Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Mi sina mpango wa kuchangisha mtu ili baada ya hapo nsiletewe card za michango ya harusi ila cha kushangazaa nikimwambia iviiii uyuu mdada ananiambia nkamuoe paka ivyooo hahahahaha ye bila ukumbiniii hatak wakat harusi ni sherehe inayoandaliwa na mwanaume ye unamualika tuu ila nnavyojibiwaaa ni tatizo pia
 
hivi sasa nina txt 8 zinanilumbusha michango ya harusi....tena michango mingine unaletewa tu txt whatsapp.....aiseee msitake sifa za kijinga eti sherehe ilitumia 25m ilihali watu wanakula dagaa....watu wagonjwa....watu wanaeaza skul fizi....cha maana huwa nawapotezea tu
 
Kwani lazima uchangie?we kama hutaki kuchangia usichange nakushangaa unaleta mada ya kijinga kama hii
Hii sio mada ya kijinga, ni mada ya kuwaondoa watu katika utumwa wa uvivu wa kufikiria. Plan your wedding, secure your own funds, and get financial assistance from your close friends and relatives. Harusi sasa hivi unamvamia mtu hata ambaye hana uhusiano wowote na muolewaji/muoaji, eti mtoto wa kaka yangu, mara mdogo wangu unatembeza kadi mtaa mzima au ofisi nzima, ni UJINGA. Fanya simple wedding, kulingana na uwezo wako, usinganganie makubwa usiyoyaweza, mie nshagombana na ndugu zangu kutaka kufanya harusi za kufuatilia michango kama DENI mpaka BWN harusi anaambiwa usilale, tafuta kiatu maalumu ya kufuatilia michango. Sasa huu si ujinga bwana!!!
 
Mwambie tu kwamba hufagilii michango ya harusi.

Tatizo michango hampendi halafu kulalamika.mnakija kulalamikia JF.

Jamii yetu inagubikwa na kutokuwa na uwazi.

Ukifanya harusi bila kuchangisha watu utaambiwa unajisikia, ukichangisha watu unaulizwa kwa nini uchangishe watu kwenye harusi yako.

Ingawa inaweza kuwa socially awkward kukataa kuchangia harusi, kama michango inakukera kweli, unatakiwa kusema hilo na kukiweka wazi kwa wahusika.

Wakijua hilo kesho hata kadi ya mchangi hawatakupa.

Kitu ambacho kitamaanisha hata kadi ya harusi unaweza usipate.

But I guess you are not too big on weddings.

You are right br.Mii niliwahi kuletewa kadi zamichagoya ya sherehe za kipaimara na ubatizo; nikawa nawaabia aziwazkuwa michago ninayochangiani ya harusi tu, kipaimara na ubatizo sichangii. Jamaa zangu wakaacha kuniletea kadi za Vipaimara na Ubatizo, kwenye harusi tunashirikiana kama kawaida na bado tunaheshimiana.
 
wabongo bwan!!!ulimbukeni wakuta makuu ndo maana wanasumbua watu...andaa kitu kidogo kizuri cha uwezo wako alika watu wafurahi na ww sio kwa michango tena eti yakuwapangia kiwango cha pesa cha kutoa....
 
Kuna watu wa ajabu sana,unapanga kuoa huku huna hela unataka watu wengine wakuchangie,huu ni ujinga mkubwa.

Raha zako ziwape wengine shida.

Unakuta mtu anataka kuoa,bajeti milioni 10, yeye ana milioni 1 na nusu,hizo zinginge anataka watu wamchangie, ukipanga kuchangiwa harusi jiandae pia kuchangia mke.

Acheni kusumbua watu na harusi zenu.

Katika masuala kama haya ni vema kutumia busara zaidi. Ukienda kama unavyosema tutafika mbali kwenye tafsiri. Harusi yake na raha zake, kwa hiyo abebe mzigo mwenyewe. Kwani kuna vingapi vinavyokuhusu ambavyo umechangia na wenzako?

Siku ukiuguliwa utahitaji msaada? Mgonjwa si ni wako mwenyewe?
Siku ukifikwa na msiba (kufiwa) utahitaji msaada? Marehemu si alikuwa ndugu yako peke yako?
Siku ukivamiwa na majambazi, utahitaji msaada? Nyumba hiyo na mali si vyako mwenyewe?
Siku ukioa/olewa ama kuozesha utahitaji msaada?

Na kwenye msaada tusiwaze pesa tu, maana najua ndio msingi wa uzi huu. Kama tukianzisha ubinafsi kwenye pesa, haitaishia hapo, inabidi tuwe wabinafsi hasa, yaani tusishirikiane katika mambo yote maana lako halinihusu na langu halikuhusu wala halimhusu yule mwingine.

Hali hiyo na maisha hayo nakuachia mtoa uzi ishi peke yako na wengi(ne) wanaokuunga mkono. Kama unajitosheleza kwa kila jambo hakuna shaka kabisa, uamuzi huo ni halali yako kabisa. Mimi jitajitahidi kuchanga pale nitakapoweza, nikishindwa nitajua nimeshindwa na mhusika nitamtafadhalisha atambue hali si shwari. Na mimi yakinifika, nitaomba msaada, na ushirikiano si katika raha tu, hata majanga pia.

After all, sina hakika kama ni sahihi kusema 'anataka', nina imani anaomba wamchangie na washirikiane naye. Kama huwezi au hutaki tu huwa hakuna kesi baada ya hapo.

Unayo haki ya kukataa.
 
