Misemo kutokana na Vichwa vya Treni

Misemo kutokana na Vichwa vya Treni

Na ndipo SIZONJE akanena mimi na kiongozi imara najitambua na sikushindikizwa na mtu kwenda kuchukua form. Hakuna yeyote wa kumwambia SIZONJE afanye nini kwenye utawala wake au amteue nani na kumfukuza nani, na WADANGANYIKA wakajibu kwa sauti kubwa AMINA na jina lako litukuzwe milele mpaka na vitukuu vyetu. WAKOLOMIJE 15:22-35
 
Kuna baadhi yao bado hawajasadiki na wamefanya mioyo yao kua migumu, bado wanasubiri noah zao.
Hakika watakesha wakiomba kusubiri noah zishuke toka mbinguni kama vichwa vya treni lakini hakuna. kitakachotokea
Faru johhny 21:4
[emoji38] [emoji38] [emoji38] jamani
 
Hivi ni nani kati yenu mwanae akimuomba samaki atampa nyoka? Ama nge akimuomba yai? Nimevunjika mkono kwa ajili yenu leo mwanisulubisha kwa kunitolea bastola mbele ya umati huu? Eloi eloi la masaba kitani
1 Punyeto 6-9
 
Baada ya vichwa vya treni kuwasili ktk nchi ya ahadi vikakosa mwenyeji wa kuvipokea na hivyo kubakia vikilandalanda beach vikipata upepo mwanana mpaka mkombozi alipooteshwa na bwana na kwenda kuviona
 
Basi yule kuhani mkuu akanena!"ni kwa maombi ya nani miujiza hii?kwa ruhusa ya nani maombi hayo?hakika haya ni makufuru na siyatambui ,ondoeni vichwa hivi madhabahuni kwangu!majipu 06:7-17
Wasaidizi wa makuhani wakasemezana wao kwa wao "je ni nani kati yetu aliyeomba muujiza huu ?wale wasaidizi wakuu wakakana wakisema hakika hatutambui kufuru hii!
Mchecheto 05:7-17
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] aisee waTZ akili zetu tunazijua wenyewe, asanteni sana.
 
Injili chakavu kutoka kitabu cha chama cha makinikia kama ilivyoandikwa na nabii Nusrat Hanje.
"Basi vikashuka vichwa vya treni kutokea mbinguni kupitia baharini, naye mfalme akastaajabu na kushangilia ukuu wa mungu, Kisha mfalme akauliza kwa hamaki, vichwa hivi ni vya nani? Lakini hakukuwa na jibu, hata makutano nao wakastaajabu.

Maigizo 2:16-19
 
Hivi ni nani kati yenu mwanae akimuomba samaki atampa nyoka? Nimevunjika mkono kwa ajili yenu leo mwanisulubisha kwa kunitolea bastola mbele ya umati huu? Eloi eloi la masaba kitani
1 Punyeto 6-9
Na ni nani hasa mwanae akiomba mvua analetewa vichwa vya treni...? Hakika haijapata tokea maajabu katika nchi ile ya mfalme sizonje.
Punyeto dhambi:4-22
 
Mfalme alipokuwa akitoa sadaka ya kuteketezwa ya vichwa vya scania, tazama vichwa vya treni vikaanguka toka mbinguni, na aliye juu akapaza sauti yake akamwambia, nimeiona imani yako, viache vichwa vya scania. Injili ya Paramagamba 7: 2015-2025
Hahhhhhaa aisee nyie watu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mbabe wa vita hajaiona hiyo? Au wapambe wake wamededi
 
Na ni nani hasa mwanae akiomba mvua analetewa vichwa vya treni...? Hakika haijapata tokea maajabu katika nchi ile ya mfalme sizonje.
Punyeto dhambi:4-22
Teh teh hiyo Punyeto unafikiria nimeweka kimakosa? Aliye tolewa bastola si ndie alisema ikulu tutaenda hata kwa bao la mkono? Sasa bao la mkono ni lipi kama sio Punyeto?
 
Back
Top Bottom