Mkakati wa mama mwenye nyumba kushinda uchaguzi mkuu wa 2025 kwa 95% huu hapa umeshawiva tayari

CCM imewahi kupitisha nchi kwenye hali ngumu, kwa sasa mambo si magumu, nchi itapita kwa wepesi tu.

Lini serikali imewahi kulipa mishahara kwa mikopo kutoka nje?. Lini Deni la Taifa limewahi kufika 91 trilion?. Mwakani tu litafika 100 Trilioni. Uchumi hovyo na siasa ni hovyo.
 
Chadema wanataka katiba mpya ipi ikiwa ya kwao wenyewe imewashinda?
Je wakiingia madarakani na kuirudisha hii iliyopo ili imnufaishe mwenyekiti na genge lake kama alivyofanya kwa katiba ya chama chake ni nani atamzuia?

Kwani Mbowe atakaa milele?. Yani katiba Ni mbovu kisa haina ukomo wa Mwenyekiti?. Hicho tu?. Mbowe akistaafu inakuwaje?. Katiba itaendelea kuwa mbaya?
 
Lini serikali imewahi kulipa mishahara kwa mikopo kutoka nje?. Lini Deni la Taifa limewahi kufika 91 trilion?. Mwakani tu litafika 100 Trilioni. Uchumi hovyo na siasa ni hovyo.
Serikali ya CCM imewahi kupita nyakati ngumu ambazo huenda hukuwahi kuzisikia au kutangaziwa. Deni kuwa 100T sio tatizo iwapo ni himilivu na nchi inalipa. Uchumi wa Tanzania umeendelea kuwa imara. Ccm itaeendelea kuwa chama sahihi kuiongoza Tanzania 2025-2030.
 
Kwani Mbowe atakaa milele?. Yani katiba Ni mbovu kisa haina ukomo wa Mwenyekiti?. Hicho tu?. Mbowe akistaafu inakuwaje?. Katiba itaendelea kuwa mbaya?
Atakaa milele mara mbili mbona tayari yupo milele
 
Unajitahidi kuandika ushuzi kwani kati ya uchaguzi aliogombea urais lowasa 2015 na ule wa2010 niupi uliongoza kwa changamoto kwa CCM kama kampen hakushiliki huyo slaaa aliondoka nakundi lake ila CDM ilitisha vilevile
Kilicho fanya upinzani kudorola ninguvu nyingi alizo tumia magu kununua baadhi yaviongozi,kuwatisha watu kwakudili naviongozi mfano kipigo alichopokea lissu nahakuna kingine kilicho warudisha nyuma
Kuhusu uandishi wangu hatufanani kielim chamsingi umeelewa andiko langu
 
Tunajua Tanzana hakuna upinzani mkuu.Vyama mbona ni madili ya CCM.Ni wadanganyika tu ndio wanaopoteza muda kupigia upatu walamba asali.
 
Umeandika upuuzi mtupu kwa kutanguliza hisia zako badala ya ukweli wako. Unajaribu kuangalia changamoto za uchaguzi wa mwaka 2010 na zile za 2015 bila kutaja uhalisia uliosababisha hizo changamoto hizo.

Ngoja sasa nikufungue kichwa chako ambacho kimekaa tu kusubiri kumezeshwa uongo na hawa wapinzani uchwara.

Mwaka 2010 chadema chini ya mgombea wake dr Slaa waliingia katika uchaguzi ule wakiwa peke yao bila kushirikiana na chama chochote, Mwaka 2015 chadema ikishirikiana na vyama vingine kama vile nccr mageuzi, cuf na vingine ambavyo sio lazima kuvitaja majina vilishiriki uchaguzi huo dhidi ya chama kimoja CCM. Kwahiyo angalia tofauti kati ya chadema ya dr slaa ikiwa peke yake na ile ya lowasa ikiwa na vyama vingine zaidi ya 5 na bado walishindwa na CCM.

Kingine usije ukaleta habari za mipasho zisizokuwa na fact. Unasema kuna wapinzani walionunuliwa bila kuweka fact ya kuonesha kuwa walinunuliwa kwa bei gani kupitia account gani na kwa ushahidi gani?
Kuhusu utawala wa Magu kutumia nguvu sio kweli, nguvu zilianza kutumika toka wewe haujajua siasa.

