Mishahara mikubwa waliokuwa wanalipana Nyerere na viongozi wenzake kweli ilikuwa ni sahihi

Mishahara mikubwa waliokuwa wanalipana Nyerere na viongozi wenzake kweli ilikuwa ni sahihi

Vyovyote itakavyokuwa, baba yako anamshahara kidogo lakini anatumia mabilions ktk safari za kila
mwezi ambazo watanzania hatuna cha kujivunia zaidi ya kushuhudia rasirimali zetu zinayoyoma kwa kasi
kwenda ng'ambo, uk,china,Canada,USA,nakwingineko duniani.
 
Naona tarehe 14 october inakuja !
Sijui ni nani anayeratibu zoezi la kumkashifu Nyerere?
 
Mkuu Nguruvi3.

Haya maneno niliyoyaleta siyo yangu ni maneno ya Nyerere mwenyewe akiwaambia wanafunzi wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam walioandamana mpaka Ikulu kupinga mishahara waliokuwa wanalipana viongozi.

Wala hakuna popote niliopofananisha na mishahra hiyo na kipindi hiki.

Nimeweka haya maneno tujadili kama watanzania hata kama tunapishana mitazamo yetu kisiasa.
 
Last edited by a moderator:
Naona tarehe 14 october inakuja !
Sijui ni nani anayeratibu zoezi la kumkashifu Nyerere?
Unaweza kutuonyesha ni kashfa ipi kafanyiwa Nyerere?
 
Kwa mantiki yako mkuu kama mnahalisha kulipana mishahara mikubwa kwa nini mnatuibia???
Rushwa za ajabu hadi kujengewa ma paradise Bilira Kempisk!!
Hamuoni aibu???
 
Wanaukumbi.Rais wa Tanzania Julius Kambarage Nyerere "MSHAHARA wangu ni Shilingi elfu tano kwa mwezi. Shilingi elfu tano katika nchi masikini. Masikini anayepata shilingi 200 kwa mwezi itamchukuwa miaka 25 kufikia kiwango cha mshahara wangu kwa mwezi. ndiyo nakubaliana na nyinyi kwamba tunalipana (Viongozi) mishahara mikubwa mno, na nitahakikisha mishahara hii tunayolipana inarekebishwa." Maneno haya aliyatamka mwaka 1966.
Mkuu Ritz,"Tulipokuwa tukitawaliwa na wakoloni tuligawanywa katika makundi matatu. Wazungu walikuwa juu, wahindi walikuwa katikati na waafrika walikuwa chini, kwa hali zao za elimu, mali na vyeo. Yawezekana wachache wa kundi Fulani la chini walipata bahati ya kuwa miongoni mwa kundi la juu, lakini kwa ujumla, hivyo ndivyo tulivyokuwa.....
Nimewataja mawaziri kama mfano tu. Lakini maneno haya yanawahusu waafrika wote wenye hali nzuri. Leo Permanent Secretary Mwafrika mshahara wake ni Shs. 4,000/- kwa mwezi. Hatujali permanent secretary kupata mshahara mkubwa kuliko waziri wake. Sababu ni kwamba hatutaki mawaziri wetu walinganishe mishahara yao na Ma – Permanent secretary wao, na kusema ni midogo. Tunataka mawaziri wetu walinganishe mishahara yao nay a wale vibarua wanaopata Shs.71/50, na watambue kuwa ni mikubwa. Hatutaki Waziri wetu awe na tama ya kupunguza tofauti ya pengo kati ya mshahara wake wa Shs. 3,000/- kwa mwezi na mshahara wa permanent secretary wake wa Shs.4,000/- kwa mwezi. Tunataka waziri wetu awe na tamaa ya kupunguza tofauti kati ya mshahara wake wa Shs. 3,000/- kwa mwezi na ule wa kibarua wa Shs 71/50 kwa mwezi. Kadhalika mshahara wa permanent secretary mzungu ni Shs.4,800/- au zaidi. Hatutaki permanent secretary mwafrika aseme kuwa huu ni ubaguzi, na adai yeye pia apate mshahara huo. Tunamtaka afikirie njia za kusaidia kupunguza tofauti iliyopo sasa kati ya mshahara wake wa Shs. 4,000/- kila mwezi na ule wa kibarua wa Shs. 71/50 kwa mwezi. Tunataka kila mwafrika ambaye sasa hivi hali yake ni nzuri ailinganishe hali yake na wale walio wengi ambao hali yao ni mbaya."
@Ritz , kati ya habari yako na ya Mchambuzi ipi inaweza kuchambuliwa kwa uhalisia
 
