Mjadala - Kitabu cha unyama wa Paul Kagame: Behind the Presidential Curtain: Inside Out of real Paul Kagame

Mjadala - Kitabu cha unyama wa Paul Kagame: Behind the Presidential Curtain: Inside Out of real Paul Kagame

Nnyie ambao lugha haipandi ndio mnaotuharibia. Mnashindwa kusoma kingereza rahisi namna hii halafu mna simu janja kali mko JF.

Nyie ndio mnaopigia makofi kila kitu sababu hamjui tofauti ya maigizo na uhalisia. Eti Mods atafsiri mkafie mbele !!!!

OK inawezekana mko Kigali mnajua French zaidi ila kana ni Wabongo humu nendeni mkale maharage Mods hawezi kutafsiri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nashukuru sana wakuu kwa kusoma kitabu hiki,ukweli ni kwamba you do not know what you have untill you loose it,ninavyoangalia hali iliyopo sasa na iliyopita naweza kusema kikwete alikuwa na akili nyngi sana na aliona mbele,usalama wa nchi kwake ilikuwa priority kubwa ,kaondoka tu ghafla vijana wetu huko congo wanakufa kama kumbikumbi,watu wameingia kichwakichwa kwa dikteta kagame na bado hapa jukwaani watu wanasifu TISS ipo makini?kivipi?
kama hadi IGP anafanya ziara za mafunzo Rwanda tupo serious kweli?tumekumbatia miiba itatuchoma tu kumbuka hiyo njemba inaondoka madarakani 2034 only God knows anatujua kiundani kiasi gani,hapokatikati atafanya nini?sina imani na sytem ya awamu ya tano inamvyomkumbatia huyu muuaji hata Burundi wamepigwa na butwaa maana walikuwa wanatutegemea dhidi ya jitu liliowahi kuchoma hadi soko lao kuu la gikomba kuwakomoa.
 
Jana kwangu ilikuwa siku nyingine ya kufurahia kuwa sehemu ya member wa jamii forum. Hii ilitokana mwanajamii mmoja nzagambadume kupost link ya kitabu kilichoandikwa na mlinzi wa raisi Kagame aliyekimbilia UK kuepuka kifo kilichokuwa tayari mlangoni mwake.

KWA NINI NAMTAJA KIKWETE NA MEMBE

Kwanza ijulikane wazi kuwa Watanzania wengi tulifahamu kuwa Kikwete alikuwa raisi mpole na kufikia hatua ya tukamuita raisi dhaifu aliyezungukwa na marafiki wabaya (walio na hulka ya kujinufaisha wao na familia zao). Nakumbuka nikiwa navuka Mtukula kwenda Kampala siku hiyo sitausahau hasa baada ya kukuta kundi la raia wa Rwanda wakiwa na mizigo yao wakifurushwa kurudishwa Rwanda bila kujali walikuwa na mifugo au makazi,wameoa Watanzania au Watanzania wamewaoa walilazimishwa kurudi makwao kwa amri ya raisi Jakaya Kikwete!!.

Pale mpakani alikuwepo mama mmoja na mwanae wamelala kandoni kidogo mwa barabara huku mtoto akiwa na hali mbaya bila nguo ndipo utu wa Kitanzania niliuona pale kwani yule mama kama alitoka hapo basi hatasahau maisha yake yote kwani alichangiwa na abiria wa Kitanzania kwa kupewa vyakula, nguo na pesa na katika basi gumzo ilikuwa Kikwete ana bifu na Kagame lao binafsi lkn limesababisha hadi wasiohusika wanataabika ukweli hata mimi nilikuwa mmoja wa waliokuwa wanamshutumu raisi. Tulienda mbali kwa kusema huu ukatili si angeuelekeza kwa wezi walioko serikalini mwake lkn msimamo wa Kikwete ulikuwa palepale na hadi anatoka madarakani sikumbuki kama Kikwete alishawahi kwenda ziara Rwanda.

MEMBE ambaye alikuwa mtu wa karibu wa raisi Kikwete wengi tulijua ni usalama wa Taifa (TISS) hivyo tulifahamu kuwa linalotokea baina ya Tanzania na Rwanda basi kwa namna moja Membe alikuwa anafahamu tukizingatia kuwa alishakuwa waziri wa mambo ya nje kwa miaka kadhaa.