Vyama kama vile CUF vilianza kukutana na misuko suko toka miaka ya 2000 huko watu walikuwa wanakamatwa, wanateswa, wanapigwa nk lakini hawakuacha kuandamana. Hata wakati wa Kikwete watu walipigwa, waliteswa, walikamatwa na hata kuuwawa katika maandamano mbali mbali lakini bado watu hawakuogopa kuandamana. Ilifikia kipindi mpaka waandishi wengine waling'olewa kucha, na wengine kupotezwa katika mazingira ya kutatanisha lakn bado watu waliendelea kuandamana.

Sasa baada ya ule uozo wa mwaka 2015 watu ndo wakashtuka na kuamua kuachana na ujinga wa kuandamana kwa ajili ya kuwajengea umaarufu wanasiasa uchwara huku wao waandamanaji wakiishia jela, kufa na wengine kutiwa ulema wa maisha.
 
Sio kila anaewakandia ni ccm. Hizi akili hizi ndo zinafanya msishike dola.
Huko kwao hakuna demokrasia au uhuru wa kukosoa. Ndio maana akitokea mtu akakosoa lazima wajue kuwa ni CCM ambako uhuru wa kukosoa ni ruhusa.
Kwao swala la kukosoa ni usaliti mkubwa, nikiwa na maana kwamba kwao ni bora mtu amkosoe Mungu kupitia biblia au qur ani, lakini sio kumkosoa mwenyekiti wao kupitia katiba ya chama chao.
 
Hili huwa hawakubali kamwe, humshambulia aliekosoa vilivyo. Hawachelewi kumuita "mlamba asali"
 
Hili huwa hawakubali kamwe, humshambulia aliekosoa vilivyo. Hawachelewi kumuita "mlamba asali"
Na wakati "mlamba asali" wanae ndani ya chama chao ila kwa vile kawatia mfukoni, basi hawana ujanja wa kumwita jina hilo.
 
Nyie vijana wa Tz tambueni:-

KAMWE CCM HAITAONDOKA MADARAKANI kama mnaacha vyama vya upinzani ndivyo vidai usawa. Kama mnaona ccm inawaonea, jiungeni wote bila kujali chama muwaambie wanawaonea vipi.

Nyie mnadai vyama vya upinzani vinawekwa mfukoni. Angalieni IRAN. Ni nchi ya siasa kali sana ya Kiislamu na wanaopinga serikali wanauawa. Lakini WANAWAKE wameanzisha maandamano nchi nzima bila kujali vyama na japo wanauawa kwa kupigwa risasi, hawaachi kuandamana. Hao ni WANAWAKE.
 
Kuanzia mwaka 2000 hadi 2015 vijana wengi waliandamana sana bila kujali kupigwa, kuumizwa, kufungwa, kuteswa na hata kuuwawa. Kilichotokea Zanzibar mwaka 2001, Soweto kule Arusha mwaka 2012 na patashika zingine zilizopelekea watu kufa na wengine kupewa vilema vya kudumu ni vielelezo tosha kuwa vijana walikuwa tayari kujitoa kwa ajili ya haki zao huku wakiongozwa na misingi haswa ya vyama vyao.

Lakini kiini cha pingamizi la maandamano au mgomo wa kuandamana ulianza mwaka 2015 baada ya viongozi waliopewa dhamana ya kupigania haki za wale walikuwa wanahisi wanaonewa kubadili gia angani na kuwakaribisha wale waliokuwa wanasababisha vijana waandamane hadi kufa wagombee uraisi tena katika mazingira ambayo hakuna mtu aliyategemea. Na kibaya zaidi viongozi hao waliobadili gia angani wanashtumiwa kwa kutumika na serikali kupitia kile kitengo cha siri. Huku wanawazuga wadanganyika kwamba wanapambania haki zao, huku wanavuta mshahara safi kwa kuhakikisha mambo yanakwenda kama yanavyokwenda sasa.
 
Hawezi kuwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…