MJADALA: Kwanini Padri Luther aliondoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia, na kwanini alijiondoa kanisa Katoliki?

MJADALA: Kwanini Padri Luther aliondoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia, na kwanini alijiondoa kanisa Katoliki?

Ngoja nifuatilie kimyakimya labda nitajifunza kitu, vinginevyo kama sielewi vile!
 
kuna mambo luther hakuwa sahihi. ila mengi alikuwa sahihi. kuna vitabu alikuwa sahihi kutoa na vingine hakuwa sahihi. hatupaswi kuangalia in black and white.
Nataka uniambie mamlaka hayo yakutoa vitabu kwenye Biblia ukiyokamilika, yenye pumzi ya Mungu alipata mamlaka hayo wapi...???
 
Suala sio ubinadamu, hata yesu alikua binadamu ,binadamu wote walikufa no watakufa ila utofauti ni aina ya vifo vyetu, yesu alikufa ila kifo chake kilikua si kifo kama cha binadamu wengine, mama Maria na yy alikufa ila kifo chake naye hakikua kama cha watu wengine (kwa kukuhakikishia katafute kaburi au ulizia kaburi lake kama utakaa ulione)
kwanza, Yesu hakuwa binadamu
Pili, biblia inatumika kama nyenzo ya ushahidi kuwa alifufuka na sasa yupo hai.
Tatu, Nauliza ni wapi biblia imeeleza kwamba Maria alipaa na yupo hai mpaka sasa?
Nne, ni wapi biblia imetutaka tumtumie Mariam kama muombezi wetu?
 
Mkuu hayo maandiko usiyatafsiri kwa akili zako na utashi wako! Neno la Mungu lina pumzi ya Mungu ndani yake,hivyo unaposoma neno bila kuwa au kuongozwa na roho mtakatifu ambaye ndo huwa anayafunua na kuyadadavua hayo maandiko utajikuta unalibeba andiko kama lilivyo bila kufahamu linamaanisha nini,Naomba nikukosoe kbsa kwmba warumi (roman) ndio walio waua hao mitume walio kuwa wanasambaza injili ya Yesu kristo alie hai,ndo maana petro alipokamatwa na warumi walitaka kumsulubisha kama yesu lakini yeye akakataa akasulubishwa kichwa chini miguu juu msalabani na wakati kasulubishwa aliendelea kuwahubiria habari njema ya wokovu,sasa nashangaa unanambia ye ndo kaanzisha u katoliki,how?? na nyie warumi ndo mlimtesa??? haya mtume mwningne ni paulo yeye alikatwa kichwa na warumi ili asiendelee kueneza injili!! Hv maandiko huwa hamyaoni??? kama Yesu ndo muanzilishi wa ukatoliki au petro mbona mafundisho yao hamyabebi na kuyatekeleza??? Ni kwann mnabatiza watt wadogo??? wachanga??? na akati mitume wote walipokuwa wanaeneza injili walisema tubuni mkabatizwe katika Jina la Yesu,hata Yesu pia alibatizwa akiwa mtu mzima na baada ya ubatizo akaanza kueneza injili,sasa hao watt mnaowabatiza mnatoa kwnye andiko gani hayo mamlaka ya kubatiza watt wadogo?? je watt wadogo wana dhambi hata watubishwe ndo muwabatize??? maana kutubu ni kujutia na kutamka kwa ukiri lakini nyie hata hao watt wengine hata kuongea hawawezi na hawana ufahamu wa mabaya na mema,then useme kanisa katoliki lilianzishwa na Yesu?? au Petro?? how kwnza Yesu hakuja kuleta madhehebu wala dini.,nna mengi ya kuongea lakini ngoja niishie hapo
nakuunga mkono mkuu.siku wakiufahamu ukweli watakuwa huru kama mimi ambavyo niko huru sasa.i hope waujue ukweli before its too late.
 
