Misururu ya magari kwenye misafara ya ziara za viongozi wetu ni ushamba wa kizamani sana!

Misururu ya magari kwenye misafara ya ziara za viongozi wetu ni ushamba wa kizamani sana!

View attachment 2903613
Kuna vitu ukiviona bado vinafanywa na viongozi wa kiafrika katika karne hii unabakia kucheka na kuwaza kuwa kumbe viongozi wa kiafrika bado wana akili za kitoto mnoo.

Moja ya vitu vya kipuuzi kabisa ni msururu wa msafara wa magari ya kifahari kwenye ziara za viongozi duni wa nchi za kiafrika (Tanzania ikiwa ni mfano mzuri). Mambo ambayo yalipaswa kufanywa karne iliyopita wakati watu wakiwa harusini, eti ndio trend fashion ya viongozi wa kiafrika wa sasa.

Mbwembe hizo na ufahari hazina faida yoyote, zinawaudhi mnoo raia wa kawaida wanaokuwa busy na maisha yao na wala hawana time na hizo takataka.

Misafara hiyo hufunga barabara kwa muda, huacha vumbi la hatari vijijini, hupelekea matukio ya ajali nk. Utasikia viongozi wakisema eti wako busy kwenda kusikiliza kero, kuzindua ujenzi wa vyoo vya shule vilivojengwa kwa pesa za misaada ya wazungu, kukagua mradi wa bomba la maji la kijiji, kukata utepe ili kuzindua kivuko cha miguu cha kijiji

Inatia kinyaa mnoo.
Kila mtu na urefu wa kamba yake.
 
Msururu wa magari 50 weka mafutaaa..weka PER DM hapo ndo utajua afrika tuna laana hizo gharama za mafuta na per DM zinaweza fika gharama za mradi husikaaa
 
Kuna kiongozi simjui Ila anapitaga yeye tu na dereva wake na Gari ni ndogo Ila vimwakumwaku vya Polisi kuonyesha huyu anaepita ni kiongozi sio hio mi LC300 halafu safi Ila dereva wake ana kazi 2 kumlinda kiongozi na kuendesha Gari maana hakuna ulinzi
 
Na wengine utawaona wamezungukwa na maaskari wakiwa na mabunduki utafikiri nchi ipo vitani! Lakini hayo huwezi kuyaona kwa viongozi wa nchi zilizoendelea kama USA,UK,France au Germany,yote ni kwa sababu ya kujikweza,kupenda utukufu na ulimbukeni tu.
 
View attachment 2903613
Kuna vitu ukiviona bado vinafanywa na viongozi wa kiafrika katika karne hii unabakia kucheka na kuwaza kuwa kumbe viongozi wa kiafrika bado wana akili za kitoto mnoo.

Moja ya vitu vya kipuuzi kabisa ni msururu wa msafara wa magari ya kifahari kwenye ziara za viongozi duni wa nchi za kiafrika (Tanzania ikiwa ni mfano mzuri). Mambo ambayo yalipaswa kufanywa karne iliyopita wakati watu wakiwa harusini, eti ndio trend fashion ya viongozi wa kiafrika wa sasa.

Mbwembe hizo na ufahari hazina faida yoyote, zinawaudhi mnoo raia wa kawaida wanaokuwa busy na maisha yao na wala hawana time na hizo takataka.

Misafara hiyo hufunga barabara kwa muda, huacha vumbi la hatari vijijini, hupelekea matukio ya ajali nk. Utasikia viongozi wakisema eti wako busy kwenda kusikiliza kero, kuzindua ujenzi wa vyoo vya shule vilivojengwa kwa pesa za misaada ya wazungu, kukagua mradi wa bomba la maji la kijiji, kukata utepe ili kuzindua kivuko cha miguu cha kijiji

Inatia kinyaa mnoo.
Naunga mkono hoja
P
 
Leo kwenye follen barabara ya Bagamoyo niliona gari inapiga king'ora ili ipishwe, nyuma ni "W" , nauliza nae waziri ana king'ora?.
 
Back
Top Bottom