Kwa mantiki yako mkuu kama mnahalisha kulipana mishahara mikubwa kwa nini mnatuibia???
Rushwa za ajabu hadi kujengewa ma paradise Bilira Kempisk!!
Hamuoni aibu???
Kwa mantiki hiyo pia inawezekana hawa viongozi wa sasa hivi wanaolipana mishahara mikubwa wameiga huu utaratibu kutoka miaka hiyo viongozi walivyokuwa wanalipana mishahara.
 
Nilijua utatia team una kiherehere dah ngoja ninyamaze nisije nikapigwa ban kwasababu ya huu utumbo ulioandika hapo juu

wewe achana na mimi.. sio level yako. mmezidi kumdhalilisha baba wa taifa
 
Ritz , kati ya habari yako na ya Mchambuzi ipi inaweza kuchambuliwa kwa uhalisia
Mkuu Nguruvi3.

Sijui umetumia vigezo gani ili habari ichambuliwe kwa uhalisia labda habari ikiwa na paragraph nyingi ndiyo inakuwa na uhalisia.

Siku zote kauli za viongozi hata kama ameandika mistari miwili au kasema maneno machache huwa yanazua mijadala. Mfano kauli ya Waziri Mkuu Pinda "Wamezidi wacha wapigwe"
 
Last edited by a moderator:
kwa kweli mishahara hii haikuwa sahihi kabisa.Je na viongozi wa sasa wanavyolipana mishahara mikubwa ni sahihi??
 
Sio sahihi na ndio maana alikuwa muwazi kupita kiasi na kusema kuwa watarekebisha maana ni mikubwa huku nchi ni maskini!

Huyu Babu yetu alikuwa muwazi na mwenye uzalendo uliotukuka tofauti na marais waliomfuata akiwemo Babaako nawewe ka-rais msaidizi na tajiri kuliko hata mzee Mengi!

Tunajua janja yako kwanini umeleta uzi huu; ni wazi unataka kuhalalisha mishahara mnazolipwa za kufuru kwamba hata enzi za Nyerere haya pia yalikua yanatendeka! Kwamba sio ajabu na ninyi mkifanya!

Inaonyesha dhahiri jinsi mlivyokosa vision lakini bado kitambo kidogo tu mtavuna mlichokipanda! Mtatuambia ni kwanini mmeifanya nchi yetu Mama-Tanzania shamba la Bibi yenu! Poor you..


Mimi nafikiri ulitakiwa ujue alipunguza hiyo mishahara ya viongozi na kuongeza ile ya walalahoi. kabla kumwita muwazi.

labda nikupambanulie kidogo wakti huo tanzania ilikuwa inahishimu WANASIASA na WATAALAMU wa fani nyingine zote walikuwa hawathaminiki. Hivyo unaposema viongozi wakti huo wote walikuwa wanasiasa na ililazimika watu wengi wasomi wasomee Siasa ili uwe na maisha mazuri.

Hicho ndicho kilichopelekea kuuwa uchumi wa Tanganyika kwani hata maamuzi yao waliyafanya kwa mtazamo wa kisiasa zaidi bila kushirikisha wataalamu na hata kuwaandaa wananchi.

