Mkaka mzuri, ana magari na kazi nzuri ila amenikosa kwa utongozaji wake wa kitoto

Mkaka mzuri, ana magari na kazi nzuri ila amenikosa kwa utongozaji wake wa kitoto

Nilikuwa nimekaa zangu kwenye mgahawa fulani. Akaja mkaka mzuri tu na alikuwa amependeza. Akakaa kiti cha mbele yangu.

"Mambo? Nimependa nikae na wewe hapa." Akaniongelesha.

"Haina shida." Nikajibu.

"Mbona huna kinywaji au chochote? Agiza chochote. Usikae kinyonge hivyo" Aliuliza.

Nikamjibu "Nimeagiza chakula. Ndio nakisubiri."

"Oh sawa. Vizuri tufahamiane. Me naitwa James, naishi (******). Nafanya kazi hapo (****) Bank kama branch manager. Nikufahamu na wewe please!"

"Naitwa Ederra. Naishi (******).". Nikajitambulisha.

Akaendelea na stori nyingine kwa dakika chache kisha akainuka na kusema angerudi pale punde. Baada ya dakika tatu akarudi.

"Nimerudi Ederra. Nilienda kuangalia gari yangu. Nilikuwa na wasiwasi kama nilikuwa nimepandisha vioo." Akasema huku akikaa tena kwenye kiti.

"Sawa. Karibu tena."

"Asante. Nilikuwa naogopa isije kunyesha mvua au watu wakaniibia KiBMW changu. Unajua gari yenyewe ni mpya nisije kupata hasara. Nilichoka kutembelea Harrier nikaona ninunue na hii"

"Yeah wasiwasi ndio akili." Nikamuunga mkono.

Chakula kikafika. Na yeye akaagiza. Nikawa naendelea kula huku nikisikiliza stori za magari yake, kazi yake nzuri, anapoishi na nyingine kama hizo mpaka nikamaliza kula.

Mhudumu alipokuja kuleta chakula cha jamaa nikamuomba bill.

"Acha tu nitalipa Ederra. Unalipaje wakati mimi niko hapa?" James akaingilia kati.

"Oh sawa. Nashukuru sana."

Nikamuaga kuwa naondoka. Akaniomba namba ya simu. Nikamwambia anipe yake ningemtafuta. Akanipa business card yake na kung'ang'ania nimpigie pale pale lakini nikamwambia asijali ningemtafuta tu. Nikaondoka.

Ile business card niliitupa kwenye dustbin baada ya kupotea kwenye upeo wa macho yake. Nisamehe James. Sio kwa ubaya.

Mwanaume unapotumia nguvu kutaka kuonesha magari unayoendesha, kazi yako unayoiona nzuri, unapoishi na mafanikio yako mengine kwa mwanamke ambaye ndiye kwanza unakutana naye unadhani ndiyo utamvutia?

Hii tabia haivutii. Meseji ya nje unayoileta kwa kufanya hivyo ni kuwa wewe ni mtu wa maana sana na mwenye mafanikio. Meseji hii ya nje sio inayoathiri mvuto wako kwenye akili ya mwanamke.

Meseji iliyojificha (ya ndani kabisa) ndio inayoathiri mvuto wako. Hiyo ni kwamba hujiamni na unadhani huna thamani wewe kama mwanaume na hivyo unalazimika kutumia vitu kama magari, kazi, mafinikio ili uonekane una thamani. Hakuna mwanamke anayejielewa anavutiwa na mwanaume wa hivi.

James asante kwa kunilipia chakula. Lakini wewe na wanaume wengine wenye akili kama zako badilikeni. Itawasaidia.

Jifunzeni kuwa na tabia zinazowavutia wadada. Mnaweza kusoma vitabu hivi viwili mtanishukuru baadae.

1) "UNLOCK HER LEGS: How to Effortlessly Attract Women..." By Dominic Mann

2) "MWANAUME WA DHAHABU : Jifunze Namna ya Kuwatawala Wanawake na Kutawala Mahusiano." By Anita Shija

Mwanaume tafuta uvisome yasije kukukuta ya James. Hasa hicho cha Kiswahili. Usipovipata njoo nikutumie bure tu. Utachangia bando lakini.
Kwa hiyo mwamba watu hao wanakukata stimu kinoma noma
 
Yani niwe na nia ya kumtafuta halafu nimuandike humu? Is this possible?!
Si ajabu kuona mwanamke anampomda mshikaji lakini mwisho wa siku anaishiwa kuliwa na mwanaume huyo huyo.
 
Nitumie hicho kitabu cha mwanaume wa dhahabu afu nije nikutongoze
 
Object or a goal determines the approach..james alipokuona automatically ...aproach ikaja ni hiyo..materialistic.na hii mara nyingi inatumika kwa ma manz cheap and desparate.hatuna uhakika kama kweli alikukosa..maana mpaka utake time kucompose hizo detail zote..kuna kitu unaficha either uliliwa saa hii unajifariji because unajichukia kwa kuonekana cheap..
 
