TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Bukoba Mjini

TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Bukoba Mjini

Waliingia choo cha kike wakakutana na usanii wa kuzungusha mikono. Wazee wa "mabadiriko" na sasa sijuhi hapo Bukoba kama kuna hata vidariri vya hayo "mabadiriko' waliyoyakimbilia pasipo kujua.

Lwaka ni bonge la msanii
Acheni propaganda uchwara. Huyo kagasheki alifanya kipi cha maana hapa bukoba mjini zaidi ya kila matanuzi, mtu ndege ya watu 13 anaikodi binafsi toka mwanza kuja hapa bukoba kila mara. Kwanza hakunaga mbunge anaefanyaga chochote Tanzania.Wote wanategemea miradi iliyopangwa na serikali. Kama bajeti ya miradi haijapita ktk Jimbo hata mbunge apige kelele vipi haisaidii maana bajeti za nchi hii ni ndogo na hazitekelezeki.
 
MAFANIKIO YALIYOFIKIWA KATIKA KIPAUMBELE CHA MIKOPO KWA WANAWAKE NA VIJANA

MATEGEMEO SACCOS (VIJANA)

1. Mpaka sasa vimekopeshwa vikundi 19 na vi3 vinasubili.

2. Marejesho yako vizuri kutokana na mikataba yao kuwa na mkazo mkubwa na faini kwa wazembe.

3. Pesa hiyo inakopeshwa kwa kipindi kisichozidi miezi sita unatakiwa kuwa umemaliza marejesho na riba ni 5% tu.

4. Changamoto ni kwamba pesa haipo ya kutosha kiasi kwamba wanachoomba vikundi hawapati kiasi sahihi kwa vile wanalazimika kuzigawagawa ili kuwapatia wote.

5. Mwezi January ndiyo mara ya mwisho *MATEGEMEO SACCOS* kupokea pesa za manispaa ili hali ilisemekana zitakuwa zikipelekwa kila mwezi.

6. Mwisho wameomba tuzidi kuhamasisha umma hasa vijana wafuate utaratibu wa vikundi ili wakapate mkopo uwasaidie kujikwamua.

WANAWAKE TUINUANE SACCOS.

Vikundi vilivyokwisha nufaika na mikopo ni 11 na vinavyotarajiwa kukopeshwa mwezi huu ni vi 3.

Pesa zilizokwishaelekezwa na manispaa kwa saccos hii ni jumla ya Tshs. 40,227,000/=.

Mara ya mwisho kupokea fedha za halmashauri ni tarehe 03/03/2017 ambapo wamepokea kiasi cha fedha Tshs. 6,172,657.50/=

Marejesho si haba na si ya usumbufu sana kwa sababu vikundi vilihakikiwa vizuri kabla ya kupewa mikopo hivyo ufuatiliaji ni mwepesi.

CHANGAMOTO.

1. Vikundi vingi vilivyosajiliwa na manispaa ni vikundi hewa, hivyo yalikuwepo mazoea ya kuchukua mikopo ya halmashauri kirahisi na kuitafuna na kupotea, kwa sasa kikundi kinahakikiwa vilivyo hivyo kuondoa mianya ya wapiga dili.

2. Siasa zinaingilia ufanisi wa shughuri nzima ya utoaji mikopo, wanasiasa katika maeneo yao wanawasukuma wananchi wakaombe mikopo hata kama hawana sifa na vigezo vya kukopeshwa wanasiasa wanataka kusimamia makundi hayo yapewe pesa kwa masrahi yao ya kisiasa hata kama vikundi hivyo havikidhi vigezo.

3. Taarifa zinazotolewa na manispaa kwa umma kuhusu mikopo ni za kimalengo lakini ni tofauti na uhalisia, pesa hazipelekwi kwa wakati na hata cheki zinapokuwa zimesainiwa kunakuwa na uzungushwaji mpaka kuipata, wakati huo wananchi hawayajui wao wanachotaka ni pesa na wanakuwa wameshaelezwa kuwa pesa inapelekwa kila mwezi jambo ambalo sio kweli.

4. Riba iliyopangwa na manispaa ni ndogo ukilinganisha na garama ya uendeshaji wa huduma kwa vikundi.

5. Vikundi vinakuwa na wanachama wengi na pesa inayokuwepo inakuwa kidogo kiasi kwamba haziwatoshi, mf. kikundi cha watu 20 unawapa mil 2 au 3 zinakuwa kidogo sana na vikundi vinakuwa ni vingi na vyote vinahitaji. Na kingine ni kwamba pesa hazipelekwi kila mwezi.

