Elections 2010 Misikiti nayo yaanzisha mkakati kuhusu uchaguzi mkuu ujao!

Elections 2010 Misikiti nayo yaanzisha mkakati kuhusu uchaguzi mkuu ujao!

Kama kuna kitu kinakera ni kujiona dhaifu, unaonewa n.k. Ndugu zetu waislamu kila siku wao ni kulalamika tuuu, mara udini mara n.k. Why..?? Mambo yafuatayo yamewahi kunikera sana tena sana..!!

1. Malalamiko Juu ya Uteuzi wa Viongozi na Selection Wanafunzi:

Wakati wa Mwinyi hawa jamaa waliwahi kudai kuwa uteuzi wa viongozi unabase sana kwenye udini. Wakaongeza kuwa, hata selection ya wanafunzi from Form IV to V nao unabase kwenye udini bila kusahau kuwa waziri wa elimu by then alikuwa Professor Juma Kapuya. And I remember Kapuya naye aliwaponda kwa kuwaambia kuwa, uongozi plus shule inaangalia uwezo wa mtu.

2. Malalamiko Dhidi ya Mchakato wa Kanisa:

Unless sijauelewa vizuri, ila lengo kuu la huu mchakato si kuwapenyeza vingozi wa kikristo kwenye ubunge au urais, la hasha. Lengo ni kuwaelemisha wananchi juu ya maandalizi ya uchaguzi kama wakristo. Ikiwa ni pamoja na kusali, na hata kwa wale watakaopenda kujiweka katika mchakato, then wawe wameelimika kidini lengo likiwa ni kupunguza ufisadi. Ufisadi ni ugonjwa wa kiroho, yaani mtu mwenye roho chafu ya kifisadi, hata umpe Twin Towers umwambie ni ya kwake, bado kesho atafanya ufisadi. So, ni swala la kiroho zaidi, na ndio maana kanisa likaonelea liwaelemishe waumini juu ya ufisadi, uchaguzi, na hata uongozi wa nchi. Hii ikiwa ni kupunguza dhana potofu ya kuwa ukipata uongozi umeula.

3. Mahakama ya Kadhi:

Niliwahi kusikia malalamiko juu ya kwanini serikali yetu ina ubalozi Rome plus why tuna baraza la maaskofu and why pasiwe na mahakama ya kadhi. Huu kwangu mimi ni upungufu wa confidence. Ubalozi Rome ni sawa na sisi tulivyo na balozi pale Iran na nchi nyingine za kiarabu ambazo mlengo wake ni wa kiislamu zaidi. Ikaja mada ya why tuna Baraza la Maaskofu, it's ok ila cha muhimu isiingilie taratibu wala katiba ya nchi. Mahakama ya kadhi ililenga kwenye kuingia hadi kwenye katiba na ukichimba zaidi, ndio maana walitaka hata Stamp ya serikali. Kama ni baraza tu la kawaida kama baraza la maaskofu, why wahitaji baraka za serikali. It means ilitaka kuingilia Judiciary system ya nchi. Ambapo, mkristo ukichangamana na muislamu kwenye anga zake then unakandamizwa kwenye mahakama ya kadhi. Wasifiche fiche concept ya mahakama ya kadhi, we know it very well. Kwa mantiki hii, huo udini wanauleta wao and not wakristo.

4. Kipindi cha Makwaia - Je Tutafika:

Huyu mzee kwa kweli ananikera and I even doubt uwezo wa mamlaka (MOAT) juu ya professionalism ya huyu mzee. Ukiwa mwandishi wa habari, hutakiwi kuwa biased in any topic inayojadiliwa. Huyu mzee ikijaga mada ya kiislamu and since yeye ni muislamu huwa anasimama kiislamu zaidi and huwa hapingani na upande wa uislamu. Pia nimeanza hadi kudoubt kuwa mada zake kama ile ya Kadhi, hii ya Kanisa na Uchaguzi plus hii ya juzi ya Iran; huwa anaandaa hadi waislamu wa kuja kudiscuss. Kwa kweli huyu mzee anakokwenda yapaswa kuzuiwa mapema otherwise atachochea machafuko kwa pande zote mbili hasa kwa watu ambao ni innocent kabisa na haya mabishano. Issue ya mchakato wa kanisa, alipaswa kumleta Pengo au Kilaine as ndio wahusika wakuu and not Lusekelo. Issue ya Kadhi alipaswa kuwaleta vingozi wa dini ya kikristo au wataalamu wa maswala ya sheria kama kina Mvungi n.k. and not wafata upepo kama kina Mrema.

