Mjue Jini Mahaba: Fahamu mengi kuhusu jini mahaba

Mjue Jini Mahaba: Fahamu mengi kuhusu jini mahaba

Naomba unieleweshe hili ndugu.Kwa mjibu wa utaratibu wa kimajini na tiba zake na hata kumuita jini inaonyesha j mosi ni siku mbaya na hata huo mda unaoonyesha saa sita usiku mda huo huo mtawala anakuwa ni mtu wa damu je inakuwaje uite jini mda huo.lingine kwa mjibu wa mambo ya majini chumba unachomuitia jini kinakuwa hakina kitu chochote tofauti na mikeka au jamvi la kukalia ww sasa hiko kitanda cha chuma inakuwaje!
Swali zuri,
Kwa mujibu wa utaratibu wa kimajini na tiba zake na hata kumuita jini inaonyesha j mosi ni siku mbaya hili si kweli na wala si sahihi.

Kipengele kingine cha swali lako ni kuwa mtawala wa saa hiyo anakuwa ni mtu wa damu si kweli.

Kipengele kingine cha mwisho ni kuwa chumba kinatakiwa kiwe tupu hii ni kwa baadhi ya majini tofauti na huyu mahaba. na sio wote waliobaki,

Kiujumla swali lako naweza kukujibu hivi, siku ya Jumamosi ni siku kielimu ya juu zaidi kuliko hiyo uliyoishia ni Siku ya Zohali (Saturn) Siku hii hutawala sana jini aina ya MAIMUN, ambaye ni mfalme miongoni mwa majini wasiokuwa na sheria ya kuolewa au kuoa hasa kwa waliokufuru, Usiku wa siku hiyo ya Jumamosi kielimu huitwa usiku wa Atwarid (Jumatano) sasa kimahesabu ya juu kabisa saa hiyo inakuwa ni saa ya Shamsi (Jua au Jumapili) ambayo hudeal zaidi na commandment ya Shamhurash jini wa Jumapili, sasa hawa mahaba mfalme wao huwa ni Maimun au wabongo humuita

MAIMUNA, na huyu huwa yupo chini ya SHAMHURAASH ambaye ni mfalme wa Jumapili. mkuu hadi hapo nahisi utakuwa unajua nazungumzia nini nikiendelea naweza kukuvuruga tu, yule anaekwambia jumamosi ni siku mbaya na saa hiyo ni ya damu elimu yake bado ni Shallow kwa maana anategemea nguvu ya MARUHANI/Majini katika shughuli zake wala hataki kuhangaika na kuwashurutisha ndio hawa huwapa sadaka majini bila kujua kampa sadaka jini wa namna gani,

Rakims
 
Hongera mkuuu kwa somo zuri,swali langu ni kwanini MTU akiwa na jini mahaba mambo yake mengi huaribika hasahasa uchumi ushuka,kila mipango yak3 inafeli,na je kuna uhusiano wa jini makata na jini mahaba kiutendaji?
Habari mkuu, huyu jini mahaba na makata katika generation tano kuu za majini, Huyu mahaba huwekwa kwenye kundi la 2 kutoka mwisho huwekwa katika kundi la Ghoul/al-ghuul hawa hupatikana katika giza na mwanzo wa asubuhi na pia huwa hawapandi kichwani kwa mtu hadi itumike nguvu ya ziada sasa kwa hawa MAKATA kwanza hili ni jina limetungwa pia kibongo hapa lakini hawa kiasili huitwa SILA nao ni kundi la wenye nguvu na madhaifu miongoni mwa majini wote kwa maana huwa na generation ya mapepo yaani majini wanaoruka kwa nguvu ya upepo

Rakims
 
Kweli kabisa tuombe sana kwa Allah atuepushe na hivi viumbe
 
Duh, Kumbe hivi viumbe ni hatari sana.Mungu niepushie mbali
 
Nadeal na mambo ya kiroho mkuu sina tunguli,
Knowledge of spiritual science and Magic.
zaidi ya unavyofikiria

Rakims
Ahaa okay, unajua kiroho na magic huwa wanadai havichangamani, ndio maana niliuliza nilidhani unatibu kwa dawa za kienyeji ambao tuna waita waganga.

Maana yaliyoandikwa niliona kama mauchawi fulani hivi.
 
Jini mahaba analetaje ufukara maana wengi wenye mali ufanikiwa kupitia kwake?
 
Ndugu hivi ni kweli huyu jini mahaba anaweza kualibu maisha ya mtu namaanisha yani unapata pesa kwa tabu na ukiipata inaisha ovyo ovyo pesa haikai na ugomvi kwenye ndoa yani kutoelewana na mwenzio
 
Mkuu, niliwahi kusikia kuwa kila mwanadamu anapozaliwa huwa na jini wake wa asili ambaye humlinda. Na pia kila mwanadamu ana nyota yake, na kila nyota ina jini wake ambaye anatawala nyota hiyo.

Swali1:
Je, huyu jini wa nyota na huyu jini wa asili anayezaliwa naye binadamu kwajili ya kumlinda wana mahusiano gani?

Swali2:
Je, binadamu unaweza kumwita na kuwasiliana na jini ambaye anatawala nyota yako? Au jini yule ambaye umezaliwa nae kiasili anayekulinda unaweza kumwita na kuwasiliana nae ikiwa una haja ya kufanya hivyo?

Swali3:
Utaratibu wa kumwita huyo jini upoje?

Naomba kuwasilisha.
 
Jini mahaba analetaje ufukara maana wengi wenye mali ufanikiwa kupitia kwake?
Katika mafundisho ya kiislamu kuna sehemu inasema hawatakuacheni hadi mfuate ya kwao kitu kama hicho, sasa hivi akikuona huna shida nae anakutafuta kukutesa ili uingie kwako, kwa ajili ya kumtii
 
Ndugu hivi ni kweli huyu jini mahaba anaweza kualibu maisha ya mtu namaanisha yani unapata pesa kwa tabu na ukiipata inaisha ovyo ovyo pesa haikai na ugomvi kwenye ndoa yani kutoelewana na mwenzio
ndio mkuu hana tofauti na kuzini na mwanamke mwenye nuksi au mwanaume malaya! ni laana
 
Mkuu, niliwahi kusikia kuwa kila mwanadamu anapozaliwa huwa na jini wake wa asili ambaye humlinda. Na pia kila mwanadamu ana nyota yake, na kila nyota ina jini wake ambaye anatawala nyota hiyo.
Swali1:
Je, huyu jini wa nyota na huyu jini wa asili anayezaliwa naye binadamu kwajili ya kumlinda wana mahusiano gani?
Swali2:
Je, binadamu unaweza kumwita na kuwasiliana na jini ambaye anatawala nyota yako? Au jini yule ambaye umezaliwa nae kiasili anayekulinda unaweza kumwita na kuwasiliana nae ikiwa una haja ya kufanya hivyo?
Swali3:
Utaratibu wa kumwita huyo jini upoje?

Naomba kuwasilisha.

Habari mkuu kabla sijakujibu swali lako nikuulize swali uliyoshindwa kujiuliza! Je, Uliwahi kusikia wapi hizo habari?
 
Hongera mkuu, mada yako ni nzito sana. Ulichoongea kuhusu namna anavyoingia ni kweli na wanadamu wengi ni wahanga wa jini hili. Linatesa wengi sana tena sana.
 
Aisee kama jini mahaba ndo huyo mzuri hivyo potelea mbali. Acha anikute tu. Mademu wanatuchuna tu. Huyo akija hachukui hata mia yako na uroda unakula
 
Back
Top Bottom