Mfano.
1.Azimio la Arusha. Japo lilikuwa zuri lakin lilifeli kuinua uchumi wa nchi.
2. Ujamaa Vijijini ulikuwa na lengo zuri sana lakin uliacha wananchi mmoja mmoja katika umasikini mkubwa.
3. Siasa ni kilimo. Hili liliuwa uwezo wa nchi katika kuweza kujimudu kwa chakula na kuleta njaa kubwa.

na mengine mengi yaliletwa kwa mamuzi ya kisiasa na kutowaandaa wananchi kiasi cha kuleta maafa makubwa japo kimtazamo yalikuwa na lengo zuri.

kifupi uchumi wa Tz umedidimizwa na maamuzi ya wanasiasa.

Poleni sana
 
Mchambuzi
Kwanza siku zote unapotaka kuchangia hoja kama hii ambayo imetolewa NUKUU ya Nyerere mwenyewe na amekuwekea mpaka source yake unatakiwa kuwa makini na kupunguza ushabiki. Kumbuka kuwa Nyerere hakuna mwenye kumchukia bali kinachojadiliwa na uongozi wake ambao kama mwanadamu unaona wazi ulikuwa na mapungufu ambayo mengi hivi sasa mnayapata.

nakukumbusha. Mkoloni alikuwa na Utawala mzuri ambao ulitoa haki kwa kila tabaka na ndio lililopelekea hakuweza kuwa njaa wala rushwa. na kila mtu alilipwa kwa mujibu wa kazi yake na ilmu yake. Japo kulikuwa na matabaka ya rangi ambayo yaliwekwa pale kuhakikisha kuwa maamuzi na maslahi ya wakoloni yanatimizwa na malengo yao yanafikiwa.

Kumbuka kuwa wakoloni kila walichokifanya utakiona kilikuwa na mana sana kiuchumi na kilileta tija sio tu katika utawala wao bali na hata wananchi wa kawaida wa tabata la chini. Kumbuka kuwa Mkoloni hakuweza kukubali kuitawala nchi tegemezi isiyoweza kujitegemea kiuchumi bali alitaka makoloni yake yote yazalishe zaidi na kupata Ziada ambayo ndio iliyokuwa inainufaisha nchi inayotawala.

kwa msingi huo Tz wakti huo ilikuwa inajimudu kiuchumi na ndio maana hata mlipopata uhuru wenu 1962 , Thamani ya Tanzania shiling ilikuwa karibu sawa na Dola ya marekani( Dola 1 ya marekani ilikuwa sawa na Tshilin 1.20).


sasa jiulize ni kipi kilipolomosha uchumi wa Tanzania kiasi cha kufika miaka kumi ya uhuru wenu nmwaka 1972 Dola ya marekani 1 ilikuwa sawa na T Shiling 28. Na kiasi cha kumfanya Nyerere kushindwa kutimiza ahadi yake aliyoitoa siku anakabidhiwa nchi na kuwa ahidi wakoloni atawaalika baada ya miaka kumi kuja kuangalia Tz inaendeleaje?

nafikiri haihitaji ilmu ya uchumi hapo na kama ulikuwepo wakti huo utaona hali ilikuwaje. Utaona kilichotokea pamoja na Azimio la arusha sasa mlianza kulana wenyewe kwa wenyewe na thamani ya pesa yenu kuporomoka kwa kasi sana.

je unaweza pambanua kwanini?
 
Last edited by a moderator:
Hizo ni fikra zako wapi nimekuambia kuwa natetea mishahara wanayolipana viongozi sasa hivi.

Mimi sina uhusiano wowote na Rais Kikwete, unachofanya ni makosa Name Calling.

Huu ni mjadala huru.

hata mimi humu nawaambiaga hauna uhusiano wowote na "Rais" bali unauhusiano na "Mama Salma" hawasikii. Jamani mumuwache Mutoto wa Mujini.!
 