In short, hii nchi jinsi waislamu wanavyotaka kuivuruga, sijapenda kabisa. Wanataka kuwa muhimu kuliko dini zingine, everytime. Na yote hii ni dalili ya mtu/watu kujiona udaifu.

Mungu awafungue macho na akili muweze kuona athari za mabishano haya yenye nia mbaya. Mungu ibariki Tanzania.
 
Ni wajibu wa kila Dini kuelimisha waumini wake kuhusu mambo mema kutokana na misingi ya dini husika, kama dini imeona viongozi wanachaguliwa kwa rushwa shahada zinanunuliwa, kura zinaibwa, viongozi wanasema uongo na kuahidi wananchi uongo. Viongozi wanaiba fedha za kodi sheria za nchi hazifuatwi ni lazima wakemee na wawaelimishe waumini wao kwamba kiongozi anatakiwa kuwa wa namna gani na wananchi wamchague mtu mwenye tabia gani kwani viongozi hao hao ni baadhi ya waumini.

Si Jambo baya kabisa kwa dini yeyote ile kutoa elimu ya kupiga kura kwa waumini wake kwani wanaoathirika na matokeo ya uchaguzi ni pamoja na waumini hawa.

Na vile vile wakati umefika hata polisi na Jeshi nao wapewe elimu ya kupiga kura na kiongozi gani wa kumtii si kila kauli ya kiongozi ni nzuri kuna nyingine zinaleta maafa makubwa kwa wananchi, kwani utii bila akili ni uwendawazimu.

Mazingira haya ya viongozi wa dini kuamua kuingilia kati yameletwa na utawala mbovu wa CCM. Ni ukweli usiofichika kwamba mwisho hautakuwa mzuri kwani si rahisi mpagani kufurahia au mkristo kuwa ok na mwisilamu kuona poa pale kundi moja linapojipanga kwa ajili ya nani anafaa kuchaguliwa kwani mafundisho ya dini zenyewe yanakinzana some how. Lazima CCM itabeba lawama kwani utawala wa sheria na usawa haujazingatiwa sasa kila mmoja inabidi amwamini shehe, askofu, padri, mchungaji wake kuliko mwanasiasa.

Ikumbukwe viongozi wa dini wana-nguvu sana ktk jamii, baada ya kuwahubiria wananchi kuwa serikali imeshindwa na viongozi wake kuwaletea maendeleo na huduma bora za jamii kama maji, elimu, hospitali na makazi wao (dini) wanawaonyesha hospitali bora za dini, maji safi , elimu bora kwa kutumia shule za dini. Viongozi hawa hawatachelea kuwaambia waumini wao kuwa pamoja na kulipa kodi kubwa serikali imeishia mifukoni mwa akina Rostam Aziz na safari za Rais USA na kwingineko, wao wakiaachwa kalubandike.Wakati watoto wao wakikosa elimu wao viongozi wanagawana Meremeta kwa kusingizia usalama wa Taifa. wakati mwananchi anakufa kwa safura wao wanagawana MSD. Wakati wananchi wanakufa kwa sumu ya machimbo wao wanagawana dhahabu. Hasira itatupanda tutawaamini sana viongozi wetu wa dini na tutasaliti uongozi wetu na Mtanzania ataaanza kuwa huru.
Kitim Tim je wakati viongozi wa CCM wanakata roho nini kitatokea? Hapo na mwachia Mwanakijiji amalizie.
 
Kiongozi according to whmo? kama ni kwa ajili ya makanisa then huo ni UDINI! (opportunitiscs)
a)Kazi ya kutoa elimu ya uraia siyo ya Kanisa wala msikti ni Tume ya uchaguzi (serikali)
b) Kanisa limepanga mkakati wa kumiliki uchaguzi tutegemee shida baadaye nchi imeshakos umoja naona hatari ya kubaguana imekaribia
c) tunahitaji kiongozi atakayeaminiwa na wakristo na waislamu wote (yaani atakayeaminiwa na watanzania wote bila kujali dini...otherwise
d) Conclusion: Walichofanya kanisa katoliki ni ubaguzi!, Walichofanya waislamu ni ubaguzi! (Wote hawafai)
Tusichague Mkatoliki wala muislamu inabidi tuchague (otodox) wale wanaosali jumamosi watakuwa afadhali.

