Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Utakuta karibu ya 50% ya kipato chako kinaenda kwenye michango isiokuwa na tija.


Kwakweli, mimi nimepunguza kabisa, nikiwa njia moja kuachana kabisa na michango ya sherehe ZA harusi
 
utakuwa mdogo wangu, si bure.
Nina zaidi ya miaka 5 nimeachana na huo upuuzi, kwenye elimu, magonjwa na misiba ndipo ninapotoa my hard erned money.

Dada Kaunga safi sanaaa
 
Ni kweli mtoa mada hili swala mm limenikuta.nina cousin wangu Mkoa amepata tatizo la figo na akapata rufaa kuja MNH.Kwa kuona gharama za matatibu ya figo ni kubwa na dogo wazazi wako kijijini hali ngumu,ikabidi nibebe mzigo ,nikajarabu kutuma SMS kwa ndugu kama 30 tujaribu kuokoa maisha ya dogo ,kati ya hao 1 alitoa30,20,15,na 10 .ni watu 5 walijitoa.wakati huo kuna harusi ya ndugu mwishoni mwa novemba kuna watu wamehaidi mpaka laki wakishindwa kumsaidia dogo hata buku.Hapa ndiyo nimehapa kuto changia harusi nitasaidia tu watu wenye huitaji.
 


Yaani inashangaza sana KWA kweli, Sherehe ZA harusi ni mbwembwe tu, watu wanashindwa kuokoa uhai??? So sad
 
Hii michango imekuwa kero sasa hivi watu wamechanganyikiwa au nini maana kipindi cha nyuma hakukuwa Na mambo haya.
 
Hii michango imekuwa kero sasa hivi watu wamechanganyikiwa au nini maana kipindi cha nyuma hakukuwa Na mambo haya.

Nadhani tumeendekeza, mtu anakufuatilia utadhani hela ni ya kwake, shame! Mbaya zaidi WALA hana NA Huruma NA mazingira, ni kuachana Kabisa, watu wafanye mbwembwe zao KWA fedha zao wenyewe
 
Kuna watu wa ajabu sana,unapanga kuoa huku huna hela unataka watu wengine wakuchangie,huu ni ujinga mkubwa.

Raha zako ziwape wengine shida.

Unakuta mtu anataka kuoa,bajeti milioni 10, yeye ana milioni 1 na nusu,hizo zinginge anataka watu wamchangie, ukipanga kuchangiwa harusi jiandae pia kuchangia mke.

Acheni kusumbua watu na harusi zenu.
 

ukweli mchungu
 
i think na huu uzi umekaa kiusumbufu zaidi..

biblia imesema kila jambo na wakati wake...

kuna wakati wa kulia....lia!

kuna wakati wa kucheka...cheka!

kuna wakati wa kulalamika..lalamika

kama sasa imekuja time ya michango kwa ajili harusi ambayo ni sehemu ya furaha...changa japo kiduchu! au kama hauna basi jitolee hata kwenye kamati ya ulinzi! lol..
 
Ha! Ha! Kweli, japo kuna wadada bila harusi ya siku moja inayosaga mamilioni kwa siku moja, humtoi kwao. Wala humtishi kwa penzi la dhati, hilo peleka kijijini kwa bibi yako!
Ha! Ha! Kufukarishana.
^^
 

Mfano wako hauhusiani na mada. Biblia haijasema usumbue watu kila siku vikao,michango ili kufanikisha harusi yako. Kupotezea watu muda kila siku vikao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…