Kaka Mambo ya dini sio Magumu ni watu kuwa wagumu wa kuelewa na wengi hawampi Roho Mtakatifu muda wa kuwafunulia maandiko na Wachungaji na Wainjilisti ndio wanakuwa kila kitu

Kuhusu Bikira Maria, hiyo ni Habari kubwa na sio ya mchezo mchezo,
Kiimani ya Kikatoliki Yesu ni Neno la Mungu nae pia ni Mungu, na Kimaandiko sisi wote ni wakosefu kwa maana tuna dhambi ile ya kurithi, ile laana waliopewa Adam na Hawa mpaka leo tunayo, Mungu akalifanya Neno lake lije Duniani kuwakomboa wanadamu kwenye ile laana iliyotoka kwenye Mti wa katikati kupitia mti wa Msalaba
Yesu kama Mungu alikuwa hawezi kuja kupitia binadamu mwenye dhambi, Hivyo Bikira Maria alikingwa na ile dhambi ya ya Urithi, alikuwa PURE AND FRESH
Malaika Gabriel anatumwa kwa Mungu na anampa Maria ujumbe huu, kwamba MARIA AMEJAA NEEMA, BWANA YUKO NA WEWE NA UMEBARIKIWA KULIKO WANAWAKE WOTE, Pia hiyo Mimba itakuwa ni kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, So Maria ndio Binadamu wa kwanza Duniani kuzipokea nafsi zote tatu za Mungu, BABA, MWANA NA ROHO MTAKATIFU

Baada ya Malaika Gabriel kumwacha Maria, Bikira Maria hakuwa wa Dunia hii tena, alikuwa anatembea na Nafsi zote tatu za Mungu, na alikuwa kwenye Dunia ya Kiroho, Dunia ya watakatifu kwani alikuwa na Mwana wa Mungu ndani yake kwa Uwezo wa Roho mtakatifu

Alipofika kwa Elizabeth na kumsalimia, Yohana aliruka ndani ya tumbo la Elizabeth na Elizabeth alijazwa roho mtakatifu hapohapo Maria hakuwa mtu wa kawaida, na Eliza akijazwa na Roho mtakatifu akajikuta ananena kuwa MARIA WEWE UMEBARIKIWA KULIKO WANAWAKE WOTE

Nae Maria akiwa kwenye utakatifu wake Akasema Luka 1:48- vizizi vyote vitaniita MBARIKIWA

Na kwenye kitabu cha ufunuo kinaonyesha ni kwa jinsi gani Shetani akupenda mpango wa Mungu wa mkombozi kuzaliwa,
Na ishara kubwa ikaonekana Mbinguni, mwanamke mwenye mImba , mwanamke ALIYEVIKWA JUA NA MWEZI UKIWA MIGUUNI MWAKE, anataka kujifungua, na Shetani (Joka) anajitahidi kwa nguvu zote azuie mwokozi asizaliwe
Kasome Ufunuo 11:19 na 12:1-6 kwa habari kamili

Lakini pamoja na hayo yote, kwa Wakatoliki, BIKIRA MARIA SIO MUNGU, BIKIRA MARIA HAWEZI KUSAMEHE DHAMBI, BIKIRA MARIA HAWEZI KUOKOA MTU

KIKATOLIKI BIKIRA MARIA NI KAMA DARAJA LA KUTUUNGANISHA NA MWANAE (Yesu Kristo)
Nitaelezea baadae kivipi?
Umesahau na yale makabidhiano ya Yesu na Yohana pale msalabani..."Mama tazama mwanao na Yohana tazama mamaako" halafu watafakari kazi ya mama nini kama sio ku harmonize kati ya baba na Mtoto.
 
Samahani mkuu, naomba nipe andiko linalosema Mungu aliruhusu matumizi ya ubani, please
 
Ukienda kwenye lugha ya Kiingereza inaeleza kwa uwazi zaidi:

54. And when he was come into his own Country,he taught them in their synagogue.....
55. Is not this the Carpenter's son?is not his mother called Mary?and his brethren James, and Josef, and Simon, and Judas?
56. And his sisters, are they not all with us?....

Walishangaa kwa sababu kwa macho ya kibinadamu hakukuwa na tofauti kati ya familia zao na familia ya Yusufu waliyemtambua kama ndiye Baba yake Yesu.

Kama walivyokuwa wao na watoto wengi wenye tabia tofauti ndivyo familia ya Yusufu ilivyokuwa.Ila walimshangaa mtoto Yesu kapata wapi ufahamu mkubwa hivyo?

Yohana 7:2-5 inatuambia pia juu ya kaka zake Yesu na inaenda mbali zaidi kwa kutuambia pia kuwa sio watu wa Galilaya peke yao bali ata kaka zake Yesu pia hawakumuamini Yesu kuwa ni Kristo.
Unajua maana ya brethren na brother, unaweza kuzitofautisha na maneno sibling na blood brother......nway Amini unacho Amini...atlast tubaki watanzania.
 
