TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Nzega

TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Nzega

IMG-20160930-WA0006.jpg
IMG-20160930-WA0005.jpg


IMG-20160930-WA0002.jpg
Maendeleo ya ujenzi wa mabweni ya kidato cha tano na cha sita katika shule ya sekondari Bulunde nzega mjini

Mabweni yamefika kwenye lenta vile vile ujenzi wa vyoo umeanza kama inavyoonekana katika picha
 
Changamoto ya huduma ya maji bado ni kubwa Nzega. Ule mpango wa kufikisha maji ya Ziwa Victoria sijui umefikia wapi?
 
Changamoto ya huduma ya maji bado ni kubwa Nzega. Ule mpango wa kufikisha maji ya Ziwa Victoria sijui umefikia wapi?
Kiongozi tunaomba uendelee kufuatilia huu mjadala wetu kwani moja ya huu mpango kazi ni kutatua kero ya maji katika mji wa nzega na makubaliano ni hatua ya awali kipindi huo mradi wa maji kutoka ziwa Victoria unasubilia basi makubaliano yamefanyika kuwa kipindi huu mradi upo mjini nzega basi hatua ya awali ya kupunguza changamoto ya maji nzega ifanyike na sasa imeanza fanyiwa kazi

Hatua hiyo ni ujenzi wa matanki makubwa ya maji

Kwaiyo nakusihi endelea kuwa nasi vile vile usisite kutoa maoni, ushauri, hata kuelezea changamoto yoyote iliyopo mjini nzega na inaitaji utatuzi
 
Bado tatizo la kutokuwepo high school ni kuubwa sana
iwepo moja au mbili bado haitoshi
Hapa Boss upo sahihi, pamoja na shule ya Bulunde kuwa high school, Halmashauri iangalie sasa shule nyingine ambayo itaendelezwa kuwa high school ndani ya kipindi hiki cha miaka mitano. Kwakuwa Nzega ilikuwa nyuma sana ni wakati muafaka wa kukimbia sasa mbio za maendeleo
 
Mambo ya bashe hayo si mchezo Mh JPM Kijana hyo mpe wizara akusaidie Kijana anajua kupambana ajasinzia
 
TARIFA YA MWEZI AGOSTI-SEPTEMBER 2016 KUHUSU MAENDELEO YA MRADI WA TUSHIRIKIANE KATIKA JIMBO LA NZEGA MJINI

Ni mwezi mmoja sasa tangu kuzinduliwa kwamradi wa tushirikiane katika jimbo la Nzega mjini,

lengo kuu la mradi huu wa tushirikiane ni kuweka wazi utekelezaji wa majukumu ya maendeleo wanayoyafanya na walioahidi wabunge au madiwani wakati wa kipindi cha kampeni za uchaguzi mkuu wa Octoba 2015


Ahadi zilizokubalika zingie katika mradi huu wa tushirikiane katika jimbo la nzega mjini na kupewa kipaumbele ni miongoni mwa ahadi zilizokuwa katika ilani ya mgombea ubunge wa jimbo la nzega mjini ambaye kwa sasa ndie mbunge wa jimbo hilo mh, Husen bashe ambazo aliahidi kipindi cha kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2015, kwa wanainchi wa jimbo la Nzega mjini.


Vipaumbele hivi vilichaguliwa na wadau wa tushirikiane katika jimbo la nzega mjini ambao walihudhuria warsha ya siku tatu iliyofanyika katika ukumbi wa Tanganyika,wadau hawa ni wakazi na wapiga kura wa jimbo la nzega mjini ambao waliwasilisha makundi tofauti tofauti, walikuwepo wakilishi wa

>wajasiria mali

>Boda boda

>Mama lishe

>watumishi wa serikali

>wafanya biashara

>walemavu

>wamama wa nyumbani

>vijana jinsia zote mbili vijana wa kike na kiume

>viongozi wa dini

makundi haya yalikuwepo kuwakilisha wakazi, na wapiga kura wa jimbo la nzega mjini.


