Mitoto unaihangaikia peke yako ikifika ukubwani inaenda kutafuta ukoo wao...

Safi [emoji122]
 
Aisee [emoji848]
 
Duh Kama Ni hivyo pole Sana jaribuni kuweka kikao na watu wazima na yeye mnaweza kupata muafaka namna ya kumtunza mtoto
 

Ivi wewe Mtoto azaliwe uletewe umkatae alelewe mwaka mmoja mpk 27 bila msaada wowote na pengine upo kwenye nafasi nzur ya kutoa msaada af hutoi...dah af mi ndo Anko ake na uyo Mtoto aisee utaisoma namba
 
Kuna wakati mwingine kina Mama wanakosea wenyewe, wanamficha mtoto ukweli kuhusu baba yake na ukoo wake kisa eti babake alimtelekeza. Zamani wanawake waliweza kutudanganya kuhusu watoto wetu ila siku hizi kuna msema ukweli aitwaye DNA ambaye anapingwa na kila mwanamke. Utakuta mwanamke hata kama kaolewa anajirusha na mtu bila kinga mwisho wa siku akipata ujauzito anatafuta mwanamme aliyetulia atajirahisisha kwake kisha aje kumsakizia mtoto ambaye si wake. Mwanamme mwerevu anaomba matokeo ya DNA, Mama anapinga na kumkataza mwanawe kujihusisha na baba yake na ukoo wake.
 
Huyo mama anakosea. Hata yy binafsi atakuwa na ukoo wake
 
Ivi wewe Mtoto azaliwe uletewe umkatae alelewe mwaka mmoja mpk 27 bila msaada wowote na pengine upo kwenye nafasi nzur ya kutoa msaada af hutoi...dah af mi ndo Anko ake na uyo Mtoto aisee utaisoma namba
Sema mpwa wako ndiyo ataisoma namba kwa sababu ndiye anayetafuta baba yake. Na usishangae ukajikuta unaisoma namba wakati mtoto anakutana na baba yake na wanaelewana.

Sisi tulilea mtoto wa aina hiyo. Dada yetu alianza kazi akiwa binti mdogo, enzi hizo post yake aliyoanzia iliitwa "afisa ujamaa na ushirika" ndio kwanza alikuwa amemaliza form four akaajiriwa baada ya kozi ya mwaka mmoja. Mwaka wa pili akaja nyumbani na mimba. Akajifungua mtoto wa kike, baba hajulikani, akiulizwa anajibu hovyo. Mtoto alipofikisha miaka miwili, mamake akapata nafasi ya kujiendeleza akaenda kusoma diploma akatuachia mwanae wazazi wetu wakaendelea kulea. Kule alikoenda akapata mchumba, akaolewa akaanza familia na anayo mpaka leo. Huku nyumbani binti akakua na ikafika muda tukapokea barua ya uchumba. Tukiwa tunaandaa sendoff tukashangaa binti anasema amempata baba yake na anataka aje kwenye sendoff. Dada yetu akawa mkali kama mbogo, hataki kumuona huyo "mhuni". Binti akaweka msimamo anataka baba yake awepo. Tulikuja kugundua mambo mawili yaliyotushangaza: kwanza, kumbe binti alimfahamu baba yake kitambo na walikuwa wakiwasiliana. Pili, na hii ilitushangaza zaidi, kumbe huyo baba yake ni mtu ambaye hata sisi tulikuwa tukimfahamu, mtu mzima mwenye mji wake na watoto wakubwa kama huyo dada yetu aliyezaa naye! Katika mazingira hayo wajomba tulipaswa kumlaumu nani, na kwa faida gani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…