Mjue Jini Mahaba: Fahamu mengi kuhusu jini mahaba

Mjue Jini Mahaba: Fahamu mengi kuhusu jini mahaba

Niendelee kuwa looser wa kitu gani??, hivi mimi na wewe nani looser??.

Wewe ndiye looser kwa kuifanya Qur'an ionekane ni kitabu cha ngano za majini badala ya kuwa kitabu cha kuongoza mwanadamu kiroho na kimwili.

Leo watu wengine wanaogopa hata kuigusa Qur'an kwa khofu kwamba watapatwa na majini yenu mnayoyaamini katika mila zenu.

Leo waganga wa kienyeji wanaandika aya za Qur'an katika sahani kwa kutumia zafarani na kuuosha kwa maji na kuwanywesha watu (kombe)!!!, Quran imekuwa kitu cha mchezo kiasi hicho!!;;, inasikitisha sana..
Wewe huna hoja tena heri ukae kimya tu!
 
Wewe huna hoja tena heri ukae kimya tu!


Wewe ndiyo huna hoja, kwani unanipinga halafu unashindwa kutoa hoja mbadala zinazokuunga mkono katika kile unachoamini,, umebaki tu kupiga kelele.😜😜.

Mungu akikupa ufahamu wa Qur'an ni raha sana.


Ewe Rakims, fanya swala ya Istikhara au Hajja ili Allah akupe heri ya kujua maana za aya za kitabu chake Qur'an.
 
Good.iyo elimu ya kuwaona ina itwaje? Na je ukimuona akajua umemuona!
Ok kuhusu pazia lililowekwa kutokuonekana kwa macho ya mtu ya kawaida ni kwa sababu ya maumbile yao na kutokuwa na umbo moja thabiti ambalo wamepewa wengi hubadirika badirika hivyo kwa maumbile yao ya kutisha na kuogopesha ndio wakawa wamehifadhiwa wasionekane kwa macho tu ya dhahiri kwa maana dunia ingekuwa ni vurugu tu, lakini kwa wenye kutaka kuona ndio ikawepo elimu jinsi ya kuweza kuwaona, na kuhusu nguvu baina ya jini na binadamu ni sawa na kutaka kujua nguvu kuhusu binadamu na mnyama sasa hapo nguvu binadamu anazidiwa na jini isipokuwa yeye ndio mtawala wa ulimwengu huu na alijaliwa akili zaidi kuliko jini na kuna baadhi ya majini wanawazidi watu akili wasioweza kuzitumia!

Rakims
 
Sasa ni kwambie hiyo gaibu imefichwa na wanadamu wenzako sio mungu psychic abilities to compress human to the maximum is a big secret for humanity. Most important thing is an "EYE"
Mkuu, kwanza nilikosea (misspell) maandishi, ilitakiwa liwe "Psyche" katika muktadha nilikuwa na maana ya mawazo au jambo linalohusiana na akili na fikra za mtu.

Ghaibu ni kitu kisichoonekana au kisichojulikana, kitu ambacho kipo katika siri. Unaposema elimu ya ghaibu maana yake ni elimu ya mambo yaliyojificha, yaliyofichikana., mambo ya siri nk, (the unseen).
 
Eti, sahihi !!, sahihi kitu gani??!!.

Wageni wanaozungumzwa katika Qur'an ni wale wageni wa Nabii Ibrahimu (as), na imeandikwa hivi;

------ ضيف إبراهيم المكرمين--- (dhwaifi Ibrahiim almukramiin), yaani; Wageni waheshimiwa wa Ibrahimu.

Neno lililotumika kwa maana ya wageni hapo ni "dhwaifi" (ضيف).

Neno lililotumika katika kamusi (Lane &Aqrab) kwa maana ya neno "jinn" (جن), ni neno "Stranger" ambalo kwa kiarabu ni "gharib" (غريب).

Neno "stranger" limetokana na neno la kilatini "strange" (adjective), na lina maana pana sana na maana zote hizo kimsingi zinaashiria hali/ sifa ya "ugeni" katika vitu na watu (unfamiliarity), hivyo neno "strange" likazaa "stranger" na maana yake hasa kwa kiingereza linapohusu mtu/watu ni ""FOREIGNER(S) ", hivyo niliposema wale majini waliotajwa kwenye Surah Jinn ni wageni nilikuwa na maana ya "strangers" au "Foreigners" kwa sababu maana za hayo maneno ni sawa japo katika kamusi limeandikwa hilo moja tu yaani "strangers".

