Mjadala kwa wanaokataa Kuoa (Ndoa)

Huu ni uzi Mod wakauunganisha au ni comment ndugu yangu Carlos The Jackal 😂
 
1. Je, uanaume umewaisha mnajua fika hamuwezi kutegemewa na familia?
2. Je, mmeyumba kiuchumi? Mali zinatafutwa. Leo huna kitu kesho unacho?
3. Mnaogopa kugongewa? Sababu ya kishamba saana..... lini wanaume tumeanza kuwa na insecurities? Timiza majukumu yako kama baba na mume...unatoa wapi muda wa kuanza kumfuatilia mkeo eti anakucheat...

4. Binafsi naona mmekutana na watoto wetu wa kike tuliowalea vizuri, wanaoweza kujisimamia... they are intimidating you!!!

5. Unaogopa kugawana mali?.... Mkeo akichukua mlichokitafuta wote kuna shida gani! Mwisho wa siku wanawake sio wabinafsi kama sisi... sehemu kubwa ya mali watatumia wanao.

Malezi bora ya huanzia nyumbani...baada ya miaka 10 tutegemee kuwa na kizazi cha hovyo kupindukia.
 
Sababu kubwa nafikiri ni uwezo wao mdogo wa kufanya uchaguzi kwa mwanamke sahihi.
Macho ya kuona ndio tatizo.
 
""Nilikutana na wewe mke wangu ukiwa ni mwanachuo katika chuo cha Mwalimu Nyerere kigamboni.

Tukaanzisha mahusiano ya kimapenzi.

Mimi ni muislamu.

Lakini mwaka 2008 nikaamua kukuoa kwa ndoa ya kikistru kanisa la Assemblies of God Upanga.

Bila ya shaka nimefanya hivi kwa kuwa nakupenda sana mke wangu.

Tunaishi maisha mazuri, tunafanikiwa kumiliki nyumba kadhaa na magari manne.

Ninakufungulia biashara ya duka la kuuza madawa huku mimi nikiendelea na biashara yangu ya kununua na kuuza viwanja.

Tunapata mtoto mmoja aitwaye Gracious.

Mke wangu unabadilika.

Unaanza kuninyima haki yangu ya ndoa bila sababu za msingi.

Hali inaendelea hadi inafikia hatua tunalala vyumba tofauti katika nyumba yetu ya ghorofa mimi chumba cha juu wewe cha chini.

Inafikia hatua mimi naanzisha mahusiano nje na wewe unaanzisha ya kwako.

Unaweza kulala nje bila taarifa na mimi vivyohivyo.

I and you deny each other conjugal rights (horizontal engagement).

Jambo hili linajulikana kwa wazazi wa pande mbili.

Hata majirani wanajua mambo unayonifanyia kama kunimwagia maji machafu, kunipiga na fagio na hata kunivuta makende yangu mbele ya mama yangu mzazi.

Mke wangu,

Kuna siku ulinichoma na kisu mkononi.

Nikaenda Polisi lakini wakanirudisha kuwa tumalizane wenyewe.

Yote nilivumilia.

Kila wakati unani provoke kuwa nikupige nikuue lakini sifanyi hivyo.

Nilishakuomba twende mahakamani tuvunje hii ndoa yetu lakini ukakataa.

Ikafikia hatua sili wala siogi nyumbani kwangu kwani naogopa usije niwekea sumu.

Ndipo kuna siku niliondoka nyumbani bila kurudi kwa muda wa siku tano""

Story juu, imepatikana kwenye maelezo ya onyo (Cautioned statement) ya Hamisi Saidi Luwongo

Maelezo haya aliyatoa mbele ya mpelelezi kituo cha polisi Temeke.

Leo mitandao ya kijamii imeshereheshwa na hukumu ya kesi hii ila ukweli kabisa usiojificha kama asingeoa ""YASINGEMKUTA""

Ambacho hakisemwi mitandaoni:-
1. Gracious (mtoto) kapoteza wazazi sababu ya UPUUZI UITWAO NDOA.

