Miundombinu ya Arusha na Moshi inaleta aibu katika soko zima la utalii na uwekezaji

Miundombinu ya Arusha na Moshi inaleta aibu katika soko zima la utalii na uwekezaji

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963
Katika kipindi hichi cha mwezi wa sita hadi mwishoni mwa mwaka tumeshuhudia kabisa idadi ya watalii ilivo kubwa na inazidi ikiongezeka kadri siku zinavyozidi kwenda katika miji hii miwili ya kitalii.

Ni aibu kwa mji wa kitalii kama Arusha na Moshi kuwa na aina ya masoko na vituo vya mabasi makubwa ya kwenda mikoani kama vilivyopo.

Masoko pamoja na vituo vya Mabasi makubwa ni vile vile vya tangu tupate uhuru, hamna ujenzi wowote uliofanyika kuendana na Ongezeka la idadi ya watu pamoja na ukuaji wa miji na teknolojia.

Rushwa na siasa imekuwa ikitawala haswa katika miji hii kuhusiana na wapi pajengwe kituo cha mabasi makubwa,swala hilo ndio haswa limekuwa likichelewesha ujenzi wa miundombinu muhimu ya masoko ya kisasa pamoja na stand ya mabasi makubwa ya mikoani.

Kukosekana au kucheleweshwa kwa ujenzi wa miundombinu muhimu kama hiyo inasababisha pia ucheleweshaji kwenye uwekezaji katika mambo mbalimbali ikiwemo viwanda, Sekta za utalii nk.

Ni wakati sasa wa viongozi wa miji hii miwili mikubwa kuweka siasa pembeni na kufanya uboreshaji wa miundombinu
 
Unaongela Moshi ipi? Ukiachilia mbali stand ya Magufuli kuna mji wenye stand nzuri kuliko ya Moshi?
NB: unajua kuwa watalii hutumia magari ya kampuni za utalii na siyo usafiri wa umma?
Sio wote wanaotumia zile cruiser za kitalii, wengine hupanda Costa na mabasi kwa trips za Arusha to moshi, lushoto, na wengine huoendelea pia kutembelea masoko ya ndani pamoja na kununua vitu humo
 
Unaongela Moshi ipi? Ukiachilia mbali stand ya Magufuli kuna mji wenye stand nzuri kuliko ya Moshi?
NB: unajua kuwa watalii hutumia magari ya kampuni za utalii na siyo usafiri wa umma?
You must be kidding aisee.
Stand ya Bus ya Mosho haifiki hata theluthi ya uzuri wa stand ya Mpanda.

Ya Moshi linganisha na ya Geita na ya Geita imejengwa miaka karibu 13 iliyopita
 
You must be kidding aisee.
Stand ya Bus ya Mosho haifiki hata theluthi ya uzuri wa stand ya Mpanda.

Ya Moshi linganisha na ya Geita na ya Geita imejengwa miaka karibu 13 iliyopita
Sawa
 
Sio wote wanaotumia zile cruiser za kitalii, wengine hupanda Costa na mabasi kwa trips za Arusha to moshi, lushoto, na wengine huoendelea pia kutembelea masoko ya ndani pamoja na kununua vitu humo
Hakuna mtalii anayesafiri kwa costa wala. Hata kulala lodge za kawaida tu hairuhusiwi. Pia siyo kila mzungu ni mtalii, wengine wako kazini
 
Very sad, vile vile Serikali imefanya haraka sana kuipa "jiji" kwakweli hata hao wazungu wanaokuja huko kutalii wanakuja tu kwa lengo la kuona wanyama na wengine kutimtimkia serengeti, lakini kwa upande wa mji kama arusha mhhhh!,boresheni mji jamani, jengeni majengo mazuri yenye kuvutia, mahotel mazuri katikati ya mji na nje ya mji jengeni jamani, angalau mufikie hata nusu ya Mwanza.

Kitombile
 
FB_IMG_1658353936696.jpg
Usilie huu ndo uchafu wa Moshi!
FB_IMG_1658354327354.jpg
Ni sawa na huu uchafu wa Geita

futa kauli yako ya stand kali maana hata tukizitaja 15 bora ya moshi haipo
 
Ni mji gani una miundo mbinu mizuri isiyokuwa ya aibu?
Dar kule city centre hakunagana sewage system. Barabara zipo flat juu ya ardhi. Sasa ukitoka pembezoni inakuwaje?
 
Very sad, vile vile Serikali imefanya haraka sana kuipa "jiji" kwakweli hata hao wazungu wanaokuja huko kutalii wanakuja tu kwa lengo la kuona wanyama na wengine kutimtimkia serengeti, lakini kwa upande wa mji kama arusha mhhhh!,boresheni mji jamani, jengeni majengo mazuri yenye kuvutia, mahotel mazuri katikati ya mji na nje ya mji jengeni jamani, angalau mufikie hata nusu ya Mwanza.

Kitombile
Arusha hakuna mahotel? Itakuwa ajabu kama unaiona Arusha hapa Tanzania kama mji usiokuwa na mahotel. Utakuwa hujawahi kufika Arusha.
 
Very sad, vile vile Serikali imefanya haraka sana kuipa "jiji" kwakweli hata hao wazungu wanaokuja huko kutalii wanakuja tu kwa lengo la kuona wanyama na wengine kutimtimkia serengeti, lakini kwa upande wa mji kama arusha mhhhh!,boresheni mji jamani, jengeni majengo mazuri yenye kuvutia, mahotel mazuri katikati ya mji na nje ya mji jengeni jamani, angalau mufikie hata nusu ya Mwanza.

Kitombile
Hakika mkuu watu waarusha wanaendekeza porojo, ujinga pamoja na kulewa sifa za ajabu kila siku kujifananisha na geniva, et mara oh geniva ya africa mara the republic of arusha, kama hujawahi fika utazani arusha ni bonge la mji.
Tukiwaambia arusha bado wanatoa povu.
Arusha ni babati iliyochangamka😂😂😂
 
Na vipi kuhusu mitaa ya Arusha ilivyo giza usiku ? Utafkiri uko msitu wa Congo.. Aibuuuuuuuu ! Geneva of Africa au Amazon forest of Africa ?
 
Kwenye mahoteli, majengo mazuri, miundo mbinu ya barabara na Mandhari Arusha wako vizuri zaidi kuliko Mwanza, lakini kwenye stand ya mabasi Arusha ni sifuri.
 
Kwenye mahoteli, majengo mazuri, miundo mbinu ya barabara na Mandhari Arusha wako vizuri zaidi kuliko Mwanza, lakini kwenye stand ya mabasi Arusha ni sifuri.
Tupia hayo majengo mazuri ya arusha na hizo barabara nzuri kuliko za mwanza nasi tuone na tufanye comparison.
 
Hivi jamani hiyo Mwanza inavyosifiwa ni kweli maana nimefika mwanza Airport duu nikaenda stendi ndio usiseme, ccm kirumba nikajua pengine nimepotea njia ila all in all watu huwa wanasifia vitu kulingana na mapenzi tuu. Kipindi cha magufuli aliparekebjsha sana. Wekeni hata sanamu ya kumbukumbu
 
Back
Top Bottom