TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Nzega

TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Nzega

Hapa ndipo mnakosea mnajenga nyumba ya mganga wauuguzi hakuna hata nyumba mmoja na 80% ya kazi za hosptal hufanywa na wauguzi.

Mganga na muuguzi ni sawa na meno na fizi
 
Hayo madarasa mbona hayana madirisha?
kiongozi madirisha yapo upande wa nyuma makubwa tu, ujenzi wa sasa madarasa mengi madirisha makubwa huwekwa upande wa nyuma wa darasa eneo ambalo mwanafunzi hawezi kubuguziwa na vitu vya nje endapo anajifunza hivyo upande wa mbele ambapo zipo Ofisi za walimu na watu wengi hupita pita pamekuwa yanawekwa madirisha mdogo ya juu ambayo mwanafunzi hawezi kuona vitu vya nje akiwa amekaa
 
Heri yenu nzega mjini mb wenu anawakumbuka wananchi wake sisi huku nzega vijijini majangu tupu!!!
Mbunge wetu anadili na uwaziri kuliko watu wake,
 
Alafu miye na swali katika utangulizi tumeona watu wataohusika hapa ni afisa mawasiliano, katibu wa Mbunge, na Mbunge ila nimefuatilia hapa naona afisa mawasiliano tu ndiye anawajibika yupo wapi Mbunge wetu haya kama Mbunge yupo bize uyo katibu wake mbona atumuoni humu ebu afisa mawasiliano Waite waje hapa tuna hamu nao sana hao maana tuna mengi sana kuhusu wao Mbunge na Ile ofisi yake
 
Yani wana Nzega wakishirikiana kupajenga kwao ni moja ya mji ambao upo vizuri sema una changamoto chache sana ambazo zikitiliwa mkazo utasonga mbele. Mbunge wa sasa mheshimiwa Bashe kaonyesha nia hivyo wananchi hawana budi kumpa ushirikiano na hata sisi ambao si wazawa Nzega pamekaa vizuri kwa kuwekeza na watu wanaongezeka na kuna mwingiliano wa makabila mbalimbali so ule uswahili unapotea kidogokidogo
 
Alafu miye na swali katika utangulizi tumeona watu wataohusika hapa ni afisa mawasiliano, katibu wa Mbunge, na Mbunge ila nimefuatilia hapa naona afisa mawasiliano tu ndiye anawajibika yupo wapi Mbunge wetu haya kama Mbunge yupo bize uyo katibu wake mbona atumuoni humu ebu afisa mawasiliano Waite waje hapa tuna hamu nao sana hao maana tuna mengi sana kuhusu wao Mbunge na Ile ofisi yake
Atakuja kabanwa na majukumu Bashe hawezi kuwaangusha kama wabunge wengine mizigo
 
Mheshimiwa diwani wa kata ya Mbogwe leo nimetembelea kata ya Mbogwe katika kuliza ipi changamoto yao ya sasa inayoweza taturika kwa mda mfupi wakazi wa Mbogwe kati walisema Kuna tatizo la kisima cha maji cha serengeti

Wanadai Kuna baazi ya kikundi cha watu watuwalitoa tope katika kisima hicho kipindi kisima kimejaa tope hivyo wamejipa mamlaka nani ateke maji na nani asiteke maji kisa tu walitoa tope suala hilo limeibua migogoro baina yao

Wanainchi walipoamua kumuona mwenyekiti wa kata mwenyekiti akipokufuata diwani kukushirikisha diwani ulimjibu wewe ni diwani wa kata si diwani wa kijiji hivyo si jukumu lako hilo

Kwa maana hiyo mpaka sasa utata upo swali tu kwako mheshimiwa diwani wa Mbogwe hivi kile kisima Mali ya nani ya kikundi furani hapo Mbogwe au Mali ya wakazi wa kata nzima ya Mbogwe

Tunakuomba mheshimiwa diwani saidia kuondoa huo utata uliopo katika kata yako

Kwani watu waaokwaruzana wote wewe ndio kiongozi wao na wote wapo katika kata moja usimtupie mpira mwenyekiti kata au wa kijiji peke yake

Nzega yetu sote kuijenga nzega mpya ni wajibu wetu wote asante
 
Taarifa ya mwezi wa tatu hadi mwezi wa Tisa mwaka 2016 juu ya shughuli mbali mbali zinazofanywa mojakwamoja na Ofisi ya Mbunge na Halmashauri ya Mji wa Nzega.
__________________

Ni takriban miezi tisa sasa tangu Mh Mbunge Hussein Mohammed Bashe apewe ridhaa na wananchi wa jimbo la Nzega mjini ya kuwawakilisha bungeni.

