Mjadala: Je, ni kweli Magari aina ya Nissan Xtrail ni mabovu?

Watanzania ni wajuwaji tu lakini hamna kitu..
Tatizo watanzania si watunzani na ni wavivu wa kufikiri
Haya maxtrail mnayosema ni mabovu mbona wapo watu wamekaa nayo karibu miaka kumi sasa...
Kuna mtu hapa ana namba BAK na linapiga kazi freshi tu..
 
Watanzania ni wajuwaji tu lakini hamna kitu..
Tatizo watanzania si watunzani na ni wavivu wa kufikiri
Haya maxtrail mnayosema ni mabovu mbona wapo watu wamekaa nayo karibu miaka kumi sasa...
Kuna mtu hapa ana namba BAK na linapiga kazi freshi tu..
Mtanzania mpaka akikubali jitu Basi ujue dunia nzima kitakubalika
 
mkuu ushawah pata shida ya nissan xtrail kuchemsha?
Mimi ninayo Extrail, mwaka wa nne huu ipo poa kabisa ila baada ya kuijulia. Bahati mbaya sikuinunua mpya bali niliuziwa na wachina fulani wajanja! Nilipoichukua kwa miezi miwili au mitatu ilikuwa poa, baadae ikaanza kuchemsha nikawa sielewi why maana kila kila kitu kipo poa. Baada ya kuhangaika muda kidogo, Fundi wangu akagundua kwamba wachina walichange rejeta, wakatoa yake wakaweka ya gari dogo hivi kama baloon! Basi nikaenda Ilala nikapata rejeta nikaifix, tangu wakati huo (mwaka wa nne huu) haijawahi kuchemsha hata kidogo.

Kitu muhimu ni kuwa na discipline ya service inayoendana na kutumia recommended oil. Ukiweka oil hizi za vibaba umeliwa. Pia ina sensors nyingi, niliwahi kusumbuliwa na Gearbox Sensor, gari ilawa inasumbua kuchange gear, ila baada ya kuweka mpya, sijawahi, kupata usumbufu wowote.

Nissan Extrail, ni gari gumu na very stable barabarani hata kwenye njia zetu za uswahilini. Kwa walio na bajeti ambayo si kubwa sana ila wanataka gari imara, go for Nissan Extail!
 
Nimekusoma kiongozi
 
Watanzania ni wajuwaji tu lakini hamna kitu..
Tatizo watanzania si watunzani na ni wavivu wa kufikiri
Haya maxtrail mnayosema ni mabovu mbona wapo watu wamekaa nayo karibu miaka kumi sasa...
Kuna mtu hapa ana namba BAK na linapiga kazi freshi tu..
Yes, nimekutana nazo namba B kibao zikiwa katika hali nzuri
 
Naona umeongea kitheory zaidi. Ni vema unapotoa ushuhuda then uwe specific na open detailed.

Sasa unaposema oil za vibaba ndio kitu gani?!

Unaposema oil nzuri ndio zipi hizo?!
 
Kwa msio jua hicho kifaa kinaitwa thermostat ambacho mafundi wengi husema kitolewe basi nawawekea hapa mkione chenyewe na kikiwa ndani ya jumba lake.....
 
Safi kabisa kijana. Najivunia kama mwalimu wako nilichokufundisha umekisema sawia kabisa kumaanisha ulinielewa darasani. Safi kabisa....... Umesema sahihi kabisa....
 
Hizi gar ni majanga ipo moja ya jamaa yangu kaipaki ana lalamika spea tabu,
Huyo jamaa yako ametafuta spare gani ikakosa? Mimi nimekaa na Nissan Extrail mwaka huu wa tano, tena niliinunua kwa mtu, ila haijawahi kusumbua. Spaire zake zipo nyingi sana, ukitaka za mtumba au za dukani zote zipo.

Gari hilo linahitaji umakini kidogo tu, mfano specified engine oil na gear box, ukiweka oil mradi tu ni oil, utalia! Service yake inatakiwa iwe ndani ya muda uliopangwa.

Pili gari hii inatumia sensors nyingi na karibu zote zipo hata pae Ilala maduka ya vifaa vya magari. Tatizo mafundi gereji wetu wengi wanashindwa kudetect tatizo la gari hivyo unaweza kukuta unashauriwa kununua spare isiyohusika kwa tatizo lako.

Unless useme huyo jamaa yako amekosa spare gani, otherwise tutashindwa kumsaidia. Kwa maoni yangu Nissan Extrail ni gari zuri sana.
 
There is a special oil for nissan xtrail....sikumbuki jina lake but mafundi wa nissan xtrail wanazijua....
Giabox oil inaitwa Matic, imendikwa kwenye oil stick. Ila Matic zipo za ina tofauti inabidi pia uwe specific.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…