Miti ipi inakua haraka inafaa kwa fensi?

Miti ipi inakua haraka inafaa kwa fensi?

Aya majina yanampa mtoa mada kizunguzungu.
.
..
...
Kuna miti inafaa sana kwa fans tafuta huu Allocasuarina luehmannii
alafu utapata pesa lazima watu waje kujifunza jinsi ulivyoitunza 😁!.
Wallah mtaniua na haya majina...
Google watapata shida na mimi😀
 
Sawa. Sasa umeweka vema. Mwanzoni nilikuw na mawazo ya majumbani. Miti mizuri kwa hicho unachotaka ni hii hapa chini (fungua link). Kitaalamu huitwa Milicia excelsa. Uitaji majina kwa mimiea ni kizungumkuti, utaona hapo common name wameuita mvule (sina hakika kama ndo mivule hiyo). Ni miti safi mno. Inanyooka na kuwa na mbao ngumu safi sana. Changamoto yake ni kukua taratibu. Mti mwingine ninaona unatumika sana Uchagani ni Grevillea. Cheki link ya pili. Hii haichukui muda kukomaa, nayo ni chanzo kizuri cha mbao laini.


1.https://en.wikipedia.org/wiki/Milicia_excelsa#/media/File:Milicia_roadside_small.jpg


2.https://en.wikipedia.org/wiki/Grevillea_robusta#/media/File:Silveroak.jpg


zingatia

Hali ya hewa ya mahali ulipo ni muhimu sana. Waone wataalamu wa misitu wakupe shule na ushauri.Popote ulipo, tafuta ofisi za wakala wa misitu, huwa wanauza mbegu za miti ya aina nyingi. Ninajua Morogoro,kwa mfano, wapo. Usiende kwa wabongo, akina sisi tunaojiuzia miti chini ya kivuli,nenda ama tafuta mtaalamu.

Badala ya mivule (Milicia excelsa) anaweza kupanda mijohoro (Senna siamea), inakua haraka sana tofauti na mivule atasubiri sana.
 
Majani yanachafua sana.

Ujiandae kuweka bajeti ya kufagia kukusanya na kupeleka dampo kuchoma.

Kwa mazingira ya mjini saingine ni ngumu kuchoma takataka nyumbani.
Utasumbua majirani kwa moshi, hatari ya kuchoma nyaya za umeme n.k
 
Back
Top Bottom