MJADALA: Kwanini Padri Luther aliondoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia, na kwanini alijiondoa kanisa Katoliki?

MJADALA: Kwanini Padri Luther aliondoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia, na kwanini alijiondoa kanisa Katoliki?

9 Ni nini basi? Tu bora kuliko wengine? La! Hata kidogo. Kwa maana tumekwisha kuwashitaki Wayahudi na Wayunani ya kwamba pia wamekuwa chini ya dhambi;
10 kama ilivyoandikwa, ya kwamba, Hakuna mwenye haki hata mmoja.
11 Hakuna afahamuye; Hakuna amtafutaye Mungu.
12 Wote wamepotoka, wameoza wote pia; Hakuna mtenda mema, la! Hata mmoja.
fst,
 
MESHACK WARIOBA,
Kuna jambo huwa hatuelewi. Nalo ni elimu, uelewa na mazingira. Kuhusu dini wazungu wana elimu na uelewa mkubwa akilinganisha na wafrika.

Aidha, mazingira ya wazungu na wafrika yanatofautiana.

Kati ya mambo ambayo hupaswi kuyaelewa kama ni BINAFSI ni dini. Dini au imani sio jambo binafsi. Kuelewa hivi ni kazi bure.

Kwa sababu hiyo, dini na kile inachokibeba ndio maisha yenyewe ya mwanadamu. Jambo la kujiuliza, hatahivyo, ni je, kwanini kuna dini au makanisa tofautitofuauti? Ni kweli Mungu alikusudia dini au makanisa tofautitofauti?

Aidha, dini inakuwaje jambo binafsi ikiwa watu ni uzao?
 
Martin alikuwa padre wa shirika la Mt. Agustino wakati wa kipindi cha Papa Leo.Anyways does God love Rebellion?

Ukihama kanisa sababu padre/mchungaji amekosea kosa ni la nani kama sio lako?

Kanisa ni la Padre/ mchungaji au ni la Mwenyezi Mungu? Mwanzo wa kosa moja ni Mwanzo wa makosa mengine kama unavyoona leo kila mtu anajifungulia kanisa lake na watu kupotea................
 
Kwanini Papa wa Kikatoloki alitoa amri Martine Luther auwawe na ahesabiwe kama mnyama?
Katoliki ni dhehebu la kishetani wanamwabudu mungu wa kipagani.

Ndio maana ukiwa Mkatoliki hurusiwi kuhoji wala nini unatakiwa kukubaliana na maelekezo ya miungu (Mapadri) Deogratius Kisandu,
 
Aidha, dini inakuwaje jambo binafsi ikiwa watu ni uzao?
Ndugu yangu, Je unaelewa maana ya neno BINAFSI? Kuamini unachoamini ni hiari yako mkuu..! Ndio maana unaweza kuamini unachochagua wewe? Ndio maana nikasema ni suala Binafsi, yaan linategemea na Uamuzi wako.

Ile kwamba Umezaliwa kwenye budhist, Muslim, Christianity haimaanishi kwamba huwezi hama kama utakuwa radhi na imani nyingine, ishu ipo kwa mtu binafsi, na ndio nikasema watu wanaogopwa kutengwa na jamii; of which kama uko commited naamini hakuna kutengwa na jamii isipokuwa unabadilisha jamaa kutoka uliokuwa nao Muslim, kwenda Budhist kama utakuwa umehamia huko.

Hivyo ni suala BINAFSI, uzao unatoa msingi tu;
 
Kwanini Papa wa Kikatoloki alitoa amri Martine Ruther auwawe na ahesabiwe kama mnyama?
Katoliki ni dhehebu la kishetani wanamwabudu mungu wa kipagani.
Ndio maana ukiwa Mkatoliki hurusiwi kuhoji wala nini unatakiwa kukubaliana na maelekezo ya miungu (Mapadri)
Ndugu yangu unaongea kwa kashfa sana na si Ustaarabu;
Lakini pia nadhani Hufahamu Historia Vizuri, Katika masuala ya Denomination za Christianity, Wakatoliki ndio watu wametoa mwanga kwenye Denomination unazozijuwa zote, wao walifanya toka Karne ya kwanza wakiwa wanaitwa Warumi.

Kama umesoma History ya Church utaona kwamba Walikuwa wakibadilika Karne hata Karne; hayo mambo unayosema inawezekana hawakupatika watu wa kuyaweka sawa Mapema.

