Ashasembeko
JF-Expert Member
- Dec 14, 2017
- 225
- 910
Ni siri iliyo wazi kuwa Hayati Benjamin Mkapa alikuwa nguzo muhimu sana CCM haswa katika utawala huu wa Magufuli. Mkapa alikua mtu pekee ambae alikua haogopi kumpa Magufuli za uso. Magufuli mwenyewe alikua sio tu anamheshimu sana, bali alikua anamchukulia kama baba yake maana Mkapa ndiye aliyemsaidia kuingia kwenye ulingo wa siasa, na alichangia sana yeye kuwa Rais 2015.
Mkapa ndiye alimnadi Magufuli jukwaani 1995 wakati anaomba ubunge Chato ambao Magufuli alishinda. Akamteua kuwa Naibu Waziri na baadae kuwa Waziri kamili. Tunajua Mkapa alizungumza wazi uchapakazi wa Magufuli mpaka kumuita Askari wake wa Mwavuli, hali iliyosababishwa Magufuli kunyweshwa sumu na "watu" waliodhani anaandaliwa na Mkapa kuwa Rais 2005. Mkapa aliendelea kumlinda na hata kumpa ulinzi wa usalama wa taifa.
Mchakato wa Urais 2015
Tunajua Lowassa alikatwa 2015 sababu Kikwete alitaka Membe amrithi Urais. Vyanzo mbalimbali ndani ya chama vinasema Kamati ya Wazee, kwa ushawishi mkubwa wa Mzee Mkapa, vilionya Membe asingeweza kumshinda Lowassa sababu wananchi wangeona ni muendelezo wa miaka mitano wa Rais Kikwete. Ndipo jina la Magufuli likapendekezwa na Mkapa, na alitetea kuwa Magufuli ni mtu ambae amefanya kazi zake "consistently" na kuwa ni mtu ambae hana "roots" ndani ya chama hivyo itakua rahisi CCM kunadi sera za Rushwa ambayo ndio ilikua agenda kuu ya Upinzani. Kikwete ikabidi akubali, na kilichofuata ilikua tu itifaki ya kupitisha jina la mgombea.
Baada ya Urais 2015
Mkapa alifurahishwa na jinsi Magufuli alivokuwa anaendesha nchi mwanzoni, ila baada ya kama mwaka hivi, akaona jinsi mtu aliempigania alivokuwa ameaza kubadilika. Alikua ananadi mafanikio ya serikali kama ya kwake (Magufuli) binafsi na sio ya CCM. Pia, Magufuli, mara kadhaa alikua anaponda jinsi MaRais wezake walivyoendesha nchi na mida mengine aliponda sera za Mkapa za ubinafsishaji.
Hata hivyo, uhusiano kati ya hawa ulizorota sana kwa takribani mwaka hivi maana Magufuli aliona anamuingilia sana katika kazi zake. Mkapa akanawa mikono. Waliohudhuria mkutano wa Mkapa kule kigamboni 2018 mnajua alisema kuwa anaomba asihusihwe na mambo yanayoendelea nchini maana kama mstaafu amejaribu kwa nguvu zote kutoa mchango wake ila hausikilizwi.
Kwa mnaofuatilia kwa ukaribu sana siasa za nchi mtajua kuna wakati, Rais Mkapa alikuwa haonekani katika hafla za kitaifa, ni kwa sababu alikuwa anagomea mialiko. Magufuli, kuona mtu anaemuheshimu hampi support, alijirudi, akaongea nae na uhusiano wao ukaanza kurudi taratibu.
Baada ya hapo alikua moja wa watu wachache sana ambao Magufuli alikua anawasikiliza. Hata baadhi ya wazee (kina Kikwete) walikua wanamtumia yeye kuwasilisha madukuduku yao. Kama unakumbuka ile audio ya Kinana iliyovuja mtandaoni, Kinana alisikika akimwambia Nape kuwa Mkapa alitaka kumuona Magufuli kuongea nae kuhusu maswala ya Chama, ila Magufuli alikua anamkimbia. Hii ilidhiirisha influence ya Mkapa kwenye uRais wa Magufuli.
Nini sasa baada ya kifo?
Wastaafu waliobaki tunajua hawana nguvu kama aliyokuwa nayo mzee Mkapa kumshauri Magufuli kwenye maswala mbalimbali, Kikwete analinda maslai ya familia yake - mtoto na Mke wake waendelee kuwa Wabunge, na pia kulinda baadhi ya bishara zake. Mwinyi anataka mwanae awe Rais wa Zanzibar na pia ukweli ni kuwa amekua mzee sana na hata mawazo yake (kama lile la kutaka Magufuli apewe zawadi ya kuongezewa muda wa uongozi) hayachukuliwi kwa uzito.
Ndio maana Kikwete amesikitika sana, anajua jinsi huyo mzee alivokuwa na nguvu katika kutoa kauli ya wastaafu. Mkapa alikua moja ya watu wachache sana ambao walikua hawamwogopi Magufuli, and he spoke his mind whenever necessary.