Hapo kuna makosa ya kiuandishi ama ni nini??!!!! Maana 5000 kwa 200 inapatikana ndani ya miezi 25 ambayo ni miaka 2 na mwezi mmoja na sio miaka 25. Mkuu Ritz, au Mwl alisema 50,000??
 
Last edited by a moderator:
Hapo kuna makosa ya kiuandishi ama ni nini??!!!! Maana 5000 kwa 200 inapatikana ndani ya miezi 25 ambayo ni miaka 2 na mwezi mmoja na sio miaka 25. Mkuu Ritz, au Mwl alisema 50,000??
Mkuu mjasiria.

Rais aliongea hivyo kutokana hekima rais ana marupurupu mengi sana tofauti na huo mshahara.
 
Last edited by a moderator:
Leo rais Kikwete analipwa mshahara na masurufu yake milioni 47.8, wakati kima cha chini cha mshahara wa mfanyakazi wa umma ni 180,000,

Mwezi wa saba mwaka huu 2013 kuliibuka mgogoro idara ya uratibu na maslahi ya rais baadhi wakitaka mshahara wa rais na masurufu yake upandishwe hadi milioni 60,

Mwaka 1966 uchumi wa nchi ulikuwa kwenye vipimo vya wastani wa nchi inayokua kistaarabu, na leo mwaka 2013 uchumi wa nchi upo kwenye kasi ya mdororo usioridhisha!
Tafteni tofauti ni asilimia ngapi?

Mwalimu Nyerere ni mmoja wa viongozi wachache duniani
waliokufa MASIKINI kabisa, hakuwa na hisa kwenye kampuni yoyote ya ndani au nje ya nchi, hakuwa na biashara yoyote zaidi ya utumishi, hakuwa na hata nyumba ya sifa zaidi ya kulazimishwa kujengewa, na zaidi Mwaka 1966 mshahara wake ALIUPUNGUZA kutoka shilingi 5,000/= hadi 3,000/= pesa nyingine alisema iende kwa Walimu na Madaktari,

Leo tunamjadili kwakumlinganisha na wafanyabiasha waliopo ikulu? Wauza madawa ya kulevya waliopo ikulu? Mafisadi waliopo ikulu?


Kuokoteza visababu vya kipuuzi kwaajili ya kuziba udhaifu na ufedhuri wenu havitawaokoa!

Kumbe mambo yenyewe ndio haya?
 
Hapo kuna makosa ya kiuandishi ama ni nini??!!!! Maana 5000 kwa 200 inapatikana ndani ya miezi 25 ambayo ni miaka 2 na mwezi mmoja na sio miaka 25. Mkuu Ritz, au Mwl alisema 50,000??

Umeiona hii?

Leo rais Kikwete analipwa mshahara na masurufu yake milioni 47.8, wakati kima cha chini cha mshahara wa mfanyakazi wa umma ni 180,000,

Mwezi wa saba mwaka huu 2013 kuliibuka mgogoro idara ya uratibu na maslahi ya rais baadhi wakitaka mshahara wa rais na masurufu yake upandishwe hadi milioni 60,

Mwaka 1966 uchumi wa nchi ulikuwa kwenye vipimo vya wastani wa nchi inayokua kistaarabu, na leo mwaka 2013 uchumi wa nchi upo kwenye kasi ya mdororo usioridhisha!
Tafteni tofauti ni asilimia ngapi?

Mwalimu Nyerere ni mmoja wa viongozi wachache duniani
waliokufa MASIKINI kabisa, hakuwa na hisa kwenye kampuni yoyote ya ndani au nje ya nchi, hakuwa na biashara yoyote zaidi ya utumishi, hakuwa na hata nyumba ya sifa zaidi ya kulazimishwa kujengewa, na zaidi Mwaka 1966 mshahara wake ALIUPUNGUZA kutoka shilingi 5,000/= hadi 3,000/= pesa nyingine alisema iende kwa Walimu na Madaktari,

Leo tunamjadili kwakumlinganisha na wafanyabiasha waliopo ikulu? Wauza madawa ya kulevya waliopo ikulu? Mafisadi waliopo ikulu?