AHADI TULIZOKUBALIANA

>Kukamilisha ujenzi wa kituo kipya cha mabasi Nzega

>Ujenzi wa Nyumba ya Daktari katika kituo cha Afya Nhobora

>Kukamilisha mpango wa muda mfupi wa upatikanaji wa Maji safi na salama –nzega kwa kuongeza mita za ujazo 1300

>Kukamilisha mabweni na madarasa ya kidato cha tano na cha sita katika shule ya sekondaro Bulunde


MAENDELEO YA MRADI

>Kukamilisha ujenzi wa kituo cha mabasi Nzega

Kipindi mradi huu unaanza kituo hichi cha mabasi kilikuwa tayali kimekamilisha ujenzi wa choo, na kituo cha polisi
lakini mradi ulipoanza ujenzi uliendelea kwa kuendeleza mamba yafuatayo

ujenzi wa banda la kupumzikia abiria kipindi wakisubilia usafiri ujenzi huo wa banda mpaka sasa umekamilika kwa asilimia zote

usogezaji wa nguzo za umeme pamoja na kuunganisha nyanya za umeme, tendo lililobakia sasa ni kunganisha hizo nyanya katika transfoma na kuwasha umeme

ukarabati wa barabara za ndani ya kituo cha mabasi hatua ya awali kwa kiwango cha moramu umefanyika

Kinachoendelea sasa ni mpango wa upatikanaji maji kwa hatua ya awali kipindi wakisubilia miundombinu ya maji ya bomba kusogezwa

hivyo hatua ya awali ni uchibwaji wa kisima suala hili linategemea kuanza mda wowote kuanzia sasa

Vile vile tenda la ugawaji wa maeneo ya mabanda ya biashara inatengemewa kutangwazwa wiki hii iliyoanza juma tatu ya tarehe 3/10/2016


mfumo unaotumika katika ujenzi wa hivi vibanda ni wa ‘’private public partnership’’ (PPP) yani makubaliano baina ya serikali na secta binafsi, au mtu mmoja mmoja au kikundi cha watu

Hivyo mnaingia mkataba na halmashauri ya mji wa nzega, na katika mfumo huu halmashauri ndio atakuwa mtoa huduma kuu na kusimamia hiyo huduma kwa makubaliano maalumu mtakayo kubaliana

Hivyo basi halmashauri itatoa tenda la ujenzi wa mabanda kwa mtu yoyote au tasis, hivyo basi mtu au tasisi inayoitaji kujenga hayo mabanda, au kibanda ataenda chukua fomu ya maombi ya huo ujenzi halmashauri ya mji wa nzega, na maombi yake yakikubaliwa basi uyo mtu atajenga kibanda chake kwa gharama zake yeye mwenyewe


lakini atakuwa anasimamiwa na halmashauri kipindi cha ujenzi hususani kuhusu ramani iliyokubalika ijengwe hapo katika kituo kipya pamoja na kuangalia ubora wa ujenzi wenyewe hivyo basi injinia wa halmashauri ya mji wa nzega atakuwa na jukumu la kusimamia ujenzi huo


Vile vile imekubalika kuwa mtu yoyote au tasisi au kikundi kitakachojenga banda au vibanda basi garama za huo ujenzi mpaka kibanda kinaisha hutakiwi kuzidi milioni saba ndio imekubalika hivyo

Kwaiyo mfumo wa malipo na kodi baada ya ujenzi wa banda kukamilika na mtafidiana vipi hayo mambo yapo ndani ya mkataba


kwaiyo mtu ambaye atashinda atapata kuyajua kwa sasa hayo mambo bado hayajawa wazi kwani mikataba bado haijatoka pindi ikitoka tareta tarifa rasmi


>ujenzi wa nyumba ya Daktari katika kituo cha afya Nhobora

kipindi mradi huu unaanza, tayari ujenzi wa nyumba ya Daktari ulikuwa umeanza, na umefikia hatua ya kuweka bima (renta)kama picha mnavyoina katika tarifa za awali za kuanza kwa huu mradi ambazo zinapatikana katika huu mjadala,hiyo bima bado haijawekwa mpaka sasa, ujenzi huu ulisimamam kwa changamoto ambayo ilijitokeza


mpaka sasa ujenzi wa nyumba hii upo hatua ile ile ujenzi haujaendelea kutokana na changamoto iliyojitokeza, na changamoto ambayo ilisababisha ujenzi huu kusimama ni kutokana mtendaji wa kijiji cha Nhobora ambaye ni mmoja wa watia saini wa akaunti ya pesa za kijiji ambazo zipo benki kusimamishwa kazi kutokana na wanakijiji wa Nhobora kukataa endelea kuwa kiongozi wao


suala hili lilipelekea ugumu wa upatikanajia wa pesa kutoka benki, kwani pesa haiwezi kutoka pasipo saini ya huyo mtendaji wa kijiji aliyesimamishwa kazi,kwaiyo kipindi suala la mtendaji kukataliwa na wanakijiji kufika katika kijiji chao masuala ya kiutendaji ya utumishi wa umma yalikuwa yanaendelea ili kuweka jambo hilo sawa hatua hiyo ikaendeleakukwamisha kuendelea ujenzi wa nyumba ya Daktari


hali iliyopo sasa, suala hilo linashugulikiwa ikiwa ni ubadilishaji wa saini ili pesa ziweze kutoka benki nakuja endelea na ujenzi, kwaiyo mda wowote kuanzia sasa ujenzi unaweza kuendelea