6. Kwa sababu za msingi bila shaka, manispaa imezitaka saccos hizi ziwasilishe majina ya vikundi vilivyoomba mikopo ili yajadiliwe kwenye kamati ndogo ya mikopo ya manispaa na kupitishwa kupata mikopo, saccos kwa mjibu wa sheria za ki ushirika wana miongozo yao namna ya kuvijua vikundi, sifa na vigezo na zinaouwezo wa kwenda mpaka maeneo ya waombaji ili kujiridhisha kabla ya kukopesha, hivyo hawaoni sababu ya vikundi hivyo kupitiwa na kujadiliwa tena jambo ambalo linaweza kuua ufanisi wa huduma kwa sababu kamati inaweza kupendekeza kinyume. Majadiliano juu ya jambo hili bado yanaendelea ili kupata muafaka.

MAONI

1. Saccos hizi kama zilivyoaminiwa na kupewa mikataba basi ziachwe huru kutekeleza huduma kwa wananchi kwa kuzingatia vigezo na masharti, kuingiliwa na wanasiasa kwa kutaka vikundi flani vipewe kipaumbele hata kama havikidhi vigezo kutaua ufanisi wa huduma.

2. Halmashauri kuingilia utaratibu wa saccos katika kuvipitisha vikundi kupata mikopo kunaweza kuleta mwanya wa kuchomeka vikundi hewa hivyo kusababisha upotevu wa pesa za serikali jambo litakalosababisha wadhamini wa saccos kupoteza mali/dhamana zao ili kufidia pesa zilizopotea.

3. Uhamasishaji na uelimishaji kwa wananchi kuunda vikundi halali uendelee ili kuchukua nafasi ya vikundi hewa lukuki vilivyosajiliwa manispaa ili umma mkubwa unufaike na mikopo hiyo.

4. Pesa zielekezwe kwa wakati kwenye saccos ili kukidhi uhitaji wa vikundi.

5. Riba ya 10% isitafsiriwe kwa kigezo cha muda, kama ulivyo mkataba baina ya halmashauri na saccos ni kwamba riba itakuwa 10% kwa mwaka na kama ni miezi 6 itagawanyika kwa mbili na kuwa 5% na kama ni miezi 3 itakuwa 2.5%. Saccos inaomba 10% iwe uniform bila kujali muda.

Imeandaliwa na Katibu wa Mbunge

Alex Xavery
Jengeni sitendi kwanza kitu kinachomgusa kila mtu
 
Acheni propaganda uchwara. Huyo kagasheki alifanya kipi cha maana hapa bukoba mjini zaidi ya kila matanuzi, mtu ndege ya watu 13 anaikodi binafsi toka mwanza kuja hapa bukoba kila mara. Kwanza hakunaga mbunge anaefanyaga chochote Tanzania.Wote wanategemea miradi iliyopangwa na serikali. Kama bajeti ya miradi haijapita ktk Jimbo hata mbunge apige kelele vipi haisaidii maana bajeti za nchi hii ni ndogo na hazitekelezeki.
Mimi na wewe hatubishani na hatuna haja, kikubwa ni kukubaliana kwamba mji wetu umerudi nyuma kwa mwonekano na unarudi nyuma kwa kasi. Sasa mie na wewe tunakubaliana kufanya nini kwa ajiri ya mji wetu badala ya kulumbana kusiko na tija? Wanasiasa achana nao kwasababu hitaji lao ni kula na miaka 5 ni mingi kwao, wanavuna na wanakula milele. Mimi na wewe ndo tunhangaika na tunachanganywa na hawa mabwana matumbo
 
Mji umegubikwa na sintofahamu inayotokana na uoga na kutojiamini kwa viongozi.Huwezi kujua kama Manispaa inaongozwa na UKAWA zaidi ya %90 madiwani wote niwa Chama cha Demokrasia na maendeleo.(Chadema) jambo la ajabu uoga wa Meya Chief Karumuna ndo inapelekea wakosa radhi wanapitia kwenye udhaifu wao na kutukana matusi ya nguoni kama Ukimwi,Katerero,Buterangoma Mwaafaa na maneno mengine ya ovyo kama hayo nimatunda ya kupoteza nafasi kwa Meya uyo madiwani na Chama kwa ujumla wake.Mbunge kaishia kwamaneno ya mipasho ,,Mimi ni Nyani mzee nimeisha kwepa mishale mingi"Sasa nataka niwaambie Bukoba hatuhitaji nyani mzee tunahitaji Simba kijana.Mji wa Bukoba ni mchafu kila kona kunzia kwenye sura ya jimbo kukiwa na kaeneo kadogo ambapo nipachafu huwezi kufika pale pana kinyesi na vitu vingi vya hovyo.Lami mashimo hakuna tofauti kati ya utawala wa ccm na chadema.Tumechoshwa na sanaa za wanasiasa.View attachment 459556View attachment 459557View attachment 459558View attachment 459559View attachment 459560View attachment 459561View attachment 459562
Ni mara kumi ingeongozwa na CCM kuliko hawa macoward wa Ukawa.
 
