Mjadala kuhusu Babu wa Loliondo na dawa yake.

Namuunga mkono jenerali pia wa2 hawakatai babu kutibu bt masharti anayotoa babu ni ya kitapeli na cyaki mungu ki ufupi
BABU + 500 = DECI MPYA
 
Huu ULIMWENGU nao umetoka wapi?

Huyu pia anahitaji tiba ya babu maana mawazo haya ni ya karne ya 10.

Lengo la huyu ULUMWENGU ni kuuza gazeti tu.
 
Hivi mtu aikipona ni lazima aanze kujitangaza kama mlivyozoea baadhi ya wanambembwe aka wanasiasa amabo wakitoa msaada ya pipi wanautangazia Umma?, hao wachache ni sample mimi binafsi nimesikia na nimeona watu watano tofauti ambao nilikuwa najua dhahiri wanasumbuliwa na maradhi sugu wameanza kurudisha afya na kwa vinywa vyao kwa nyakati tofauti wamethibitisha kupata nafuu sana. hao ni sample sasa ndugu yangu maggid unataka wakufuate na kukueleza kuwa Maggid sasa nimepona? Amini watu wamepona acha Mbwembwe, unmeshazoe kudanganywa na wanasiasa wewe na watawadanganywa sana!!!
 
Kibohehe unapotumia mobile epuka kureply with quote maana inajaza page na kuwapa wengine tabu kufuatilia hasa thread inapokuwa ndefu
 
Good comments. Waamshe hao waliolala na kiini macho from Nigeria. Sasa hivi watakuona mpingaji ila badae watakaa kimya. Tutawakumbusha humuX2 JF. Yani hao wanaokubali danganya toto/mazingaombwe nao wanajiita GreatThinkers! kweli kuishi kwingi kuona mengi. Furaha ya kutibiwa HIV/kisukari ingesambaa kila mtaa na mifano hai,lkn sasa utasikia shangazi yake yule kapona,mtoto wa mzee flan kapona Fix fix fix. Halaf wavivu wakufikiria wanatetea wakidai Iman unaingilia. Watu wanajificha kupitia migongo ya dini Amkenii wabongo.
 
kwani hapa mnamzungumzia Maggid yupi? ni yule mwenyewe watoto wazungu wakati yeye ni mweusi kama mjaluo! au ni Maggid yupi huyo? kama ni yule ninaemjuwa mimi mbona akili zake alishazifungia stoo tangu kipindi cha kampeni? sitegemei jipya kutoka kwa mtu huyu.
 

wewe ulieamka mbona uko hapa hapa wakati nchi hii inaibiwa kila kukicha na akina Mkwere & co? akili zako ndogo ndio zinakusumbuwa, unao uhuru wa kutoamini, lakini usiladhimishe watu waamini kile unachoami wewe. mfano kama wewe unaona kuingiliwa kinyume na maumbile nisafi, unataka kutulazimisha na sisi tufate msimamo wako? mshamba kabisa wewe.
 
Jenerali as a thinker may enjoy the right to theoretical analyis. However, I think he should ponder a little more about characterising Babu as a probable exploiter of people's gullibility of the same kind like the DECI crooks. That appears to me to be a stretch. It's hard to imagine in the TZ of today for such a person to maintain himself at such a squalid location and ask for only 500/= and leave transporters and others to make a kill out of it! Collusion with the bloodsuckers? Highly improbable. And, you've never suffered that much as the so-called "victims", Jenerali.
 
Hakuna huu ni shida ya wenzetu mnaingiza mambo yenu ya Udini Hivi mnataka kusema muujiza ni kama ile yakina Shekh Yahya wa majini kila siku huyu ni mtu kaoteshwa na Mungu wetu TENA WATU WANAKUNYWA KWA JINA LA BWANA NA WAMEPONA!!!!!!!!

Jaribuni kuwa mnakubali ukweli ndugu zetu. Mwenzetu kupitia jina la baba kaonyeshwa.:washing:
 
Duh! Kwanini watu mnashindwa kuwagundua walaghai ? Hawa jamaa wanaona babu kawaharibia maslahi yao. . .may be wanafanya kazi angaza na kama angaza hivyo kupoteza ajira.
Hivi umeshaskia m2 kaenda kwa babu na hajapona! Eeh.
 
Generali is right.ustaarabu wa karne hii hauendani na utumbo anaofanya babu.
 
Namuunga Mkono Ulimwengu 100% .. Kisukari na magonjwa mengine yanatibika na herbs za kawaida pia.. hapo babu si mpingi lakini linapokuja swala zima la HI5 "HIV" .. ni utapeli "nukta"
 
Hivi kweli serikali au respectable medical Drs/group wameshindwa kufanya simple investigation ya hii dawa ili kutoa opinion zao ambazo zitakuwa more based in science /lab? kwanini wasitafute sample ya wagonjwa 50 or any number wawapime in the lab na kuweka records zao then wawapeleke kwa babu kupata kikombe bila kumwambia mtu na wahakikishe wanakuwa chini ya uangalizi,then warudi baada ya muda wawapime tena...may be majibu yanaweza kutupa idea kama kweli hi dawa inaponya au laa,idea ni kuangalia kama kweli hii dawa inaponya na kama kweli kuna mtu amepona hata kama ni 10% itabidi kukaa chini na babu kumwomba kibali ili dawa yake iangaliwe zaidi inavyofanya kazi in scientific ways.....personally siamini mambo ya imani/mungu ndio anaponya hii,kama inaponya ni huo mti anaotumia,dawa zote tunazotumia nyingi zimetengenezwa kutokana na hii miti/plants au chemicals ambazo zinachimbwa ardhini
 
Mbona tutasikia mengi mwaka huu!!. Kama cancer inapona wazungu watajenga airport Loliondo
 
Yaani watu kama nyie ndio tatizo. Jenerali anataka ushahidi wagonjwa wenye proven medical record waliokunywa dawa wakapima wakaonekana wamepona. Sio kutuambia tutizame idadi ya watu wanao miminika kule! Kumbuka mulitoa hoja hii hii kwenye DECI kuwa watu wengi wanavuna! Mwisho mkaumbuka ilipogundulika ni ushetani mtupu! Kuweni makini mnamdhalilisha Mungu
 
Jenerali Ulimwengu ur nt correct .pastor Ambilikile Masapila was nt proud himself in any media bt still visitors are visiting him for his cure. science can nt interfere God will.
 

Mimi binafsi nimepona kisukari baada ya kunywa hii dawa last week. Nilikuwa natumia insulin kabla ya mlo lakini baada ya kunwa hii dawa sijatumia insulin na ninakula vyakula ambavyo hapo mwanzo nilikuwa sigusi kabisa.
 

Asante
 
Namuunga Mkono Ulimwengu 100% .. Kisukari na magonjwa mengine yanatibika na herbs za kawaida pia.. hapo babu si mpingi lakini linapokuja swala zima la HI5 "HIV" .. ni utapeli "nukta"

Generali kasha pata kikombe cha babu katoka huko juzi, halafu anatuandikia upupu, acheni bwana nasie tukapate dozi. We endelea kumuunga mkono mwenzio kesha tibiwa:tongue:
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…