Mjadala kuhusu Babu wa Loliondo na dawa yake.


Holy Crap....Mjengwa...Usinge waka uko ungeishia kwenye uso wa kitabu na blog yako sasa umepost uku dah ona sasa watu umewavuruga akili wanatukana....Hii Watu wanao umwa magonjwa ambayo wanasanyasi wamekuwa wakizungua kila siku kuwa hayana tiba mwisho wao ni kufa tu....Unafikiri akiambiwa kuna tiba afanyaje?
 
Ubarikiwe kwa mtazamo huo. Hakuna upuuzi mkubwa na wa kihistoria tuliofanya watanzania kama kumrejesha kwenye madaraka makubwa ya nchi yetu mtu anayesema hajui kwa nini watu wake ni maskini na wakati huo huo anawaahidi maisha bora kwa kila mtu!!!!!

Alirejeshwa au alijirejesha na sisi kumfagilia kwa kujaza uwanja siku aliojiapisha fasta fasta kabla zengwe halijaanza?
Tunajimaliza wenyewe kwa uzumbukuku wetu na ndio mtaji wa CCM.
 
hapa udom chuo kimefunguliwa wanafunzi hawaonekani wahadhiri siwaoni sijui wameenda loliondo kwa babu
 
Kosa kubwa alilolifanya Maggid ni kujenga hoja yake kwa kutaka kuthibitisha suala la kiimani kwa kutumia sayansi...kosa kubwa...masuala haya hayachangamani hata siku moja. Na maggid utakuwa umefanya kosa hili aidha kwa makusudi ili kufanikisha malengo fulani au kwa kutokujua. Sipendi kuamini kuwa umefanya kosa hili kwa kutokujua au kwa kukosa uelewa , na hivyo kunifanya niamini kuwa una lengo lako maalum kuandika haya ambalo si lingine bali ni upotoshaji wa makusudi.
 
Usiandike tu ili KUSOMWA bali andika with facts,je umewauliza wale wanaotumia tiba za huyu babu wakupe shuhuda zao??
Unaandika kiimani zaidi kua 'its impossible" but one thing,fanya utafiti kisha andika.
Wasalimie Iringa
 
Desperation always calls on desperate measures too. That's fact, or do we need a scientific explanation?

Wanaoenda kwa Babu sio watu wenye mafua, au kikohozi au malaria. Ni watu walio kwenye different levels of desperation, they are suffering from the 'incurables'. Sidhani kama kuna yeyote ambaye anataka kuishi katika maumivu maisha yake yote, hata kama sayansi imemwambia kuwa anachosumbuliwa nacho hakiponi. Desperation!

Mimi sidhani kuwa 'maji' anayotoa Babu ndiyo yanayoponya, desperate people develop staunch beliefs too, on MIRACLE on the impossibilities becoming possible. They are sick, so sick, so sick and yet no cure for them. But they have not given up, they think (or being made to think) that someone somewhere (or something) has the cure. The cure is on the FAITH, HOPE that these people are having. they are ready to go heights and lenghts, and whatever that comes in between

So, maybe Babu is cunning, just like other evangelists and 'miracle' doctors. Maybe this Babu is using this FAITH that people have on the 'possibilizing' impossibilities. And he's using it, just like Kakobe and company are doing.

We all live because there is HOPE (remember whenever you are using the Future tense, means you BELIEVE) the hope that some things may change. And Babu is giving just THAT!
 

Pumba Tupu shwain we!! Watanzania tumezoea sana siasa..na ndo inayotufanya maskini wakutupwa...sasa wewe unaambiwa watu wanapona,ndugu jamna na marafiki tunaowajua wameepuka kifo...sasa unataka eti zoezi lisimame kuingiza siasa za uchunguzi wa madahara nk nk...upumbavu mtupu,kitaalam uwezekana wa dawa za herbs kuwa na madhara is almost 0%!....we hayajakufika mwehu
 
sisi ni wepesi kuamini kwa kusema eti uthibitisho wa kisayansi..........lakini hatujiulizi hii sayansi tuliyo nayo na unayoiamini ni nini imesaidia dunia acha watu wakajaribu kwani hata hii ndio sayansi yetu ambayo tulikataa kuiendeleza kwa kuamini kila kitu kutoka magharibi sasa sitoshangaa vipimo vyao vikishindwa kupima ubora na uwezo wa dawa ya babu kwani kwakuwa sayansi yao ni ndogo na hawajaweza kufika huku alipofika babu.
 