Mimi na wewe hatubishani na hatuna haja, kikubwa ni kukubaliana kwamba mji wetu umerudi nyuma kwa mwonekano na unarudi nyuma kwa kasi. Sasa mie na wewe tunakubaliana kufanya nini kwa ajiri ya mji wetu badala ya kulumbana kusiko na tija? Wanasiasa achana nao kwasababu hitaji lao ni kula na miaka 5 ni mingi kwao, wanavuna na wanakula milele. Mimi na wewe ndo tunhangaika na tunachanganywa na hawa mabwana matumbo
Kikubwa tusubirie hiyo reli ya SGR tuone italeta impact gani kwa jiji la mwanza.Ikileta impact nzuri mwanza na sisi bukoba tutaona mabadiliko kwetu. Vifaa vya ujenzi wa makazi na vifaa vya ujenzi wa miundombinu yetu vitafika hapa kwa wingi na kwa gharama nafuu.Tetemeko lilituathiri sana kutokana na ujenzi duni wa makazi yetu unaochangiwa na gharama kubwa za kununua vifaa bora vya ujenzi.Mji hujengwa na watu wake. Wabunge hawa Kazi yao kubwa ni kutunga sheria na Kuipigia kelele serikali ktk upatikanaji wa maji, umeme, hospital na miundombinu kama barabara na anga.Vyote hivi vinategemea bajeti ya serikali na serikali yetu vyanzo vya bajeti ni vya aibu Sana Sana japo nchi hii Ina kila Kitu.Watanzania tungekuwa tunajielewa tungedai katiba mpya na tume huru ya uchaguzi.Hii ingekuwa silaha yetu. Kama nchi Ina kila Kitu na mambo yanaenda kwa mwendo wa kobe chama kilicho madarakani kwenye kura kinapigwa chini kinawekwa kingine. Lkn hii ya hata ukipiga kura ama usipige chama kinashinda ni laana kwetu.
 
Kikubwa tusubirie hiyo reli ya SGR tuone italeta impact gani kwa jiji la mwanza.Ikileta impact nzuri mwanza na sisi bukoba tutaona mabadiliko kwetu. Vifaa vya ujenzi wa makazi na vifaa vya ujenzi wa miundombinu yetu vitafika hapa kwa wingi na kwa gharama nafuu.Tetemeko lilituathiri sana kutokana na ujenzi duni wa makazi yetu unaochangiwa na gharama kubwa za kununua vifaa bora vya ujenzi.Mji hujengwa na watu wake. Wabunge hawa Kazi yao kubwa ni kutunga sheria na Kuipigia kelele serikali ktk upatikanaji wa maji, umeme, hospital na miundombinu kama barabara na anga.Vyote hivi vinategemea bajeti ya serikali na serikali yetu vyanzo vya bajeti ni vya aibu Sana Sana japo nchi hii Ina kila Kitu.Watanzania tungekuwa tunajielewa tungedai katiba mpya na tume huru ya uchaguzi.Hii ingekuwa silaha yetu. Kama nchi Ina kila Kitu na mambo yanaenda kwa mwendo wa kobe chama kilicho madarakani kwenye kura kinapigwa chini kinawekwa kingine. Lkn hii ya hata ukipiga kura ama usipige chama kinashinda ni laana kwetu.
Mh. yawezekana wewe ni mwanasiasa na na unayaona matatizo yetu kisiasa sana sijuhi unamwogopa nani ama una hofu ya nani. Unawezaje ukayakubali matatizo yako eti kisa hakuna reli, uko sawa kweli? Yaani wewe unaridhika hapo mjini kuwa mashimo hivyo utafikiri ni maandaki ya kambi, mjini kumekuwa kama zizi la nguruwe halafu huoni kama ni tatizo. Yaani hiyo kata ya bilele ina diwani lakini mitaa ni michafu kama machungoni na bado unafikiri ni kukosekana kwa SGR! Pathetic sana, nimeshindwa kukutafakari jinsi unavyoyaona maisha.
 