Katika kipindi hiki kifupi cha uwakilishi wake wa jimbo hili kuna miradi mingi ambayo imeanzishwa mengine tayari imekamilika na mingine ikiendelea na ipo kwenye hatua nzuri. Miradi hii imegawanywa katika sekta;

[emoji117] Uchumi
[emoji117]Afya
[emoji117] Elimu.
[emoji117] Maji
Kwenye sekta ya uchumi tuna miradi ifuatayo;

1. [emoji117] Stendi mpya ya mabasi Bulunde

2. [emoji117] Mgodi wa Namba saba Halisi

3. [emoji117] Fursa sawa kwa wote wa Airtel kwa kupitia Nzega Urban Trust Fund

4. [emoji117] Uwezeshwaji wa Mamantilie na ofisi ya Mbunge mojakwamoja

5. [emoji117] Mikopo kutoka Halmashauri ya asilimia 10% kwa makundi ya vijana na wanawake.

6. [emoji117] Mradi wa kutoa elimu ya ujasiriamali na kuwawezesha wananchi na rasilimali fedha kupitia shirika la TYEEO ( Tanzania Youth Enterprenurship and Empowerment Organization

7. [emoji117] Mikopo ya Pikipiki bodaboda kwa vikundi.

Kwenye sekta ya Afya kuna miradi ifuatayo;

1. [emoji117] Bima ya afya ya CHF

2. [emoji117] Kituo cha Afya cha Kijiji cha Nhobola Kata ya Mbogwe .

3. [emoji117] Ujenzi wa jengo la upasuaji kituo cha agya Zogolo Kata ya Nzega Ndogo

4. [emoji117] Mchakato wa kurudisha hospitali ya Wilaya kuja kwenye mamlaka ya Mji wa Nzega.

Sekta ya elimu ina miradi ifuatayo;

1. [emoji117] Mradi wa shule ya Bulunde ambao umelenga kuanzisha shule itakayotoa kidato cha 5&6.

2. [emoji117] Ujenzi wa majengo manne yaani madarasa 3 na ofisi ya walimu shule ya msingi Shalemwa.

3. [emoji117] Ujenzi wa madarasa mawili shule ya msingi maporomoko.

4. [emoji117] Ukarabati wa madarasa mawili shule ya msingi Kitengwe.

SEKTA YA UCHUMI:

1.[emoji117] Mradi wa stendi mpya ya mabasi Bulunde
__________________

Mradi huu umeshakamilika kwa asilimia 90% na ni moja kati ya miradi ambayo itazinduliwa na Mwenge tarehe 25.09.2016. Mambo ambayo tayari yameshakamilika katika mradi huu phase 1 ni;

[emoji810] Ujenzi wa kituo cha polisi

[emoji810] Ujenzi wa jengo la abiria yaani 'waiting hall'

[emoji810] Ujenzi wa vyoo vya abiria

[emoji810] Jengo la ofisi yaani 'Administration Block'

[emoji810] Miundombinu ya Umeme

[emoji810] Matenki ya Maji na miundombinu yake.

Shughuli zinazoendelea kwa sasa:
_________________

[emoji810] Ujenzi wa vibanda vya biashara kwa kupitia mfumo PPP ( Public Private Partnership ) ambapo kamati ya zabuni imeshaketi na kamati ya fedha imesharidhia na kubariki mikataba itayotolewa.

Katika mfumo huu wananchi watakua wanajenga vibada vyao na kurudisha gharama zao kwa kupitia makato yao ya kodi ya pango.

Kuanzia wiki ijayo wananchi wataanza kupewa mikataba.

2.[emoji117] Mgodi wa Namba saba Halisi.
_________________

Katika kutimiza ahadi yake ya kuwatafutia wananchi wake fursa za kiuchumi na kujiajiri, Mh Mbunge aliomba serikalini mgodi huu ambao hapo awali ulikua chini ya mwekezaji mmoja.