Neno "Foreigners" kwa kiarabu ni (اجنبي) angalia hapo, kama wewe ni mjuzi wa Lugha ya kiarabu japo kidogo tu, utaona mzizi wa neno "janna" (جن) hapo ndani ukiwepo katika hilo neno licha ya hiyo "conjugation" iliyoongeza herufi ya ب na ي mwishoni na ا mwanzoni lakini hapo kati bado utaona huo mzizi wa ج na ن.

Hivyo sasa wale wageni wa Nabii Ibrahim (as) walikuwa "guests" wake na wale majini waliotajwa katika surah Jinn ni Foreigners (strangers).

Katika lugha ya kiswahili huwezi kutofautisha kati ya guests, foreigners / strangers. Wote tunawaita wageni.

Qur'an inasema yenyewe ni muongozo kwa watu, na ukisoma katika mwanzoni mwa hiyo sura jinn utaona hao majinn wakiisifia Quran wakisema hakika tumeisikia Quran ya ajabu inayoongoza kwenye uongofu" --- na baadaye wakaikubali, sasa Quran ni muongozo kwa watu na kwakuwa wale majinn waliipokea iwe kiongozi chao basi wale majinn lazima walikuwa ni watu (binadamu).

Kinyume na ufafanuzi huu aje ulamaa yeyote na alete hoja kupinga.

Quran ni kitabu cha watu wenye akili na fikra wala sio kitabu cha kupungia mapepo na majini mahaba, makata, na subiani na hayo yote ni uongo mkubwa hakuna vitu kama hivyo.
Sikuwaumba wanadamu na majini ila waniabudu?
wewe unaelewa vipi hii aya?
 
Wewe ndiyo huna hoja, kwani unanipinga halafu unashindwa kutoa hoja mbadala zinazokuunga mkono katika kile unachoamini,, umebaki tu kupiga kelele.😜😜.

Mungu akikupa ufahamu wa Qur'an ni raha sana.


Ewe Rakims, fanya swala ya Istikhara au Hajja ili Allah akupe heri ya kujua maana za aya za kitabu chake Qur'an.
Mkuu kama wewe ni muislam basi unatakiwa urudi darasani ukasome vema uislamu wako kwa maana umepotoka kuamini kuwa maelezo ya Qur.an kuhusu majini ni wageni na kama umesali istikhara ndio ukaambiwa hivyo basi wewe umemzidi hata mtume kwa maana yeye mwenyewe kwenye hadithi yake kuhusu majini anasema:
Allah kaumba aina tofauti za majini. Miongoni mwao wapo wale wanaoweza kujibadili katika maumbile tofauti kama mbwa na nyoka; na baadhi yao hupaa kama upepo na wengine wanaweza kusafiri na kupumzika.
Abu Tha`labah al-Khushni pia alisema kwamba Mtume (swala llahu aleyhi wasalam) alisema:
:“Majini wapo wa aina tatu: Aina moja wapo ni ya upepo wanaweza kupaa kama upepo; aina nyingine huonekana kama mbwa au nyoka; na aina nyingine ni wale ambao hupumzika na kuendelea na safari zao.”(Ilipokelewa na At-Tahawi katika Mushkil Al-’Athar)

Sasa kama mkuu umeoteshwa hivyo huna tofauti na manabii wa uongo waliopo hivi sasa

Rakims
 
Good.iyo elimu ya kuwaona ina itwaje? Na je ukimuona akajua umemuona!
Kuna elimu nyingi za kuwaona lakini zote kati ya hizo zipo zinazoishia katika kushukuru au kukufuru itategemea na uliyojifunza au kufundishwa aina ya kwanza na ambayo wengi hutumia ni Mandal hii unaweza kutumia kwa kioo au macho ya kawaida lakini aina zingine si salama na pia ikiwa una imani thabiti na kinga ya mwenyezi Mungu wakikuona hawawezi kukufanya chochote sema ikiwa unawaita na huna uhakika unachofanya basi ni sawa na kumuita mwanajeshi au jambazi kwa ghadhabu na vishindo halafu akija unacheka cheka. atakacho kufanya mtajuana nyinyi wawili,

Rakims
 
Sasa ni kwambie hiyo gaibu imefichwa na wanadamu wenzako sio mungu psychic abilities to compress human to the maximum is a big secret for humanity. Most important thing is an "EYE"
how can a young man like him know this kind of stuff mkuu?
 
Eti, sahihi !!, sahihi kitu gani??!!.

Wageni wanaozungumzwa katika Qur'an ni wale wageni wa Nabii Ibrahimu (as), na imeandikwa hivi;

------ ضيف إبراهيم المكرمين--- (dhwaifi Ibrahiim almukramiin), yaani; Wageni waheshimiwa wa Ibrahimu.