Hivi huku haya yalilenga nini kama hamkuwa na ya kufanya na kuwaambia wananchi?
 
Mbunge na timu yako mna hoja za kujibu kwa wapiga kura wenu. Mshahara wa bunge mle lakini mkae mkijua hapo mwisho. Tutawasihi CDM watafute damu zingine mpya tuwape kura. Hata wapinzani mmekuwa wasindikizaji bungeni mnanywea kama kipande cha mkate kwenye chai. You are simply vocaless!
 
Asante sana, namtanguliza Mungu mbele naamini ndoto yangu/yetu itakuwa. Najipa mda kufika June niwe nimeiweka hewani na kuileta kwenu wana wa mkoa wetu mzuri sana wa Kagera. Naamini tunayo mazuri mengi sana kuhusu mkoa wetu na ni naamini hili litadhihirika kupitia blog yetu, waitu wakola.

Asante sana kwa kuniunga mkono mkuu, tuwe pamoja.
Ndugu zangu kwanza naomba nianze kwa kumshukuru Mungu wetu kwa kuendelea kutupigania wana Kagera. Tunapitia magumu mengi lakini tunazidi kukomaa pia. Tunakomaa kwa vyote, kiakili na kifikra pia. Tuendelee kupambana na kusaidiana sisi wenyewe na hii ndo njia pekee ya kuuinua mkoa wetu wa Kagera.

Nirudi kwenye mada, ndugu zangu majuma kadhaa huko nyuma nilitoa ahadi kwenu. Niliwahaidi kuanzisha blog yetu kwa ajiri haswa ya kutusaidia kuongea yoote yanayotuhusu kama mkoa. Ninapenda kuwajuza kwamba sasa mambo yako tayari na yameiva, niliwahaidi na nimetekeleza. Blog tayari imeshaanza kazi na inatumia jina la ...kaitabakwetu.blog, lakini pia tumeifungulia page fb kwa jina hilo hilo la kaitabakwetu ...kwa ajiri haswa ya mkoa wetu wa Kagera.

Ombi langu ni moja, kwasababu mie siko hapo mkoani nahitaji mtu mmoja aliye tayari tuone namna ya kuyaongea na kuyaweka hewani yale yote tunayoona yanatugusa kama mkoa. Nikimpata huyu naamini kazi itakuwa imesha na hazma yetu ya kuuongelea mkoa wetu itakuwa successful 100%

Asanteni Sana. Mwije twombeke eyaitu ichwena amoi. Munyegele inywena!
 
Jj
Niliwahaidi na nimetekeleza ndugu zangu, ahadi yangu ya kuanzisha blog imetimia na ipo tayari ishaanza kazi. Inaitwa kaitabakwetu.blog ... kwa ajiri haswa ya mkoa wetu.

Ombi langu ni moja, kwasababu mie siko hapo mkoani nahitaji mtu mmoja aliye tayari tuone namna ya kuyaongea na kuyaweka hewani yale yote tunayoona yanatugusa kama mkoa. Nikimpata huyu naamini kazi itakuwa imesha na hazma yetu ya kuuongelea mkoa wetu itakuwa successful 100%

Asanteni Sana. Mwije twombeke eyaitu ichwena amoi.
Mtafute uyo afisa habari tunayemuona hapa au kwakua ni mwajiriwa wa JF hawezi fanya kazi na wewe ebu ongea naye
 
Mh. yawezekana wewe ni mwanasiasa na na unayaona matatizo yetu kisiasa sana sijuhi unamwogopa nani ama una hofu ya nani. Unawezaje ukayakubali matatizo yako eti kisa hakuna reli, uko sawa kweli? Yaani wewe unaridhika hapo mjini kuwa mashimo hivyo utafikiri ni maandaki ya kambi, mjini kumekuwa kama zizi la nguruwe halafu huoni kama ni tatizo. Yaani hiyo kata ya bilele ina diwani lakini mitaa ni michafu kama machungoni na bado unafikiri ni kukosekana kwa SGR! Pathetic sana, nimeshindwa kukutafakari jinsi unavyoyaona maisha.
Napata mashaka kama hakika umesoma nlichoandika.Sijui uwezo wako wa kuelewa ukoje.Rudia tena kusoma naona unajichanganya.
 