>kukamilisha mpango wa muda mfupi wa upatikanaji wa maji safi na salama kwa kuongeza mita za ujazo 1300

Mpango huu utekelezwaji wake bado haujaanza, kwani pesa inayoitajika katika ujenzi wa miundombinu katika mpango huu ikiwa ni pamoja na ujenzi wa mantanki ya maji, ilikuwa ni pesa kutoka serikali kwaiyo pesa hiyo mpaka nandika ripoti hii inasemekana bado haijatoka

hali iliyopo sasa, ni ufuatiliaji wa hiyo pesa ambapo mda wowote kuanzia sasa miye au katibu wa mbunge bwana Anyona, tunaweza kuja na mrejesho rasmi kwani wahusika wakuu wapo katika ufuatiliaji wa hiyo pesa

>kukamilisha mabweni na madarasa ya kidato cha tano, na cha sita katika shule ya sekondari burunde


kipindi mradi unaanza tayali ujenzi wa madarasa mawili ulikuwa umekamilika kama mlivyoona katika tarifa picha za awali kipindi mradi huu unaanza katika mjadala huu, vile vile ujenzi wa mabweni mawili ulikuwa umeanza kwa jitihada binafsi za mh, Husen bashe

mwanzoni mwa mradi huu ujenzi ulikuwa umesimama kwa kusubilia taratibu mbali mbali zifuatwe kwani kuna pesa ilitoka serikali kuu kuja endeleza ujenzi huu

hali iliyopo sasa,mwishoni mwa mwezi wa tisa ujenzi ujenzi huu umeendelea kwa kujenga vyoo, kama mlivyoona tarifa picha za maendeleo ya maendeleo ya mpango huu,vile vile kumwaga renta katika majengo ya mabweni, mpaka mda huu ujenzi unaendelea


imeandaliwa

Afisa mawasiliano (Nzega)

Josephat Sanga
 
maendeleo ya mpango wa kukamilisha mpango wa muda mfupi wa upatikanaji wa maji safi na salama kwa kuongeza mita za ujazo 1300


kama mnakumbuka katika tarifa ya mwezi agosti na septemba kuhusu maendeleo ya mpango huu , mpango huu utekelezwaji wake ulikuwa bado haujaanza kutokana na kukosekana kwa pesa ya kuanzisha utekelezwaji wake ambazo zilikuwa zinatoka serikali kuu

hali iliyopo sasa tayali milioni mia mbili zimetolea (200) ajili ya kuanza utekelezwaji wake kwaiyo mda wowote kuanzia sasa kazi inaanza.
 
Nzega haiwezi kuendelea ktk upatikanaji wa maji mpaka mtakapotoa wezi wa vipuri wa mashine/pampu za maji, pili ni lazima kufanyia marekebisho bwawa la uchama kwa kutoa tope yote iliyojaa hivi sasa, tatu fikirieni kuchimba visima (shallow wells) kule kashishi..nawatakia mafanikio mema
 
mawazo ya ngisibara msiyapuuze jambo jingine idara yamaji wale watu wao wanasimamia mgao wa maji kwa sasa waache uhuni wao wakuwa wanapendelea uzunguni tu uku kwingine maji wanafungulia usiku wa manane wyani mtu umepumzika ndio maji yanatoka, hii tabia mbaya sana waache
 
Jamani tatizo la maji siyo matanki pump za maji zimechoka mbona hilo lipo wazi ikiwa pump hazina uwezo wa kusukuma maji vizuri hata muongeze lita za ujazo bado tatizo litakuwepo
 
View attachment 391755 View attachment 391755 View attachment 390727 View attachment 390728 View attachment 390729 picha ni madarasa mawili ya kidato cha tano na cha sita ambayo yamekamilika, pia jengo ambalo ni bweni la wanafunzi ambalo lipo katika ujenzi unaoendelea katika shule ya sekondari
Bulunde