Mbona na wewe unakuwa MDINI???
 
kama kunawakati roho huwa inaniuma na kumjutia mwenyezi mungu kwa kuniumba MTANZANIA ni pale nchi inapokuwa kwenye wakati mgumu kama huu lakini watu wake wanaishia kujibizana na kujadili upuuzi usiokuwa na kichwa wala mkia kama UDINI, MAHAKAMA YA KADHI, IOC NA NYARAKA ZA VIONGOZI WA DINI.....MUNGU NAOMBA UNINUSURU NA TAIFA HILI LA WAPUMBAFUUUU KABISA....

badala ya kujipanga na kutafakari jinsi ya kuwatoa hawa viongozi wajinga wanaoleta upuuzi huu tunaungana nao kuwashangilia then 2010 wanarudi MJENGONI na kututia umasikini wa kufa KWA MIKATABA FEKI, UFISADI, WIZI WA RASILIMALI ZETU....
 
wana-JF tunafulia...yani kwa akili zetu tunabishana UDINI???....Hatujui madhara ya udini ni makubwa kuliko hata ya UKABILA WA RWANDA NA BURUNDI?...au TUMESAHAU HABARI ZA WASHIA NA WA-SUNNI?
 
Mimi ninachofahamu ni kuwa hilo jopo la maulamaa wa kiislamu chanzo cha kuanzishwa kwake sio kujibu mapigo ya kanisa katoliki. Wazo la kuanzishwa jopo hilo lilitolewa pale Mzee Mwinyi alipopigwa kofi na kijana mmoja. Lengo la jopo hilo ni kutoa matamko mbalimbali (fatwa) kuhusu masuala mbali yanayowahusu waislamu, na kupunguza ile hali ya kila mtu kuamua kuwa msemaji wa waislamu.

Nathani hayo yanayojadiliwa hapa ni maoni ya mwenyekiti wa jopo hilo ambayo yamekuwa quoted out of context. Kwa utaratibu hayo majopo yana majina mbabalimbali mfano, Council of Scholars au Kule Irani wanaliita Guardian Council. Kwa kawaida rai ya jopo (fatwa) inatolewa kwa makubaliano ya wajumbe wote. Alichofanya mwenyekiti wa jopo hilo ni kutoa baadhi ya maeneo ambayo jopo linawaza kuyatolea tamko, na hiyo haiwezi kuwa ndio rai ya jopo kwani lilikuwa ndio linazinduliwa.
 
Hii concept ya ndg zetu waislamu kabla hata haija-mature mijitu tiyari mimacho imewatoka kwa chuki zao..Yaani hawataki hata kupata full story tayari wameshatoa hukumu!

Ukisoma muelekeo wa thread utagundua watu wengi humu wanakosa objectivity kwa kiwango cha kusikitisha. Nijuavyo JF ni ile cream ya waTz ambao wamefuta ujinga. Kujua kutumia PC na kutuma post ni dalili umepitia phases basic za kufuta ujinga..Sasa kama top cream can think this low, nadhani hali ni mbaya zaidi kule vijijini na majiani..

Mungu atunusuru.

Waambie ukweli.
 
Last edited:
Kuna viongozi wa kidini wanaotumika katika siasa hawa ndio maadui ,mahubiri yao hujihusisha sana na siasa wengine kufikia kusema kuwa fulani ni chaguo la Mungu ,sasa ukifikia kusema hivyo ni sawa na kuwaelekeza wafuasi wa dini wakumchagua.

Usije ukafikiri wale ambao hawakusema chaguo la fulani walikaa kimya tu. Kadi za uanachama wa chama cha CUF ziligawiwa sana misikitini na mazoezi karate ya kulinda kura (baadhi yao walidai hiyo ilikuwa ni suna ya mtume kufanya mazoezi) yalifanyika sana misikitini mwaka 2005, ukiacha mahubiri misikitini na mihadhara mbalimbali ya kiislamu kuhusu siasa na uchaguzi. Usiwafanye watu hawakuona kilichofanyika, siku hizi kila kitu kiko wazi!
 