Serikali iliridhia ombi hilo na hatimae wananchi wakapewa eneo hilo kwaajili ya uchimbaji mdogo. Kwasasa eneo hilo lina takriban vijana 3000 ambao wanajishughulisha na uchimbaji na wana kipato halali.

3. [emoji117] Mradi wa Airtel fursa sawa kwa wote ambapo Airtel wametoa millioni 20

4. [emoji117] Mikopo kwa vikundi vya ujasiriamali vya Mamantilie ambapo mpaka sasa jumla ya vikundi 25 vimeshakopeshwa, na kupata mikopo isiyokuwa na riba.

5. [emoji117] Asilimia 10% ya mapato ya ndani ya Halmashauri fedha zinakopeshwa kwa vikundi vya wanawake na wanaume.

6. [emoji117] Mradi mkubwa ambao ni endelevu unaoendeshwa na shirika la TYEEO(Tanzania Youth Enterprenurship and Empowerment Organization ) likishirikiana na ofisi ya Mbunge . Katika mradi huu ambao upo jimbo zima wananchi watakua wana wanapewa elimu kwa muda wa miezi mitatu wakiwa wameandaliwa katika makundi ya watu wasiozidi 30 na baada ya miezi mitatu ya elimu ya ujasiriamali, wataanza kukopeshwa.

7. [emoji117] Mradi wa mikopo ya pikipiki za bodaboda ambapo jumla ya pikipiki 31 zimeshakopeshwa kwa vijana.

SEKTA YA AFYA:

1. [emoji117] Ujenzi wa jengo la upasuaji kituo cha afya Zogolo Kata ya Nzega Ndogo

2. [emoji117] Ujenzi wa nyumba ya Mganga katika kituo cha Afya cha Nhobola Kata ya Mbogwe

3. [emoji117] Ujenzi wa Zahanati ya Idudumo ambapo ofisi ya mbunge imechangi mifuko ya cement na Matofali ya ujenzi

4. [emoji117] Jitahada na mikakati inayoendelea ya kurudisha hospitali ya Wilaya kuja kwenye. mamlaka ya Mji.

5. [emoji117] Huduma ya Bima ya Afya ya CHF ambapo Mh Mbunge alikatia Kaya 200 zisizojiweza kwaajili ya huduma hii na wanachama wote wa chama cha bodaboda Nzega mjini.

SEKTA YA ELIMU :

1. [emoji117] Mradi wa Shule ya Bulunde ambapo ukikamilika utatoa nafasi kwa jimbo la Nzega kuwa na shule ya kidato cha 5&6. Phase 1 yaani awamu ya kwanza ya mradi huu imeshakamilika ambapo madarasa mawili yamejengwa. Phase 2 yaani awamu ya pili ni ujenzi wa bweni na vyoo vya bweni ndio unaendelea . Awamu ya kwanza imegharimu takriban millioni 40 fedha ambazo zimetoka mojakwamoja kwa Mh Mbunge.

2.[emoji117] Ujenzi wa nyumba ya mwalimu Mwanyagula 2 in 1.

3. [emoji117] Nyumba ya mwalimu shule ya Nhobola
4. [emoji117] Ujenzi wa madarasa matatu na ofisi ya walimu shule ya msingi Shalemwa . Ujenzi wa madarasa haya utawaokoa wanafunzi wanaotembea km 10 kwenda shule. Ikimbukwe kwamba shule hii ujenzi wake unafadhiliwa mojakwa moja na mbunge kwani ndio mwanzilishi wa shule hii baada ya kupokea maombi ya wananchi kuhusu watoto wao ambao walikua wakitembea km 10 kwenda kutafuta elimu.

5. [emoji117] Ujenzi wa madarasa matatu shule ya msingi maporomoko .

6. [emoji117] Ukarabati wa madarasa mawili shule ya msingi ya Kitengwe. Haya ni madarasa ambayo watoto walikua wanasoma kwenye sakafu ya vumbi.


7. [emoji117] Ujenzi wa madarasa mawili shule ya msingi ya Undomo.

