Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Half an hour ago jamaa tuliyepoteana zaidi ya 10 yrs na kuonana wiki tatu zilizopita kanipigia simu eti kuna jamaa yake anataka kuoa hivyo tushirikiane ili kuongeza network.... Nimemshangaa sana kwani hata hiyo network na yeye haipo sasa sijui ndo anataka kuiactivate kwa style ya mchango kwa jamaa yake yaani wabongo tunashangaza sana. Hapo Kenya watu wana harambee za kusomesha watoto sisi tunachangishana kwa ajili ya bia na ubwabwa wa siku moja halafu ndoa zenyewe life expectancy zake zinadecline kila siku
 
NAPENDEKEZA UANZE UTARATIBU WA BYO (bring your own) / COME WITH A PLATE hapo no kulaumiana, utakula/kunywa ulichobeba
 
Wewe umeoa? Ulipooa ulichangiwa? Kama ulichangiwa nawe inabidi uchangie wenzako (vicious circle). Lakini kama hujaoa na huna mpango wa kuchangisha mtu utakapokuwa unaoa zipotezee tu hizo kadi.
 

Ulizani ukubwa kupewa ''shikamoo'' peke yake?
Majukumu mzazi.
Luku vere.
 
Waafrika tuna copy vingi toka Ulaya lakini hili la michango hatujawaiga Wazungu ?wenzetu wa Ulaya hawachangishi watu wala hawasumbui watu na kadi za michango isipokuwa wao hufunga ndoa kwa bajeti zao Binafsi au za wana familia kisha kuwaalika watu kuja kusherekea tu pasipo kuwachangisha tujifunze kwa hili ! Kwani kuoana si lazima Harusi mnaweza mkaishi kwa upendo hadi mkiwa na uwezo mtabariki ndoa yenu
 
simple, kuwa na fixed amount ambayo upo radhi kutoa,
e.g 4000,5000 ,20000 etc.
ukipewa kadi ya mchango pale pale unampa mtu elfu 5, za mchango wako. baada ya muda watu watakujua kuwa unatoa chini ya matarajio yao,wataacha kukusumbua na kadi za mchango.
mimi huwa namwambia mtoa kadi, sitochanga nikiweza ntakupa zawadi,na nitakuja Kanisani,au nyumbani ,so inapunguza usumbufu.
 
Dah! Hi wabongo ni aibu yenu, kwnn mnapenda makubwa wakati mwengine hamna hata uwezo? Huwa naona ni mambo ya ajabu sana munapenda kuiga tamaduni za watu weupe.

Munarejeshana nyuma, kwann wabongo wengi huwa wanafanya mambo kwa sifa? Haya mambo ya kadi za harusi hayana msingi au huwa mtu hana jamaa?

Hizi tabia zinawakera wengine acheni. Kama ni harusi fanyeni kwa uwezo ulionao na uache kutembeza bakuli kwa ajili ya kuwafurahisha wengine.
 

nakubaliana na wewe mkuu 100%
 
Habari za asubuhi wakuu? Hii wiki tu nimepokea sms na kupigiwa simu zaidi ya 5 watu wanakudai mchango uchangie harusi yake. Namaanisha kudai mchango nawala sio kuomba uchangie. Mtu anakupigia simu alafu anakwambia taja "pledge' yako kwenye harusi yangu. Unamjibu kistaarabu tu ondoa shaka muda ukifika nitakuchangia tu. Yeye anakulazimisha usiwe na wasi ahidi kiasi chochote kile haina tatizo. Baada ya kukubana sana unamweleza kiasi fulani, huyo anayedai anakujibu samahani kaka/dada kiwango changu cha chini cha kunichangia ni laki moja.

Samahani lakini sijui kwa vile mimi ni mgeni na haya maswala au ndio kawaida kwa wote.
Maana ndani ya mwezi mmoja natakiwa niwachangie watu zaidi ya 5.
Swali hiyo hela anayodai mtu aliiweka mfukoni mwako? Maana kwa mimi ninavyojua mtu unapoguswa na swala hili na ukaribu na mhusika ndivyo utakavyotoa kiasi kikubwa.
Chakushangaza kingine unapigiwa simu na marafiki nao utoe pledge kwa mtu ambaye humfahamu.

Mimi binafsi sitamkwaza mtu wakati wa kuomba kuchangiwa.

NIMEMALIZA, NAWAKILISHA.
 
Hilo ni tatizo sana mijini,vijijini huku hakuna mambo hayo, hatahivyo kama ulivyosema inategemeana na ukaribu wenu na muoaji!
 
Harusi za kuwekeana vima vya chini sichangi na wala usisumbuke kuniita.

Zaidi ya harusi ya kaka angu na za wadogo zangu, hizo nyingine ni anasa.

Ukitaka kuoa hakikisha unaweza kufinance harusi yako kwa 80% nyingine watachanga wenzako, sio huna mbele wala nyuma unakimbilia kufanya harusi kubwa kwa mifuko ya wenzako.
 
Hilo ni tatizo sana mijini,vijijini huku hakuna mambo hayo, hatahivyo kama ulivyosema inategemeana na ukaribu wenu na muoaji!


Ifike wakati ndugu zangu tubadilike, mambo ya arusi yabaki kuwa ya kifamilia zaidi ili sasa tuelekeze michango kwenye elimu na afya maana ukifika kwenye mashule ya serikali hali inatisha ukienda hospital watanzania wenzetu wamepoteza matumaini, nadhani kuna haja ya kuwepo mabadiliko makubwa kifikra
 

Tena wapo watu katika familia utakuta kuna mtu kakosa ada ya shule au chuo hawachangishani kumsaidia ila linapokuja suala la anasa wanalazimishana,haya mambo yanatupotezea muda kutaka ufahari kwa kupitia mifuko ya wenzio
 
Wa2 mnatakiwa kujua kutoa ni moyo utanlazimlazimishaje mtu akuchangie waungwana kwani haruc siyako cmpendana nyie wawili kama mnataka kuoana muweke bajeti yakutosha mclazimishe wa2 kuwachangia.....
 
Hii mara kadhaa, nimeiona..tena 'maofisini' ndio kwenyewe.

Yaani, ndugu yeyote wa mfanyakazi mwenzio akitaka kuoa/kuolewa michango(hata kama humjui, au hamna ukaribu). Halafu michango ya sherehe hizo zimekuwa nyingi utasikia sijui kitchen party, send off, harusi yenyewe!
 
michango ya harusi ishakuwa deal siku hizi na hao wana kamati
 
mimi sichangi nina mikadi kibao kwenye droo wakiiga simu sina hela na harusi yangu na mama kayai tulijifungia wenyewe kwa raha zetu...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…