Mitoto unaihangaikia peke yako ikifika ukubwani inaenda kutafuta ukoo wao...

Mitoto unaihangaikia peke yako ikifika ukubwani inaenda kutafuta ukoo wao...

Ralph Tyler

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2015
Posts
2,828
Reaction score
3,579
Hii kauli nimeisikia jana akilalama mama mmoja katika mazungumzo na wenzie kibarazani. Anadai ametunza mtoto peke yake kwa mahangaiko makubwa, kamsomesha kwa tabu kwa pesa za kuokoteza kwenye vigenge, upatu na misaada ya kaka zake. Lakini ameshangaa sana mtoto alipomaliza chuo na kuanza kupata kipato.

Mtoto ameanza kuzunguka huku na huko akiulizia ukoo wake! Huyo mama anadai amemfuma kijana akiwa anaongea na mtu wa ukoo wa babake ambaye huyo mama anamweleza kama kisirani kabisa hataki asogeze pua karibu na mwanae. Anadai amemtishia mtoto wake kuwa akiendelea kutafuta hicho anachodai ni ukoo wake, eti atamlaani!

Nauliza akina mama, hii ni sahihi? Kwanini hutaki mtoto ajue ukoo wake? Kila binadamu ana haki ya kuijua asili yake, hata kama humpendi huyo babake.

Kama unamchukia kiasi hicho huyo baba mtoto na ukoo wake wote, kwanini ulimpa? Si ungemnyima tu kuepusha shari? Mtoto hajahusika na kosa lako/lenu/la babake, kwanini unamnyima haki? Huoni kuwa huo ni unyanyapaa mtoto ajisikie kama mtu aliyeokotwa tu?
 
Hii kauli nimeisikia jana akilalama mama mmoja katika mazungumzo na wenzie kibarazani. Anadai ametunza mtoto peke yake kwa mahangaiko makubwa, kamsomesha kwa tabu kwa pesa za kuokoteza kwenye vigenge, upatu na misaada ya kaka zake. Lakini ameshangaa sana mtoto alipomaliza
Mtoto Hana kosa anahaki zote lakini mama lazima akasirike hakuna kitu kinatia hasira Kama kulea mtoto peke yako wakati babaake yupo Ana uwezo na hawajibiki kwa chochote
 
Mtoto Hana kosa anahaki zote lakini mama lazima akasirike hakuna kitu kinatia hasira Kama kulea mtoto peke yako wakati babaake yupo Ana uwezo na hawajibiki kwa chochote
Mtoto atajuaje baba yake alikuwepo na alikuwa hawajibiki kwa lolote?

Ni afadhali mama angemfahamisha mtoto kwa baba yake tangu awali, ili kama ni kweli baba hawajibiki kwa lolote basi huyo mtoto ajionee mwenyewe hali hiyo na aamue kwa utashi wake.
 
Mtoto atajuaje baba yake alikuwepo na alikuwa hawajibiki kwa lolote?
Ni afadhali mama angemfahamisha mtoto kwa baba yake tangu awali, ili kama ni kweli baba hawajibiki kwa lolote basi huyo mtoto ajionee mwenyewe hali hiyo na aamue kwa utashi wake.
Hakuna mama mwenye akili timamu ambae atakataa matunzo kutoka kwa mzazi mwenzie Ni wazi baba alikua hawajibiki Kama baba angekua na nia ya kulea mtoto tangu mwanzo mtoto angemjua baba yake na hizo hasira za uyo mama zisingekuwepo kiasi hicho wababa wanasemaga hawalei acha walelewe huko wakikua watanitafuta Sasa hiyo inatia hasira unawajibika kulea halafu unataka kufaidi matunda ya mtoto kirahisi
 
Kwani wakati unafanya starehe zako hadi anapatikana huyo mtoto kuna sehemu ukimwambia huyo mtoto kuwa unamleta duniani aje abebe shida zako?

Wazazi ninyi akitoka Mungu ndio mnakuja nyie... Je, kuna mahali popote mlipatana na watoto wenu kuwa mnawaleta duniani? Acheni ujinga. Mtoto akikusaidia au asipokusaidia hiyo ni juu yake.

Kama ni lawama walaumu wazazi wenu kwa kutowawekea msingi imara
 
Mama zetu wanatakiwa kuwa na msimamo,mfano,bwege akiikataa mimba,akamkataa na mtoto akizaliwa,basi,mama wa mtoto ajihesabie alibakwa na jambazi.

Mtoto anavyo kua awe anaelekezwa "nilibakwa na bwege moja kumbe jambazi,waliliua raia wenye hasira kali baada ya kulifumania likibaka mwanafunzi",hadi anakua mkubwa mtoto aelewe baba yake alikuwa jambazi wa ngono.