Kitu kingine wadau tukumbushane mradi huu upo katika halmashauri ya mji nzega halmashauri ambayo ni mpya kwaiyo ndio inaanza jiimalisha

Kipindi nzega haijagawanywa ni halmashauri moja ya wilaya zilikuwepo shule za kidato cha tano na cha sita shule mbili

Shule ya sekondari UCHAMA ambayo si ya serikali na shule ya sekondari KILI iliyopo Bukene hii ni shule ya serikali

Hivyo basi baada ya wilaya ya nzega kugawanywa kuwa na halmashauri mbili ambayo ni halmashauri ya mji nzega ambayo ndio jimbo la nzega mjini Mbunge wake Husen bashe na kuwepo kwa halmashauri ya wilaya ya nzega ambayo ni jimbo la nzega vijijini Mbunge wake Mh Dr Kigwangala

Basi jimbo la nzega mjini likajikuta halina shule ya kidato cha tano na cha sita ambayo ni Mali ya umma kwani KILI SEKONDARI ilibakia katika jimbo la nzega vijijini ambayo ni halmashauri ya wilaya ya nzega

Shule iliyopo ya kidato cha tano na sita kwa sasa katika halmashauri ya mji nzega ni ya UCHAMA ambayo si Mali ya umma (serikali)

Hivyo basi huu ujenzi wa sasa nihatua ya kuhakikisha mji wa nzega unakuwa na shule ya kidato cha tano na cha sita ambayo ni Mali ya umma (serikali)

Link Kili imekuwa high school? Au mnataka kufunika aibu ya Nzega? Kifupi wilaya ya nzega haikuwa na high school hata moja ya serikali sasa Mhe.Bashe ameanza kuhamasija ujenzi was shule moja ya Bulunde.

Ikumbukwe Mhe. Kigwangala alitudanganya kuwa hadi anamaliza kipindi chake angekuwa amesaidia uanzishwaji wa high school 4 nazo ni Nzega day, Chief Ntinginya, Ndala na shule moja siikumbuki. Naomba turejee taarifa zake zipo mitandaoni tulimsifia sana akamaliza muda wake bilabila sasa hv humsikii akiliongelea.

Ninachoweza kumuomba Mhe. Bashe kuwa shule moja ya high school in mwanzo mzuri lakini ajitahidi tufikishe at least 4 za serikali kama tunania ya dhati ya kuwakomboa watu wake ki elimu.
 
karne ya 21 hamna high school hata moja?
Mama yangu mzazi!!!


Ni kweli hakuna isitoshe wilaya ilikuwa na mgodi hadi wazungu wamemaliza dhahabu yote hata kuomba tusaidiwe kujengewa ilishindikana
 
Nzega ni mji wa kinyamwezi sana, uswahili mwingi kazi sifuri. Haiwezekani mpaka leo hamna shule ya kidato cha tano na sita kwa kisingizio kuwa ni halmashauri mpya ya mji. Wewe afisa habari unazua maswali mengi sana mana hoja zako ni mfu!

Ikumbukwe nzega mji ni mji uliojengwa na mkoloni na sisi kurithi tu, majengo ya Serikali ni mengi na mji umepangika. Jibu ni rahisi tu elimu sio kipaumbele chenu wanyamwezi kwani mnazidiwa hata na wilaya ya igunga ambao wana high school na ikumbukwe wilaya hii ilizaliwa na nzega miaka 1970,s na inaendelea kwa kasi ya ajabu. ushauri wa bure acheni ujanjaujanja jengeni shule sio kutegemea serikali.

Hats Mimi nakuunga mkono hoja. Hoja za afisa habari ni mfu
 
IMG-20161008-WA0018.jpg
IMG-20161008-WA0018.jpg
IMG-20161008-WA0014.jpg
IMG-20161008-WA0017.jpg
Jana katika ziara Mheshimiwa mbunge amekagua ujenzi wa zahanati ambayo ameshirikiana na wananchi kujenga na kutoa tofali zilizobaki ili kukamilisha boma.

Pia Mheshimiwa mbunge ametembelea makazi ya walimu na kuona changamoto za nyumba za walimu na kutoa fedha za kujenga vyoo na pia kuamua kuchukua jengo ili kukamilisha .

Katika ziara hiyo, wananchi wa kijiji cha mwanzoli ambao walikua na kero yao ya bwawa na madarasa ya shule ya msingi mwanzoli yaliyokuwa katika hali mbaya leo yamepatiwa fedha kuyarekebisha.

Mh mbunge ametoa jumla ya milioni 2.2m.