2. Hamisi kapoteza kila kitu alichokipigania maishani, SABABU YA UPUUZI UITWAO NDOA.

3. Mke kapoteza uhai, SABABU YA UPUUZI UITWAO NDOA.

Kwasababu ya NDOA watanzania watatu (baba, mama na mtoto aliyeachwa uraiani) MAISHA HAYANA MAANA YOYOTE KWAO.

ENDELEENI KUSHUPAZA SHINGO.

Ila ""In this Millenial and Globalized world Marriage has nothing than offering you a War Ground""



Anyway:-
#YNWA
#YANGA_BINGWA
 
Aisee hivi nyi mnaoteswa na ndoa na mapenzi kwa ujumla mna shida gani..natoa offer anayetaka aje kujifunza jinsi ninavyoishi kwa amani na upendo na mke wangu ruksa aje kwangu.mbona Mimi sioni shida yoyote ya mwanamke au kwa kuwa nimemuoa nikampiga mimba fasta ndo maana hana ujanja maana ametulia sana kwenye ka getto changu nilijojitahidi hata sijakamalizia plaster Wala Nini ila mke ananifugia kuku zangu zaidi ya 20. Na ametulia nyumbani ananipikia na kunifulia bila ubishi WOWOTE hapa nawaza nimfungulie kagenge cha laki 2 hivi ashike shike vichenji.mbona maisha simple wakuu na Mimi naendelea kula starehe tu nalewa pombe na bado x naangalia kupitia ok.xxx n stripchart pia nabet na vyote anajua yaani maisha yapo vile vile tu naona mazuri
 
Sijasema kam Huwa hatugombani hapana tunagombana Tena sometimes ngumu kabisa zinapigwa


Au kwa sababu nimeoa kabila moja na dhehebu moja
 
Tatizo ni kwamba Ile nafasi ya kumpenda Mungu mmependa sana wenzi wenu...

Biblia inasema; Mpende Bwana Mungu kwa moyo wako wote na mpende jirani kama nafsi yako...
 
Tatizo ni kwamba Ile nafasi ya kumpenda Mungu mmependa sana wenzio wenu...

Biblia inasema; Mpende Bwana Mungu kwa moyo wako wote na mpende jirani kama nafsi yako...
Comment # 3,166

#YNWA
#YANGA_BINGWA
 
Yote uliyoandika HAYANA UHUSIANO WOWOTEE NA NDOA.

#YNWA.
#YANGA_BINGWA
 
Wakuu,

Wakati mwingine kataa ndoa huwa wana hoja muhimu sana wasikilizwe.

Mimi nilioa miaka mitatu iliyopita,tukajaliwa kupata mtoto wa kiume mmoja,tangu mama mtoto wangu ajifungue miaka miwili iliyopita,hataki tuzichape kavukavu anasema tutumie condom,sababu kuu ni kuwa mtoto bado ni mdogo hivyo tusubiri angalau miaka 5 au 4 hivi ndipo tupate mwingine, sababu nyingine ni kuwa hali ya maisha bado ni duni tukipata mtoto mwingine tutashndwa kuwahudumia hivyo tujitafute kwanza.

Basi bwana matumizi ya condom yaliendelea na sikuwahi kuacha kutumia kondomu kwa kila tendo

Cha ajabu mwezi wa kwanza nimekuja kugundua mke wangu ni mjamzito,ndipo ulipoibuka ugomvi mzito kuwa mimba amempa nani, akawa ananificha

Ndipo nikaamua kuwaita wazazi wake, viongozi wa dini serikali na wazee wa kimila,akaulizwa aliyempatia mimba,ndipo alipomtaja kuwa ni mwalimu wa kwaya kanisani kwao aliyekuwa amekuja kanisani kwa muda sasa hayupo.

Nimemkimbia kwa sasa nipo mkoani kusaka maisha mapya.

Kataa ndoa wameshinda.
 

Jamaa ndo alikuwa anamwambia utumie kinga, hawa watu sio binadamu
 
Kwako imekuwa rahisi kukwepa mtego wakulea mtoto asiye wako. Kwaya kwaya
 
Alikua anasisitiza matumizi ya Kinga ili amkinge mpenzi wake mwalimu wa kwaya dhidi ya magonjwa ya zinaaa kutoka kwako ....pole sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…