8. [emoji117] Ulipiaji wa ada ya wanafunzi kama ifuatavyo;

[emoji810]Vyuo vikuu wanafunzi 14

[emoji810] VETA wanafunzi 19

[emoji810] SEKONDARI wanafunzi 34.

UJIO WA MWENGE TAREHE 25.09.2016
_________________

Ujio wa Mwenge katika Jimbo letu la Nzega Mjini utakuja kuzindua miradi ifuatayo;

1. [emoji117] Ujenzi wa stendi mpya ya mabasi

2. [emoji117] Mradi wa Bima ya afya kwa wazee waliozidi fikisha miaka 60 na zaidi

3.[emoji117] Kufungua Ofisi ya Serikali ya Kata katika kata ya Mbogwe.

4. [emoji117] Ujio wa Mwenge pia utatoa fursa kwa jimbo letu kupata msaada wa shillingi millioni 10 ili kusaidia jitiada za Mbunge za kuwawezesha wananchi kwa mikopo nafuu.

Lakini nimalizie kwa kutaja jitahada za Mh Mbunge ambazo anaendelea kuzifanya katika kuwaletea wananchi wake maendeleo;

1. [emoji117] Kurudisha eneo la uwanja wa ndege kwa wananchi ambapo tayari Mh Mbunge ameshaongea na waziri husika na tayari taratibu za kiserikali zinaendelea

2. [emoji117] Mh Mbunge ameshaongea na waziri wa elimu kuhusu madai ya walimu tofauti na mishahara yao. Tayari serikali imeshapokea maombi hayo na muda wowote kuanzia sasa walimu wataamza kulipwa madai yao.

3. [emoji117] Mh Mbunge ameongea na waziri wa nishati na madini kuhusu uwezekano wa kuongeza eneo la uchimbaji kitalu cha 3 kwenye mgodi wa Namba 7 halisi. Maombi haya yamepokelewa wizarani na maendeleo ni mazuri.

4. [emoji117] Maombi ya kuchukua majengo ya mchina kwenye kambi ya mkandarasi huyo ili kukigeuza kituo icho kuwa cha VETA. Tayari serikali imeshaachia majengo ya Tanroad.

5. [emoji117] Uwepo wa kituo pekee cha uwekezaji cha EPZ Kata ya Nzega Ndogo ambapo eneo tayari limeshapimwa na taratibu zingine za kiserikali zinaendelea.

6. [emoji117] Jitahada za kutatua kero ya maji. Suluhisho la muda mfupi tayari changamoto yake imeshatatuliwa ambapo takriban Tsh millioni 520,000,000/= zimeshapatikana kwaajili ya kujenga machujio mapya na kukarabati ya zamani.

Suluhisho la muda mrefu ni mradi wa Ziwa Victoria ambapo fedha zake zimeshapatikana kupitia Bank ya Exim India.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI JIMBO LA NZEGA MJINI.

Imeandaliwa na;

Katibu wa Mbunge Ofisi ya mbunge Jimbo la Nzega Mjini.
1474714065619.jpg
1474714073000.jpg
1474714081565.jpg
1474714091180.jpg
1474714099565.jpg
1474714106805.jpg
 
Picha ya kwanza ni madarasa ambayo yamejengwa Bulunde Secondary kwaajili ya kidato cha 5&6

Picha ya pili vijana wakikopeshwa bodaboda kwa gharama nafuu katika jitiada za Mh Mbunge kukuza sekta ya ajira.

Picha ya tatu Mh Mbunge akishiriki zoezi la kuhamisisha kukata Bima ya Afya ambapo bodaboda wote jimbo la Nzega walikatiwa.

Picha ya nne ni Mh Mbunge akifungua rasmi mgodi wa namba saba ambao hapo awali ulikua chini ya mwekezaji na sasa umetoa ajira kwa vijana 3000 wa Nzega.

Picha ya Tano ni Mh Mbunge akikabidhi hundi ya Million 9 kwaajili ya uendelezi wa mrado wa Bulunde sekondari itakayotoa kidato cha 5 na 6.

Picha ya 6 Mh Mbunge akikabidhi hundi ya million 9 kwa Mtendaji wa Kata ya Mbogwe kwaajili ya ujenzi wa nyumba ya Mganga zahanati ya Nhobola.
 
