Mjue Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa undani

Mjue Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa undani

Hivi jamani mbona wachafuzi wa Lugha wamekuwa wengi sikuhizi...
 
Nyelele sijuwi historia yake ila Nyerere naijuwa.
 
Mshana,
Hii hapo chini si sawa:

Mwaka 1953
alichaguliwa kuwa raisi wa chama cha Tanganyika African
Association (TAA), chama ambacho alikisaidia kukijenga
alipokuwa mwanafunzi katika chuo kikuu cha Makerere
.

Hebu soma hii kutoka kitabu cha Abdu Sykes:

''Uchaguzi baina ya aliyekuwa rais wa TAA, Abdulwahid na mwalimu wa shule asiyefahamika vyema pale mjini, Julius Nyerere, ulifanyika kwenye Ukumbi wa Arnatouglo tarehe 17 Aprili, 1953. Nje ya uongozi wa TAA ambao ulimpendekeza kugombea nafasi hiyo, Nyerere alikuwa mgeni kabisa kwa wote aliokuwa akiwaomba kura zao. Maisha ya Nyerere katika siasa yalianza hapo. Nyerere alikuwa mgeni na alikuwa hana historia ya kuongoza mapambano ya umma dhidi ya serikali ya kikoloni. Ukoo wa Sykes ulikuwa unatambulikana katika siasa za Dar es Salaam kwa takriban robo karne. Ukoo huu ndiyo ulioanzisha na kuongoza vyama vyote viwili, African Association na Al Jamiatul Islamiyya. Ukoo wa Abdulwahid, mtoto wa Kleist Sykes ulikuwa unafahamika kwa kuongoza mapambano dhidi ya serikali. Ushahidi wa haya ulikuwa unapatikana katika nyaraka kati ya ukoo huu na serikali ya kikoloni. Katika kipindi cha miaka zaidi ya ishirini, serikali kwa nyakati tofauti, kati ya mwaka 1929 hadi 1953 ilikuwa na barua za Kleist Sykes na za mwanaye Abdulwahid wakiwa viongozi wa African Association kuhusu madhila tofauti yaliyokuwa yakiwakabili wananchi.''

Nyerere angekuwa ameijenga TAA akiwa Makerere asingekuwa
mgeni katika uchaguzi uliomwingiza madarakani 1953.

Ukipenda kusoma habari hizi zaidi angalia:
Listowel, Judith, ''The Making of Tanganyika,'' Chatto and Windus, London, 1965.

Ukipenda kusoma historia iliyokamilika ya Baba ya Taifa Mwalimu Nyerere na jinsi
alivyoingia katika siasa alipofika Dar es Salaam, 1952 soma kitabu cha Abdul Sykes.

dVJ_zwk0Zjnq3yBiAGQP54g0aWqLKc0y3RdQnYi-u5ll06Lb50pwdYkZ2bgoml1pMzmS25m8JBv7E3mUGveI9tio7cEhq4yzvHfPx04Mn9wn1VtZmtlcOax4CUga7xr9M8sq2r1uW98voQjaydmXExmNJ3ZY7dgfQBhwXKzgU4unHxQnRsMkt7xnxjidDDGrxmWkpnG7JMd2t_elgi3SqptutNWTBa9vyM74FcXGjcxB7uLfGvSgLc3cc_CrPuhM84ftMNjp4vMFTKOtM6AG6FjwxKApOs2SDxF_4xi2UcBrADgz5tTGlUx3IvCylvc1nBELG9c7vGTY73HnANbwXFPAYzMxtdEmupwG2vMUr9MankCr2UDHR7PTl2FACizfsNxIlpAGdtib1gS1t6UQKz13PEt05ziUFzNsZ7r5ljU_T5Dx0ejwYzr7FXj6dgOMmSxSokE4goNEPy9ruti2oh48zcGZ_eRP3z8OaEU7bWEEZ3VFs1JJ-Y5q1OYl2l_jQTB8-WHypnlIkII8PRaOjgrJxAiPXDlLFBuUdaFQ3JOm_kz4ikXkMwSlzJAkiZa9az9ow40viDsez5j52iN-96tf1_WAgU3O95I7Goj0-_FP_cKlpoHXS8VR=w800-h588-no
 
Sheikh Mohamed Said pole kwa usumbufu wa hawa wengine ila mimi nakupa shukrani zangu za dhati na pia nasubiri kupokea historia na mafunzo toka kwa wazee wetu wengi wengine.
[HASHTAG]#ShukranMohamedSaid[/HASHTAG]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mshana,
Hii hapo chini si sawa:

Mwaka 1953
alichaguliwa kuwa raisi wa chama cha Tanganyika African
Association (TAA), chama ambacho alikisaidia kukijenga
alipokuwa mwanafunzi katika chuo kikuu cha Makerere
.