Neno lililotumika kwa maana ya wageni hapo ni "dhwaifi" (ضيف).

Neno lililotumika katika kamusi (Lane &Aqrab) kwa maana ya neno "jinn" (جن), ni neno "Stranger" ambalo kwa kiarabu ni "gharib" (غريب).

Neno "stranger" limetokana na neno la kilatini "strange" (adjective), na lina maana pana sana na maana zote hizo kimsingi zinaashiria hali/ sifa ya "ugeni" katika vitu na watu (unfamiliarity), hivyo neno "strange" likazaa "stranger" na maana yake hasa kwa kiingereza linapohusu mtu/watu ni ""FOREIGNER(S) ", hivyo niliposema wale majini waliotajwa kwenye Surah Jinn ni wageni nilikuwa na maana ya "strangers" au "Foreigners" kwa sababu maana za hayo maneno ni sawa japo katika kamusi limeandikwa hilo moja tu yaani "strangers".

Neno "Foreigners" kwa kiarabu ni (اجنبي) angalia hapo, kama wewe ni mjuzi wa Lugha ya kiarabu japo kidogo tu, utaona mzizi wa neno "janna" (جن) hapo ndani ukiwepo katika hilo neno licha ya hiyo "conjugation" iliyoongeza herufi ya ب na ي mwishoni na ا mwanzoni lakini hapo kati bado utaona huo mzizi wa ج na ن.

Hivyo sasa wale wageni wa Nabii Ibrahim (as) walikuwa "guests" wake na wale majini waliotajwa katika surah Jinn ni Foreigners (strangers).

Katika lugha ya kiswahili huwezi kutofautisha kati ya guests, foreigners / strangers. Wote tunawaita wageni.

Qur'an inasema yenyewe ni muongozo kwa watu, na ukisoma katika mwanzoni mwa hiyo sura jinn utaona hao majinn wakiisifia Quran wakisema hakika tumeisikia Quran ya ajabu inayoongoza kwenye uongofu" --- na baadaye wakaikubali, sasa Quran ni muongozo kwa watu na kwakuwa wale majinn waliipokea iwe kiongozi chao basi wale majinn lazima walikuwa ni watu (binadamu).

Kinyume na ufafanuzi huu aje ulamaa yeyote na alete hoja kupinga.

Quran ni kitabu cha watu wenye akili na fikra wala sio kitabu cha kupungia mapepo na majini mahaba, makata, na subiani na hayo yote ni uongo mkubwa hakuna vitu kama hivyo.
Umehama tena kutoka guest kwenda foreigners/strangers?

unaizungumzia vipi Surat Asabaa aya ya 15

"Na Tulipomkidhia kifo chake
(Suleimani) hakuna kilichowabainishia
kwamba yeye amekwisha kufa
isipokuwa mnyoo wa ardhini ambaye
alikula fimbo yake (Suleimani). Basi
alipoanguka wale majini walitambua
waziwazi kwamba kama wangaliyajua
yasiyoonekana, wasingalibakia katika
hali ya mateso ya kufedhehesha"

Sasa wewe unang'ang'ania uongo wako ili hapo ubadirishe mada baina yangu na wewe rejea kwenye mada yako ulivyoileta hapa:

Ulisema huo ni uongo mtupu na hakuna viumbe wa aina hiyo na kanusho lako ni kuwa hakuna majini na hapa sikuambii kuwa Qur.an ni kitabu cha majini au ni ngano za majini hapana isipokuwa nakuelimisha kuhusu usilofahamu kuhusu majini na usifanye watu wanielewe kuwa natetea mada za majini kwa msaada wa kitabu kitukufu hapana!

Rakims
 
Mkuu, huyo mwenzako aliyenitusi kabla ya mimi kumjibu hukuona matusi yake au yeye hakustahili kupewa hizo nasaha unazonipa??--- yeye kaanza kunitusi na mimi nilikuwa najibu mapigo, juu ya yote mimi niko peace tu.

Tuje katika mada, umeandika maneno katika lugha ya kiarabu nadhani ni watu wachache sana humu ndani wanaojua lugha ya kiarabu na hata kama wapo sio fasaha sana katika lugha hiyo kama waiivyokuwa fasaha katika Kiswahili na kiingereza, hivyo ni vyema unapoona "raha" kuandika kwa kiarabu basi pembeni weka tafsiri yake kwa kiswahili ili wengi wetu tusiojua vyema kiarabu tupate kufahamu.