Last edited:
Haya mambo wakati mwingine yana kila aina ya upuuzi! Haya makundi mawili yanataka kufundisha vitu viwili tofauti kuhusu haki za uraia au masuala ya uraia? Ni kwa sababu hiyo tu ndiyo utaona ulazima wa Makanisa kuwa na elimu yao ya "uraia" na Misikiti kuwa elimu yao ya uraia na vile vile taasisi nyingine kuja na elimu yao ya "uraia".

Kama hawa wote wangekuwa na nia nzuri ya kumfundisha mwananchi kanuni na misingi ya uraia na ushiriki wa kidemokrasia basi wangekaa chini wasomi wa kiislamu na wa kikristu na asasi nyingine na kutunga somo hilo la uraia na watu wake waweze kuelewa na hivyo shehe wa kiislamu anaweza kuja kufundisha kwenye jamii ya wakristu (baada ya ibada n.k) mambo ya uraia na mchungaji au mwalimu wa dini anaweza kuzungumza mbele ya waislamu juu ya uraia bila hofu ya kuwa anaeneza mambo kwa misingi ya udini.

Nje ya hapo ni ujuha na kufukuza upepo! NI kuleta migongano isiyo ya lazima.
 
Haya mambo wakati mwingine yana kila aina ya upuuzi! Haya makundi mawili yanataka kufundisha vitu viwili tofauti kuhusu haki za uraia au masuala ya uraia? Ni kwa sababu hiyo tu ndiyo utaona ulazima wa Makanisa kuwa na elimu yao ya "uraia" na Misikiti kuwa elimu yao ya uraia na vile vile taasisi nyingine kuja na elimu yao ya "uraia".

Kama hawa wote wangekuwa na nia nzuri ya kumfundisha mwananchi kanuni na misingi ya uraia na ushiriki wa kidemokrasia basi wangekaa chini wasomi wa kiislamu na wa kikristu na asasi nyingine na kutunga somo hilo la uraia na watu wake waweze kuelewa na hivyo shehe wa kiislamu anaweza kuja kufundisha kwenye jamii ya wakristu (baada ya ibada n.k) mambo ya uraia na mchungaji au mwalimu wa dini anaweza kuzungumza mbele ya waislamu juu ya uraia bila hofu ya kuwa anaeneza mambo kwa misingi ya udini.

Nje ya hapo ni ujuha na kufukuza upepo! NI kuleta migongano isiyo ya lazima.

Umesema sawi, na hii ndio inaitwa objectivity, wala sio mbali na wala hakuhitaji shule kubwa kuona hilo.

Wanachoshindwa kuona wengi ni kuwa nia inaweza kuwa nzuri ( na ndivyo ilivyo ) lakini utekelezaji wake inaleta mashaka kwa sehemu kubwa na muhimu katika jamii.

Wanasheria wanasema "haki sio tu lazima itendeke, bali ionekane inatendeka"
 
Kama wewe uliona CUF wakigawa kadi misikitini ulishindwa nini kusema kwa vyombo husika acha elimu yako na thinking yako iko chini sana, akili yako kama omary mahita? unanikumbusha mbali kweli ulivyo mjinga? unadahni nchi haina usalama? acha propaganda na unafiki?

Una uhakika gani kwamba sikutoa taarifa? Hiyo thinking capacity yako na elimu yako iliyo kubwa iko wapi hata ukaita watu wajinga bila haya? Wasomi huwa wanajibu hoja kwa hoja na sio kuweka defensive mechanism kwa matusi ambayo hayabadilishi fact! Ninachoongea nina uhakika nacho hata kama hukitaki. Huwezi kubadilisha fact kwa jazba na matusi. Mahita aliongea alichokiona (whether it is true or not I have no comment) na mimi naongea nilichokiona. Sasa ubaya uko wapi? Grow up plse!
 
Sasa nao wanataka mtu ambaye ataanzisha Mahakama ya Kadhi japokuwa CCM katika Ilani yao wanasema hivyo lakini Waislam wana haki ya kuidai CCM ile Ilani inayosema kuwa wataanzisha mahakama ya kadhi

Wanasiasa kipindi cha kuomba kura ni sawa na kijana wa kiume anavyoweza kuongea maneno matamu kwa binti ili tu akubaliane na matakwa au mpango wake. oooooo nitaku...., halafu nitaku......., kisha nita.....
Wanasiasa wanasema barabara zote tutaweka lami! masha yatakuwa safi... nk.