Kwa hali ya siasa ilivyo nchini, kilichobaki ni kumuomba Mungu tu, maana kizingiti kikubwa kilichokuwa kimzuie Magufuli (kama alikua na mpango wa kubadilisha katiba atawale zaidi ya 2025) kimeondoka. Tuwaombee wastaafu waliobaki wasimame kwa umoja na nguvu moja kusemea maswala muhimu ya nchi, la sivyo tunapoelekea naona giza tu.
Mkapa ndiye alimnadi Magufuli jukwaani 1995 wakati anaomba ubunge Chato ambao Magufuli alishinda. Akamteua kuwa Naibu Waziri na baadae kuwa Waziri kamili. Tunajua Mkapa alizungumza wazi uchapakazi wa Magufuli mpaka kumuita Askari wake wa Mwavuli, hali iliyosababishwa Magufuli kunyweshwa sumu na "watu" waliodhani anaandaliwa na Mkapa kuwa Rais 2005. Mkapa aliendelea kumlinda na hata kumpa ulinzi wa usalama wa taifa.
Mchakato wa Urais 2015
Tunajua Lowassa alikatwa 2015 sababu Kikwete alitaka Membe amrithi Urais. Vyanzo mbalimbali ndani ya chama vinasema Kamati ya Wazee, kwa ushawishi mkubwa wa Mzee Mkapa, vilionya Membe asingeweza kumshinda Lowassa sababu wananchi wangeona ni muendelezo wa miaka mitano wa Rais Kikwete. Ndipo jina la Magufuli likapendekezwa na Mkapa, na alitetea kuwa Magufuli ni mtu ambae amefanya kazi zake "consistently" na kuwa ni mtu ambae hana "roots" ndani ya chama hivyo itakua rahisi CCM kunadi sera za Rushwa ambayo ndio ilikua agenda kuu ya Upinzani. Kikwete ikabidi akubali, na kilichofuata ilikua tu itifaki ya kupitisha jina la mgombea.
Baada ya Urais 2015
Mkapa alifurahishwa na jinsi Magufuli alivokuwa anaendesha nchi mwanzoni, ila baada ya kama mwaka hivi, akaona jinsi mtu aliempigania alivokuwa ameaza kubadilika. Alikua ananadi mafanikio ya serikali kama ya kwake (Magufuli) binafsi na sio ya CCM. Pia, Magufuli, mara kadhaa alikua anaponda jinsi MaRais wezake walivyoendesha nchi na mida mengine aliponda sera za Mkapa za ubinafsishaji.
Hata hivyo, uhusiano kati ya hawa ulizorota sana kwa takribani mwaka hivi maana Magufuli aliona anamuingilia sana katika kazi zake. Mkapa akanawa mikono. Waliohudhuria mkutano wa Mkapa kule kigamboni 2018 mnajua alisema kuwa anaomba asihusihwe na mambo yanayoendelea nchini maana kama mstaafu amejaribu kwa nguvu zote kutoa mchango wake ila hausikilizwi.
Kwa mnaofuatilia kwa ukaribu sana siasa za nchi mtajua kuna wakati, Rais Mkapa alikuwa haonekani katika hafla za kitaifa, ni kwa sababu alikuwa anagomea mialiko. Magufuli, kuona mtu anaemuheshimu hampi support, alijirudi, akaongea nae na uhusiano wao ukaanza kurudi taratibu.
Baada ya hapo alikua moja wa watu wachache sana ambao Magufuli alikua anawasikiliza. Hata baadhi ya wazee (kina Kikwete) walikua wanamtumia yeye kuwasilisha madukuduku yao. Kama unakumbuka ile audio ya Kinana iliyovuja mtandaoni, Kinana alisikika akimwambia Nape kuwa Mkapa alitaka kumuona Magufuli kuongea nae kuhusu maswala ya Chama, ila Magufuli alikua anamkimbia. Hii ilidhiirisha influence ya Mkapa kwenye uRais wa Magufuli.
Nini sasa baada ya kifo?
Wastaafu waliobaki tunajua hawana nguvu kama aliyokuwa nayo mzee Mkapa kumshauri Magufuli kwenye maswala mbalimbali, Kikwete analinda maslai ya familia yake - mtoto na Mke wake waendelee kuwa Wabunge, na pia kulinda baadhi ya bishara zake. Mwinyi anataka mwanae awe Rais wa Zanzibar na pia ukweli ni kuwa amekua mzee sana na hata mawazo yake (kama lile la kutaka Magufuli apewe zawadi ya kuongezewa muda wa uongozi) hayachukuliwi kwa uzito.
Ndio maana Kikwete amesikitika sana, anajua jinsi huyo mzee alivokuwa na nguvu katika kutoa kauli ya wastaafu. Mkapa alikua moja ya watu wachache sana ambao walikua hawamwogopi Magufuli, and he spoke his mind whenever necessary.
Kwa hali ya siasa ilivyo nchini, kilichobaki ni kumuomba Mungu tu, maana kizingiti kikubwa kilichokuwa kimzuie Magufuli (kama alikua na mpango wa kubadilisha katiba atawale zaidi ya 2025) kimeondoka. Tuwaombee wastaafu waliobaki wasimame kwa umoja na nguvu moja kusemea maswala muhimu ya nchi, la sivyo tunapoelekea naona giza tu.