#uwemwendowakuharianatu
 
Mama zetu wanatakiwa kuwa na msimamo,mfano,bwege akiikataa mimba,akamkataa na mtoto akizaliwa,basi,mama wa mtoto ajihesabie alibakwa na jambazi.
Mtoto anavyo kua awe anaelekezwa "nilibakwa na bwege moja kumbe jambazi,waliliua raia wenye hasira kali baada ya kulifumania likibaka mwanafunzi",hadi anakua mkubwa mtoto aelewe baba yake alikuwa jambazi wa ngono.
#uwemwendowakuharianatu
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] asimwambie hivyo bwana Bora aseme babaako alikufaga
 
Hakuna mama mwenye akili timamu ambae atakataa matunzo kutoka kwa mzazi mwenzie Ni wazi baba alikua hawajibiki Kama baba angekua na nia ya kulea mtoto tangu mwanzo mtoto angemjua baba yake na hizo hasira za uyo mama zisingekuwepo kiasi hicho wababa wanasemaga hawalei acha walelewe huko wakikua watanitafuta Sasa hiyo inatia hasira unawajibika kulea halafu unataka kufaidi matunda ya mtoto kirahisi
Mama anatakiwa ampe mtoto nafasi ya kujua hilo pia. Watoto hupenda kujua ukweli wa hayo madai ya mama kuwa baba alikutelekeza, na wengine wakimpata huyo baba huwa wanamhoji na kulinganisha taarifa. Kuna mmoja namfahamu aliambiwa siku nyingi na mama yake kuwa babake ni mtu mwenye roho mbaya sana.

Mtoto alipofikisha umri wa kujitegemea akamtafuta yule baba, walichoongea wanajua wenyewe, lakini siku hizi wana maelewano mazuri tu japo hakumlea utotoni. Na huyu kijana anashirikiana vizuri na ndugu zake wa upande wa baba japo alifichwa miaka yote hiyo.

Kuna umuhimu wa kuelewa kuwa mtoto ni individual mwenye hisia zake na namna yake ya kutafsiri mambo, ukimficha sana mwishowe atakuja kupewa hadithi nyingine na ataiamini. Nafikiri ndio maana baadhi ya akina mama hawataki watoto wakutane na hao baba zao, wanaogopa hiyo hadithi atakayosema baba ambayo labda mtoto ataiamini.

Kuepuka yote hayo, mpe mtoto nafasi ya kumjua baba yake tangu awali, kama kweli huyo baba ni mbaya mtoto atajionea mwenyewe na ataelewa kwanini mama alishindwa. Na kama huyo baba ni mwema, basi mtoto ataufaidi huo wema kwa nafasi yake hata kama mama hataki.
 
Mama zetu wanatakiwa kuwa na msimamo,mfano,bwege akiikataa mimba,akamkataa na mtoto akizaliwa,basi,mama wa mtoto ajihesabie alibakwa na jambazi.
Mtoto anavyo kua awe anaelekezwa "nilibakwa na bwege moja kumbe jambazi,waliliua raia wenye hasira kali baada ya kulifumania likibaka mwanafunzi",hadi anakua mkubwa mtoto aelewe baba yake alikuwa jambazi wa ngono.
#uwemwendowakuharianatu
Hapo bora iwe kweli hivyo. Vinginevyo kuna siku wambea watamwonyesha baba yake. Na akienda kwake anapokelewa vizuri kwa bashasha hadi anashangaa kwanini alidanganywa!

Na kama wewe ni mama, je unajua atakayefichua hiyo siri yako? Ni yuleyule msiri wako aliyejua hilo jambo zamani: anaweza kuwa dada yako au rafiki wa karibu. Akifika kwa baba atapewa hadithi mpya kabisa na ataiamini, japo hatoacha kumpenda mama yake.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] asimwambie hivyo bwana Bora aseme babaako alikufaga
Mkuu embu waonee huruma hawa mama zetu wanavyo hangaika na watoto kwenye malezi,wanapitia magumu sana.
Maana ya neno UKOO ni uwajibikaji wa pamoja sio jina tu.
Ukisema baba yako alikufaga hii mitoto ya fesibuku inaanzaga kutafuta ndugu mitandaoni kwa kutumia jina la ukoo.
 
Shida ya single mama wakiachana na waume zao hua wanataka ugomvi urithishwe hadi kwa watoto na hua wanataka mtoto asimjue baba kabisa, stupid.

Ukiwa responsible hata mtoto mwenyewe anaweza kupembua
 
Hapo bora iwe kweli hivyo. Vinginevyo kuna siku wambea watamwonyesha baba yake. Na akienda kwake anapokelewa vizuri kwa bashasha hadi anashangaa kwanini alidanganywa!
Na kama wewe ni mama, je unajua atakayefichua hiyo siri yako? Ni yuleyule msiri wako aliyejua hilo jambo zamani: anaweza kuwa dada yako au rafiki wa karibu. Akifika kwa baba atapewa hadithi mpya kabisa na ataiamini, japo hatoacha kumpenda mama yake.
Mkuu,ni sahihi kwa baba kumtelekeza mtoto kisa haelewani na mama yake hadi mtoto aje akue ajishughulishe kumtafuta ndipo ampokee kwa bashasha?

Kama mama wa mtoto ni jeuri,hana ndugu wa kupitishia misaada kwa ajili ya mtoto? Kukwepa majukumu ya malezi kwa mtoto wa kumzaa ni ujinga wa hali ya juu ambao hauna msamaha.
 
Back
Top Bottom