Mishahara mikubwa waliokuwa wanalipana Nyerere na viongozi wenzake kweli ilikuwa ni sahihi

Vyovyote itakavyokuwa, baba yako anamshahara kidogo lakini anatumia mabilions ktk safari za kila
mwezi ambazo watanzania hatuna cha kujivunia zaidi ya kushuhudia rasirimali zetu zinayoyoma kwa kasi
kwenda ng'ambo, uk,china,Canada,USA,nakwingineko duniani.
 
Naona tarehe 14 october inakuja !
Sijui ni nani anayeratibu zoezi la kumkashifu Nyerere?
 
Mkuu Nguruvi3.

Haya maneno niliyoyaleta siyo yangu ni maneno ya Nyerere mwenyewe akiwaambia wanafunzi wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam walioandamana mpaka Ikulu kupinga mishahara waliokuwa wanalipana viongozi.

Wala hakuna popote niliopofananisha na mishahra hiyo na kipindi hiki.

Nimeweka haya maneno tujadili kama watanzania hata kama tunapishana mitazamo yetu kisiasa.
 
Last edited by a moderator:
Naona tarehe 14 october inakuja !
Sijui ni nani anayeratibu zoezi la kumkashifu Nyerere?
Unaweza kutuonyesha ni kashfa ipi kafanyiwa Nyerere?
 
Kwa mantiki yako mkuu kama mnahalisha kulipana mishahara mikubwa kwa nini mnatuibia???
Rushwa za ajabu hadi kujengewa ma paradise Bilira Kempisk!!
Hamuoni aibu???
 
@Ritz , kati ya habari yako na ya Mchambuzi ipi inaweza kuchambuliwa kwa uhalisia
 
Kwa mantiki yako mkuu kama mnahalisha kulipana mishahara mikubwa kwa nini mnatuibia???
Rushwa za ajabu hadi kujengewa ma paradise Bilira Kempisk!!
Hamuoni aibu???
Kwa mantiki hiyo pia inawezekana hawa viongozi wa sasa hivi wanaolipana mishahara mikubwa wameiga huu utaratibu kutoka miaka hiyo viongozi walivyokuwa wanalipana mishahara.
 
Nilijua utatia team una kiherehere dah ngoja ninyamaze nisije nikapigwa ban kwasababu ya huu utumbo ulioandika hapo juu

wewe achana na mimi.. sio level yako. mmezidi kumdhalilisha baba wa taifa
 
Ritz , kati ya habari yako na ya Mchambuzi ipi inaweza kuchambuliwa kwa uhalisia
Mkuu Nguruvi3.

Sijui umetumia vigezo gani ili habari ichambuliwe kwa uhalisia labda habari ikiwa na paragraph nyingi ndiyo inakuwa na uhalisia.

Siku zote kauli za viongozi hata kama ameandika mistari miwili au kasema maneno machache huwa yanazua mijadala. Mfano kauli ya Waziri Mkuu Pinda "Wamezidi wacha wapigwe"
 
Last edited by a moderator:
kwa kweli mishahara hii haikuwa sahihi kabisa.Je na viongozi wa sasa wanavyolipana mishahara mikubwa ni sahihi??
 


Mimi nafikiri ulitakiwa ujue alipunguza hiyo mishahara ya viongozi na kuongeza ile ya walalahoi. kabla kumwita muwazi.

labda nikupambanulie kidogo wakti huo tanzania ilikuwa inahishimu WANASIASA na WATAALAMU wa fani nyingine zote walikuwa hawathaminiki. Hivyo unaposema viongozi wakti huo wote walikuwa wanasiasa na ililazimika watu wengi wasomi wasomee Siasa ili uwe na maisha mazuri.

Hicho ndicho kilichopelekea kuuwa uchumi wa Tanganyika kwani hata maamuzi yao waliyafanya kwa mtazamo wa kisiasa zaidi bila kushirikisha wataalamu na hata kuwaandaa wananchi.