KITABU CHA NOBLE MARARA
Kitty hiki ukianza tu kukisoma sio tu utastaajabu usiyoyafahamu kuhusu Kagame ila utashangaa kwa nini tuna urafiki na mtu dizaini hii (Kagame na Rwanda). Kitabu kimemweka wazi Kagame maisha yake,tabia yake,ukatili wake,namna anavyosuka mipango ya mauaji na namna anavyoplan kujisafisha namna alivyokuwa anazini na wake za watu wake wa karibu akiwa analindwa na ma body guards wake!!

Mtu anayeandika kitabu hiki kumbuka ni mtu aliyekuwa anamlinda Kagame kuanzia asubuhi gadi asubuhi nyingine, yeye mwenyewe kashiriki mauaji akifikiria anailinda Rwanda na Kagame kumbe ni chuki na kujiimarisha tu kwa Kagame rafiki wa karibu wa Tanzania kwa sasa!! Hadi anatoroka alikuwa tayari yuko kwenye target za Kagame

Katika haya maelezo mafupi sana nimeelewa sasa kuwa Mh. raisi Mstaafu Kikwete alibaini na kujilidhisha pasipo shaka kuwa urafiki na huyu mtu sio kabisa hasa baada ya majeshi ya Tanzania kuwapa kichapo M23 jeshi katili la Kagame kipindi hicho huko DRC

Sent using Jamii Forums mobile app
Asante mkuu,ni muhimu tujue haya yote sababu system ya awamu ya tano ilivyomkumbatia huyu mtu inasikitisha sana haswa ukichukulia awamu hii imejaa wachumia tumbo,hawaangalii mbele future ya watoto wetu,naogopa sana Tanzania ya mbele nina hakika mr slim anatujua hadi chupi yetu sasa hivi.TUKIMALIZA HUU MJADALA NITAWEKA LINK NYINGINE YA KITABU CHA DAVID HIMBARA ALIYEKUWA MSHAURI MKUU WA KAGAME KINAITWA KAGAME'S KILLING FIELDS
 
hebu dadavua kiongoz.
weka hicho kisa

Sent using Jamii Forums mobile app
Kagame alipiga simu kwa doctor wake ikapokelewa na house girl mweye miaka 16 aliyekuwa ametoka kijijini akaamrisha ampe simu doctor dada akakataa maana jamaa alikuwa kalala,dada maskini hakujua anaongea na nani,kilichofata ni kagame kuamrisha msafara ujipange waende kwa doctor kumbuka mwandishi marara yote alikuwa anashhudia maana alikuweko PPU(presidential protection unity)
kufika pale kauliza nani alipokea simu,ka dada kakasema ni mimi,Kagame kamrukia kamipga kama mwizi,vichwa,mateke,ngumi hadi doctor kaamka na kumuombea msamaha,ila kagame akaamuru yule binti afukuzwe kazi
 
Kagame alipiga simu kwa doctor wake ikapokelewa na house girl mweye miaka 16 aliyekuwa ametoka kijijini akaamrisha ampe simu doctor dada akakataa maana jamaa alikuwa kalala,dada maskini hakujua anaongea na nani,kilichofata ni kagame kuamrisha msafara ujipange waende kwa doctor kumbuka mwandishi marara yote alikuwa anashhudia maana alikuweko PPU(presidential protection unity)
kufika pale kauliza nani alipokea simu,ka dada kakasema ni mimi,Kagame kamrukia kamipga kama mwizi,vichwa,mateke,ngumi hadi doctor kaamka na kumuombea msamaha,ila kagame akaamuru yule binti afukuzwe kazi
ahahha huyo Basi ni kichaa siyo bureee.

So,Huyo mdada now Ni muimbaji wa kwaya au namna Gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ntakisoma badae
yanasikitisha mengi humo,jamaa kagonga sana wake za washkaji zake,kaua sana na bado anaua,kapiga sana mke wake,kambadilisha mke wake kutoka kuwa sweet Mom hadi muuaji maana wife na yeye sasa hivi katili kukiwa na mipango ya kumpa U rais kama jamaa ataachia
wakiwa porini yeye na wakubwa wa jeshi wamegonga sana vibinti vidogo hadi vya miaka 14,personally akaagiza kubakwa na kuuliwa kwa nesi aliyekuwa amejitolea kuwatibu RPF tangu wakiwa maporini huo Uganda
Ana ulcers na mara nyingi huwa anatapika na kuharisha kuna wakati alipata hilo tatizo doctor akasema kapewa sumu,wapishi wake wawili wakateswa sana kumbe haikuwa sumu,kuna siku wakiwa kwenye msafara akatapika kwenye gari mwandishi wa kitabu akawahi kusafisha seat jamaa akazuga anatoka nje ya gari kuongea na simu,mwandishi marara akamuuliza if he is okay jamaa akampiga ki pepsi cha kichwa
 
Nnyie ambao lugha haipandi ndio mnaotuharibia. Mnashindwa kusoma kingereza rahisi namna hii halafu mna simu janja kali mko JF.