Kuokoteza visababu vya kipuuzi kwaajili ya kuziba udhaifu na ufedhuri wenu havitawaokoa!
 
Last edited by a moderator:
Kiukweli Ritz ulitakiwa ulete matini ya kauli ya Mwalimu kama ilivyofanywa na Mchambuzi. Kwani imetupa ufahamu mpana wa kujua sababu ya kutolewa kwa kauli ile. Lakini vilevile sijaelewa kama ulikuwa unakusudia kutoa hoja yenye kujenga nini in future. Ndio maana imeleta tafsiri tofautitofauti kwa wachangiaji wako lakini tupongeze ufanisi wa Mchambuzi na Nguruvi3 kujaribu kuijenga hoja ijadilike na hatimaye ije na sunstantive idea on the way forward.

Pamoja na mapungufu aliyokuwa nayo Nyerere kama binaadamu, lakini mapungufu ya waliomfuatia ni makubwa sana ukilinganisha na yeye. Mfumo wa maendeleo yoyote duniani unaongozwa na transparency katika miradi, mikakati na takwimu za Serikali ambayo sifa yake kubwa ni kuruhusu ukosoaji stahiki kutoka katika kada mbalimbali. Leo hii watu wanaamini kwamba kuna uwazi na ukosoaji wa kiwango cha juu kuliko wakati mwingine, lakini ukweli ni kwamba watu hawakosoi bali "wanalalamika" kunakoendana na kukosa taarifa zilizo wazi na sahihi kutoka Serikalini. Hili kwangu naona ni kosa kubwa ambalo katika kipindi cha Nyerere halikuwepo. Tukubali kwamba Nyere aliongoza katika kipindi cha changamoto nyingi sana za kiuhaba wa wataalam, teknolojia, mawasiliano na idadi kubwa ya wasiojua kusoma na kuandika. Kwa kifupi "overall" performance ya viongozi wa sasa Afrika nzima ni ya hovyo kabisa na ina tofauti kubwa na wale wa baada ya Ukoloni. Viongozi wa kileo wanashindwa hata "kauli" ili kufanya jambo liende au litendeke.

Lakini, tunapojadili suala la mishahara, nadhani hatuna budi kumtafuta mchawi halisi. Muundo wa utumishi wa umma leo hii, wahitimu wenye sifa sawa wakiajiriwa katika taasisi mbili tofauti mmoja (say) EWURA na mwingine Wizara ya Elimu; kuna tofauti kubwa sana ya mishahara na marupurupu yao. Je ni nani aliyeasisi na kupitisha upuuzi huu? Ni kweli mishahara mikubwa TRA inawafanya wasiwe wezi wa rushwa, muda na mengineyo? Je ni kweli Mhadhiri wa Chuo Kikuu mwenye cheo cha "Associate Professor" anayefanyakazi masaa zaidi ya 12 kwa kutafiti na kuhadhiri huku akitakiwa kufikia "performance delivery standards" anastahili kuzidiwa Mshahara na marupurupu na Mganga wa Kienyeji aliyeshinda ubunge na kuhudhuria vikao vya Bunge mara 4 kwa mwaka huku hana "performance delivery standards"? Is this logical?

Nimefaidika na jambo moja kwenye thread hii, kwa kuwa ilishatokea Mshahara wa Ngazi ya uwaziri kupunguzwa huko nyuma, nadhani ni wakati muafaka wa "Level-basis salary" badala ya hii institutional-basis salary kwa nchi nzima.
 
hata mimi humu nawaambiaga hauna uhusiano wowote na "Rais" bali unauhusiano na "Mama Salma" hawasikii. Jamani mumuwache Mutoto wa Mujini.!
wewe mbona mtoto wa kwanza wa Josephine.
 
Back
Top Bottom