Safi
Mtafute uyo afisa habari tunayemuona hapa au kwakua ni mwajiriwa wa JF hawezi fanya kazi na wewe ebu ongea naye
Safi mkuu japo niliwahi kumtrace na akaonesha ushirika lakini namba yake sina na hata nilivyojaribu kum pm hakuweza kurespond tena

Any way, ntajitahidi tena nione kama naweza kuongea tena nione
 
Napata mashaka kama hakika umesoma nlichoandika.Sijui uwezo wako wa kuelewa ukoje.Rudia tena kusoma naona unajichanganya.
Sawa mkuu, tuendelee na mengine tuijenge Kagera yetu.
 
Napata mashaka kama hakika umesoma nlichoandika.Sijui uwezo wako wa kuelewa ukoje.Rudia tena kusoma naona unajichanganya.
Sawa mkuu, tuendelee na mengine tuijenge Kagera yetu.
 
Wananchi wanaotumia barabara ya Kashozi wamelalamikia adha ya ufinyu wa barabara ya hiyo hasa eneo ilipokua shule ya msingi ya Tumaini ambayo iliamishwa kutokana na upanuzi wa uwanja wa ndege. Malalamiko hayo yametokana na kuzungushiwa senyenge eneo hilo ilipokuwepo shule na hivyo kufanya eneo la watembea kwa miguu na wamachinga kuwa finyu kiasi cha kulazimisha watembea kwa miguu kutumia njia ya vyombo vya moto. Aidha, meneja TANROADS ameishauri halmashauri kuhamisha wamachinga kutoka katika eneo hilo ili libaki kwa matumizi ya watembeao kwa miguu pekee.
66da0a42ec095d8c4797f03c894bb805.jpg
1b4705b0a79a6ab0f269738b41e8d46f.jpg
1dffbf723280dd6c9d310810bfb589a1.jpg
0121766bc75a62e95f3d34b0e43b6e46.jpg
6cea7a6993c63054601b83d6dfb0be09.jpg
e4f5f8d41a733fde69a8427bea738ab7.jpg
88bd5788dbee9b6ebe22f95024e50410.jpg
53d16ce91b1e3f894af2b3efbd484266.jpg
b061d3ea4e8492f451df3f1396e501fd.jpg
 
Hiki kizazi kilichoko hapo Bukoba kina matatizo vichwani mwa watu. Ni sala tu zinazoweza kuwasaidia walau kuweza kujitambua, wanakula stahiki yao
 
CCM wangeweza kumweka mama Tibaijuka hapo manispaa nina uhakika atashinda na atatusaidia sana vinginevyo sioni mtuwingine mkoani kwetu wa kutusaidia. Tunafanya kazi ya kupeleka ma dumbs tu bungeni masaa yote wako kimya kama vile hawana meno mdomoni
 
DODOMA 9/06/2017.

Wabunge wa Mkoa wa Kagera wamefanya kikao na Mhe Balozi wa Uingereza Bi Sara Cooke kujadiliana juu ya misaada kwa maendeleo ya mkoa hususan ujenzi wa shule ya sekondari ya Ihungo iliyoharibika katika tetemeko la tarehe 10/09/2016. Serikali ya Uingereza inajenga shule hiyo upya kwa msaada wa Shs bilioni 6 uliotangazwa tarehe 2/01/2017 wakati. Bi Cooke alipokuwa mgeni rasmi wa mhe Rais John Pombe Magufuli alipotembelea mkoa wa Kagera kuwafariji wahanga wa tetemeko la tarehe 10/09/2016. Balozi huyo amethibitisha kwa Mwenyeji wake aliyemkaribisha katika kikao hicho Prof Anna Tibaijuka ambaye pia ni Mwenyekiti wa Wabunge wa Mkoa wa Kagera kwamba Uingereza pia itajenga nyumba za walimu katika shule ya sekondari ya wasichana ya Rugambwa zilizoharibiwa na tetemeko. Itakumbukwa kwamba tarehe 2/01/2017 baada ya ziara ya Rais Profesa Tibaijuka alimsindikiza Balozi huyo akaione pia shule ya Rugambwa iliyoathirika kwa tetemeko. Juhudi hizo sasa zimezaa matunda.
Profesa Anna ni mmojawapo wa wasichana waliosoma shule ya Rugambwa ilipofunguliwa mwaka 1965.

Wahe Wilfred Lwakatare (Bukoba Manispaa) na Innocent Bashungwa (Karagwe) wapo katikati. Nd. Sylvester Ernest Afisa Mwandamizi wa Siasa Ubalozi wa Uingereza yu kulia.

Taarifa ya Aidan Mapala

ceb7bcee0653349e70e52db399e68a85.jpg
b6bf8e8457223a0bdb9c4935805276a2.jpg
 
Back
Top Bottom