Hebu soma hii kutoka kitabu cha Abdu Sykes:

''Uchaguzi baina ya aliyekuwa rais wa TAA, Abdulwahid na mwalimu wa shule asiyefahamika vyema pale mjini, Julius Nyerere, ulifanyika kwenye Ukumbi wa Arnatouglo tarehe 17 Aprili, 1953. Nje ya uongozi wa TAA ambao ulimpendekeza kugombea nafasi hiyo, Nyerere alikuwa mgeni kabisa kwa wote aliokuwa akiwaomba kura zao. Maisha ya Nyerere katika siasa yalianza hapo. Nyerere alikuwa mgeni na alikuwa hana historia ya kuongoza mapambano ya umma dhidi ya serikali ya kikoloni. Ukoo wa Sykes ulikuwa unatambulikana katika siasa za Dar es Salaam kwa takriban robo karne. Ukoo huu ndiyo ulioanzisha na kuongoza vyama vyote viwili, African Association na Al Jamiatul Islamiyya. Ukoo wa Abdulwahid, mtoto wa Kleist Sykes ulikuwa unafahamika kwa kuongoza mapambano dhidi ya serikali. Ushahidi wa haya ulikuwa unapatikana katika nyaraka kati ya ukoo huu na serikali ya kikoloni. Katika kipindi cha miaka zaidi ya ishirini, serikali kwa nyakati tofauti, kati ya mwaka 1929 hadi 1953 ilikuwa na barua za Kleist Sykes na za mwanaye Abdulwahid wakiwa viongozi wa African Association kuhusu madhila tofauti yaliyokuwa yakiwakabili wananchi.''

Nyerere angekuwa ameijenga TAA akiwa Makerere asingekuwa
mgeni katika uchaguzi uliomwingiza madarakani 1953.

Ukipenda kusoma habari hizi zaidi angalia:
Listowel, Judith, ''The Making of Tanganyika,'' Chatto and Windus, London, 1965.

Ukipenda kusoma historia iliyokamilika ya Baba ya Taifa Mwalimu Nyerere na jinsi
alivyoingia katika siasa alipofika Dar es Salaam, 1952 soma kitabu cha Abdul Sykes.

dVJ_zwk0Zjnq3yBiAGQP54g0aWqLKc0y3RdQnYi-u5ll06Lb50pwdYkZ2bgoml1pMzmS25m8JBv7E3mUGveI9tio7cEhq4yzvHfPx04Mn9wn1VtZmtlcOax4CUga7xr9M8sq2r1uW98voQjaydmXExmNJ3ZY7dgfQBhwXKzgU4unHxQnRsMkt7xnxjidDDGrxmWkpnG7JMd2t_elgi3SqptutNWTBa9vyM74FcXGjcxB7uLfGvSgLc3cc_CrPuhM84ftMNjp4vMFTKOtM6AG6FjwxKApOs2SDxF_4xi2UcBrADgz5tTGlUx3IvCylvc1nBELG9c7vGTY73HnANbwXFPAYzMxtdEmupwG2vMUr9MankCr2UDHR7PTl2FACizfsNxIlpAGdtib1gS1t6UQKz13PEt05ziUFzNsZ7r5ljU_T5Dx0ejwYzr7FXj6dgOMmSxSokE4goNEPy9ruti2oh48zcGZ_eRP3z8OaEU7bWEEZ3VFs1JJ-Y5q1OYl2l_jQTB8-WHypnlIkII8PRaOjgrJxAiPXDlLFBuUdaFQ3JOm_kz4ikXkMwSlzJAkiZa9az9ow40viDsez5j52iN-96tf1_WAgU3O95I7Goj0-_FP_cKlpoHXS8VR=w800-h588-no

Watu wengine wanasoma au wanasikiliza bila kujua kuna kitu kinaitwa critical thinking

Kuna hoja mbili kuhusu hili

1.Mohamed ameondoa ushiriki wa watu makusuadi katika historia anayosema ni ya Tanganyika, ingawa mambo yakibana husema ya wazee wake na ikiwa ngumu zaidi husema ya Waislam

Kosa ambalo Kivukoni walifanya kwa kutotambua michango mingine, kwake lina uhalali

2. Historia ina formula, kuieleza au kuiandika kwa mujibu wa matukio na wakati kama ilivyo
Jaribio la ku ''interject'' personal feelings or ideas, historia husota madole ya machoni dhahir shahir

Kwa waliosikiliza video, Mohamed anasema Kleist Sykes aliunda AA na kisha Jamii fil Islamiya 1933. Mohamed hakueleza chochote kuhusu Cecil Matola.

Kumtaja Cecil ni kumtaja Rais wa kwanza na hivyo hoja ya Kleist kuunda AA inakufa.
Katika maandishia anasema, Kleist aliunda kwasababu alikuwa na pesa na mashuhuri.

Mohamed haelezi Cecil Matola alikuwa msomi na 'immunity' dhidi ya Wakoloni kuliko Kleist
Tendo la kutomtaja Matola, historia haikukaa kimya imemnyooshea kidole

3. Mohamed anasema Abdul Aliunda TANU, Nyerere akiwa Rais wa TAA kabla ya 1954.

Kitendo cha kumuondoa Nyerere, historia inamzaba kibao Mohamed.
Huwezi kuwa Rais wa chama asiyejua transformation. Abdul hakuunda TANU, alishiriki

1929 cecil akiunda AA hadi uchaguzi katika miaka ya 1950 Abdul ni takribani miaka 23.
Kleist na Mwanawe Abdul walibaki na uana harakati kwa miaka 23.