Watu wengi tunaishia kusoma Bible pekee, bila kufahamu Historia ya Kanisa Duniani; Ukisoma Historia ya Kanisa utagundua Dini kuu mbuli Christian na Muslim zilifanya mauaji sana Kulazimisha watu wa enzi hizo Kufuata Imani yao; Hivyo hakuna Dini ambayo haikupitia Mfumo Fulani;

Mimi si mkatoliki lakini kutumia Maneno ya kashfa kwenye imani za watu si sawa. Kama Mungu alivyochagua Israel, lakini wengi wao wamekataa kuchaguliwa, Ndivyo ilivyo Katoliki, Denomination zote zimetokea hapo.
 
Mtabishana sana, bado itabaki historia iliyosimuliwa na waliosimulia ni vizuri kusoma kwani inawakilisha walichokiamini lakini pia ni wajibu wetu kutafuta ukweli katika walichokiamini. Tu kamili kama wao, waliwezaje sisi tushindwe kwani tumaumbo kamili yalioumbwa na Mungu,

hivyo basi tuko na Mungu ndani yetu na hatuhitaji simulizi wala maandishi kuthibitisha hilo. KABLA YA KUTAFUTA NA KUJUA MUNGU NI NANI? HEBU TUANZE KUTAFUTA SISI WA UKWELI TUKOJE? ( The true self) Kwani TUMEUMBWA KWA MFANO WA MUNGU. TUKIIJUA NAFSI YETU YA KWELI TUTAJUA NJIA YA UKWELI YA UHAI NA MAISHA YETU tutaacha kubishania masimulizi ya vitabuni. YOH: 4: 23 -24

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtoa post nimpotoshaji mkubwa ningekuona ningekuhukumu kwa Sheria ya Mussa kukufungia jiwe jiwe la kilo 70 shingoni nakukutumbukiza baharini.

Sasa nakujibu Mnamo mwaka 333 kabla ya kuzaliwa Yesu nchi ya Palestina (Israeli) ilitawaliwa ns Wagiriki.Iliopopita miaka 70 yaani mwaka 403 Ndipo ilitolewa tafsiri ya kwanza ya torati na vitabu vya manabii katika lugha ya Kiyunani(Kigiriki).

Tafsiri hiyo iliitwa SEPTUAGINT,viliingizwa vitabu 11 ambavyo havikuwa katika orodha rasmi ya maandiko matakatifu ya Wayaudi wa Parestina.Vitabu hivyo vya nyongeza vilikuwa vimetafsiriwa kuanzia mwaka wa 363 ikiwa nimiaka 30 wa utawala wa Kagiriki na vilitokea Iskanderia (Alexanderia) ambavyo vilikuwa vikitumiwa na watu waliojiita Wayahudi.Kuingizwa vitabu hivyo kwenye SEPTUAGINT kulifanya Wayahudi waitishe mkutano mkuu wa wazee 70 wa Palestina.

Kikao kile kilijadili suala la maandiko ya Iskanderia yasiyokuwa matakatifu kuingizwa kwenye SEPTUAGINT ya Palestina.

Kikao hicho kijulikanacho kwa jina la Canon na ndicho kilichoviondoa vitabu 11 vya Iskanderia nakuvithibitisha kuwa ni batili.

Swari apo Martine Ruther alikua ameishazaliwa?
Kwamujibu wa maelezo ya Padre J.Bouguet des Chaux mwandishi wa kitabu cha JIFUNZE BIBLIA TAKATIFU,mnano karne ya 5 baada ya Yesu Kristo yahani karibu miaka 700 ya mkutano mkuu Canon,Papa Augustno aliamua aliamua kuongeza vitabu 6 kati ya vile 11 vya Iskanderia vilivyoondolewa na wazee 70 katika agano la kale.

Miaka 1,000 baadaye (1546) uamuzi wa Papa Augustino ulipata kibali rasmi kwenye mkutano mkuu wa Maaskofu wa kanisa Katoliki mjini trent-Uingereza bila kuwashirikisha wale wazee sabini wa Kipalestina.Lakini wale wazee hawakukata tamaa kufuatia matengenezo ya kanisa (Reformation) Vitabu hiyvo viliondolewa tena na ndipo palipotokea mpasuko wa Kiprotestanti ambao hadi leo wanaitambua orodha rasmi ya vitabu vya Wayahudi wa Palestina tu nakuvichukulia vile 6 viloongeza na Papa Austino kuwa ni batili.

Kwakumbukumbu sahii kati ya mwaka 93 hadi 130 baada ya Yesu viliandikwa vitabu vingine vingi ambavyo navyo vilionekana batili .kimojawapo kilifahamika kwa jina la Protevangelium, nyaraka za Clement,Iginatius,na Polycarp ambavyo vyote havikuruhusiwa kuingizwa ata kama maandiko kadhaa yalifanana na nyaraka sahii za Biblia lakini havikuwa maandiko matakatifu kwamaana tuipotayo 2Petro1:20-21.

