MJADALA: Kwanini Padri Luther aliondoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia, na kwanini alijiondoa kanisa Katoliki?

MJADALA: Kwanini Padri Luther aliondoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia, na kwanini alijiondoa kanisa Katoliki?

KWANINI PADRE Luther ALIFUKUZWA KANISA KATOLIKI? NA KWANINI ALIONDOA BAADHI YA VITABU KWENYE BIBLIA AGANO LA KALE?

Padre Luther alikuwa miongoni mwa Mapdre wenye karama nyingi ndani ya Kanisa katoliki wakati wake, Yeye alikuwa na Madai mengi sana juu ya mapungufu kwa kanisa. Hata hivyo madai yake mengi hayakuwa na msingi wowote.

Moja ya madai yake ilikuwa ni kuondoa kibali cha kwamba baada ya kuungama muumini asipewe stakabadhi ya kuonesha ameungama kwa kuwa kitubio ni siri ya MTU. Hili lilifanyiwa kazi. Mengine ikiwemo kurekebisha mfumo WA sala ya Kanuni ya Imani. Na mambo mengine mengi ambayo alipojibiwa, yeye hakuridhika pamoja na kueleweshwa vya kutosha. Alikuwa ni Great Thinker sana.


Mbaya zaidi alipokuja kusababisha mpaka akajitenga na kanisa ni kitendo cha kuondoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia ikiwemo pia kupunguza baadhi ya mistari kwenye vitabu kama cha Esta na Cha Danieli.
Aliondoa vitabu vya Deutrokanoni na vingine baadhi na kuwa jumla ya vitabu 7 vilivyotolewa kwenye Biblia. Na kila kitabu alikuwa na sababu yake aliyoibainisha. Kimsingi alipata wafuasi wengi WA kumuunga mkono hoja yake hasa wale ambao walikuwa wanatafta njia ya kuchuma pesa kiulaini. Na hapo Biblia mpya ilianza yenye Vitabu pungufu.

Na ndio maana Leo watu hawaujui Ukristo vizuri na wanakinzana bila kujua historia ya kanisa. Watumishi wengi WA Mungu hasa HAWA WA kileo wasiojua historia vizuri wao kila kitu wanapinga. Sio kosa lao Bali ni kosa la kutokujua historia ya kanisa.
Matumizi ya Ubani yalipingwa sana, na hapa ilikuwa ni kuondoa idadi ya waelewa. Kutokana na watu wengi walikuwa wamegeuka kama waganga kila mapepo ya kiwakabili walitumia ubani kuyafukuza na yalikimbia, lakini watu walijisahau kusali na kuomba na hata kufika ibadani ikawa nadra maana wanajua kujiponya kuondokana na majini na wachawi. Hapa Padre Luther na wenzake wakapiga marufuku matumizi ya ubani na kuwa sihi wakazanie Neno zaidi.

Hapa walichotakiwa kufanya ni kuliishi Neno la Mungu na wakati WA ibada basi ubani uchomwe kama Mungu alivyo agiza.
Luther na wenzake lengo lao lilikuwa ni biashara hapo baadae na kimsingi mpango huo ulifanikiwa. Na ndio maana mpaka Leo watu wametawaliwa na mfumo WA majini katika maisha yao kwa kuwa wamefungwa akili ya kujitambua na wanaamini maneno ya mdomoni na sio Maandiko ya Biblia kama yanavyosema.
Nimengi ya kujifunza sana Leo hii lakini kwa Leo naishia hapa.

deogratius Nalimi Kisandu.
1. 1. 2017.
 
Ndio maana sala zote za kikatoliki mwisho tunamalizia "tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu amen"

Kaka unajua kila siku huwa tunawaambia kuwa, wawe wanasoma Biblia na kujaribu kuitafakari kila andiko lina maana gani, pili wanatakiwa kujifunza sana kwa nini wenye Biblia (Wakatoliki) wanafanya hiki au kile na wao hawakifanyi

Shida kubwa ya hawa jamaa ni ya kumfanya Mungu hana uwezo, yaani wanampa Mungu mipaka, wanafanya dhambi kubwa sana kwenye hilo

Musa alikufa na Kuzikwa kabla ya kuingia nchi ya ahadi, lakini pale mlimani Yesu alikuwa na Musa, huyo Musa alitokea wapi? Eliya alipaa kwenda Mbinguni huku Elisha akishuhudia, Pale Mlimani Elia aliyokea wapi? Hao sio watakatifu? Na wale watakatifu wanaofanya maombi (kwenye ufunuo) wanatokea wapi?