Nyerere aliandika katiba ya TANU katika transformation ya chama kuwa ya kisiasa
Akafungua milango UN kwa kutumia usomi, na kupata Uhuru katika miaka 10

Mohamed hasemi hilo, lakini historia inamsuata bila mtu kuandika kitabu kingine

Miaka 23 Kleist na mwanae Abdul Sykes hawakuwa na wazo la kuandika katiba
Wazo amekuja nalo Nyerere. Ndio maana Mohamed hajibu hoja za nani aliandika katiba
Hataki kumsikia Nyerere mtu anayemchukia sana katika dunia hii

Mohamed anasema hotuba ya Nyerere UN iliandikwa na kamati ya watu watano.
Katika hao Mohamed hamtaji Nyerere aki back date kuandikwa kwake.

Historia inamshataki Mohamed, kama hotuba iliandikwa kabla ya Nyerere ni nani aliyetarajiwa kwenda UN?

Historia inasema kama kamati iliandika hotuba, kulikuwa na tatizo gani ikiwa lilikuwa suala la chama?
Kuna shida gani chama kuandika hotuba kubwa kama ya UN na kumkabidhi mhusika!

Mohamed anaingiza hoja kuonyesha Nyerere alisoma tu bila kujua maudhui ili kumdhalilisha.

Historia inamtetea Nyerere. Wakati hotuba inaandikwa yeye ni mmoja wa watu wachache sana waliokuwa na degree katika kiwango cha Master. Alishakuwa exposed katik siasa za dunia

Mohamed anaweza kumdhalilisha Nyerere atakavyo, wanaosoma kwa critical thinking watakuwa na rafiki yao mmoja anayeitwa Historia atakayewasaidia kuchambua chuki na ukweli
 
Baba wa taifa la Tanzania Mwl. Julius Kambarage Nyerere mzaliwa Kijijini butiama.

Alizaliwa tarehe April,1922 na alikua ni mtoto wa chifu Nyerere Burito Alipewa Jina la Kambarage kumaanisha “roho inayotoa mvua”
kwakuwa alizaliwa siku ambayo mvua ilikua inanyesha.

IMG_3979.jpeg


Shujaa huyu wakizanaki ndiye mtanzania wa kwanza kupewa shahada ya uzamili nchini Uingereza.

Apo awali alikua ni mwalimu wa shule kwakuwa alihitimu katika chuo kikuu cha makerere shahada yake ya kwanza ya uwalimu

Na baadae aliiongoza nchi kwa awamu nne mfululizo.

IMG_3980.jpeg


Afrika ilimpa heshima kama mpinga ukoloni na kwenye kampeni za uhuru wa Tanganyika alitumia mbinu zisizo za vurugu.

Nyerere alichochewa na kiongozi wa uhuru wa India, Mahatma Gandhi.

Nyerere alifanya kampeni kwa ajili ya uhuru wa Tanganyika na alifanikiwa mnamo Machi 1961.

IMG_3981.jpeg


Baada ya Mapinduzi ya Zanzibar 1964.

Abeid Karume alijitangaza kuwa rais wa zanzibar na alianza kugawa ardhi iliyokuwa ikimilikiwa na Waarabu kwa wakulima weusi.

Mwezi Aprili 1964 alitembelea Karume; siku iliyofuata walitangaza muungano wa kisiasa wa Tanganyika na Zanzibar.

IMG_3982.jpeg


Mapinduzi ya zanzibar yalitimia Januari 1964 na kusababisha kuangushwa kwa Sultan wa Zanzibar, Jamshid bin Abdullah, na serikali yake ambayo ilikuwa na Waarabu wengi.

John Okello, kiongozi wa vijana wa tawi la ASP Pemba, aliandaa wanaume wapatao 600–800 kisiwani unguja.

IMG_3983.jpeg


Baada ya kushinda nguvu za polisi wa sultan walichukua silaha zao
Na walielekea mjini, ambako walipindua serikali ya Sultan.

Long story…short 🤕,

Inaelezwa sababu ya muungano ilikuwa kuzuia Zanzibar isiingie kwenye mzozo wa vita baridi sawa na ile iliyokuwepo ndani ya Kongo

IMG_3984.jpeg


Turudi kwa mwalimu

Alifanya mengi katika taifa hili yakiwemo:

- KuioTanzania kwenye vita dhidi ya iddi Amin wa Uganda mwaka 1978-1979. Na alimsaidia Milton Obote kwa kushinda vita kati yake na bregedia Iddi Amin Dada.

IMG_3986.jpeg
IMG_3985.jpeg


Pia alikuwa mtoa wosia mzuri sana kwetu sisi watanzania

Am out waungwana

For more follow me on X @AbdoullrahmanY1

Kama umependa uzi unaweza tuma ata vocha 😂
+255694950301
 
Back
Top Bottom