Tarjama ya maneno yako ya kiarabu ni kama ifuatavyo (nakubali kurekebishwa nitakapo kosea);-

" Majini ni viumbe, mbali na kujibadili, haiwezekani kuonekana kwa macho ya kawaida ili kuwaona lazima uwe na maarifa".


Katika hadithi fulani za mtukufu mtume Muhammad (saw, aliwakataza masahaba zake kutumia mifupa na vinyesi vikavu vya ngamia kuchambia na akasema mifupa na vinyesi hivyo ni vyakula vya majini, na pia akatufundisha tuingiapo vyooni tusome dua ili kujikinga na majini waliomo vyooni.

Elimu ya kisayansi inatuambia kwamba katika mifupa na vinyesi vya wanyama kuna bakteria kibao ambao kama utatumia hivyo vinyesi na mifupa kuchambia utakuwa na nafasi kubwa sana ya kupata maambukizi katika njia ya haja kubwa halikadhalika chooni kulingana na mazingira yake kuna aina mbalimbali za bakteria wa maradhi mfano, Chorela, dysentery, hepatitis, kisonono nk, (hasa vyoo vya umma).

Hivyo mtukufu mtume (saw), aliposema neno "jinn" alikuwa na maana ya wadudu wadogo wasioweza kuonekana kwa macho ya kawaida na hapa nakubaliana na maneno yako ya kiarabu, na ili uweze kuwaona ni lazima utumie nyenzo maalumu kama darubini (microscope) au kwa maneno mengine uwe na maarifa (معرفة) kama ulivyosema.

Sifa kuu ya jinn ni kutokuonekana kirahisi kwa macho ya kawaida na mzizi wa neno "jinn" ni neno "janna" ambalo maana yake ni kutokuonekana, hivyo basi katika lugha ya kiarabu, kitu chochote au tukio lolote lenye sifa ya kutokuonekana kirahisi linawezwa kwa ki-SIFA likaitwa kwa jina la "jinn", na hii ipo karibu katika lugha zote hata katika kiswahili mtu shujaa anaweza kuitwa "Simba" kwa sababu tu ya ushujaa wake.

Kwa muktadha huo ki-sifa , jinn anaweza kuwa mtu mkubwa, kiongozi, tajiri, mtu mashuhuri nk--- ambao kwa hizo sifa zao kuonekana kwao mbele za watu huwa ni kwa nadra sana na inapotokea akaonekana basi lazima kuwae na jambo muhimu, na hapa ndipo Allah katika Qur'an aliposema; "Sikuwaumba majini na watu isipokuwa watuabudu"-- Majini waliotajwa hapa ni viongozi, watu mashuhuri, matajiri nk, ambao kwa umashuhuri na utajiri na uongozi wao wanaweza kujawa na kiburi kujiona kwamba wao hawastahili kufanya ibada, Watu katika aya hiyo ni watu wa kawaida wasiokuwa na utajiri, umashuhuri, uongozi nk ambao nao kulingana na hali zao za kimaisha wanaweza kusema ibada haiwahusu ila inawahusu hao waheshimiwa wakubwa (majini), ndipo Allah akakata mzuzi wa fitna akasema wote lazima tumuabudu hakuna adhuru.

Allah katika Qur'an anasema "Na majinni tumewaumba mwanzo kwa mwale wa moto," (sikumbuki aya). sayansi ambayo ni elimu kutoka kwa huyohuyo Allah inasema kwamba viumbe wa mwanzo kabisa kuumbwa walikuwa ni bakteria ainavya (Eukaryotes na prykaryotes. Check spelling) ambao waliumbwa kutokana na nuru ya radi (lightining sparks).

Qur'an katika Surah jinn, Majinn waliposikia Qur'an ikisomwa walisema, "hakika tumesikia Qur'an ya ajabu inayoongoza kwenye uongofu"(sikumbuki aya) na tena wakasema; "hakika tumesikia kitabu kilichoteremshwa baada ya Musa"(sikumbuki aya), na baadaye mtume (saw) alikuwa akifanya maombi na hao majinn "wakamzonga/ wakamzingira" (sikumbuki aya). Majinn waliotajwa katika hiyo sura ni watu wageni wasiokuwa waarabu, katika lugha ya kiarabu neno "jinn" linaruhusiwa kutumika kwa mgeni/wageni kwa sababu mgeni anaonekana kipindi tu anapokuwa na wenyeji lakini yeye sio mtu wa hapo na hivyo kuonekana kwake ni kama kuonekana kwa "jinn" na hii ni katika matumizi yale yale ya Ki- sifa ya neno jinn--, na hao wageni walikuwa ni mayahudi kutoka Nasibin, ndiyo maana wakasema; "innaa sami'i'naa kitaaba unzila min baa'd Musa" (Hakika tumesikia kitabu kilichoteremshwa baada ya Musa).


Ugonjwa unaowashika kina mama na akina dada, (Hysteria), kama nilivyosema hapo awali kuwa neno "jinn" linaweza kutumika hata kwa jambo lenye sababu isiyoonekana bali athari inayoonekana (unseen cause but seen effects). Akina mama maranyingi husumbuliwa na ugonjwa wa akili ambao watu wengi huuita mapepo, majinni na hata Maruhani, mtu anayeshikwa na ugonjwa huo kutokana na sababu mbalimbali za ndani ya mwili na nje ya mwili anashindwa kabisa kujidhibiti (uncontroll) kiakili na hivyo wakati huo akili inajiendesha yenyewe (run amok), na mgonjwa anaweza kutamka maneno au hisia alizokuwa nazo kichwani kabla ya kushikwa na huo ugonjwa (ravings) au anaweza kutamka maneno katika lugha ngeni kabisa (labda aliisikia zamani alipokuwa mdogo kwani akili ni kama memory card), na watu wakashangaa na wakaanza kuhisi kwamba; "LAZIMA KUNA KIUMBE KISICHOONEKANA KWA MACHO KUTOKA NJE KIMEMUINGIA KICHWANI NDICHO KINACHOZUNGUMZA HIYO LUGHA"😁😁---- na hapo ndipo dhana na fikra za upotishaji juu ya majinn zinapoanzia hapo, kwamba majinni ni viumbe mithili ya watu na wanaweza kumuingia mtu kichwani na wanapenda kuishi chooni, kwenye milima mirefu, magogu, baharini, katika misitu minene nk, ilmradi kila mtu anatoa fikra zake anazojenga juu ya majinni, mbaya zaidi Waalimu na Masheikh Ubwabwa biashara ya kupunga majinn kwa akina mama imekuwa ni dili kubwa na Wachungaji pia hawako nyuma katika kukemea majini mapepo. Kifupi, hayo yanayoitwa mapepo, Maruhani, jinn, Mahaba nk, yanaweza kuitwa kwa jina la "jinn" kwa sifa tu kwasababu kitu kinachosababisha mama au dada ashikwe na hali ya kuweweseka haionekani kwa macho lakini madhara yake yanaonekana kwa mgonjwa, hakuna jinn mahaba, Subiani, Affrit nk, mwenye umbo la mtu kutoka nje anayemuingia mtu, hakuna, never ever there is none.

Kutupiwa "jinn"--- unaweza kusikia watu wakisema, mfano; " Jamaa katupiwa "jinn" ndiyo maana kapata ajali, naam-- zipo elimu za "spirits", mfano, Telepathy, Hynotism (mesmerism) nk, ni elimu ambazo baadhi ya watu wanazaliwa nazo naturally au kwa kujifunza, ni elimu ambayo mtu anaweza kumuathiri mtu mwingine kwa kufanya baadhi ya mambo fulani na mtu akaathirika hata akiwa maelfu ya kilometres na mtu akaathirika huko alipo, nalo jambo hili waweza kuliita "jinn" kwasababu tu nguvu inayotenda kazi haionekani kwa macho, lakini si kwamba kuna kiumbe mfano wa mtu au watu kinaruka hewani baada ya kutumwa na "fundi" kwenda kufanya madhara kwa mlengwa.

Majini kuumbwa kwa moto, naomba nimalizie kwa kutoa ufafanuzi wa maana nyingine ya jinn kuumbwa kwa moto, mtu au kitu kuumbwa kwa moto maana yake pia yaweza kuwa ni mtu mwenye kiburi, majivuno, mwenye asili ya ukali nk, kama alivyokuwa Firauni na Ibilisi katika Qur'an.
REJEA PIA DAI LAKO HILI KUHUSU MAJINI UJUE NAZUNGUMZA NINI!?

Ndio maana nakwambia huna hoja wewe kaa kimya umeshashindwa huna la kusema zaidi ya uzushi tu na uongo na kawaida ya muongo huona wengine ni waongo pia usisahau kichaa huhisi anaakili kuliko watu wenye timamu lau kama angejua angebadilika!?
wacha kuzalisha mada ndani ya mada

Rakims
 
Wewe ndiyo huna hoja, kwani unanipinga halafu unashindwa kutoa hoja mbadala zinazokuunga mkono katika kile unachoamini,, umebaki tu kupiga kelele.😜😜.

Mungu akikupa ufahamu wa Qur'an ni raha sana.


Ewe Rakims, fanya swala ya Istikhara au Hajja ili Allah akupe heri ya kujua maana za aya za kitabu chake Qur'an.
“Malaika waliumbwa kutokana na mwanga na MAJINI waliumbwa kutokana na moto”
(Saheeh Muslim)
Kitabu wanachokubaliana nacho waislamu wote
Hivi unaumwa mkuu au hujasoma? basi soma. au kama hujui kaa kimya

Kipande hiki kinaelezea mambo mengi sana kuhusu majini sasa kama hawa majini ni bacteria mwanasayansi yupi kwenu alithibitisha maumbile yao kwa moto. Kwa sababu wao waliumbwa kwa moto, na mahusiano yao na wanadamu yamejengwa juu ya hili. kama wanadamu, wao pia wanatakiwa kumuabudu Mungu na kufuata dini ya haki na kuabudu kama wanadamu na malaika. wao jambo waliloumbiwa ni sawa na sisi kama vile mwenyezi Mungu aliposema,.

“Sikuwaumba wanadamu na majini ila waniabudu.” (Quran 51:56)

Majini pia wanaweza kuwa waislamu au sio waislamu vyovyote vile kwa asili yao ya moto wengi wao pia sio waislamu kwa nafasi kubwa sana Wote hawa majini wasiokuwa na dini wengi wao hufuata yale waliopelekewa na Jini maarufu zaidi kuliko wote ambaye ni shetani, sasa kwa hakika hawa majini wote wanaopinga na wasiokuwa na dini huitwa mashetani, Majini pia wengi hubadili na kuingia katika dini ya Uislamu kwa utajo au kauli nzito zenye ukumbusho mkubwa ambayo ni maneno au aya za Qur.an ambazo ni ukumbusho kwa wenye akili na wenye kujua. na pia hawajabadili dini katika kipindi hiki tu isipokuwa hata zama za Mtume Mtukufu wa Uislamu walibadiri na kuingia katika uislamu kwa kusikiliza Qur.an ya Ajabu yenye kusema kweli na iliyokamilika na Mwenyezi mungu akamuamuru mtu kusimulia hiki kisa. Cha majini

Na hii ndio maana ya hiyo aya unayong'ang'ania kuwa majini ni watu wakuu au funza na bacteria zako wewe na walimu wako:

“Sema (Ewe’ Muhammad): Imefunuliwa kwangu ya kuwa kundi la majini lilisikika kwa kusikiliza na kusema; Tumesikiliza Qur.an ya ajabu Kabisa. Ambayo ni muongozo wenye kuongoza kwenye haki na sisi tumeiamini na hatumshirikishi Mola wetu na chochote’.”(Quran 72:1-2)

katika mategemeo ya ulimwengu wanaoishi pia majini ni viumbe wenye ufanano kabisa na sisi: kwa maana wao wanakula na kunywa wanaoa na kuzaa pia wanakufa. Maisha na hadithi yao pia itaisha kama vile yetu na watahukumiwa siku ya malipo kama sisi na pia wataingia motoni na peponi kama sisi.
Mwenyezi Mungu Atuepushe na moto.
Kama bado hadi hapa hujajua majini wapo basi mwenyezi Mungu atakuongoza kupata elimu au kujua pindi atakapo hitaji na sisi ni wenye kukumbusha na sio wenye kuongozana kama Mwenyezi Mungu kakubadilishia wewe maana ya majini tunayoifahamu sisi basi ikifika wakati wetu na sisi atatuongoza kama vile anavyowaongoa waliopotea na kuwaweka kwenye mstari au njia sahihi! Allahuma Amin. sina cha kubishana na wewe tena kuhusu uwepo au kutokuwepo kwa majini.

Rakims
 
Umehama tena kutoka guest kwenda foreigners/strangers?

unaizungumzia vipi Surat Asabaa aya ya 15

"Na Tulipomkidhia kifo chake
(Suleimani) hakuna kilichowabainishia
kwamba yeye amekwisha kufa
isipokuwa mnyoo wa ardhini ambaye
alikula fimbo yake (Suleimani). Basi
alipoanguka wale majini walitambua
waziwazi kwamba kama wangaliyajua
yasiyoonekana, wasingalibakia katika
hali ya mateso ya kufedhehesha"

Sasa wewe unang'ang'ania uongo wako ili hapo ubadirishe mada baina yangu na wewe rejea kwenye mada yako ulivyoileta hapa:

Ulisema huo ni uongo mtupu na hakuna viumbe wa aina hiyo na kanusho lako ni kuwa hakuna majini na hapa sikuambii kuwa Qur.an ni kitabu cha majini au ni ngano za majini hapana isipokuwa nakuelimisha kuhusu usilofahamu kuhusu majini na usifanye watu wanielewe kuwa natetea mada za majini kwa msaada wa kitabu kitukufu hapana!

Rakims



Sasa tufanye jambo moja, ewe rafiki yangu Rakims.

Tufafanulie hayo majini katika hiyo aya, yaani toa maelezo ili mtu anayetaka kujua hayo majini katika hiyo aya ajue ni kitu gani !!----- kutokana na jibu lako ndipo nitajua msimamo wako.

Mimi niliisha fafanua katika post moja aina 3 za majini waliotajwa katika Qur'an pamoja na aina 1 ya "majini"/ maruhani wanaowashika akina mama, yote hayo nilitoa ufafanuzi wake.

Ufafanuzi wangu ni kinyume na itikadi potofu inayoshikiliwa na watu wengi hususan Waislamu kwamba majini ni viumbe fulani wasioonekana na wanaweza kufugwa kama mbwa na kutumwa kufanya kazi fulani, pia eti, kuna watu wanaweza kuwatengeneza majini na katika hao majinni wapo jini makata, subiani, kishkish, jini mahaba nk, na pia wanasema hayo majini yanayowashika hasa kina mama hutokea nje na kumuingia mwanamke kichwani (anapokuwa kapandisha). Kuna dhana ya uongo inayoaminiwa juu ya "majini".

Narudia tena, kwamba kuna majini wa aina 3 waliotajwa katika Qur'an, na mimi sipingi majinni waliotajwa na Allah ndani ya Qur'an, ninachopinga ni dhana za uongo zinazosemwa kuhusu "majini", mfano eti kuna jinni mahaba nk,😛😛.


Mtu akichukua ufafanuzi huo wa uongo kuhusu majini na akaenda kusoma Qur'an na akakuta majini wamezungumzwa humo, moja kwa moja anapata hisia kwamba majini hao ndio wale wanaitumwa kudhuru watu au ndio hao jini mahaba wanaoingilia watu usiku au ndio hao popobawa nk, sasa hatuwezi kuruhusu Qur'an iaminike kuwa ni kitabu cha "fables and tales" za majini popobawa, watu wengine wataogopa kuishika Qur'an kwa sababu ya woga wa " kukumbwa na majini mliowaaminisha kwa uongo wenu".
 
Sasa tufanye jambo moja, ewe rafiki yangu Rakims.

Tufafanulie hayo majini katika hiyo aya, yaani toa maelezo ili mtu anayetaka kujua hayo majini katika hiyo aya ajue ni kitu gani !!----- kutokana na jibu lako ndipo nitajua msimamo wako.

Mimi niliisha fafanua katika post moja aina 3 za majini waliotajwa katika Qur'an pamoja na aina 1 ya "majini"/ maruhani wanaowashika akina mama, yote hayo nilitoa ufafanuzi wake.

Ufafanuzi wangu ni kinyume na itikadi potofu inayoshikiliwa na watu wengi hususan Waislamu kwamba majini ni viumbe fulani wasioonekana na wanaweza kufugwa kama mbwa na kutumwa kufanya kazi fulani, pia eti, kuna watu wanaweza kuwatengeneza majini na katika hao majinni wapo jini makata, subiani, kishkish, jini mahaba nk, na pia wanasema hayo majini yanayowashika hasa kina mama hutokea nje na kumuingia mwanamke kichwani (anapokuwa kapandisha). Kuna dhana ya uongo inayoaminiwa juu ya "majini".

Narudia tena, kwamba kuna majini wa aina 3 waliotajwa katika Qur'an, na mimi sipingi majinni waliotajwa na Allah ndani ya Qur'an, ninachopinga ni dhana za uongo zinazosemwa kuhusu "majini", mfano eti kuna jinni mahaba nk,😛😛.


Mtu akichukua ufafanuzi huo wa uongo kuhusu majini na akaenda kusoma Qur'an na akakuta majini wamezungumzwa humo, moja kwa moja anapata hisia kwamba majini hao ndio wale wanaitumwa kudhuru watu au ndio hao jini mahaba wanaoingilia watu usiku au ndio hao popobawa nk, sasa hatuwezi kuruhusu Qur'an iaminike kuwa ni kitabu cha "fables and tales" za majini popobawa, watu wengine wataogopa kuishika Qur'an kwa sababu ya woga wa " kukumbwa na majini mliowaaminisha kwa uongo wenu".
Quote number 195,
kipengele cha kwanza hadi mwisho.

Rakims
 
“Malaika waliumbwa kutokana na mwanga na MAJINI waliumbwa kutokana na moto”
(Saheeh Muslim)
Kitabu wanachokubaliana nacho waislamu wote
Hivi unaumwa mkuu au hujasoma? basi soma. au kama hujui kaa kimya

Kipande hiki kinaelezea mambo mengi sana kuhusu majini sasa kama hawa majini ni bacteria mwanasayansi yupi kwenu alithibitisha maumbile yao kwa moto. Kwa sababu wao waliumbwa kwa moto, na mahusiano yao na wanadamu yamejengwa juu ya hili. kama wanadamu, wao pia wanatakiwa kumuabudu Mungu na kufuata dini ya haki na kuabudu kama wanadamu na malaika. wao jambo waliloumbiwa ni sawa na sisi kama vile mwenyezi Mungu aliposema,.

“Sikuwaumba wanadamu na majini ila waniabudu.” (Quran 51:56)

Majini pia wanaweza kuwa waislamu au sio waislamu vyovyote vile kwa asili yao ya moto wengi wao pia sio waislamu kwa nafasi kubwa sana Wote hawa majini wasiokuwa na dini wengi wao hufuata yale waliopelekewa na Jini maarufu zaidi kuliko wote ambaye ni shetani, sasa kwa hakika hawa majini wote wanaopinga na wasiokuwa na dini huitwa mashetani, Majini pia wengi hubadili na kuingia katika dini ya Uislamu kwa utajo au kauli nzito zenye ukumbusho mkubwa ambayo ni maneno au aya za Qur.an ambazo ni ukumbusho kwa wenye akili na wenye kujua. na pia hawajabadili dini katika kipindi hiki tu isipokuwa hata zama za Mtume Mtukufu wa Uislamu walibadiri na kuingia katika uislamu kwa kusikiliza Qur.an ya Ajabu yenye kusema kweli na iliyokamilika na Mwenyezi mungu akamuamuru mtu kusimulia hiki kisa. Cha majini

Na hii ndio maana ya hiyo aya unayong'ang'ania kuwa majini ni watu wakuu au funza na bacteria zako wewe na walimu wako:

“Sema (Ewe’ Muhammad): Imefunuliwa kwangu ya kuwa kundi la majini lilisikika kwa kusikiliza na kusema; Tumesikiliza Qur.an ya ajabu Kabisa. Ambayo ni muongozo wenye kuongoza kwenye haki na sisi tumeiamini na hatumshirikishi Mola wetu na chochote’.”(Quran 72:1-2)

katika mategemeo ya ulimwengu wanaoishi pia majini ni viumbe wenye ufanano kabisa na sisi: kwa maana wao wanakula na kunywa wanaoa na kuzaa pia wanakufa. Maisha na hadithi yao pia itaisha kama vile yetu na watahukumiwa siku ya malipo kama sisi na pia wataingia motoni na peponi kama sisi.
Mwenyezi Mungu Atuepushe na moto.
Kama bado hadi hapa hujajua majini wapo basi mwenyezi Mungu atakuongoza kupata elimu au kujua pindi atakapo hitaji na sisi ni wenye kukumbusha na sio wenye kuongozana kama Mwenyezi Mungu kakubadilishia wewe maana ya majini tunayoifahamu sisi basi ikifika wakati wetu na sisi atatuongoza kama vile anavyowaongoa waliopotea na kuwaweka kwenye mstari au njia sahihi! Allahuma Amin. sina cha kubishana na wewe tena kuhusu uwepo au kutokuwepo kwa majini.

Rakims



Read posts No, 111 na 132. Ili ujue nilichosema.

Malaika kuumbwa kwa nuru na majini kuumbwa kwa moto, hii haina tofauti na mtu kuumbwa kwa haraka,--- خلق الاسن من عجل---

(21:37) Mtu ameumbwa kwa haraka--


👆🏻Unaelewa nini kuhusu hiyo aya??
 
Read posts No, 111 na 132. Ili ujue nilichosema.

Malaika kuumbwa kwa nuru na majini kuumbwa kwa moto, hii haina tofauti na mtu kuumbwa kwa haraka,--- خلق الاسن من عجل---

(21:37) Mtu ameumbwa kwa haraka--


👆🏻Unaelewa nini kuhusu hiyo aya??
Quote number 195,
kipengele cha mwisho.

Rakims
 
Quote number 195,
kipengele cha mwisho.

Rakims


(1)"Kila kitu chenye uhai kimeumbwa kutokana na maji"

(2) "Na tumemuumba mtu kutokana na udongo utoao sauti" ---- Qur'an hiyo.

👆🏻Na hapo umeelewa nini??
 
Back
Top Bottom