TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Nzega

TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Nzega

Nzega ni mji wa kinyamwezi sana, uswahili mwingi kazi sifuri. Haiwezekani mpaka leo hamna shule ya kidato cha tano na sita kwa kisingizio kuwa ni halmashauri mpya ya mji. Wewe afisa habari unazua maswali mengi sana mana hoja zako ni mfu!

Ikumbukwe nzega mji ni mji uliojengwa na mkoloni na sisi kurithi tu, majengo ya Serikali ni mengi na mji umepangika. Jibu ni rahisi tu elimu sio kipaumbele chenu wanyamwezi kwani mnazidiwa hata na wilaya ya igunga ambao wana high school na ikumbukwe wilaya hii ilizaliwa na nzega miaka 1970,s na inaendelea kwa kasi ya ajabu. ushauri wa bure acheni ujanjaujanja jengeni shule sio kutegemea serikali.
 
Nafikiri wakazi wa Nzega wasife moyo. Wameanza kujipanga na haisaidii kuangalia hali ya sasa kama hakuna focus. Mipango ya elimu ipangwe na kutekwlezwa kitu cha muhimu ni leadership and commitment. Historia audio kutangulia si muhimu na kama kutangulia kungekuwa muhimu basi matajiri wote wangekuwa wazee na kusingekuwa na mzee masikini hata mmoja.
 
Acha kukosa kidato cha tano na cha sita halmashauri ya mji haina hata blog maana tukisimamia website itakuwa tumeenda mbali, mji ulikuwa na mgodi umekosa hata radio yani mji wa miaka hata local radio haina shame on you viongozi kuanzia wabunge waliopita mpaka wakurugenzi wanazidiwa hata na wilaya ya nsimbo katavi wana website.
 
Utandu, hoja zako zina maana sana, maendeleo hutokea pale dosari zinaonjeshwa mapema na hatua kuchukuliwa. Nadhani viongozi wako wamekusikia.
 
IMG_20160812_162259.jpg
Kipindi daraja limejegwa na kuachwa
IMG_20160905_080102.jpg
baada ya mdau utandu kuhoji Siku ya ijumaa vipi hili daraja mbona limekamilika mwezi sasa ujenzi ila kuweka kifusi tu waanze kulitumia imekuwa tatizo au mpaka mwenge uje ndio kifusi kiwekwe

Tunashukuru uongozi umesikia kifusi kimewekwa kama tunavyoona hizo picha hiyo ya juu ni ya awali kabla ya kifusi na hii ya chini ni baada ya kifusi kuwekwa na watu sasa wanalitumia hilo daraja
 
IMG_20160812_161932.jpg
IMG_20160905_075410.jpg
hili nalo ni moja ya madaraja ambayo yalipigiwa kelele hapa kuwa ujenzi umekamilika ila kuweka kifusi imekuwa tatizo Tunashukuru uongozi umesikia kifusi kimewekwa ila kwa kifusi cha hili daraja tuwe wakweli hakistahili warudie kwani mvua ikinyesha hapo kisawawa kifusi chote kinasambaa kwani ni kidogo


Jamani haya madaraja yapo kata ya Mbogwe umbali usiopungua kilometa kumi na nne kutoka kati kati ya mji wa nzega
 
.jpg
Wiki tatu zilizopita mafundi wakiwa katika ujenzi wa banda la kupumzikia wageni katika kituo kipya cha mabasi Nzega
IMG_20160916_155703.jpg
IMG_20160916_155703.jpg
IMG_20160916_155602.jpg
.jpg
IMG_20160916_155602.jpg
Baada ya wiki tatu kuanza kwa ujenzi wa banda la kupumzikia wasafiri katika kituo kipya cha mabasi Nzega ujenzi unaoendelea mafundi wapo hatua ya kuweka vigae
 

