Marco Polo
JF-Expert Member
- Jan 16, 2014
- 11,786
- 18,562
Nikitulia ntasoma vizur
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Yameibuka tena huko dodomaHapa sasa yanatokea huku kuna kundi linaamini jiwe ni mungu mtu baadhi ya wabunge wameanza kampeni ya kumuongezea muda wanaopinga wanaitwa wasaliti jamaa anaiga mambo ya rwanda watanzania tuwe macho hapa sasa kuna funzo picha limeanza kuja
KwelHili ndo tatizo la kufanya maendeleo huku ukikandamiza uhuru wa watu hata ya uongo utatungiwa , kwakweli mimi nilifika kigali before 1990's na late 2000's kwakweli rwanda kunavutia mabadiliko ni makubwa sanaa kosa kubwa analolifanya jamaa ni kuminya uhuru wa watu kujieleza hakuna utawala bora ndo maana washirika wake wazamani wanakokotoa yale mabaya yote aliyoyafanya kipindi cha nyuma na kuyaexpose sasa hata hivyo huyu mzee ana roho mbaya sanaa kama mzee wetu huyu sema kutokana na ukubwa wa nchii huyu huyi anashindwa ila angekuwa na kanchii ka kuzungukwa kwa lisaa kama rwanda tungesaga meno , watawala wa kiafrika bado sanaa .kagame is silent killer hana tofoute na huu wetu. Ila mungu yupo ipo siku yake.
View attachment 1073689View attachment 1073690hawa nao wanadanganya?
Kizuri kula na nduguyo
Inamaana hujaona pdf attached,⁉️🤔Mkuu km una full book nisaidie
Wewe naona ndiyo Kagame mwenyewe hutaki tupate point kwenye uzi huu sasa haahhaahaaaaaaHivi kabla hamjaanza kushangilia yaliomo kwenye hicho kitabu mnamjua aliekiandika ni nani kwanza? Huyo jama Marara kweli alikua kati kikosi cha kumlinda raisi na alikua dereva katika miaka hio ya mwishoni 90's alikua anaendesha vifaru walivhoachiwa na UN kwa ajili ya usalama wa viongozi. Kwa vile alikua uneducated young man hakua anakaa na senior officers mpaka ahadisiwe kinachoendelea. Alitimuliwa jeshini na kukimbia nchi na huko ulaya aliko anatafuta attention tu watu kwani ameshakosana na aliokimbia nao wengi huko ughaibuni.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hichi kitabu kinatishaAlikuwa anamtmbea luten mmoja akiwa Marekani hadi mkewe Jannet akastukia. Unajua mkuu hiki kitabu kinavutia sana ukizigatia aliyekiandika ni Mlinzi (mtu wa karibu sana na raisi).
Sent using Jamii Forums mobile app
Nondo zimejaa humoKatika ukurasa wa 79, bwana Marara anatuambia kuhusu kifo cha Asiel Kabiera, mshauri mkuu wa Rais Kagame ambaye kabla ya hapo alikuwa mshauri mkuu wa Rais Bizimungu kipindi hicho Kagame akiwa Waziri Mkuu.
Kabera anasifiwa na wengi Rwanda kwa kuwa na roho ya kibinadamu na alikuwa hapendi mambo mengi yanayofanywa na Kagame, ukiachilia mbali hilo pia alikuwa rafiki wa karibu wa spika wa Bunge Mr Kabuye ambaye baadaye alikimbia nchi kwa hofu ya kuuawa, spika huyo alikuwa anachukiwa sana na Kagame.
Mwandishi katika ukurasa huo anasimulia kwamba siku moja alikuwa anatakiwa kumpeleka mke wa Kagame kumtembelea mama yake, akiwa kwenye gari alisikia mlio wa risasi ukitokea karibu na Presidential Palace, akapiga radio call kuuliza wenzake kuna shida gani, kuna mwenzao akamuambia usijali kila kitu kipo sawa wewe endelea na safari yako na first lady. Baadye akaja kumuambia kwamba Mr. Kabera alikuwa ni msaliti so they sorted him out
Kwani Tanzania tunakaogopa sana haka kajamaa??? Hata mwili hakana, hata ngumi hakawezi kurusha.... daaaah😄😄😄Jana nilitoa link ya ku download hiki kitabu, kwa ambao hawaja download ingia JF Store, wandugu naomba msome vizuri hicho kitabu baadaye turudi kwenye mjadala hapa maana niliyoyasoma yanasikitisha.
View attachment 1072722View attachment 1072723
Kumbe ndiyo maaana Museveni kamchoka,wanajuana nje ndani, na Kagame hizo tabia zake ni za hatari siye yule tunayemuona sisi, SO SAD.
Kitabu kina pages 110(hard copy)ila kwenye pc hapa inaniambia ni pages 302 ,kwenye page ya 71 tunaona kitu fulani kuhusu tabia ya Kagame(familiar )
--
--It was President Kagame himself who briefed his senior intelligence commanders to use the tactic of being friendly to those they were planning to kill, at some point they gave out sugar and salt, cooking oil and soap to the locals that our soldiers had looted from shops just to make them come out of the hiding only to be killed in the end.----
Ni kwamba mwaka 1992 katika mazungumzo ya amani Arusha,Rais Juvenal Habryimana alisema wakimbizi wa Rwanda walioko nje kurudi ni ngumu sababu hakuna ardhi ya kutosha kwa hiyo akawasambaza wahutu mipakani huko na kuwapa ardhi ili ionekane kweli pamejaa na pia sababu nyingine ilikuwa ni kuwapeleleza RPF waliokuwa wanavamia kutokea Uganda
So,trick ya Kagame ikawa ni kwenda kwenye vile vijiji na wanajeshi wake kujifanya marafiki zao wakiwapa sukari,chumvi,nguo,siku moja katika kijiji cha Kagitumba wakaitisha mkutano mkubwa wahutu wakajaa wake,waume kwa watoto,katikati ya mkutano askari wa RPF wakarusha risasi na mabomu ya kutosha wakaua maelfu ya wahutu.
Niko page ya 72 ila dah hadi hapo nilipofika jamaa aliua marafiki zake waliomsaidia kupindua nchi karibu 10 tena wenye vyeo vya juu jeshini akiwemo FRED RWIGEMA swahiba mkuu wa Museveni kiasi cha kusababisha mdogo wake Museveni meja Salim Salehe kwenda kuua mameja wawili wasio na hatia waliosingiziwa na Kagame kwa Musevni kwamba walimuua Rwigema
Jamaa alikuwa anawaogopa makamanda wa ukweli waliomtoa dikteta Habrayimana , walikuwa hawamkubali sababu hakupigana vita muda mwingi alikuwa masomoni Marekani alipopelekwa na Museveni.
Mwandishi anasema jamaa ana tabia ya kujifanya rafiki yako huku akikutafutia muda sahihi wa kufanya yake(does that sound familiar?
Haka ni kama Israeli kanapiga mataifa yoote na hakuna anayekawezaKwani Tanzania tunakaogopa sana haka kajamaa??? Hata mwili hakana, hata ngumi hakawezi kurusha.... daaaah😄😄😄