Mfano.
1.Azimio la Arusha. Japo lilikuwa zuri lakin lilifeli kuinua uchumi wa nchi.
2. Ujamaa Vijijini ulikuwa na lengo zuri sana lakin uliacha wananchi mmoja mmoja katika umasikini mkubwa.
3. Siasa ni kilimo. Hili liliuwa uwezo wa nchi katika kuweza kujimudu kwa chakula na kuleta njaa kubwa.

na mengine mengi yaliletwa kwa mamuzi ya kisiasa na kutowaandaa wananchi kiasi cha kuleta maafa makubwa japo kimtazamo yalikuwa na lengo zuri.

kifupi uchumi wa Tz umedidimizwa na maamuzi ya wanasiasa.

Poleni sana
 
Mchambuzi
Kwanza siku zote unapotaka kuchangia hoja kama hii ambayo imetolewa NUKUU ya Nyerere mwenyewe na amekuwekea mpaka source yake unatakiwa kuwa makini na kupunguza ushabiki. Kumbuka kuwa Nyerere hakuna mwenye kumchukia bali kinachojadiliwa na uongozi wake ambao kama mwanadamu unaona wazi ulikuwa na mapungufu ambayo mengi hivi sasa mnayapata.

nakukumbusha. Mkoloni alikuwa na Utawala mzuri ambao ulitoa haki kwa kila tabaka na ndio lililopelekea hakuweza kuwa njaa wala rushwa. na kila mtu alilipwa kwa mujibu wa kazi yake na ilmu yake. Japo kulikuwa na matabaka ya rangi ambayo yaliwekwa pale kuhakikisha kuwa maamuzi na maslahi ya wakoloni yanatimizwa na malengo yao yanafikiwa.

Kumbuka kuwa wakoloni kila walichokifanya utakiona kilikuwa na mana sana kiuchumi na kilileta tija sio tu katika utawala wao bali na hata wananchi wa kawaida wa tabata la chini. Kumbuka kuwa Mkoloni hakuweza kukubali kuitawala nchi tegemezi isiyoweza kujitegemea kiuchumi bali alitaka makoloni yake yote yazalishe zaidi na kupata Ziada ambayo ndio iliyokuwa inainufaisha nchi inayotawala.

kwa msingi huo Tz wakti huo ilikuwa inajimudu kiuchumi na ndio maana hata mlipopata uhuru wenu 1962 , Thamani ya Tanzania shiling ilikuwa karibu sawa na Dola ya marekani( Dola 1 ya marekani ilikuwa sawa na Tshilin 1.20).


sasa jiulize ni kipi kilipolomosha uchumi wa Tanzania kiasi cha kufika miaka kumi ya uhuru wenu nmwaka 1972 Dola ya marekani 1 ilikuwa sawa na T Shiling 28. Na kiasi cha kumfanya Nyerere kushindwa kutimiza ahadi yake aliyoitoa siku anakabidhiwa nchi na kuwa ahidi wakoloni atawaalika baada ya miaka kumi kuja kuangalia Tz inaendeleaje?

nafikiri haihitaji ilmu ya uchumi hapo na kama ulikuwepo wakti huo utaona hali ilikuwaje. Utaona kilichotokea pamoja na Azimio la arusha sasa mlianza kulana wenyewe kwa wenyewe na thamani ya pesa yenu kuporomoka kwa kasi sana.

je unaweza pambanua kwanini?
 
Last edited by a moderator:
Hizo ni fikra zako wapi nimekuambia kuwa natetea mishahara wanayolipana viongozi sasa hivi.

Mimi sina uhusiano wowote na Rais Kikwete, unachofanya ni makosa Name Calling.

Huu ni mjadala huru.

hata mimi humu nawaambiaga hauna uhusiano wowote na "Rais" bali unauhusiano na "Mama Salma" hawasikii. Jamani mumuwache Mutoto wa Mujini.!
 
Hapo kuna makosa ya kiuandishi ama ni nini??!!!! Maana 5000 kwa 200 inapatikana ndani ya miezi 25 ambayo ni miaka 2 na mwezi mmoja na sio miaka 25. Mkuu Ritz, au Mwl alisema 50,000??
 
Last edited by a moderator:
Hapo kuna makosa ya kiuandishi ama ni nini??!!!! Maana 5000 kwa 200 inapatikana ndani ya miezi 25 ambayo ni miaka 2 na mwezi mmoja na sio miaka 25. Mkuu Ritz, au Mwl alisema 50,000??
Mkuu mjasiria.

