Mjadala - Kitabu cha unyama wa Paul Kagame: Behind the Presidential Curtain: Inside Out of real Paul Kagame

Mjadala - Kitabu cha unyama wa Paul Kagame: Behind the Presidential Curtain: Inside Out of real Paul Kagame

In fact it seems to be that PK is really a tyrant leader of this era, this is due to so many killings he has committed starting from Gen Rwigyema and so many others including his army commders, funny enough he killed even European tourists!! By doing this he's creating a lot of enemies who one day will cause his downfall it's just a matter of time ..........
 
Mkuu umepotea sana, vipi kazi zimekuwa nyingi? Nilizoea kuona michango yako mingi, siku hizi imepungua sana. Kilangila.

Daaa mkuu mambo mengi sana itabidi nianze kutia timu shukrani
 
Hivi wa Rwanda JF wamo humu hizi nondo wanazisoma ?

Sent using Jamii Forums mobile app
Ujinga mtupu mkuu.
Sidhani kama mtu mwenye akili timam,anaweza akasifia upuuzi huu. Watu eti waliitikia kikao, askari wa RPF wakawamiminia risasi?! Mwaka gani huo?Wapi huko? Ina maana hiyo serikaliya Habyarimana ilikua dhaifu kiasi gani cha kutotambua uwepo wa RPF huko?
Vitu vingine, sioni sababu ya kupoteza mda.
Hii story ni sawa na kudai kwamba Tanzania ni inchi isiyo na ziwa hata moja.
 
Hiki kitabu hata kama hakina ukweli asilimia miamoja lakini ni kitabu kinachosisimua na kutisha. Kimenipa picha kwanini mpaka wa Uganda na Rwanda umefungwa lakini pia mpaka wa burundi na rwanda.

Nimeona alivyo mgusa mzee kikwete na nimekumbuka mmauzi magumu aliyoyafanya kuwaondoa wakimbizi hakika kina kitu kikubwa zaidi ya kitabu. Hongera mwandishi na hongera uliyeshare nasi
 
Ujinga mtupu mkuu.
Sidhani kama mtu mwenye akili timam,anaweza akasifia upuuzi huu. Watu eti waliitikia kikao, askari wa RPF wakawamiminia risasi?! Mwaka gani huo?Wapi huko? Ina maana hiyo serikaliya Habyarimana ilikua dhaifu kiasi gani cha kutotambua uwepo wa RPF huko?
Vitu vingine, sioni sababu ya kupoteza mda.
Hii story ni sawa na kudai kwamba Tanzania ni inchi isiyo na ziwa hata moja.
mkuu kunywa maji kwanza tuliza munkari
 
Mh! Huyu mtu ni katili sana na mikono yake imejaa damu ya wanyarwanda wengi sana wasio na hatia. Huyo mwendawazimu wa Ikulu ndiyo anachukua darasa toka kwa huyu dikteta mwingine.

Jana nilitoa link ya ku download hiki kitabu, kwa ambao hawaja download ingia JF Store, wandugu naomba msome vizuri hicho kitabu baadaye turudi kwenye mjadala hapa maana niliyoyasoma yanasikitisha.

View attachment 1072722View attachment 1072723

Kumbe ndiyo maaana Museveni kamchoka,wanajuana nje ndani, na Kagame hizo tabia zake ni za hatari siye yule tunayemuona sisi, SO SAD.

Kitabu kina pages 110(hard copy)ila kwenye pc hapa inaniambia ni pages 302 ,kwenye page ya 71 tunaona kitu fulani kuhusu tabia ya Kagame(familiar )

--
--It was President Kagame himself who briefed his senior intelligence commanders to use the tactic of being friendly to those they were planning to kill, at some point they gave out sugar and salt, cooking oil and soap to the locals that our soldiers had looted from shops just to make them come out of the hiding only to be killed in the end.----

Ni kwamba mwaka 1992 katika mazungumzo ya amani Arusha,Rais Juvenal Habryimana alisema wakimbizi wa Rwanda walioko nje kurudi ni ngumu sababu hakuna ardhi ya kutosha kwa hiyo akawasambaza wahutu mipakani huko na kuwapa ardhi ili ionekane kweli pamejaa na pia sababu nyingine ilikuwa ni kuwapeleleza RPF waliokuwa wanavamia kutokea Uganda

So,trick ya Kagame ikawa ni kwenda kwenye vile vijiji na wanajeshi wake kujifanya marafiki zao wakiwapa sukari,chumvi,nguo,siku moja katika kijiji cha Kagitumba wakaitisha mkutano mkubwa wahutu wakajaa wake,waume kwa watoto,katikati ya mkutano askari wa RPF wakarusha risasi na mabomu ya kutosha wakaua maelfu ya wahutu.

Niko page ya 72 ila dah hadi hapo nilipofika jamaa aliua marafiki zake waliomsaidia kupindua nchi karibu 10 tena wenye vyeo vya juu jeshini akiwemo FRED RWIGEMA swahiba mkuu wa Museveni kiasi cha kusababisha mdogo wake Museveni meja Salim Salehe kwenda kuua mameja wawili wasio na hatia waliosingiziwa na Kagame kwa Musevni kwamba walimuua Rwigema

Jamaa alikuwa anawaogopa makamanda wa ukweli waliomtoa dikteta Habrayimana , walikuwa hawamkubali sababu hakupigana vita muda mwingi alikuwa masomoni Marekani alipopelekwa na Museveni.

Mwandishi anasema jamaa ana tabia ya kujifanya rafiki yako huku akikutafutia muda sahihi wa kufanya yake(does that sound familiar?
 
Tena naona ni mwanafunzi mzuri kweli! Kibaya zaidi, (baada ya kusoma hiki kitabu) naona hata hulka zinafana - wote hawashahuriki, wote wana visasi, n.k.