Attachments

  • IMG_20160916_155621.jpg
    IMG_20160916_155621.jpg
    140.5 KB · Views: 64
Nawashauri, mpande miti hapo kwenye kituo panaonekana jangwani sana. Halmashauri lazima iwe mstari wa mbele kuweka mazingira bora (green town) igeni wenzenu wa Moshi kuna miti mingi ,bustani na usafi wa mji. Anzeni sasa ktk stendi na baadae muwahamasishe watu kupanda miti. huko embe inastawi tafuteni mbegu bora ya embe na miti mingine pia.
Pili, mtakapo ruhusu watu kujenga vibanda hapo ni lazima muwe na ramani moja tu na kila mtu aifuate hiyo lasivyo patakuwa na majengo shagala bagala kila mtu kivyake vyake , huu ni uchafu ni lazima muwe smart hata kwenye majengo
 
Step usemacho ni kweli tena halmashauri kupitia wadau mbali mbali wa mazingira alafu nzega si Kuna shule hapo basi watumie zile club za mazingira zilizopo katika mashule


Sema kitu kingine nzega Kuna changamoto kati halmashauri wewe nenda idara ya misitu wambie wakuonyeshe bustani ya misitu kama wanayo wapo bize kukamata mikaa tu na baiskeli


Sasa Sijui hiyo miti wataitoa wapi halmashauri ni aibu sana kitengo cha misitu kukosa bustani ya miti nilishangaaga sana Siku moja ya mei mosi eti idara ya misitu wanaenda kuazima miti katika bustani ya mtu mtaani ndio wanaenda fanyia maonyesho

Shame on you
 
pasipokuwa na ulinzi na usalama hakika hakuna maendeleo, niwaombe pia boresheni ulinzi mana kuna matukio ya ukabaji nyakati za usiku mitaa ya kachoma, nyasa, kitongo, ushirika, musoma road na mitaa mingine. vijana hawana kazi wanakula unga na viroba ucku wanakaba. pia maji ni shida
 
NG'HOMELE usemacho ni sahihi kabisa suala la ulinzi shirikishi ni tatizo katika mji wa nzega mfano hiyo mitaa uliyosema ukienda utasema vijana wana serikali yao na utawala wao

Natumai wahusika huu ujumbe wameuona na wataufanyia kazi
 
Afisa mawasiano tunaomba utuambie ni lini ugawaji wa maeneo ya ujenzi wa vibanda vya biashara katika stand mpya unafanyika

Tunaitaji kujua na tunaomba uwezi uwepo ili kila anaye staili kupata eneo apate ikiwezekana watutangazie kabisa mtaani siyo wapeane wao kwa wao mtu mmoja amiliki maeneo zaidi ya mawili hatutaki

Tunaomba ikiwezekana na Mh Bashe asimamie hili suala la ugawaji maeneo kwani sina imani na watu wa halmashauri wanaweza jigawia wao kwa wao

Afisa mawasiano tunaomba uje na mrejesho wa omba langu hili ni lini ugawaji wa maeneo ya mabanda unafanyika na kama zipo taratibu za kufuata tuambie
 
Mradi wa Tushirikishane (JamiiForums yazindua rasmi mradi wa "Tushirikishane") umeanza rasmi jimbo la Nzega mjini chini ya Uongozi wa Mheshimiwa Mbunge Hussein Bashe

Tokana na misingi ya TUSHIRIKISHANE iliyoelemea katika kuwawezesha wabunge wa kuchaguliwa kutekeleza ahadi 4 kati ya jumla ya ahadi walizotoa wakati wa uchaguzi kwa urahisi kwa kushirikiana na wananchi; mada hii itatumika kuwasilisha, kujadili na kupeana taarifa ya kile kinachojiri Nzega mjini.

Ahadi walizochagua kufuatilia wananchi wa Nzega mjini kwenye mradi wa TUSHIRIKISHANE

a. Kukamilisha ujenzi wa kituo kipya cha mabasi-Nzega

b. Ujenzi wa Nyumba ya Daktari-Kituo cha Afya Nhobora

c. Kukamilisha mpango wa muda mfupi wa upatikanaji wa Maji safi na salama-Nzega kwa kuongeza mita za ujazo 1300

d. Kukamilisha mabweni na madarasa ya kidato cha 5&6-Sekondari ya Bulunde​

View attachment 390312
Picha ya pamoja na washiriki toka Nzega. Waliokuwa wamekaa ni madiwani
Mada hii itatumika zaidi na Wana Nzega kutupa taarifa.