Mi sina mpango wa kuchangisha mtu ili baada ya hapo nsiletewe card za michango ya harusi ila cha kushangazaa nikimwambia iviiii uyuu mdada ananiambia nkamuoe paka ivyooo hahahahaha ye bila ukumbiniii hatak wakat harusi ni sherehe inayoandaliwa na mwanaume ye unamualika tuu ila nnavyojibiwaaa ni tatizo pia

Bibi harusi mtarajiwa anamwalika mumewe mtarajiwa. Bwana harusi anawezaje kumwalika mke wake wakati wameshakuwa mwili mmoja bhana?

Anyway, kama hutaki harusi kubwa na kuchangisha watu na yeye anataka, mi nakushauri umwache tu maana naye ni gharama tu kama gharama za harusi, au unasemaje?
 
Mi sina mpango wa kuchangisha mtu ili baada ya hapo nsiletewe card za michango ya harusi ila cha kushangazaa nikimwambia iviiii uyuu mdada ananiambia nkamuoe paka ivyooo hahahahaha ye bila ukumbiniii hatak wakat harusi ni sherehe inayoandaliwa na mwanaume ye unamualika tuu ila nnavyojibiwaaa ni tatizo pia

Huyo wewe ndio unamdekeza. Shemeji yangu mke wa bro alikua na nyodo kama hizo,eti hawezi kuolewa bila harusi,tena avishwe pete maana dhehebu lake mchungaji aliwaambia kuolewa bila harusi unakua umeolewa kama kuku.

Basi bro akatupia mimba kabla ya hiyo harusi,kisha akakaa kimia,mbona binti kila siku akawa anauliza utanioa lini,bro anajibu bado sijapata pesa za kufanyia harusi binti anasema wewe nioe hivyo hivyo,mwisho wa siku binti akajileta mwenyewe hom kama kuku.
 
Huyo wewe ndio unamdekeza. Shemeji yangu mke wa bro alikua na nyodo kama hizo,eti hawezi kuolewa bila harusi,tena avishwe pete maana dhehebu lake mchungaji aliwaambia kuolewa bila harusi unakua umeolewa kama kuku.

Basi bro akatupia mimba kabla ya hiyo harusi,kisha akakaa kimia,mbona binti kila siku akawa anauliza utanioa lini,bro anajibu bado sijapata pesa za kufanyia harusi binti anasema wewe nioe hivyo hivyo,mwisho wa siku binti akajileta mwenyewe hom kama kuku.

Ahahahha hapo Ali surrender mwenyeweee ndiooo dawaaa yaooo hiooo
 
...heri ya awa wanandoa..!
hrs.jpg

Hii nimeipenda. Mwana harusi anakaa na Bibi harusi. mia
 
Harusi humchangii mwenye harusi unatoa hela ya kutumia wewe mwenyewe.....utakula chakula,vinywaji,unaburudika na muziki kidogo na kurefresh wakati mtu akienda kusoma hela yako hairudi na hufaidiki na chochote kwa hela uliyotoa

Dah! Bado tuna safari ndefu sana
 
mtoa mada sizani kama umefikiria sawa. Unaposema hatuchangii elimu unamaana gani? Mfano mimi ni mtumishi wa serikali na kila mwezi nakatwa 68000 kama kodo hapo kwa mwaka ni sh ngp?. Kodi nachangia kila mwaka lakini harusi ni mara moja moja sema tu tunachangia hela za elimu ila wajanja wanakula bora hata hii michango ya harusi ambapo na sisi tunaziona zinavyotumika
 
kbm = Kibomu
Utajiuliza na kushangaa na hao unaowashangaa nao wanakushangaa kwanini huchangii harusi.
Nyumbani nina kadi 21 za harusi mpaka sasa, nimetafakari na sijapata jibu ni kwanini tunapenda makuu uwezo hatuna?? harusi burget 32 milioni Tzs umepanga 2 rooms sinza unalipa monthly 150,000Tzs?? Mangi hainiingii akilini

Hiyo inaonyesha kwamba jamii yetu tunatatizo la kufikiria sawasawa, na kujua ni lipi la muhimu kufanya, huwezi kuchangia harusi laki 5 halafu una mdogo wako hata ada hana akija kwako unamwambia huna fedha..
Juzi akaja jirani yangu mmoja anaomba mchango wa harusi, kusema ukweli hali kimaisha ni ngumu sana, nikamwambia nikijaaliwa nitakupatia 50,000Tzs, huwezi amini alikataa akasema kamati imepanga singo ni 80,000 Tzs, nilijikuta nimewakwa na hasira ndani yangu nashukuru Mungu sikumjibu vibaya,
Nadhani wote mnakutana na hali kama hii.
 
Kwa mkoa wa kilimanjaro na arusha usipochangia wanakutenga ,hata kama Uko ughaibuni lazima wakutumie email .wanakupa na a/c # au wanasema Tuma kwa money gram au western union

sidhanii kama kuna ukweli hapo........usipotoshe jamii.....
 
Nafikiri shida kubwa ipo kwenye nmna pesa inavyotumiw na kamati ktk kukamilisha zoezi Zima la sherehe. Lbd tungejitahidi kubadili hii mitazamo iliyopo kwenye hizi kamati za sherehe badala ya kutumia pesa yote kwenye sherehe kuwe na utaratibu wa kumuinua/kuwainua maharusi kama vile kuangalia mambo muhimu ambayo hawana. Kwa bahati mbaya sisi si wakweli iwapo maharusi wataamua kutumia pesa za michango kwa maendeleo yao basi utasikia mengi.

Tatizo lipo kwenye jamii haina nia thabiti ya kusaidiana
 
Back
Top Bottom