Katibu, nikushukuru mapendekezo ya wadau humu yafikishe pia kwa mbuge. Umeona wadau wanaimani na mbunge wao ni vizuri mmeanza hivi japo kidogo lakini inaleta maana kwa wakazi wa Nzega. Kazi zifanyike na zionekane zinafanyika, mpigane kushinda umaskini, ujinga na maradhi. Boresheni mazingira ili mji uvutie wageni hapo mji utachangamka hata kiuchumi.
 
Pili PPP ni namna nzuri ya kuharakisha miradi, hili nalo mlitazame kwa mfano niliwahi kupita huko na pale viwanja vya parking ni harufu tu ya mikojo, hapo mnaweza kumpatia mtu ajenge choo cha kulipia na hata mkaweka mazingira bora ya biashara pale kwani palikuwa uchafu tu n,mashimo mengi na vumbi kweli. Eneo hilo linaweza kuwaingizia pesa sana ni kulitazama kwa jicho la tatu
 
Asante sana katibu kwa mrejesho mzuri hususani ugawaji wa maeneo ya mabanda katika kituo kipya cha mabasi Nzega ombi langu Siku mkianza kugawa mkataba mtujuze kupitia jukwaa hili



Kitu kingine nimeona hapo kuwa Mh Mbunge kakatia bima ya afya kaya 200 vile vile wanachama wa boda boda nzega naomba kuuliza hizo bima wameshakabiziwa boda boda hao boda boda wa nzega au bado zipo katika mchakato
 
IMG-20160925-WA0017.jpg
IMG-20160925-WA0015.jpg
IMG-20160925-WA0009.jpg
IMG-20160925-WA0009.jpg
IMG-20160925-WA0002.jpg
IMG-20160925-WA0014.jpg
shamra shamra za uwekaji wa jiwe la msingi wa ujenzi wa kituo kipya cha mabasi Nzega

Tukio hili limefanyika leo ikiwa ni moja ya mradi uliozinduliwa na mbio za mwenge mwaka huu

Tukumbuke mradi huu wa ujenzi wa kituo kipya cha mabasi ni moja ya mpango kazi uliopo katika mradi wetu wa tushirikiane nzega
 
Alafu miye na swali katika utangulizi tumeona watu wataohusika hapa ni afisa mawasiliano, katibu wa Mbunge, na Mbunge ila nimefuatilia hapa naona afisa mawasiliano tu ndiye anawajibika yupo wapi Mbunge wetu haya kama Mbunge yupo bize uyo katibu wake mbona atumuoni humu ebu afisa mawasiliano Waite waje hapa tuna hamu nao sana hao maana tuna mengi sana kuhusu wao Mbunge na Ile ofisi yake
Tupo. We uliza swali utajibiwa.
 
Afisa mawasiano tunaomba utuambie ni lini ugawaji wa maeneo ya ujenzi wa vibanda vya biashara katika stand mpya unafanyika

Tunaitaji kujua na tunaomba uwezi uwepo ili kila anaye staili kupata eneo apate ikiwezekana watutangazie kabisa mtaani siyo wapeane wao kwa wao mtu mmoja amiliki maeneo zaidi ya mawili hatutaki

Tunaomba ikiwezekana na Mh Bashe asimamie hili suala la ugawaji maeneo kwani sina imani na watu wa halmashauri wanaweza jigawia wao kwa wao

Afisa mawasiano tunaomba uje na mrejesho wa omba langu hili ni lini ugawaji wa maeneo ya mabanda unafanyika na kama zipo taratibu za kufuata tuambie
Ugawaji utaanza wiki ijayo kama ratiba haitabadilishwa.
Kikubwa ni mjaribu kuchangakia fursa na kama upo Nzega itakua vizuri sana
 
Katibu, afisa habari na wenzio hapo, kwa shughuli za kukuza uchumi wa watu wenu mnaweza mkawa contact Rural livelihood development company wapo Dodoma jengo la NBC, +255 262321455, www.rldc.co.tz. hawa wanafadhiliwa na serikali ya Uswiss na wanamiradi mingi ya kusaidia kujijengea uwezo wa kiuchumi poor communities vijijini. Wanaweza kuwafaa sana huko.
 
Back
Top Bottom