Wakuu,
Wakati mwingine kataa ndoa huwa wana hoja muhimu sana wasikilizwe.
Mimi nilioa miaka mitatu iliyopita,tukajaliwa kupata mtoto wa kiume mmoja,tangu mama mtoto wangu ajifungue miaka miwili iliyopita,hataki tuzichape kavukavu anasema tutumie condom,sababu kuu ni kuwa mtoto bado ni mdogo hivyo tusubiri angalau miaka 5 au 4 hivi ndipo tupate mwingine, sababu nyingine ni kuwa hali ya maisha bado ni duni tukipata mtoto mwingine tutashndwa kuwahudumia hivyo tujitafute kwanza.
Basi bwana matumizi ya condom yaliendelea na sikuwahi kuacha kutumia kondomu kwa kila tendo
Cha ajabu mwezi wa kwanza nimekuja kugundua mke wangu ni mjamzito,ndipo ulipoibuka ugomvi mzito kuwa mimba amempa nani, akawa ananificha
Ndipo nikaamua kuwaita wazazi wake, viongozi wa dini serikali na wazee wa kimila,akaulizwa aliyempatia mimba,ndipo alipomtaja kuwa ni mwalimu wa kwaya kanisani kwao aliyekuwa amekuja kanisani kwa muda sasa hayupo.
Nimemkimbia kwa sasa nipo mkoani kusaka maisha mapya.
Kataa ndoa wameshinda.