Misemo kutokana na Vichwa vya Treni

Misemo kutokana na Vichwa vya Treni

Kuna baadhi yao bado hawajasadiki na wamefanya mioyo yao kua migumu, bado wanasubiri noah zao.
Hakika watakesha wakiomba kusubiri noah zishuke toka mbinguni kama vichwa vya treni lakini hakuna. kitakachotokea
Faru johhny 21:4
Bwana mmoja alivuna pesa kutoka shamba la iptl akaziprunii vizuri kumbe wengine wanamuonea donge ...kwa kuwa wadanganyika washaambiwa kuwa noah zitadondoka kutoka kule ziliko ndo wakashadadiaa alipe alipe ili wanapate hata lita 5 za mafuta
 
Teh teh hiyo Punyeto unafikiria nimeweka kimakosa? Aliye tolewa bastola si ndie alisema ikulu tutaenda hata kwa bao la mkono? Sasa bao la mkono ni lipi kama sio Punyeto?
Mkuu nakupa salute...
Da bao la mkono halikumuacha salama yule msemaji wa wafarisayo, nae kalipwa kutokana na makufuru ya maneno yake mbele ya taifa.
Waraka wa jimbo la mtama 5-7
 
...Akawaambia nifuateni,nami nitawafanya kuwa wavuvi wa vichwa vya treni:[Shonza 4:19]
Na ndipo vichwa vya treni vikavuliwa baadae vikakosa mtu aliyevivua haya kweli ni maajabu ya utawala wa rafiki yake na ufunguo
 
Mi nadhani ndugu zangu ifikie hatua tukue kifikra. Tunapaswa tuendeshe mijadala yenye tija kuhusu vichwa vya treni itakayomsaidia Rais wetu JPM na sio mizaha na kejeli za kipuuzi.
Kwan nyie mnavyosema vichwa vya treni vimeingia na kushushwa bandari bila kuwa na mwenyewe c mnaamini fikra zetu hazijakua na hata picha hatuoni.....basi tuacheni na fikra zetu hiz hiz,

Bahat yko cna andiko hpa.....ningekupa moja.
 
Basi baada ya Bashite mwana wa Kaisari kusikia habari kwamba kuna mtu kutoka mashariki ya mbali jina lake kimepewa kitongoji kimoja cha Galilaya basi haraka haraka akawatuma mafalisayo waende wakashuhudie kama ni kweli.Basi Mafalisayo wakaenda wakashuhudia na kurudi kwa mwana wa mfalme wakasujudu wakasema
"Tumepata kuona kibao kimeandikwa VICTORIA CHUI"
Ndipo akawauliza kwa gadhabu
"Ni nani aliyefanya hivyo? Mimi nimekuwa mwana wa mfalme lakini jina langu halijapewa hata banda la mbwa wa Tiro na Sidoni(Manzese na Gomz)"
D
Ndipo kuhani mmoja akamjibu.
"Ni mzee wa baraza la hapa Galilaya ndo kafanya hivyo" basi Bashite akauliza tena. "Naweza kumteka na kumtesa kama yule kijana wa Kiroma ili naye apate shika adabu yake?" Ndipo wazee wa baraza wakamwambia "humuwezi mtu huyo maana anatumia vifungu vya sheria za wayahudi" basi Bashite akagadhabika na kuwaamuru mafalisayo wakaking'oe hicho kibao, nao kama walivyoagizwa wakaking'oa hukuwakijisifu "hakika tumemuweza bwana huyu(meya)" lakini cha ajabu mpaka mwana wa Mungu anarudi hicho kitongoji kikaendelea kuitwa jina la VICTORIA CHUI huku Daudi akiendelea kutafta kiki kwa pikipiki iliyoisha mafuta.(wivu wa Mwana wa mfalme 1;1_15)
 
Na baada ya hayo Mfalme alikuwa akitembea kanda ya ziwa,maana hakutaka kutembea nchi za nje.Na sikukuu ya saba saba ilikuwa ikikaribia,basi ndugu zake wakamtaarifu juu ya ujio wa vichwa vya treni.[Wadanganyika 7:1-4]
Nae akajibu akiwaambia kweeni ninyi mkaile sabasaba,maana majira yangu mimi bado..mpaka nitakapokipata kichwa cha Harrison. Kwani hatakuwa na nafasi tena ktk ufalme wangu. Mtumbuzi 5:4
 
Akanena malaika mkuu mbele ya umati kubwa wa Wadanganyika na kuwajuza kapata mialiko chungu nzima kwenda kuhiji majuu, lakini akawahakikishia hatoki nchini ng'o kwa kuwahofia wapiga madili ndani ya ufalme wake. Wadanganyika wakajibu AMINA mtukufu AMINA ufalme wako utukuzwe milele na milele FARU JOHN 13:27
 
Kwan nyie mnavyosema vichwa vya treni vimeingia na kushushwa bandari bila kuwa na mwenyewe c mnaamini fikra zetu hazijakua na hata picha hatuoni.....basi tuacheni na fikra zetu hiz hiz,

Bahat yko cna andiko hpa.....ningekupa moja.
Mwenye vicha vya treni kumbe tunae humu mbona povu linamtoka utafikiri hivyo vichwa vimedondoka nae
 
Hii nadhani ni fani mpya ya kuchangamsha JF - huu ni mmoja ya uzi katika nyuzi
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom