Mjapan: Kwa kasi hii ya maendeleo Rais Magufuli alistahili kuishi Japan maana anaamini katika kazi siyo siasa

Mliongea nae kwa lugha gani
 
Aache kimsifia alale sero kama wale wachina
 
Rwanda na Tanzania zimepata viongozi wenye kuleta maendeleo. Si wanademokrasia lakini ni wasimamizi thabiti wa ujenzi wa nchi.

Siungi ccm mkono ila namwunga Magufuli mkono kwa dhati. Mola amjalie maisha marefu. I know a good thing when I see one.
 


Stori za kutunga
 
Umemkosea heshima huyo bwana kimwita Mjapan.

Siyo kila aloyebimba macho ni mjapani. Hiyo uloyekutana naye ni Mtanzania. Na huenda anatpkea Tandale. Ni wale wanaozaliwa kutoka kwa dada poa baada ya kukutana na wageni pale wawapo kwenye harakati zao.
 

Huyo uliyekutana naye sio mjapani, bali ni MATAGA aliyevaa wigi la kijapani. Angalia usije ukatapeliwa hapa mjini.
 
Wajapan wanaamini katika kazi siyo siasa uwe unaelewa bwashee!

Huwa nacheka sana nikisikia eti Magufuli ni mtu wa kazi na sio mwanasiasa. Mtu ana zaidi ya miaka 20 kwenye siasa, na mafanikio yake yote kayapatia kwenye siasa kisha mnasema sio mwanasiasa? Kichekesho hiki kiko chattle tu.
 
Kusinyaa kwa uchumi ni mgomo baridi ili ionekane ajafanya kitu. Ona Tanzania inavyojitangaza duniani kwa madege, tena yanetokana na kodi za watanzania. Kama wewe unampenda aluyetujazia mateja tz

Mkuu tuna ndege saba tena zisioenda nje, kisha unasema tunajitangaza kwa madege huko duniani!?
 
Hizi sifa za kusifia sifia wanaume wenzio hizi ,shauri yako...!
Yaani maongezi yako na Mjapan mmoja tu umekurupuka kuja huku!
 
Kusinyaa kwa uchumi ni mgomo baridi ili ionekane ajafanya kitu. Ona Tanzania inavyojitangaza duniani kwa madege, tena yanetokana na kodi za watanzania. Kama wewe unampenda aluyetujazia mateja tz

Kwani kafanya nini kwa wanainchi wa kule kijijini kwetu. Ona sasa maisha haya wanayoishi. Halafu mnajisifia ujinga tu.
 

Yaani

Haya mambuzi ya Jiwe yataongea anything

Ni Mjapan what makes him superior?

Sababu ni race ya Kijapan?

Y'all monkeys are hillarious!
 
Mkuu ungetuwekea na kapicha au ka video clip ingekuwa poa!
 
Huyo Engineer wa Kijapani asingekuwa sahihi zaidi.Siasa kweli ni porojo za kijinga zilizoingizwa kwa siri as a system of divide and rule.Nia ya system hii ni kuleta strife and sometimes even war when desired by the "World Establisment." Nia pia ni kututoa kwenye maswala ya msingi,and in this case I mean mainly development.Sisi kwa ujinga wetu tume-adopt the system as something real.Very stupid indeed.Ni wakati muafaka sasa wa kuachana na porojo za siasa na kurudi kwenye msingi,ambao ni kazi.Slogan ya "Hapa Kazi Tuu," wouldn't have been more appropriate.
 
Rwanda na Tanzania zimepata viongozi wenye kuleta maendeleo. Si wanademokrasia lakini ni wasimamizi thabiti wa ujenzi wa nchi.

Siungi ccm mkono ila namwunga Magufuli mkono kwa dhati. Mola amjalie maisha marefu. I know a good thing when I see one.
Amen!
 
Hizi sifa za kusifia sifia wanaume wenzio hizi ,shauri yako...!
Yaani maongezi yako na Mjapan mmoja tu umekurupuka kuja huku!
Mbona hata wewe umekurupuka na kuji huku kwa mjapan..... Hahahaaa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…