Samahani mkuu, naomba nipe andiko linalosema Mungu aliruhusu matumizi ya ubani, please
Soma kitabu cha zaburi pale Daudi anapomtolea Mungu Sadaka kisha kusema "Sala yangu na Ipae mbele zako kama moshi wa Ubani..."

Pia ukisoma Kitabu cha Ufunuo utaona..
"Malaika Mtakatifu kasimama kando ya Altare/madhabahu akiwa ameshika mkononi chetezo cha dhahabu..."
 
Tunaziombea roho za marehemu wote zipate rehema kwa Mungu zipumzike kwa amani.....
Asee!! asa kuna maana gani ya nyie kumuita Yesu mwokozi wenu??? kama mnauwezo wa kuombea hadi marehemu akasehewa??? Huyo marehemu wakati wakiwa wazima hawakusikia injili ya wokovu na wakasadiki?? Mnapotezea muda someni biblia vzuri jaman,Mtu akishafuka ni hukumu tu,huwezi kubatilisha shauri la Mungu juu ya mwanadamu aliekufa eti asamehewe?? Wokovu ni njia pekee ya sisi kuungana na Yesu kristo na kutengeneza njia zetu na kutubu na kumpokea kuwa Bwana na mokozi wa maisha yetu,hivyo mtu hawezi kwenda mbinguni bila kupitia kwake!! na je unapitiaje kwake bila wokovu??? Mtu akifa hakuna kutubu tena huko ni hukumu tu,ndo maana mkristo unatakiwa kutengeneza njia zako ukiwa hai!! maana ukifa na yako yamekwisha huko ni hukumu tu, Wakatoliki jaman mtahukumiwa kwa neno,mnaombeaje wafu wapate rehema wao wakati wakiwa wazima walishindwa kuomba toba na kutubu??? inamaana hawakulisikia neno??? Kiukwl ni mara 1000 uwe tu mpagani kuliko kuwa mfuasi wa kristo usiyeyajua maandiko kama ww ndugu.!!Mungu wa mbingu na nchi akupe neema ya kuitambua kweli nayo ikuweke huru na vifungo vya fikra.
 
Kanisa katoliki wanamuhitaji Mungu kwakwl na ndo mana wengi wanaoelewa neno huwa wanakimbia,Japo sijawahi kuwa mkatoliki lakini naskia ukifa siku ya kuzikwa padri akikuombea rehema basi unasamehewa makosa yako! Na pia mama maria ndo anawaombea wakatoliki,pia ndo dhehebu pekee ambalo pombe imehalalishwa!! Mungu atusaidie sana
Usililolijua ni sawa na ucku wa giza
 
Wewe ndio wa kusoma Biblia vizuri....Biblia ipo wazi kabisa...Marehemu wanaombewa vizuri kabisa...Kitabu cha Wamakabayo kipo wazi mbona
Anhaa ok nafkiri Biblia yenu ni tofauti na yetu tunayoitumia hii ya vitabu 66,anyway kumbe yapo maandiko yanayowa guide?? Basi mkuuu ngoja niishie hapo kwa leo
 
Nataka uniambie mamlaka hayo yakutoa vitabu kwenye Biblia ukiyokamilika, yenye pumzi ya Mungu alipata mamlaka hayo wapi...???
hayo ni makosa yake binafsi. ila kuna mengi alifanya vizuri sana. hata watumishi wa Mungu kama Musa na Daudi walifanya makosa.
 
Kwani kwenye harusi ya kana kinywaji kilipoisha, walimfuata nani ili awaombee kwa Yesu?, tatizo haya makanisa ya kilokole yanayoendeshwa na wachungaji ambao ni darasa la saba wanawapotosha, hawaijui biblia
Ushasema walikuwa harusini na mama na mwanae walikuwepo, walipomuomba mama amwombe mwanae ni kawaida kwa kimuono wa kibinadamu.
Je ni wapi katika Biblia tunaambiwa tukitaka kumuomba Mungu basi tupitie kwa mama maria?
 
Biblia inasema Bikra Maria ataitwa mbarikiwa, na dunia itamsifu kuwa yeye ni mbarikiwa. Bikra Maria kwa mujibu wa kumbukumbu za kanisha hakufa, alipaazwa. Ujui historia, huyu mama ni the special, hata waprotestant wakimtupa sisi Wakatoliki tutaendelea kutimiza unabii kwa kumuita mbarikiwa
Ingekuwa vyema ungeweka mistari ya Biblia inayoback up hicho ulichoandika.
 
Back
Top Bottom