Misemo kutokana na Vichwa vya Treni

Misemo kutokana na Vichwa vya Treni

Hahahahahaaa
Daudi mwana Wa zisonje alikua amelala hakujua ujio Wa vichwa ,hata baba yake aliyemtwika madaraka bila kuangalia ukubwa Wa kichwa chake alistaajab kuona vichwa hivi vilivyosawir katika badari Salama mbele ya milango Wa bashite
Akapaza sauti kuuliza vichwa hivi ni vya nani ?
Hata sauti ilyosikika ikitokea nyikani isiyojulikana ikasema
Mzee wewe ni mkuu iweje unatafuta kiki hadi katika vichwa vya treni?
Watanganyika Wote Waandishi Wa Habari?
 
Basi baada ya Bashite mwana wa Kaisari kusikia habari kwamba kuna mtu kutoka mashariki ya mbali jina lake kimepewa kitongoji kimoja cha Galilaya basi haraka haraka akawatuma mafalisayo waende wakashuhudie kama ni kweli.Basi Mafalisayo wakaenda wakashuhudia na kurudi kwa mwana wa mfalme wakasujudu wakasema "Tumepata kuona kibao kimeandikwa VICTORIA CHUI"Ndipo akawauliza kwa gadhabu "Ni nani aliyefanya hivyo? Mimi nimekuwa mwana wa mfalme lakini jina langu halijapewa hata banda la mbwa wa Tiro na Sidoni(Manzese na Gomz)" Ndipo kuhani mmoja akamjibu. "Ni mzee wa baraza la hapa Galilaya ndo kafanya hivyo" basi Bashite akauliza tena. "Naweza kumteka na kumtesa kama yule kijana wa Kiroma ili naye apate shika adabu yake?" Ndipo wazee wa baraza wakamwambia "humuwezi mtu huyo maana anatumia vifungu vya sheria za wayahudi" basi Bashite akagadhabika na kuwaamuru mafalisayo wakaking'oe hicho kibao, nao kama walivyoagizwa wakaking'oa hukuwakijisifu "hakika tumemuweza bwana huyu(meya)" lakini cha ajabu mpaka mwana wa Mungu anarudi hicho kitongoji kikaendelea kuitwa jina la VICTORIA CHUI huku Daudi akiendelea kutafta kiki kwa pikipiki iliyoisha mafuta.(wivu wa Mwana wa mfalme 1;1_15)
 
Nae wazir mwenye dhamana akaitwa na kaisari kuulizwa kuhusu vichwa vile akastaajabu na akajibu kwa kusema sivijui vichwa hivi!!!?

Nasi Kando ya bahari ya hindi ndipo tulipo keti tukalia na kushangilia mana ya vichwa vya treni vilivo shushwa kwa upepo wa kisuli suli Tanzania awamu ya 5:17-2020 [emoji23][emoji22]
Na jogoo akawika kwa mara ya tatu..Kiparangoto 21:5
 
Basi baada ya Bashite mwana wa Kaisari kusikia habari kwamba kuna mtu kutoka mashariki ya mbali jina lake kimepewa kitongoji kimoja cha Galilaya basi haraka haraka akawatuma mafalisayo waende wakashuhudie kama ni kweli.Basi Mafalisayo wakaenda wakashuhudia na kurudi kwa mwana wa mfalme wakasujudu wakasema "Tumepata kuona kibao kimeandikwa VICTORIA CHUI"Ndipo akawauliza kwa gadhabu "Ni nani aliyefanya hivyo? Mimi nimekuwa mwana wa mfalme lakini jina langu halijapewa hata banda la mbwa wa Tiro na Sidoni(Manzese na Gomz)" Ndipo kuhani mmoja akamjibu. "Ni mzee wa baraza la hapa Galilaya ndo kafanya hivyo" basi Bashite akauliza tena. "Naweza kumteka na kumtesa kama yule kijana wa Kiroma ili naye apate shika adabu yake?" Ndipo wazee wa baraza wakamwambia "humuwezi mtu huyo maana anatumia vifungu vya sheria za wayahudi" basi Bashite akagadhabika na kuwaamuru mafalisayo wakaking'oe hicho kibao, nao kama walivyoagizwa wakaking'oa hukuwakijisifu "hakika tumemuweza bwana huyu(meya)" lakini cha ajabu mpaka mwana wa Mungu anarudi hicho kitongoji kikaendelea kuitwa jina la VICTORIA CHUI huku Daudi akiendelea kutafta kiki kwa pikipiki iliyoisha mafuta.(wivu wa Mwana wa mfalme 1;1_15)
Hahahaaaa umevunja mkuu nilihisi nasoma holy bible daah bila shaka umetokea galilaya mwana wa uzao wa wadanganyika
 