Kwahiyo Martine Ruther alisimamia alichokikuta siokweli kwamba alifukuzwa kwasababu ya kuondoa maandiko matakatifu.Wakatoliki kwa hofu yakupinduliwa waliongeza vitabu hivyo vya sheria zao ambavyo mpaka leo Makasisi Mapadre,Maaskofu Makardinal na Papa wanajua hili na ndonapaswa kuulizia kwanini wanaendelea kushikilia vitabu batili wakijua kuwa sio sahii?

Mwisho:Tafuta kitabu kiitwacho Je nabii issa ndiye YESU KRISTO? na kingine kiitwacho Jifunze Biblia Takatifu
Usome kwa faida ya ubongo wako.
Kwahiyo hivyo vitabu unavyotaka tukavisome vimeshushwa au vimeandikwa na wanadamu kama Mimi na wewe,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii makala au riwaya ina walakini mwingi na haina mantiki kabisa! Mwandishi anapaswa kujua kuwa Bibilia haikuandikwa na mtu mmoja,na ilikuwa kazi ya watu wengi mno kutafisiri lugha ya michoro ya zamani ili kupata maana
Luther hakuwa na hoja yoyote na Bibilia as alikuja kuisoma Biblia ukubwani sana,wakati huo Wakatoliki walikuwa na Mithali/Misali za waumini ambayo ni kama Biblilia iliyochujwa sana,ni Bibilia halisi ndio ikimfungua Luther hadi akaona mistari inayosema kuwa kwa kupigwa kwake Yesu sisi tumesamehewa bure,qakati huo msamaha ulikuwa unatolewa kwa fedha! Unalipa ndio upate msahama
 
Hii makala au riwaya ina walakini mwingi na haina mantiki kabisa! Mwandishi anapaswa kujua kuwa Bibilia haikuandikwa na mtu mmoja,na ilikuwa kazi ya watu wengi mno kutafisiri lugha ya michoro ya zamani ili kupata maana
Luther hakuwa na hoja yoyote na Bibilia as alikuja kuisoma Biblia ukubwani sana,wakati huo Wakatoliki walikuwa na Mithali/Misali za waumini ambayo ni kama Biblilia iliyochujwa sana,ni Bibilia halisi ndio ikimfungua Luther hadi akaona mistari inayosema kuwa kwa kupigwa kwake Yesu sisi tumesamehewa bure,qakati huo msamaha ulikuwa unatolewa kwa fedha! Unalipa ndio upate msahama
Ndugu yangu baki kwenye siasa huku unapwaya sana. Waandishi wa vitabu vinavyounda Biblia ni wengi lakini unajua akina nani walichambua vitabu vyote wakaona hivyo unavyojua leo ndio vinastahili kuwekwa pamoja? Unajua injili zilikuwepo nyingi na sio nne tu unazoona leo?

Nani aliamua mpangilio wa hivyo vitabu? Kianze kipi, kifate kipi hadi ufunuo? Walitumia utaratibu upi kupata mpangilio? Unajua biblia unayotumia leo mpangilio wa chapters umewekwa mapema karne ya 13 na Askofu Steven Langton na chapters za bible zimewekwa kwa verses baadae kabisa! Zote hizi ni kazi za Kanisa Katoliki ambalo ndio lilisimamia michakato yote na kupitisha matumizi yake kwa waamini.

Usisahau kazi hii yote inafanyika hakuna makanisa ya kilokole zaidi ya Kanisa Katoliki ambalo baadae liligawanyika na kuzaliwa Orthodox church ambalo pia ni apostolic church.

Kanisa ni moja tu, ndio maana hutokaa usikie makanisa ya Katoliki maana Kristo hakusema atajenga makanisa yake bali atajenga Kanisa lake! Kanisa Katoliki! Ndio alama pekee ya kanisa la Kristo ulimwenguni tukiamini imani moja, ubatizo mmoja na mchungaji mmoja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wakishashiba makande bwana, watataka kutunisha matumbo yao ili watu waone la nani ni kubwa kama wale jamaa zangu wa Ethiopia wanaotembea chululu zipo nje!😂😂

All in all dini zilikuja kwa mashua tu, kinachopaswa kufuatwa ni imani thabiti ya mtu.. ukimwamini Mungu, ukaacha uovu, inatosha hayo mengine tuwaachie Wajerumani na Waitaliano.
 