Basi maneno ni 'matam tam' tu, kila msikilizaji 'meno nje' kisha kiulaini tunawapa 'kura' ili waendelee 'kula'. Tuwe macho na wanasiasa wanapotuahidi mambo ambayo ni magumu kutekeleza. Tuzipitie ahadi zile walizoto na tuone wamefaulu kwa kiasi gani. Moja tu walau ile slogan: 'Maisho Bora kwa kila Mtanzania' iko wapi leo?
 
Hiyo siyo kazi ya Kanisa? ni kazi ya vyama vya siasa, Tume ya uchaguzi na serikali...hawana jipya zaidi ya UDINI uliotukuka! walaaniwe wote wanaotaka kutugawa kwa misingi ya dini zetu hasa hawa wakatoliki.

Tatizo la wengi humu ni kudandia gari kwa mbele.wewe ni mfano hai kabisa unaojitosheleza.
 
Unapije nia nzuri?
Nia nzuri hujipajiki lazima uonyeshe kwa vitendo na uwe tayari kwa mjadala na jamii!
Kanisa limeanzisha waraka wa uchaguzi wengi tulitegemea laziam waislamu wata-counter attack... that is the nature kama unaona kuna watu wanataka kujipendelea kwa namna yeyote ile!
ushauri wangu: Kanisa liweke wazi na miskiti iweke wazi! au yote mawili yafutwe kwakuwa naona ni "UDINI" hakuna jipya wakristo wadini waislamu wadini no less than that ..futa upuuzi wa wakatoliki na waislamu waache waumini waamue kwa elimu yao wenyewe !

Dua ya kuku.. (malizia)

kanisa katoliki kama taasisi inayoendeshwa kisomi imekuwa ikitoa barua za kichungaji kwa waumin wake kuhusu nyanja mbalimbali ktk kuboresha maisha ya waumini wake..kiroho na kimwili..na haijaanza leo na wala usitegemee wataacha kwa sababu ya dua za kuku za watu kama wewe na ngumbaru Manju Msambya..
 
Haitaji unajimu kujua kwamba dini ni bomu likalo fuatia baada ya mabomu ya mbagala manake wabongo hawako tayari kujadili dini na viongozi wa dini hata kama wanachokifanya si sahihi. Dini sasa hivi inajipa majukumu zaidi ya serikali na ni untouchable sababu waumini wamekwiva kutetea bila kufikiri.

Lazima tukubali maaskofu, mashekh n.k ni raia wa Tanzania na wanahaki sawa na raia wengine hapa duniani labda huko mbinguni sina hakika, vyovyote vile wasijipe daraja la juu katika kufuata sheria.

Kama mnafikiri viongozi hawa wa dini ni salama basi kumbukeni mauaji ya kimbari ya Rwanda dini na viongozi wa dini walihusika katika kuyafanikisha, sasa subirini wabongo kujifunza kutoka katika makosa yenu. Hizi chokochoko za sasa kila mtu ajiandae kivyake manake viongozi wa dini hawana la kheri kwa sisi ambao si waumini wa dini zao.
 
Kwa jinsi ulivyo kasirika inaonyesha tu kwamba hauko huru kwenye mawazo yako grow up!
Hakuna aliyekutukana nimekwambia uwezo wako ni mdogo sana, kama ulishafikisha mbona hatukusikia watu wakipelekwa mahakamani kwa kuvunja sheria ya nchi? kwasababu kufanya hivyo ni kinyume na sheria! sijawahi kuona watu wakipelekwa kisutu kwasababu?
Akili yako kweli kama Omary Mahita mkuu (unajua alitakiwa afanyaje?) alitakiwa kuwashika na kuwashtaki wahalifu siyo kupiga siasa na ujinga na propaganda "Lakini hatajaona aliyepelekwa mahakamani upuuzi mtupu" low thinking!

Inategemeana na unayempelekea taarifa inawezekana akili yake ni kama ya kwako ila mazoezi yalikuwepo na kadi ziligawiwa! Hiyo nako inahitaji kwenda shule jamani? Kwani wewe huwa unakuwepo kwenye misikiti yote wakati wote? Mimi sijakasirika, umeniona wapi wewe mwenye akili nyingi na mtabiri kama Sheikh Yahya? Hao unaodai ni usalama wa taifa au ni usalama wa viongozi mafisadi? Walikuwa wapi wakati mabilioni yakiibwa BOT mpaka akina Dk Slaa wakaja kutoa taarifa za wizi huo?
 
Last edited:
Back
Top Bottom