Mjadala kwa wanaokataa Kuoa (Ndoa)

Hivi nyie wakati wazee wa zamani wanatoka Safar na kutofika kwake Kwanza na kutuma koti nyumbani mlifikiri ni Wajinga?

Wanajua lolote laweza tokea na hawakutaka kukutana nayo

Sasa nyie kinachowafanya mpekue Simu za wake zenu mlitarajia nini?
 
Hivi nyie wakati wazee wa zamani wanatoka Safar na kutofika kwake Kwanza na kutuma koti nyumbani mlifikiri ni Wajinga?

Wanajua lolote laweza tokea na hawakutaka kukutana nayo

Sasa nyie kinachowafanya mpekue Simu za wake zenu mlitarajia nini?
Watu hawaelewi ukiwa na mke haimaanishi hatatongozwa, ataendelea kutongozwa kama kawaida
 
Kama amegongewa kwani wanawake wameisha atafute mwingine kwani wanawake wameisha, kwa sasahivi hatuna wanaume bali tuna wanaume suruali

Nyie ndo wale ukipitia changamoto ngumu kwenye maisha mnajinyonga
 
Mimi nipo kwenye ndoa na ninapambana bila kuchoka nichomoke kwenye ndoa kutokana na mambo ya ndani ya ndoa yalivyo.

Nilikuwa kimya nasoma maoni ya wanaokataa ndoa na wanaoipa chapuo ndoa.

Hoja yangu imebase kwenye mantiki zolizowekwa na sheria. Sheria ya ndoa ya Tanzania inapeleka hasara kubwa kwa wanaume na kumfaidisha sana mwanamke.

  1. Sheria ya ndoa inamtaka mwanaume kumtunza mke wakati wote wawapo kwenye ndoa
  2. Sheria ya ndoa inammilikisha mwanamke mali za mwanaume za ndani ya ndoa. Hapa maana yake jasho la mwanaume linagawanywa kuwa jasho la wanandoa wote wakati wa ndoa
  3. Endapo wakaamua kutalikiana, mwanaume hupewa gawio lisiloakisi jasho lake na mwanamke hupata gawiwo zaidi ya jasho lake.
  4. Sheria ya ndoa haimpi jukumu mwanamke ndani ya ndoa bali majukumu.yote anapewa.mwanamume
KUna vitu vingi havijakaa sawa kwenye ndoa ambavyo vinawasababisha vijana kuwa bold and clear kukataa ndoa.


Tuzungumze maboresho ya sheria ya ndoa ndipo vijana waanze kurejea ndoani.

Mie.mwenyewe nataka leo kesho.kutemana na mwanandoa mwenzangu..
 
Unapinga ndoa then unapromote nini? Ushoga au unapinga ndoa na huna suluhu yake?

Kweli ndoa sio kwa kila mtu lakini usije na mabango yako hapa kupinga kusudi la Mungu, unataka tuwe na kizazi gani kisicho na wazazi wote wa kuwalea?
 
Unapinga ndoa then unapromote nini? Ushoga au unapinga ndoa na huna suluhu yake?

Kweli ndoa sio kwa kila mtu lakini usije na mabango yako hapa kupinga kusudi la Mungu, unataka tuwe na kizazi gani kisicho na wazazi wote wa kuwalea?
😅
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…