Lakini pia, baada ya Saul kufail kila kitu alienda kwa mganga kumuomba ampandishie Samwel, je Samwel alipandishwa?, Alipandishwa kutoka wapi?, je Samwel aliongea mambo ya ukweli au uongo? Kama Mganga aliweza kumtoa Samwel alipo na kuongea nae, iweje watu wa Mungu wasiweze? Hivi kweli watu wa Mungu hatuna Nyoka kama wa Moses atakae weza kumeza nyoka wa Farao?
 
Kaka unajua kila siku huwa tunawaambia kuwa, wawe wanasoma Biblia na kujaribu kuitafakari kila andiko lina maana gani, pili wanatakiwa kujifunza sana kwa nini wenye Biblia (Wakatoliki) wanafanya hiki au kile na wao hawakifanyi

Shida kubwa ya hawa jamaa ni ya kumfanya Mungu hana uwezo, yaani wanampa Mungu mipaka, wanafanya dhambi kubwa sana kwenye hilo

Musa alikufa na Kuzikwa kabla ya kuingia nchi ya ahadi, lakini pale mlimani Yesu alikuwa na Musa, huyo Musa alitokea wapi? Eliya alipaa kwenda Mbinguni huku Elisha akishuhudia, Pale Mlimani Elia aliyokea wapi? Hao sio watakatifu? Na wale watakatifu wanaofanya maombi (kwenye ufunuo) wanatokea wapi?

Lakini pia, baada ya Saul kufail kila kitu alienda kwa mganga kumuomba ampandishie Samwel, je Samwel alipandishwa?, Alipandishwa kutoka wapi?, je Samwel aliongea mambo ya ukweli au uongo? Kama Mganga aliweza kumtoa Samwel alipo na kuongea nae, iweje watu wa Mungu wasiweze? Hivi kweli watu wa Mungu hatuna Nyoka kama wa Moses atakae weza kumeza nyoka wa Farao?
Mkuu na wewe umeanza kua mfia dini [emoji3] [emoji3] [emoji3]

Haya mambo ni magumu sn kila upande unavutia kwake.....


Kwa mfano unasema wenye biblia.... Hapa unaniacha hoi kua hawa wenye biblia walipewa na nani hiyo biblia???


Hoja yako kwamba watakatifu wanatuombea umekusudua kusema nini hapa mkuu??? Kwamba twaweza kuomba kupitia Mama Mariamu??
 
Ntuzu,

Kaka Mambo ya dini sio Magumu ni watu kuwa wagumu wa kuelewa na wengi hawampi Roho Mtakatifu muda wa kuwafunulia maandiko na Wachungaji na Wainjilisti ndio wanakuwa kila kitu

Kuhusu Bikira Maria, hiyo ni Habari kubwa na sio ya mchezo mchezo,
Kiimani ya Kikatoliki Yesu ni Neno la Mungu nae pia ni Mungu, na Kimaandiko sisi wote ni wakosefu kwa maana tuna dhambi ile ya kurithi, ile laana waliopewa Adam na Hawa mpaka leo tunayo, Mungu akalifanya Neno lake lije Duniani kuwakomboa wanadamu kwenye ile laana iliyotoka kwenye Mti wa katikati kupitia mti wa Msalaba
Yesu kama Mungu alikuwa hawezi kuja kupitia binadamu mwenye dhambi, Hivyo Bikira Maria alikingwa na ile dhambi ya ya Urithi, alikuwa PURE AND FRESH
Malaika Gabriel anatumwa kwa Mungu na anampa Maria ujumbe huu, kwamba MARIA AMEJAA NEEMA, BWANA YUKO NA WEWE NA UMEBARIKIWA KULIKO WANAWAKE WOTE, Pia hiyo Mimba itakuwa ni kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, So Maria ndio Binadamu wa kwanza Duniani kuzipokea nafsi zote tatu za Mungu, BABA, MWANA NA ROHO MTAKATIFU

