Misemo kutokana na Vichwa vya Treni

Misemo kutokana na Vichwa vya Treni

Ikawa yule mtume na nabii mkuu alipoona umaarufu wake unashuka ,akawaita wasaidizi wake na kuwauliza watu wananizungumuziaje huku na huko. Nao wakamwambia kwasasa umaarufu wako kama unashuka kutokana na wao kukosa maziwa na asali uliyowaahidi toka mwanzo. Naye akiwa amejawa na gadhabu nyingi akauliza, je nifanyeje sasa ili nisikauke midomoni mwao na utukufu wangu udumu hadi itakapofika wakati uliokubalika?. Ndipo vijana wake aliowapenda upeo wakamwambia , ni wakati sasa wa kutengeneza miujiza ya ajabu katika nchi ambayo hakuna mtu awaye yote aliyewahi kuyafanya. Tazama kwa utukufu wako kila mkaazi juu ya nchi anaweza kupata Noah yake, tazama mvua ya vichwa vya treni vyaweza kushuka kama mana kutoka juu. Ndipo yule mwana mpendwa kuliko wote ambaye alimchagua kuongoza kile kitongoji maarufu akamwambia mtume na nabii mkuu, hakika bwana muda umefika na saa imetimia wa sisi wasaidizi wako kuwaweka ndani wale wooote wanaokupinga na kutupinga sisi watumishi wao. Nao wana wa nchi watakapouliza tutawaambia nabii ananyoosha nchi sawasawa na neno lake mwenyewe alilolinena, ( call me J 5:1_4)
 
Nae akaugeukia mkutano ule nakusema, "nimfanye nini mtu huyu?". Nao wakajibu kwa pamoja kwa sauti kuu "ATUMBULIIWEEEEE!!". Darajani 6:3-4
Umetishaaaa Nacheka Mpaka Michozi Inanitoka
 
Wana wa Lumumba wakamuendea Nabii Gwajima na Kumuuliza.... Kwa nini unamshambulia mwana wa Sizonje kuhusu vyeti vyake. Nabii akawajibu "Mpumbavu anayejaribu kuficha neno lolote atasikia uchungu kama mama anayejifungua kama vile mshale unavyopenya pajani ndivyo ilivyo neno ndani yake mpumbavu" Yoshua Bin SIRA 19:11-12
Mkuu hili neno umekosea mstari nimeliona kitabu cha daudi binkolomije[emoji23][emoji23]
 
Ikawa yule mtume na nabii mkuu alipoona umaarufu wake unashuka ,akawaita wasaidizi wake na kuwauliza watu wananizungumuziaje huku na huko. Nao wakamwambia kwasasa umaarufu wako kama unashuka kutokana na wao kukosa maziwa na asali uliyowaahidi toka mwanzo. Naye akiwa amejawa na gadhabu nyingi akauliza, je nifanyeje sasa ili nisikauke midomoni mwao na utukufu wangu udumu hadi itakapofika wakati uliokubalika?. Ndipo vijana wake aliowapenda upeo wakamwambia , ni wakati sasa wa kutengeneza miujiza ya ajabu katika nchi ambayo hakuna mtu awaye yote aliyewahi kuyafanya. Tazama kwa utukufu wako kila mkaazi juu ya nchi anaweza kupata Noah yake, tazama mvua ya vichwa vya treni vyaweza kushuka kama mana kutoka juu. Ndipo yule mwana mpendwa kuliko wote ambaye alimchagua kuongoza kile kitongoji maarufu akamwambia mtume na nabii mkuu, hakika bwana muda umefika na saa imetimia wa sisi wasaidizi wako kuwaweka ndani wale wooote wanaokupinga na kutupinga sisi watumishi wao. Nao wana wa nchi watakapouliza tutawaambia nabii ananyoosha nchi sawasawa na neno lake mwenyewe alilolinena, ( call me J 5:1_4)
We kiboko.
 