Aisee weye Mkuu utatuvunja mbavu kwa kucheka huku lol! Hahahahahahahaha

Ndipo makada wakajipiga vifua na kugalagala kwenye mavumbi kama chatu huku wakisema, "ewe Sizonje tuchukue utumwani milele"
Lumumba 4 : 5-13
 
"Muujiza Mkubwa Ulitendeka Katika Nchi Ya Bandari Ya Salama Ndipo Toashi Akakimbia Kwa Haraka Kubwa Mpaka Katika Hekalu La Mfalme, Kwa Hofu Akamwambia Ewe Mfalme Tazama Vichwa Vya Treni Vimeshushwa Bandarini Kutoka Mbinguni, Bila Kuchelewa Mfalme Akafuatana Pamoja Na Waandishi,Mafarisayo Na Masadukayo Walipofika Mfalme Akapaza Sauti Akisema Kwa Hakika Muujiza Huu Unathibitisha Kwamba Nchi Hii Bwana Ameichagua Kuwa Ya Viwanda" Miujiza 70:12-20
 
Tena amini nawaambieni yeye aliyepokea kwa mkono wa kulia atatoa kupitia tundu lolote.Na haya nimewaambieni mbele ili wakati atoapo muwe tayari kushuhudia.Naye aliyeko wodini asitoke hapo mpaka kesi yake iishe kusomwa. Mbagala 6:5.
Amini amini nawaambia ufalme wangu si wa mafisadi na wala rushwa bali nita hakikisha wanaishi kama mashetani
Fentifodi 2:1-7
 
Basi baada ya Bashite mwana wa Kaisari kusikia habari kwamba kuna mtu kutoka mashariki ya mbali jina lake kimepewa kitongoji kimoja cha Galilaya basi haraka haraka akawatuma mafalisayo waende wakashuhudie kama ni kweli.Basi Mafalisayo wakaenda wakashuhudia na kurudi kwa mwana wa mfalme wakasujudu wakasema "Tumepata kuona kibao kimeandikwa VICTORIA CHUI"Ndipo akawauliza kwa gadhabu "Ni nani aliyefanya hivyo? Mimi nimekuwa mwana wa mfalme lakini jina langu halijapewa hata banda la mbwa wa Tiro na Sidoni(Manzese na Gomz)" Ndipo kuhani mmoja akamjibu. "Ni mzee wa baraza la hapa Galilaya ndo kafanya hivyo" basi Bashite akauliza tena. "Naweza kumteka na kumtesa kama yule kijana wa Kiroma ili naye apate shika adabu yake?" Ndipo wazee wa baraza wakamwambia "humuwezi mtu huyo maana anatumia vifungu vya sheria za wayahudi" basi Bashite akagadhabika na kuwaamuru mafalisayo wakaking'oe hicho kibao, nao kama walivyoagizwa wakaking'oa hukuwakijisifu "hakika tume
 
Basi yule kuhani mkuu akanena!"ni kwa maombi ya nani miujiza hii?kwa ruhusa ya nani maombi hayo?hakika haya ni makufuru na siyatambui ,ondoeni vichwa hivi madhabahuni kwangu!majipu 06:7-17
Wasaidizi wa makuhani wakasemezana wao kwa wao "je ni nani kati yetu aliyeomba muujiza huu ?wale wasaidizi wakuu wakakana wakisema hakika hatutambui kufuru hii!
Mchecheto 05:7-17
Hahahahaaa Umetisha Mkuu Nimecheka Mpaka Majirani Wameamka
 
Sauti ikasikika ikisema sitakula unga wa maharage tena ona mali tulizo wapola washami zinarudi sisi tunajutia hapatakuwa shujaa tena wa kutuletea unga tutengeneze chapati (kazi kazi 8:4-6)
 
"Ndipo bwana yule akamwamuru mkolomije-'Inua fimbo yako juu', na bahari ikagawanyika mara mbili ili kuruhusu vichwa vya treni vipite mahali salama." Ugonjwa mpya 12:31,32
 
Kwa kuwa mwanasizonje alijipenda yeye na maisha yake ndipo alipoamua kumtuma muongoza kwata wa pekee ili kwa yoyote mdanganyika aaminiyee kuwa kule kibeat si salamaa ....ndipo mwanakwata huyo alipokumbuka kuwa wadanganyika wengi wanapotea kwa kukosa ujasiriii wa kumpinga sizonje..kibeat 9-12
 
Back
Top Bottom