Miujiza ya mafanikio ya Kiuchumi ya China yaliyowezeshwa na chama cha CPC

Hahahahah ukimaliza kula msambwanda mda wa marejesho unakula shaba😅 kama huna hela
Yaani fastafasta ushakula shaba. 😂

Yaani yule mzee Deng alikuwa kama kichaa. Maana alisema hela zikikaa benki hazina kazi. Inabidi watu wakopeshwe. Sasa watu wa benki wakasema watu hawakopesheki maana ni watu hawana hati. Deng akasema si wana roho? Asipolipa tutamuua tu! Watu wa benki waliogoma kukopesha watu na wenyewe walijipatia shaba fasta. Na walioshindwa marejesho wanapata shaba, ukitumia mkopo kwa starehe unajipatia shaba. Yaani yule mzee mambo ya upuuzi alikuwa habembelezi ni shaba tu. Ila ndio ametajirisha china mpaka leo. Yaani yeye ni shaba tu hakuna kubembelezana.
 
Hahahahha hivi huyu mzee bado yupo China tumuombe aje kwa Sub contract hapa nchini? Maana alikuwa umeme huyo ukigusa vibaya unakula shoti!
 
Hahahahha hivi huyu mzew bado yupo China tumuombe aje kwa Sub contract hapa nchini?
Kashakufa ila nyaraka zake zinatumika na marais wote wa china. Hata huyu wa sasa hivi Xi anajifanya kama anapinga mawazo ya Deng ila kiufupi anayatekeleza yote. Shida ni nyaraka za Deng zimefichwa ila ndio ukweli wa jinsi china ilivyotajirika. Hawa wachina unaowaona na makampuni yote haya ni ya serikali na nyingine ni za majimbo. Kama mfanyakazi akifanya madudu bongo akienda kwao ni shaba tu. Ujifanya mjanja wanakuteka ili upate adabu, hata Jack Ma juzi kati hapa alitekwa ili apate adabu. Yaani wachina bado wanafata mfumo wa Deng.
 
Hivi kuna evidence yoyote inayoonesha kwamba ni kweli mwaka huo tajwa china na TZ tulikua tunalingana kiuchumi? Kama hakuna evidence basi hiyo ni propaganda
Tuna silaha zimo majeshini tulipewa misaada na china miaka hiyo,wakatujengea na reli.anakuja mtu anasema tulikuwa sawa[emoji16][emoji16].
 
Wakija akina magufuli hapa tz,zinaibuka nguruwe na kudai hela zimekauka mtaani.
 
Adhabu ya ufisadi china ni kunyongwa mpaka kifo...swali la msingi ccm wapo tayari kuweka kipengele hicho kwenye katiba yetu ukizingatia wao ni chama cha mafisadi.
 
Sisi kuwekewa tozo tu, kelele kibao yani tunataka maendeleo yatoke mbinguni au ulaya watujengee, ajabu sana.
Islael wanamsemo wao kuwa wamejenga nchi yao kwa jasho na damu, ukichunguza ni kweli hawana maziwa kama sisi hawana mito kama sisi, hawana mvua kama sisi,hawana madini kama sisi,idadi ya watu sio kubwa kama sisi, hawana ardhi yenye rutuba kama sisi lakini wametuzidi kila kitu cha maendeleo ya kisasa,hovyo kabisa.
Tunafeli sana sana.
 
Ishu ni viwango vya tozo bosi
 
Ishu ni viwango vya tozo bosi
Leo nimetuma sh. 500000 nimekatwa sh. 12800 hii ina maana kila 100000 sh. 2500. Hii ni sawa ba 0.025% ta 100000. Sidhani kama ni kubwa ila tunapenda kulalamika.
Watanzania tufanye kazi tukuze kipato tujenge nchi.
Unakumbuka ishu ya bandari ya bagamoyo ?
Watu walilalamika kuwa ule mkataba ni mbaya, sasa watu wanakuja na njia nzuri za kujenga nchi bado zinakataliwa.
Kukopa kwa wachina "unauza nchi" kujichanga napo "hali yetu mbaya".
Mkuu tusipotumua maarifa hatuendelei ng'o , tutabaki kupiga domo.
Wenzeti wanatoa mpaka uhai wao ili nchi zao ziendelee sisi hatutaki kuumia tunataka mteremko.
 
CPC ndio kila kitu kwa China bila CPC hakuna China bora.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…