Baadhi ya Washiriki watakuwa:

1. Mh. Mbunge Hussein Bashe
2. Gideon Anyona (Katibu)
3. Josephat Sanga (Afisa habari Nzega)
4. Na washiriki wote wa Warsha hiyo na wale wote wenye mapenzi ya Maendeleo ya Nzega mjini.​

Karibuni...
Hongera wana Nzega, tuko pamoja. Good initistive, mie jirani yenu wa Kasubuya.
 
View attachment 391755 View attachment 391755 View attachment 390727 View attachment 390728 View attachment 390729 picha ni madarasa mawili ya kidato cha tano na cha sita ambayo yamekamilika, pia jengo ambalo ni bweni la wanafunzi ambalo lipo katika ujenzi unaoendelea katika shule ya sekondari
Bulunde

Kitu kingine wadau tukumbushane mradi huu upo katika halmashauri ya mji nzega halmashauri ambayo ni mpya kwaiyo ndio inaanza jiimalisha

Kipindi nzega haijagawanywa ni halmashauri moja ya wilaya zilikuwepo shule za kidato cha tano na cha sita shule mbili

Shule ya sekondari UCHAMA ambayo si ya serikali na shule ya sekondari KILI iliyopo Bukene hii ni shule ya serikali

Hivyo basi baada ya wilaya ya nzega kugawanywa kuwa na halmashauri mbili ambayo ni halmashauri ya mji nzega ambayo ndio jimbo la nzega mjini Mbunge wake Husen bashe na kuwepo kwa halmashauri ya wilaya ya nzega ambayo ni jimbo la nzega vijijini Mbunge wake Mh Dr Kigwangala

Basi jimbo la nzega mjini likajikuta halina shule ya kidato cha tano na cha sita ambayo ni Mali ya umma kwani KILI SEKONDARI ilibakia katika jimbo la nzega vijijini ambayo ni halmashauri ya wilaya ya nzega

Shule iliyopo ya kidato cha tano na sita kwa sasa katika halmashauri ya mji nzega ni ya UCHAMA ambayo si Mali ya umma (serikali)

Hivyo basi huu ujenzi wa sasa nihatua ya kuhakikisha mji wa nzega unakuwa na shule ya kidato cha tano na cha sita ambayo ni Mali ya umma (serikali)
Hayo madarasa mbona hayana madirisha?
 
Tabora si ndo maana CCM wanashinda asilimia 100 kila uchaguzi
tukipata hizo high school 10 na ccm inakufa
High school wala usomi haihusiani na CCM. Kama hivyo kanda ya kaskazini wangekuwa ni CCM zaidi kwa kuwa kuna high school na wasomi na lami na hospitali nzuri tu. Zote zilijengwa na CCM hiyo hiyo lakini si kwa sera bali kwa ukabila na ubinafsi wa watu wa huko kushika hatamu serkalini. Hivi hukumbuki waziri mkuu ametoka kanda ya wapinzani mara 5, na mawaziri husika, lakini hasa watendaji idara nyeti za serkalini. Kanda hiyo haikujengwa kwa sera nzuri za upinzani bali kwa ukabila wa watendaji ndani ya serkali ambao wengi wao walitoja huko - sasa wanataka dola waanze ukabila wao tena. Nzega oyee! Iramba oyee! Chunya oyee! Wote mliosahauliwa sasa CCM iko kwa faida yenu. UKAWA ni walewale waliowadumaza walipokuwa CCM wakapeleka rasilimali za taifa kwao. Sasa tuna Waziri Mkuu toka Tandahimba na CCM inaelewa fika jinsi nchi hii ilivyokuwa inaliwa na ukanda mmoja haitotokea tena.
 
Back
Top Bottom