Baada ya Malaika Gabriel kumwacha Maria, Bikira Maria hakuwa wa Dunia hii tena, alikuwa anatembea na Nafsi zote tatu za Mungu, na alikuwa kwenye Dunia ya Kiroho, Dunia ya watakatifu kwani alikuwa na Mwana wa Mungu ndani yake kwa Uwezo wa Roho mtakatifu

Alipofika kwa Elizabeth na kumsalimia, Yohana aliruka ndani ya tumbo la Elizabeth na Elizabeth alijazwa roho mtakatifu hapohapo Maria hakuwa mtu wa kawaida, na Eliza akijazwa na Roho mtakatifu akajikuta ananena kuwa MARIA WEWE UMEBARIKIWA KULIKO WANAWAKE WOTE

Nae Maria akiwa kwenye utakatifu wake Akasema Luka 1:48- vizizi vyote vitaniita MBARIKIWA

Na kwenye kitabu cha ufunuo kinaonyesha ni kwa jinsi gani Shetani akupenda mpango wa Mungu wa mkombozi kuzaliwa,
Na ishara kubwa ikaonekana Mbinguni, mwanamke mwenye mImba , mwanamke ALIYEVIKWA JUA NA MWEZI UKIWA MIGUUNI MWAKE, anataka kujifungua, na Shetani (Joka) anajitahidi kwa nguvu zote azuie mwokozi asizaliwe
Kasome Ufunuo 11:19 na 12:1-6 kwa habari kamili

Lakini pamoja na hayo yote, kwa Wakatoliki, BIKIRA MARIA SIO MUNGU, BIKIRA MARIA HAWEZI KUSAMEHE DHAMBI, BIKIRA MARIA HAWEZI KUOKOA MTU

KIKATOLIKI BIKIRA MARIA NI KAMA DARAJA LA KUTUUNGANISHA NA MWANAE (Yesu Kristo)
Nitaelezea baadae kivipi?
 
Yaani ulivyotaja mambo ya kupiga pesa tu kwa enzi hizo... Nimeshia kusoma hapo... Heri ya Mwaka mpya 2017
 
Ukiona mtu ambaye huwezi kumdanganya kirahisi unamwogopa.Unachagua watu wepesi wa kupotosha.
Hili ni jukwaa huru,ukileta mada mezani inachambuliwa na yeyote.Kama hujiamini kaa kimya kabisa.

Ikiwa mnapenda kujadili kwa kina mambo ya ndani ya Biblia nendeni mkasome Katika vyuo vya Biblia ndipo mtaandika habari za usahihi.

Luther alitafsiri Biblia sio kwa kibiashara bali alihoji kwa nini Neno la Mungu libakie katika lugha wasioielewa watu wengi? Aliwapa Wajerumani Biblia katika lugha Yao. Hakupunguza kitu kutoka Hebrew Old Testament na Greek New Testament alivyotumia Kama Source Text.

Sana aliongeza vitabu vya Apokrifa vile 6 vilivyokuwemo katika Latin Vulgate. Unaposema deutero-canonical unaelewa una maana gani? Unasema kusoma Historia ya Kanisa? Sema soma Biblical Studies, sema soma Historical Criticism ya vitabu vya Biblia, sema soma Textual Criticism ya hayo Maandiko. Sema soma Canonical texts za Biblia. Hapo ndipo utaelewa mengi kuhusu Maandiko ya Biblia.

Luther si mfanya biashara. Luther ni msomi aliyebobea katika Theolojia na kuona mapungufu na makengeufu ya Kanisa na kudiriki kusema. Luther aligundua kuwa wokovu ni kwa Imani na si kwa matendo ya kidini ama kazi za mtu. Unasema nini juu ya Luther Mwana mageuzi mkubwa alienusuru Imani sahihi ya kanisa kwa enzi hizo. Acha kabisa!!!! Nimedanganya nini hapo?
 