Ndipo waDanganyika wote walipoinua macho yao mbinguni na kusema "Amina, na aihimidiwe Bwana Mungu wetu, milele na milele. Na huyu mfalme mtumishi wake atutawale mpaka itakaposhuka Boeing Dreamliner 787 kwa mtindo wa vichwa vya treni. Amina." (Chato 13:3-7)
[emoji23] [emoji23] [emoji23] shuka boeing
 
Basi ikasikika sauti toka kwa kuhani wa zamani, Ewe Sizonje ututawale milele, kwavile umwema umewafanya watu wako waishi kama mashetani: Mzee wa rksa 3:14
 
Mi nadhani ndugu zangu ifikie hatua tukue kifikra. Tunapaswa tuendeshe mijadala yenye tija kuhusu vichwa vya treni itakayomsaidia Rais wetu JPM na sio mizaha na kejeli za kipuuzi.
Basi akasema msaidizi wake, tumsaidie aliejuu kwa manufa ya nchi. Ndipo hapo Sizoje akasema nimi sipangiwi,mimi sijaribiwi: hapa kazi tu 10:09
 
Kweli wanaJf mnasoma sana bible aise, maana mnapitia mule mule
 
Kweli wanaJf mnasoma sana bible aise, maana mnapitia mule mule
Uzi huu unaanza kupoteza ladha yake.
Kila aya inamwelekeza mtu mmoja
Kila mtu ni sizonje sizonje,
mkiendelea hivi moderator wataufuta sio muda mrefu.

Mbona ile sauti iliayo nyikani hamuielezi.
Iliyosema_

"Sauti iliayo nyikani ikasikikaa
Ewe Wemasepengaa..
Nenda Kia motors, chukua gari hapoo harakaa
Pitia flyover ya ubungoo hadi kwenye mji ufukao Moshiii
Nisubirie haapoo..
Watu walipoinasaa wakasemaa, kumbe wewe wamtorosha modo wetuuu,
Sauti nyingi zikalia, msuribishee msuribishe aachwe Barabaaaa
Hapo mkuu akajiinua akasemaa
Sio mimiii, kamwe sikunena hayoo
Wote wakalia Aaamen..
Chadomo 3 :14

Na mimi nalipa.





Sent from my TECNO-N8 using JamiiForums mobile app
 
'Ndipo kukatokea mabishano makali vijiweni hadi mjengoni,wakisema mfalme aongezewe mda wengine atawale milele''Bashite 5:8-20
 
Uzi huu unaanza kupoteza ladha yake.
Kila aya inamwelekeza mtu mmoja
Kila mtu ni sizonje sizonje,
mkiendelea hivi moderator wataufuta sio muda mrefu.

Mbona ile sauti iliayo nyikani hamuielezi.
Iliyosema_

"Sauti iliayo nyikani ikasikikaa
Ewe Wemasepengaa..
Nenda Kia motors, chukua gari hapoo harakaa
Pitia flyover ya ubungoo hadi kwenye mji ufukao Moshiii
Nisubirie haapoo..
Watu walipoinasaa wakasemaa, kumbe wewe wamtorosha modo wetuuu,
Sauti nyingi zikalia, msuribishee msuribishe aachwe Barabaaaa
Hapo mkuu akajiinua akasemaa
Sio mimiii, kamwe sikunena hayoo
Wote wakalia Aaamen..
Chadomo 3 :14

Na mimi nalipa.





Sent from my TECNO-N8 using JamiiForums mobile app
[emoji1] [emoji1] [emoji1]

Sent from my SM-J320F using JamiiForums mobile app
 
Tazama wale tenashara walikua wamelala chomboni ghafla likatokea wimbi kali likapiga chombo kikaanza kujaa maji wakasemeshana wao kwa wao tufanye nini sasa mmoja akajibu chombo hiki kimelemea upande mmoja wakaulizana tumwamshe mwalimu maana twafaaa,
hofu ya wana lumumba buku saba 25:20-20
 
Back
Top Bottom