Mkandarasi wa barabara ya Mbeya mjini inayokwenda kwenda Zambia amesusa kutokana na kutolipwa na serikali?

Mkandarasi wa barabara ya Mbeya mjini inayokwenda kwenda Zambia amesusa kutokana na kutolipwa na serikali?

Wakuu, weekend hii nimeingia Mbeya kwa ku-drive toka Dar, na nikashangaa sana kukuta maendeleo kidogo sana ya ujenzi wa hii barabara ya kwenda Tunduma hadi Zambia toka nitembelee hapa miezi minne iliyopita. Nimeuliza wenyeji kwa nini kasi ya ujenzi wa barabara hii uko chini kiasi hiki? Nimeambiwa wakandarasi wa barabara wamesusa baada ya kuwa hawalipwi na serikali.

Sasa Mbeya ni jimbo la Spika wa Bunge Tulia, na huko nyuma tuliambiwa miradi ya maendeleo Mbeya haifanyiki kama adhabu kwa watu wa Mbeya kwa kumchagua mtu wa upinzani kama mbunge wao, Sugu. Sasa kulikoni tena Mbeya mambo hayaendi na mbunge wao ndio huyo Spika wa Bunge Tulia?

Au labda sasa serikali imewasusa tena kwa sababu ya Mwabukusi wa TLS?
Mkandarasi anadai pesa miradi imesimama harafu Kuna Watu wanatumia Bilioni 34 eti kujenga makumbusho ya Marais ambayo sijui hata nani ataenda kuyasoma wakati hakuna Cha maana wamefanya hao Marais ukimtoa Nyerere.

Nchi Haina vipaombele,hovyo kabisa 👇👇

View: https://www.instagram.com/p/DAkUihpNVl5/?igsh=MXFsaWFjcTlkYTR4Yw==
 
Miradi mingi ya barabara inapumulia mashine.Kuna jamaa yangu mmoja ni mkandarasi wa ndani huwa tunapiga stori ana hali mbaya sana ,njaa ikizidi anaweza kula hata godoro.Anadai serikali haitoi hela wanategemea January,2025 labda ndio iwalipe.
 
Nipo Mbeya toka katikati ya mwezi wa nane... ujenzi kipindi hiko ulikuwa umesimama kabisa kiasi cha watu kujichukulia vifusi vilivyowekwa kwa ujenzi.

Wiki ya 39 ndio umeanza tena... na wengi wanasema kuwa sababu ya ujenzi kusimama ni malipo.

Mkandarasi anaitwa CHICCO.
Huenda ni kweli kabisa.....
 
Miradi mingi ya barabara inapumulia mashine.Kuna jamaa yangu mmoja ni mkandarasi wa ndani huwa tunapiga stori ana hali mbaya sana ,njaa ikizidi anaweza kula hata godoro.Anadai serikali haitoi hela wanategemea January,2025 labda ndio iwalipe.
Na 2025 ni mwaka wa uchaguzi.
 
Mkandarasi anadai pesa miradi imesimama harafu Kuna Watu wanatumia Bilioni 34 eti kujenga makumbusho ya Marais ambayo sijui hata nani ataenda kuyasoma wakati hakuna Cha maana wamefanya hao Marais ukimtoa Nyerere.

Nchi Haina vipaombele,hovyo kabisa 👇👇
Hii ni kwa ajili ya makumbusho yake mwenyewe Samia, asitumie kisingizio cha maraisi waliopita. Anataka tu asisahaulike kama raisi mwanamke wa kwanza Tanzania
 
Ndio,lakini tulielewa serikali ilikuwa inafanya makusudi kutopeleka miradi Mbeya kwa sanabu Mbeya hawakuitaka CCM. Sasa Mbeya si waliahidiwa wakiwaondoa upinzani miradi yao itaenda? Kulikoni sasa?
Kinashangaza na hujuma zote bado kimapato iko juu,hili fisiem linawauma sana!
 
Porojo za vijiweni 👇👇
Haya mambo inaonekana huelewi yanavyoenda. Ni kweli kwamba sasa wanaweza kuwa wamepata hela za kuendelea na kazi na kutoa video kama hizi kwa sababu wanajua watu waliona kuwa mradi umesimama. Unafiiri, kwa uwezo wa akili yako, watakuambia kweli tulipata changamoto sasa kuna fedha kidogo imepatikana tunaendelea ila mradi utachukua zaidi ya miaka miwili tofauti na ilivyokuwa imepangwa? Hata kama wamepata fedha ya miezi mitatu tu watasema hakuna tatizo mambo yako sawa mradi utakamilika -ila kukiwa na sababu za msingi za ucheleweshaji mkandarasi atatuandikia. Hebu jaribu kuwa na akili uliyopanuka kuelewa mambo ya serikali yanavyowekwa hadharani
 
Back
Top Bottom