Leo rais Kikwete analipwa mshahara na masurufu yake milioni 47.8, wakati kima cha chini cha mshahara wa mfanyakazi wa umma ni 180,000,
Mwezi wa saba mwaka huu 2013 kuliibuka mgogoro idara ya uratibu na maslahi ya rais baadhi wakitaka mshahara wa rais na masurufu yake upandishwe hadi milioni 60,
Mwaka 1966 uchumi wa nchi ulikuwa kwenye vipimo vya wastani wa nchi inayokua kistaarabu, na leo mwaka 2013 uchumi wa nchi upo kwenye kasi ya mdororo usioridhisha!
Tafteni tofauti ni asilimia ngapi?
Mwalimu Nyerere ni mmoja wa viongozi wachache duniani
waliokufa MASIKINI kabisa, hakuwa na hisa kwenye kampuni yoyote ya ndani au nje ya nchi, hakuwa na biashara yoyote zaidi ya utumishi, hakuwa na hata nyumba ya sifa zaidi ya kulazimishwa kujengewa, na zaidi Mwaka 1966 mshahara wake ALIUPUNGUZA kutoka shilingi 5,000/= hadi 3,000/= pesa nyingine alisema iende kwa Walimu na Madaktari,
Leo tunamjadili kwakumlinganisha na wafanyabiasha waliopo ikulu? Wauza madawa ya kulevya waliopo ikulu? Mafisadi waliopo ikulu?
Kuokoteza visababu vya kipuuzi kwaajili ya kuziba udhaifu na ufedhuri wenu havitawaokoa!