Sikuwa tayari. Sivutiwi na wanaume wasiojiamini. Na sio mimi tu. Kujiamini ndio silaha kuu ya kuvuta warembo.
Sasa nan kamkosa mwingine hapo. Umejipunguzia chanzo cha mapato!
 
Siyo mbaya sana James atapata tu pisi nyingine halafu maisha yataendelea tu, Mademu wenyewe mbona wengi tu
 
Upo sahihi kabisa. Na hata atakaemkubali kwa sababu hizo anazozitoa basi atakuwa hajitambu. Hiyo inaleta picha kuwa amakuweka kwenye kundi la wanawake malimbukeni. Wanaoshtuliwa na magari na kazi nzuri. Farasi kabisa!
 
Uko sahihi kwa ulichokifanya. Nakupongeza. Binafsi nakereka sana ninapokutana na mtu unayekutana naye mara ya kwanza alafu anaanza kutaja mafanikio yake kimaisha wakati hujamwuliza. Si katika mahusiano tuu hata katika urafiki wa kawaida hata ikiwa ni mwanaume mwenzako. Picha ya kwanza inayoonekana hapo ni ulimbukeni, na anaona hilo gari au kufanya kwake kazi bank au taasisi flani kubwa kubwa ndo silaha pekee ya kuwachapia wanawake. Wanasahau kuwa kuna bad boys wanakula pisi kali huwezi amini.

Back in 2007 niliwahi kukutana na class mate wangu wa advance pale UDSM karibu na hill park. huyu dogo alisoma economics na mimi nikasoma education. Sasa mbwembwe zake kwa sababu hatukuonana muda mrefu cha kwanza akaanza kuniambia anafanya kazi wizara ya viwanda, hapo hapo akanionyesha gari yake, hapo hapo kanionyesha picha ya nyumba yake anayojenga changanyikeni. Hapo hata sijamwuliza wala hajaniuliza kuhusu issues zangu. Upuuzi wake alidhani mimi nitakuwa nimeenda kufundisha sekondari kama ilivyozoeleka kumbe niko kwenye taasisi nyingine kubwa tena mshahara hatupishani sana. Hata hivyo nikaona ujinga kujitambulisha kihivyoo, tukaachana bila kumwambia nafanya kazi wapi. Na sasa hivi kama ni elimu nimeshamzidi ngazi moja. Dharau mbaya
Mkuu naamini aliumia na anaendelea kuumia kwa wewe kuondoka bila kujua unafanya nini na uko wapi kimaisha amini nalokuambia maana alitegemea na wewe utamwambia mambo yako hasa akiamini anakuzidi
 
Naona umemstahi sana ametushushia heshma sisi natamani ungemchana japo kidgo haiwezekani kwa umri aliyonao anze na swaga izo zilizo pitwa na wakati
Wanaume tuko wa dizain nyingi wengine wakitongoza huwa ponda wenzao hasa kama anajua mwingine anayekula mzigo au kufuatilia, utasikia achane na yule furani hana issue wala maajabu na uongo mwingi na uzushi mara mimi ndo bora nina moja mbili yaani upuuzi mtupu
 
Wanaume tuko wa dizain nyingi wengine wakitongoza huwa ponda wenzao hasa kama anajua mwingine anayekula mzigo au kufuatilia, utasikia achane na yule furani hana issue wala maajabu na uongo mwingi na uzushi mara mimi ndo bora nina moja mbili yaani upuuzi mtupu
[emoji23][emoji23]
 
Tafuta pesa sana kwa kufanya kazi kwa bidii. Lakini usijidanganye kuwa ukiwa na pesa utapata kila mwanamke unayemtaka. Bado kuna wanawake wengi wazuri watakuwa na pesa zaidi yako na wale ambao pesa zako haziwezi kuwa kigezo cha kuwarubuni.

Ndio maana nawaambia someni vitabu nilivyowashauri. Ukisoma hivyo vitabu, angalau kimoja tu thamani yako ya uanaume itapanda mara tatu au zaidi.
Labda wa ulaya. Hapa bongo hata wenye pesa bado wanaomba pesa. Wanatofautiana mahitaji tu ila wote wanaomba.
 
[emoji23][emoji23][emoji23] Nani aliyewadanganya ukiwa na hayo magari unapata kila mwanamke unayemtaka? Ndio maana mkiwa nayo mnahangaika kuyatangaza? Legeza ubongo kidogo. Acha uTomaso. Chukua madini yatakusaidia.
Mmmmmmhmn we umeamua tu kukaza fuvu na ubishi ila ukweli ni kuwa mnapenda wanaume wenye magari. Na mpo tayari kumuacha mwanaume mwenye upendo wa dhati na kuwa na mwanaume mwenye gari na familia yake.

Hizo pembejeo zenu mnazopakaa usoni na hilo jua la Dar unadhani mnaishi vipi kwa mfano. Gari ni zaidi ya pesa kwenu.
 
Back
Top Bottom