Hivi we kiumbe unaijua historia kweli wewe..? Au bwabwaja tu hapa?
Historia gani nisiyoijua? Ya Kanisa? Ya kipindi gani? Ancient? Medieval? Au Modern? Ama intertestamental times? Ipi? Kwa kuwa nimenena ya Luther tofauti na mtazamo wako? Nilijibu mwingine kabisa naye hajanijibu bado. Unajua kilichotokea Katika ngazi wakati Luther anapanda kwa magoti kwenda kwa Papa? Unajua andiko la Biblia mbalo lilimjia Luther likamwinua pale na akarudi kwake na usiku huo akapost hoja 95 langoni? Andiko hilo hilo ndilo lililomwongoza hadi wokovu John Wesley akaokoka pale Kanisani Adelsgate akaachana na the Church of England. Unazifahamu hizo hoja 95?
 
Maelezo yana virutubisho vya kila namna .

Sijapanga kukosa muendelezo wa maelezo yako

Kaka nitaeleza na nitakuquote,
Haya ndio wanayoyakosa,
Dhambi ilikuja kwa kupitia Mwanamke na mti, na lazima itolewe kupitia Mwanamke na mti
 
kha wew jamaa mbona mbishi hata kwa mambo usiyo yajua? Anglikana haitumii biblia sawa ma wakatoliki, anglikana inatumia biblia sawa na wa protestant wenzake, narudia tena am Anglican na ni muumini mzuri wa miaka mingi nimeshiriki semina makomgamano na mafunzo mbali mbali ya kanisa biblia tinayotumia ni sawa na wapentekoste kama hujui kaa kimya, u ar not Anglican halaf wanglikana tunakwambia unabisha, endeleeni kumezeshwa mivifungu iliyotengenezwa na watu
Wewe si Anglican. Anglican high church hawana tofauti na Catholic Church. Wanasali Rozali na wanapiga ishara ya msalaba. Mtu anayesali High Church hawezi zubaa kwenye misa za Catholic Church sababu vitu vingi vinaendana and vice versa.

Jaribu kufuatilia vizuri kuliko kuongea vitu visivyokua na ukweli
 
Deogratius Kisandu Kasome historia hujui unachoandika umekariri imani ya kirumi
 
Soma kitabu cha ufunuo. Shida hua mnakaririshwa mstari mmoja bila kujua kuna mstari mwingine unapinga ulichokariri
Leta vifungu acha kukariri yasiyokuwepo ni kifungu gani ktk ufunuo kupalizwa kwa Bikira maria?
Kwani yeye ni Ufunuo mpaka aandikwe kwa namna ya Ufunuo?

Mkuu Ufunuo umefunua machache yaliyopita na mengi yajayo mipango ya Mungu kwa mwanadamu Duniani
 
Kwa nini hakumsihi kurudisha na vile vya agano la kale? Je ni kweli kuhusu kununua cheti cha msamaha wa dhambi hayo yana fanyika ndani ya kanisa? Pamoja na kumtumia Maria katika kupitishia maombi kwa nini Abraham naye asitumiwe? Au si mtakatifu?

Na washawasha!


Historia ya Biblia ni kuwa ni Kitabu kilichotengenezwa na Kanisa Katoliki na kukamilika mwaka 300 Ad...Ilikamilika ilkiwa na vitabu 72/73 ila baadae Martni Luther aliondoa vitabu 7 na kubakiwa na vitabu 66.,
Hakuishia hapo, aliondoa vitabu 3 vya Agano jipya....Biblia ya Martin Luther ilikuwa na vitabu 39 vya Agano La Kale na Vitabu 24 vya Agano jipya..

Reformer mwenzake Calvin ndiye aliyemsihi kuvirudisha vitabu 3 ya Agano jipya..
 
suala la kumuabudu Maria na kuendelea kumuita bikira wakati alikuwa na watoto na Yusufu hunishangaza sana.
 
Back
Top Bottom