Mjadala: Mbwana Samatta ndio mchezaji Bora wa muda wote Tanzania

Mjadala: Mbwana Samatta ndio mchezaji Bora wa muda wote Tanzania

Sasa Itakuwa mahakama hii,,, anyway machache katika mengi kuna wakati ilikuja timu ya taifa ya Ghana The Black Stars kucheza na taifa stars miaka ya 90 huko.... Hussein Aman Masha alikuwa ni kiungo wa kati siku hiyo....aliwadhibiti na kuwakimbiza nyota wa Ghana waliokuwa wakicheza huko ulaya..... mwishoni mwa gem .....wale jamaa waliuliza Masha anacheza timu gani huko ulaya??...wakidhani anakipiga majuu kwa kiwango alichoonyesha.....walipoambiwa anakipiga humu humu ndani,Simba Sport Club ....jamaa walichoka..
Mkuu kwa maelezo yako hata Humud aliwahi kumzibiti Yaya toure taifa stars ilivyocheza na Ivory coast,
Hizi story hazionyeshi records zozote
 
Mkuu kwa maelezo yako hata Humud aliwahi kumzibiti Yaya toure taifa stars ilivyocheza na Ivory coast,
Hizi story hazionyeshi records zozote
Tatizo soka la kibongo halina proper records lipo kwenye story kutoka kwa watu walioona kama kina sisi
 
Kwa mafanikio Mbwana Sammata anaweza kuongoza ila kwa vipaji tulikuwa navyo vingi ila ama milango ilikuwa haijafunguka kama sasa au upeo wa wachezaji ulikuwa mdogo wachezaji wetu wengi wa zamani walikuwa wanakimbilia uarabuni kwa wachezaji kama Mogella,Ramadhani lenny, Hamisi Gaga, husein Marsha kwa uchache walikuwa na uwezo mkubwa mtu kama gaga alikuwa anakimbia wajerumani wanataka akacheze ligi yao ila Mbwana alipata mwongozo mzuri wa baba yake ndio maana kafika hapo alipo
 
Hakuna ubishi yeye ndiye GOAT wa Tanzania kma sio ukanda wa Africa mashariki

Uwe na heshima unapozungumza. Mariga na Wanyama unawachukila vipi? Mmoja ni Champion League winner na mwengine ni EPL star, halafu unawafananisha na takataka? Tusitiane aibu.
 
Kwa mafanikio yes you maybe right..

Lakini kwa burudani ya soka uwanjani, aisee hapana...
Ni kweli kwa kigezo cha mafanikio nje ya nchi ni Samata, ila Kwa kujituma uwanjani na burudani ni Lunyamila.
 
Unahitaji kuwa mshirikina haswa kukataa kuwa Samatta ni bora kuliko wachezaji waliowahi cheza soka Tz,Tena uwe na roho ngumu kuliko jiwe kumfananisha na wengine,Labda uwe umelewa au unakoleza mjadala tu,
 
Kwa mafanikio Mbwana Sammata anaweza kuongoza ila kwa vipaji tulikuwa navyo vingi ila ama milango ilikuwa haijafunguka kama sasa au upeo wa wachezaji ulikuwa mdogo wachezaji wetu wengi wa zamani walikuwa wanakimbilia uarabuni kwa wachezaji kama Mogella,Ramadhani lenny, Hamisi Gaga, husein Marsha kwa uchache walikuwa na uwezo mkubwa mtu kama gaga alikuwa anakimbia wajerumani wanataka akacheze ligi yao ila Mbwana alipata mwongozo mzuri wa baba yake ndio maana kafika hapo alipo
Hakuna ambaye anakimbia hela,hata hiyo Zamani mnayoizungumzia kma wangekidhi vigezo wangechukuliwa tu wakacheze majuu,yaani mtu aende Uarabuni akimbie EPL ,Ujerumani
 
Mbona ume tumia kigezo cha taifa stars tu
Mbwana Samatta hajayafikia mafanikio ya kina Tenga na hata mafanikio ya kina Nsajigwa na kundi lake.
Ukweli uko hapa.
Kina Tenga na wenzake walicheza fainali za AFCON.
Kina Nsajigwa na wenzake walicheza fainali za CHAN na kubeba kombe la challenge
Huyu Samatta na wenzake hawajaleta hata kikombe cha chai
Usilinganishe watoto na wanaume.
 
Uefa gani kacheza boban mkuu?
Boban kacheza UEFA champions League ujue lakini tayari ana silver wear ya kombe la challenge unamlinganisha vipi na Mbwana Samatta ambaye hajafikia hivyo vitu
 
Hakuna ambaye anakimbia hela,hata hiyo Zamani mnayoizungumzia kma wangekidhi vigezo wangechukuliwa tu wakacheze majuu,yaani mtu aende Uarabuni akimbie EPL ,Ujerumani
Hawakuwa na uwezo was kuchezaji ulaya . Full stop
 
kuna jamaaa nimemchoka humu ndani eti anasema na challenge nalo ni kombe
 
Nashindwa kukataa Samatta sio bora kwa kuwa sina rekod ya mtu yeyote ambae ana mafanikio kuzidi ya Mbwana.
 
Back
Top Bottom