Rais aliongea hivyo kutokana hekima rais ana marupurupu mengi sana tofauti na huo mshahara.
 
Last edited by a moderator:

Kumbe mambo yenyewe ndio haya?
 
Hapo kuna makosa ya kiuandishi ama ni nini??!!!! Maana 5000 kwa 200 inapatikana ndani ya miezi 25 ambayo ni miaka 2 na mwezi mmoja na sio miaka 25. Mkuu Ritz, au Mwl alisema 50,000??

Umeiona hii?

 
Last edited by a moderator:
Kiukweli Ritz ulitakiwa ulete matini ya kauli ya Mwalimu kama ilivyofanywa na Mchambuzi. Kwani imetupa ufahamu mpana wa kujua sababu ya kutolewa kwa kauli ile. Lakini vilevile sijaelewa kama ulikuwa unakusudia kutoa hoja yenye kujenga nini in future. Ndio maana imeleta tafsiri tofautitofauti kwa wachangiaji wako lakini tupongeze ufanisi wa Mchambuzi na Nguruvi3 kujaribu kuijenga hoja ijadilike na hatimaye ije na sunstantive idea on the way forward.

Pamoja na mapungufu aliyokuwa nayo Nyerere kama binaadamu, lakini mapungufu ya waliomfuatia ni makubwa sana ukilinganisha na yeye. Mfumo wa maendeleo yoyote duniani unaongozwa na transparency katika miradi, mikakati na takwimu za Serikali ambayo sifa yake kubwa ni kuruhusu ukosoaji stahiki kutoka katika kada mbalimbali. Leo hii watu wanaamini kwamba kuna uwazi na ukosoaji wa kiwango cha juu kuliko wakati mwingine, lakini ukweli ni kwamba watu hawakosoi bali "wanalalamika" kunakoendana na kukosa taarifa zilizo wazi na sahihi kutoka Serikalini. Hili kwangu naona ni kosa kubwa ambalo katika kipindi cha Nyerere halikuwepo. Tukubali kwamba Nyere aliongoza katika kipindi cha changamoto nyingi sana za kiuhaba wa wataalam, teknolojia, mawasiliano na idadi kubwa ya wasiojua kusoma na kuandika. Kwa kifupi "overall" performance ya viongozi wa sasa Afrika nzima ni ya hovyo kabisa na ina tofauti kubwa na wale wa baada ya Ukoloni. Viongozi wa kileo wanashindwa hata "kauli" ili kufanya jambo liende au litendeke.

Lakini, tunapojadili suala la mishahara, nadhani hatuna budi kumtafuta mchawi halisi. Muundo wa utumishi wa umma leo hii, wahitimu wenye sifa sawa wakiajiriwa katika taasisi mbili tofauti mmoja (say) EWURA na mwingine Wizara ya Elimu; kuna tofauti kubwa sana ya mishahara na marupurupu yao. Je ni nani aliyeasisi na kupitisha upuuzi huu? Ni kweli mishahara mikubwa TRA inawafanya wasiwe wezi wa rushwa, muda na mengineyo? Je ni kweli Mhadhiri wa Chuo Kikuu mwenye cheo cha "Associate Professor" anayefanyakazi masaa zaidi ya 12 kwa kutafiti na kuhadhiri huku akitakiwa kufikia "performance delivery standards" anastahili kuzidiwa Mshahara na marupurupu na Mganga wa Kienyeji aliyeshinda ubunge na kuhudhuria vikao vya Bunge mara 4 kwa mwaka huku hana "performance delivery standards"? Is this logical?

Nimefaidika na jambo moja kwenye thread hii, kwa kuwa ilishatokea Mshahara wa Ngazi ya uwaziri kupunguzwa huko nyuma, nadhani ni wakati muafaka wa "Level-basis salary" badala ya hii institutional-basis salary kwa nchi nzima.
 
hata mimi humu nawaambiaga hauna uhusiano wowote na "Rais" bali unauhusiano na "Mama Salma" hawasikii. Jamani mumuwache Mutoto wa Mujini.!
wewe mbona mtoto wa kwanza wa Josephine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…