mmoja wa watawala.
Kwenye ukawa nako kuna aya nyingi tu za kufurahisha.
Hapa ni kufurahi tu.
 
Mi nadhani ndugu zangu ifikie hatua tukue kifikra. Tunapaswa tuendeshe mijadala yenye tija kuhusu vichwa vya treni itakayomsaidia Rais wetu JPM na sio mizaha na kejeli za kipuuzi.
Wana wa Lumumba wakamuendea Nabii Gwajima na Kumuuliza.... Kwa nini unamshambulia mwana wa Sizonje kuhusu vyeti vyake. Nabii akawajibu "Mpumbavu anayejaribu kuficha neno lolote atasikia uchungu kama mama anayejifungua kama vile mshale unavyopenya pajani ndivyo ilivyo neno ndani yake mpumbavu" Yoshua Bin SIRA 19:11-12
 
Chai Maharage
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…