Watu wakishashiba makande bwana, watataka kutunisha matumbo yao ili watu waone la nani ni kubwa kama wale jamaa zangu wa Ethiopia wanaotembea chululu zipo nje![emoji23][emoji23]

All in all dini zilikuja kwa mashua tu, kinachopaswa kufuatwa ni imani thabiti ya mtu.. ukimwamini Mungu, ukaacha uovu, inatosha hayo mengine tuwaachie Wajerumani na Waitaliano.
Umetoa wapi hili fundisho? Au ndio umeamua kuamini unachotaka?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usisahau siasa ndio inaratibu maisha yetu ya kila siku
Hitimisho lako kuwa Biblia imeandikwa na Wakatoliki ni upotoshaji mkubwa.
Mosi.Bibilia ya kwanza inasadikiwa iliandikwa kwa lugha ya Armaic hii ni lugha ya eneo la Mashariki ya Kati pamoja na pembe ya Afrika,ni miongoni mwa lugha za kwanza kuandikwa zaidi ya miaka 4500 iliyopita
Pili.Ukiristo kwa ujumla wake umeanza miaka 2000 baada ya ufufuo wa Yesu Kristo na ndio wakati Agano la jipya,tafsiri yake ni kuwa Ukatoliki umeanza karne ya kwanza yaani baada ya Yesu kufufuka

Tatu.Dini ya kwanza ya iliyotimia Bibilia ni Judaism ambayo ilianza miaka mingi kabla ya Yesu


Ndugu yangu baki kwenye siasa huku unapwaya sana. Waandishi wa vitabu vinavyounda Biblia ni wengi lakini unajua akina nani walichambua vitabu vyote wakaona hivyo unavyojua leo ndio vinastahili kuwekwa pamoja? Unajua injili zilikuwepo nyingi na sio nne tu unazoona leo?

Nani aliamua mpangilio wa hivyo vitabu? Kianze kipi, kifate kipi hadi ufunuo? Walitumia utaratibu upi kupata mpangilio? Unajua biblia unayotumia leo mpangilio wa chapters umewekwa mapema karne ya 13 na Askofu Steven Langton na chapters za bible zimewekwa kwa verses baadae kabisa! Zote hizi ni kazi za Kanisa Katoliki ambalo ndio lilisimamia michakato yote na kupitisha matumizi yake kwa waamini.

Usisahau kazi hii yote inafanyika hakuna makanisa ya kilokole zaidi ya Kanisa Katoliki ambalo baadae liligawanyika na kuzaliwa Orthodox church ambalo pia ni apostolic church.

Kanisa ni moja tu, ndio maana hutokaa usikie makanisa ya Katoliki maana Kristo hakusema atajenga makanisa yake bali atajenga Kanisa lake! Kanisa Katoliki! Ndio alama pekee ya kanisa la Kristo ulimwenguni tukiamini imani moja, ubatizo mmoja na mchungaji mmoja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usisahau siasa ndio inaratibu maisha yetu ya kila siku
Hitimisho lako kuwa Biblia imeandikwa na Wakatoliki ni upotoshaji mkubwa.
Mosi.Bibilia ya kwanza inasadikiwa iliandikwa kwa lugha ya Armaic hii ni lugha ya eneo la Mashariki ya Kati pamoja na pembe ya Afrika,ni miongoni mwa lugha za kwanza kuandikwa zaidi ya miaka 4500 iliyopita
Pili.Ukiristo kwa ujumla wake umeanza miaka 2000 baada ya ufufuo wa Yesu Kristo na ndio wakati Agano la jipya,tafsiri yake ni kuwa Ukatoliki umeanza karne ya kwanza yaani baada ya Yesu kufufuka

Tatu.Dini ya kwanza ya iliyotimia Bibilia ni Judaism ambayo ilianza miaka mingi kabla ya Yesu
Kuna watu wanadanganya pia kuwa madhehebu yote yametoka kwenye ukatolik. Nadhani ndo wanavyodanganywa huko.
Ukweli ni kuwa ukatolik ukishirikiana na serikali ulikandamiza madhehebu mengine na kuwaua waumini wake , hivyo kupelekea kutokuabudu waziwazi
Na baada ya upinzani kutoka ndani yao wenyewe kwa wenyewe, ikashindikana kuthibitiana ndio madhehebu mengine yakaanza harakati zake waziwazi
Wakatolik hawakuandika biblia yoyote. Kwanza hawapendi watu wasome biblia kwa kuwa mambo mengi wanayofanya hayaendani nayo
 
Back
Top Bottom