Mh! Huyu mtu ni katili sana na mikono yake imejaa damu ya wanyarwanda wengi sana wasio na hatia. Huyo mwendawazimu wa Ikulu ndiyo anachukua darasa toka kwa huyu dikteta mwingine.
 
Kagame alipiga simu kwa doctor wake ikapokelewa na house girl mweye miaka 16 aliyekuwa ametoka kijijini akaamrisha ampe simu doctor dada akakataa maana jamaa alikuwa kalala,dada maskini hakujua anaongea na nani,kilichofata ni kagame kuamrisha msafara ujipange waende kwa doctor kumbuka mwandishi marara yote alikuwa anashhudia maana alikuweko PPU(presidential protection unity)
kufika pale kauliza nani alipokea simu,ka dada kakasema ni mimi,Kagame kamrukia kamipga kama mwizi,vichwa,mateke,ngumi hadi doctor kaamka na kumuombea msamaha,ila kagame akaamuru yule binti afukuzwe kazi
Duhhh may thunder strike him
 
Ujinga mtupu mkuu.
Sidhani kama mtu mwenye akili timam,anaweza akasifia upuuzi huu. Watu eti waliitikia kikao, askari wa RPF wakawamiminia risasi?! Mwaka gani huo?Wapi huko? Ina maana hiyo serikaliya Habyarimana ilikua dhaifu kiasi gani cha kutotambua uwepo wa RPF huko?
Vitu vingine, sioni sababu ya kupoteza mda.
Hii story ni sawa na kudai kwamba Tanzania ni inchi isiyo na ziwa hata moja.
kijiji cha kagitumba kipo mpakani na bukavu huko,umesoma kitabu lakini?RPF walianza kupambana na Habyarimana tangu 1990 kwa msaada wa museveni wakitokea Uganda,1992 Habyarimana pale Arusha kwenye mazungumzo ya amani alikataa wakimbizi waliopo Uganda na Tz na kiwingineko wasirudi Rwanda kwamba hakuna ardhi,akaanza kuwasambaza wahutu huko mipakani..kwa hiyo kuhusu kutambua dunia nzima ilijua RPF wapo na jeshi lake Habyarimana lilkuwa dhaifu.
 
Saiz yupo wapi huyo mlinzi?

Kwaio saiz PK anakuwa karibu ma Pogba magu kuna kitu anakusudia?

Dumelang
TZ ni nyumbani, na kwa sasa hakuna mtu ambaye anayeweza kumpa hifadhi km kitanuka zaidi ya TZ. So lazima apakumbuke nyumbani muda wote kwa kuwa ndio kimbilio & tumaini pekee
 
Hiki kitabu hata kama hakina ukweli asilimia miamoja lakini ni kitabu kinachosisimua na kutisha. Kimenipa picha kwanini mpaka wa Uganda na Rwanda umefungwa lakini pia mpaka wa burundi na rwanda.

Nimeona alivyo mgusa mzee kikwete na nimekumbuka mmauzi magumu aliyoyafanya kuwaondoa wakimbizi hakika kina kitu kikubwa zaidi ya kitabu. Hongera mwandishi na hongera uliyeshare nasi
Ndipo utaona kwamba kikwete alikuwa mzalendo kweli sio wale wanaojifanya kila siku waonekane wazalendo kwa kupiga makelele wakati vitendo ni opposite,kuna janga lilitokea jamaa wa IT jeshini alitoroka kurudi kwao Rwanda na mengineyo mengi kikwete akaanza kusafisha uozo cha ajabu leo haohao jamaa eti ndiyo ma best friend wetu hadi IGP Sirro anaenda kwenye mafunzo mafupi kigali,mara sijui wanatuletea wataalamu wa IT.
 
huyo mwandishi yupo UK,Croydon ,south london,ni Dr wa magonjwa ya akili.serikali ya UK inamlinda kiaina ,last year mwezi wa tatu ,scotland yard walimpa warning kwamba kagame kaingiza watu UK kutakaa kumuua.
 
Kila kitu kina muda na wakati wake.Walikuwa akina Mobutu Seseseko lakini leo wa[po wapi? Viongozi katili katika ukanda wa Afrika lazima kuna watu huwa wanawadhamini mpaka hao wadhamini wawachoke ndio hutolewa madarakani kama sio hivyo basi ni kifo pekee ndo muamuzi.
 
wa Afrika wengi huwa tunapenda kujiufariji kwa matukio yanatokea katika nchi jirani,mfano unakuta mtu anasema lazima huu uongozi katili lazima tuutoe kwa gharama yoyote ile mbona Sudan wameweza ikumbukwe tuu waliomueka madarakani ndio wamemtoa.
 
huyo mwandishi yupo UK,Croydon ,south london,ni Dr wa magonjwa ya akili.serikali ya UK inamlinda kiaina ,last year mwezi wa tatu ,scotland yard walimpa warning kwamba kagame kaingiza watu UK kutakaa kumuua.

After a hard week working as a mental health nurse manager, Noble Marara was relaxing at home with his family when they were visited by two police officers, Times magazine UK


Sahihisha sio Doctor acha kuharibia fani za wataaluma, huyu ni mental health nurse manager, na amekuwa manager sababu alikuwa mental health nurse kwanza
 
After a hard week working as a mental health nurse manager, Noble Marara was relaxing at home with his family when they were visited by two police officers, Times magazine UK

Sahihisha sio Doctor acha kuharibia fani za wataaluma, huyu ni mental health nurse manager, na amekuwa manager sababu alikuwa mental health nurse kwanza
Unafahamu kuna Dr of nursing?
 
Back
Top Bottom