Nyie ndio mnaopigia makofi kila kitu sababu hamjui tofauti ya maigizo na uhalisia. Eti Mods atafsiri mkafie mbele !!!!

OK inawezekana mko Kigali mnajua French zaidi ila kana ni Wabongo humu nendeni mkale maharage Mods hawezi kutafsiri

Sent using Jamii Forums mobile app

Wewe unayeandika store badala ya story ndo unawakashfu hapa watu

hebu kwanza karekebishe maandishi yako ndo urudi.
 
Niko sahihi mkuu inategemea uko Kigali au TZ kuelewa, hata hivyo kwasababu una dada wazuri sana ngoja nijirekebishe,niwe mpole . Tuko pamoja

Ila naomba mwenye kuelewa wale wadada wa ile kwaya "Kwetu Pazuriiiii" ni Watusi au Wahutu au mixer.

Wametuzingua wengi sana na mapozi yao hatari



Wewe unayeandika store badala ya story ndo unawakashfu hapa watu

hebu kwanza karekebishe maandishi yako ndo urudi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Da kagame hatari sana aliwai hata kutishia kumuua kikwete when he was in power aisee huyu mlinzi kaanika kila kitu aisee i wish watu wa TISS wakisome na tujaze watu wetu huko rwanda kufatilia movement za huyu jamaa he is a real threat kaua sana ma komredi wake waliokua wote vitani ha ha ha ha ha alafu alivyo bwege askari wenzie wanamzarau kuwa hakupigana vita kwa kuwa alikua masomoni so ile inferiority complex imemfanya awauwe wote ili abake pake yake ontop so foolish
 
Hiki kitabu nilikisoma tokea mwaka jana mwanzoni, muandishi kaelezea mambo mengi sana kiasi nikawa najiuliza alikuwa na diary ya kuandika yote hayo wakati yanatokea? Mbona anaelezea kwa ufasaha mambo mengi sana?
Hasa watu waliokumbana na dhahma za PK...

Moja kati ya mambo yaliyonishtua mwanzoni kabisa mwa kitabu kile ni page hii ktk picha
IMG_1919.JPG


Kama sikosei pia kuna sehemu muandishi anasema Mr. Slim yupo ktk gridi....

Kama mtu makini lazima upembue kwa kina anachokisema muandishi maana ni ‘adui’ wa Mr. Slim hivyo kuna mambo mengine huenda sio kweli kayafanya yeye ila juu ya ugomvi baina yao atasema vinginevyo.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Katika page ya 73 mwandishi Noble Marara ambaye ni bodyguard wake wa zamani anazungumzia roho ngumu ya jamaa akiwa na wasiwasi mkubwa wa mambo mabaya aliyowafanyia wahutu hapo Rwanda na Congo.

Kagame ali fake shambulio in 1998 kuua raia waliokuwa wakiangalia mpira hotelini ili awasingizie Interahamwe lakini aliyepewa jukumu la kusimamia hilo(captain Kwizera) alilewa chakari, matokeo yake askari wa RPF waliojifanya Interahamwe walifika hotelini hapo wakashangaa kuona kuna wanajeshi wa RPF nao wanaangalia mpira wakapiga simu kwa wakubwa yakatolewa maelekezo wale askari waondoke hapo haraka.

Raia wajanja walivyoona zile movement wakshtuka nao wakasepa, waliobaki ndani baadaye walikufa maana ile hoteli iliungua ikabaki majivu. Baadaye radio Rwanda ilitangaza ya kwamba shambulio lilifanywa na Interahamwe

Sababu ya kuwaua ikiwa nini? Nawaza kwa nguvu tu pale mwandikwa atakapomkamata mwandishi......
 
Mi nikawa nashangaa mbona kama kagame anapagawa mara agombane na burundi sijui wafungiane mipaka mara agombane na museven kumbe anajua soon jamaa wana m fix da ila kaua sana rafiki zake ngoja akipate cha moto alafu wapinzani naona wameungana saizi wanashuka nae jumla jumla in Mwanri voice
 
Back
Top Bottom