Katika kijiji cha Kitengwe Mheshimiwa alizindua mradi wa Zahanati ya Kitengwe kwa kuchangia matofali 5000 na mifukk ya cement 100.

Mradi huu wa zahanati ya Idudumo ukikamilika utagharimu Tsh millioni 40.

Imetolewa na

Katibu Ofisi ya Mbunge.
 
Link Kili imekuwa high school? Au mnataka kufunika aibu ya Nzega? Kifupi wilaya ya nzega haikuwa na high school hata moja ya serikali sasa Mhe.Bashe ameanza kuhamasija ujenzi was shule moja ya Bulunde.

Ikumbukwe Mhe. Kigwangala alitudanganya kuwa hadi anamaliza kipindi chake angekuwa amesaidia uanzishwaji wa high school 4 nazo ni Nzega day, Chief Ntinginya, Ndala na shule moja siikumbuki. Naomba turejee taarifa zake zipo mitandaoni tulimsifia sana akamaliza muda wake bilabila sasa hv humsikii akiliongelea.

Ninachoweza kumuomba Mhe. Bashe kuwa shule moja ya high school in mwanzo mzuri lakini ajitahidi tufikishe at least 4 za serikali kama tunania ya dhati ya kuwakomboa watu wake ki elimu.
Kiongozi shule ya kili sasa ina kidato cha tano na cha sita ina kama mwaka mmoja sasa na kitu tangu ianze
 
Muendelezo wa ziara ya Mheshimiwa Mbunge leo tarehe 10.10.2016 jimboni ambapo anakagua miradi iliyoanzishwa na nguvu za wananchi katika kila kata kila kijiji sambamba na kusikiliza na kutolea ufumbuzi kero mbalimbali.

Leo Mheshimiwa alianza na kata ya Nzega Mjini Mashariki kwenye shule ya Maporomoko ambapo alikagua mradi wa madarasa mawili. Huu ni mradi ambao Mheshimiwa mbunge aliuchangia matofali 2000 na baadae ukapokea shillingi millioni mbili (2000000) fedha kutoka mfuko wa jimbo kwaajili ya kuuendeleza.

Kituo cha pili kwenye kata hii kilikua shule ya Bulunde ambapo kuna mradi wa ujenzi wa bweni la wasichana. Kwenye mradi huu ambao hapo mwanzoni ulikua unafadhiliwa na Mheshimiwa mbunge kwa asilimia 100% na ambao kwa sasa umeanza kwa kupokea shillingi millioni tisa fedha kutoka mfuko wa jimbo.

Kituo cha tatu kilikua katika Kata ya Ijanija kijiji cha Butandula ambapo Mheshimiwa amechangia matofali 2000 na mifuko 20 ya cement katika kuendeleza nguvu ya wananchi. Pamoja na hayo kutokana na kero kubwa ya maji, Mheshimiwa mbunge amechangia Shillingi millioni moja (1000,000/=) kama gharama ya kuziba kingo za bwawa la Kayenze na kuliongezea kina. Mheshimiwa Mbunge pia amechangia maturubai saba kwa kila kitongoji na fedha taslim Tsh 300000 kwa akina mama wa Maselenge.

Kituo cha nne kilikua katika kijiji cha Ijanija ambapo napo kuna changamoto kubwa ya zahanati na nguvu ya wananchi imeishia katika kukamilisha msingi wa jengo hilo. Mheshimiwa mbunge aliwaunga mkono kwa kuwachangia tofali 2000 na fedha taslimu laki nne (400000) kwaajili ya kununua cement na Nondo.

Mheshimiwa mbunge pia amekichangia kikundi cha akina mama cha 'Ujamaa' shillingi laki mbili (200000/=).

Ziara bado inaendelea.

PAMOJA TUJENGE NZEGA MJINI

IMG-20161010-WA0012.jpg
IMG-20161010-WA0013.jpg
Mh Mbunge akiangalia ujenzi wa mabweni unaoendelea katika shule ya sekondari Bulunde

imetolewa na Katibu Ofisi ya Mbunge.
 
Safi sana naona bashe anakaba uku Kigwangala naye ndani ya dakika 45 ITV mda huu safi wana nzega ila pamoja na yote maji jamani maji nzega tatizo kubwa sana
 
Ufanyike uhamasishaji pia, hawa wananchi wanaweza kujiletea maendeleo wao wenyewe kukiwa na leadership. Waanze kukabana huko huko baadae mbunge awasaidie pale wamekwama.
 
Back
Top Bottom