Ubarikiwe kwa mtazamo huo. Hakuna upuuzi mkubwa na wa kihistoria tuliofanya watanzania kama kumrejesha kwenye madaraka makubwa ya nchi yetu mtu anayesema hajui kwa nini watu wake ni maskini na wakati huo huo anawaahidi maisha bora kwa kila mtu!!!!!

Mkulu na mama walikunywa dawa kimya kimya. Majjid ni mahili wa kuandika kwa mtazamo wake bila kuwainisha upande mwingine kwa ushahidi. Si mpuuzi bali ni mhafidhina wa mawazo mgando angeweza kwenda kuhoji Babu kwa swali moja Wakubwa wangapi wamekunywa kikombe? Hao ndio angewatatufa wamthibitishie.
 
Kwani ndugu magidd,
haya uanyo andika pia si ni abrakadabra?? hata hivyo si imeshatangazwa waislamu wasiende?? na redio khier cjui radio yao wenyewe? nasisi tumekubali wasiende tuachiwe hili abrakadabra letu!! full stop
 
Kuna habari zimeshaanza kuenea kuhusiana na dawa anayotoa Babu kule Loliondo kuhusiana na uponyaji wake kama tunavyoambiwa na Babu kua kikombe kile kimoja cha dawa kinatibu magonjwa sugu kama vile Kansa/Kisukari/Pumu/Presha/Ukimwi na pamoja na vidonda vya tumbo. Sasa kuna habari zisizo rasmi kuhusiana na dawa hiyo kwa wale wenye ugonjwa sugu wa Kisukari si mnajua ugonjwa huu unazoofisha nguvu za kiume na kushindwa kuwajibika kwa wanaume kushiriki tendo lile, sasa hivi ni kua eti kwa wale wagonjwa wa kisukari waliopata dawa tayari kwa babu wamedai wameshapima kisukari na pia kujaribu kula vyakula ambavyo walikua hawaruhusiwi kula kutokana na masharti ya ugonjwa huo hususani na kushuhulika vizuri ipasavyo kwa wake zao kutokana na dawa hiyo kutibu vizuri! jamani natumaini hizi ni taarifa nzuri kama kweli ni rasmi kuhusiana na dawa kutoka kwa babu. Nawasilisha.
 
Eisee! nimeambiwa na mshikaji wangu kuwa heshima imerudi make sasa hivi mama ameanza kupata haki yake kama kawa.
 
Huduma za Afya hapa Tz ni mbovu sana, zilizo bora watu wa kima cha chini hawawezi kuzimudu.Vifo vingapi vinatokea kwa uzembe, watu wangapi wanakufa kwa magonjwa ya kutibika.Maggid inaonekana hujawahi kuwa na mgonjwa ndio maana unakuja na maelezo yasiyo na msingi

Nafikiri ungeishauri serikali iboreshe huduma ya afya,tupunguze vifo, maisha ya mtanzania yawe salama.Ww utaona huko sijui kwa manabii,wachungaji,maaskofu,wazee wa upako utaona watu wenye magonjwa watapungua kwenda kuombewa.
Mambo ya imani hayapimwi kwenye test tube,yaangaliliwi kwenye x-ray,hapimwi kwenye microscope.
Mbona hao wa kina kakobe,lwakatare wanatumia vitambaa kutibu na hawahojiwi kiasi hiki?
Go ahead babu wewe tibu, ambao hawaamini waache ndugu zao au wenyewe wafe.
 
Safari hii umefanikiwa kumwona babu nini?
Maana umeangaika sana mkuu
Heshma muhimu sana nyumbani naona na mama leo kauso kamechangamka!
 
Heshima, mamlaka, uweza, usultani na enzi viina Bwana Mungu wetu milele amina. Babu ni chombo tuu tena cha udongo kilichopata neema ya Mungu kufanya hayo aliyoyafanya hivyo utukufu unamrudia Yehova Mungu, muumba mbingu na nchi ambae sasa tunamwabudu kwa jina alilotupa la "Bwana Yesu Kristo".
.
 
Lakini mkumbuke wosia wa babu,amesema kama utaendele kutenda dhambi basi ugonjwa ukirudi uponi tena sio kwa ukimwi tu bali ata hayo magonjwa mengine,kwahiyo kupona huko isiwe ndio chanzo kuwa na tabia za kifataki.....ooh ukiuliza eti HESHIMA imerudi,Jogoo anauwezo wa kupanda mtungi muda wote.....chonde chonde wajameni.....!
 
Mwenye afya haitaji daktari,Majjid ungekuwa unaumwa kama wale watu wanaoenda kwa Babu nadhani usingekuja hapa na hii mada yako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…