#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

Coming up next.......

UPDATE:FRIDAY 26 FEBRUARY 2021

MATUKIO MAKUBWA YASIYOKUWA YA KAWAIDA AMBAYO YALISHAWAHI KUMPATA MHUSIKA AKIWA NDANI YA NCHI NA AMBAYO YALIPELEKEA AWE ANAADIKIWA BARUA NA MAMLAKA ZA JUU KAZINI KWAKE, ZA KUMTUHUMU KUWA ANAELEKEA KUUGUA UGONJWA WA KICHAA


Ni maelezo ya kina yakielezea matukio mbalimbali/ kadhaa yaliyopelekea mhusika kuwekwa kwenye kundi hilo la watu wanaokaribia kuugua ugonjwa wa kichaa, baada ya mhusika kuwa amekumbana na matukio hayo na hatimaye kumpelekea kutoa taarifa za matukio hayo, ambapo ilibidi uongozi wa juu wa taasisi anayofanyia kazi, kumwelekeza kuziwasilisha kwa mtu sahihi ndani ya tasisi hiyo, na hatimaye alifanya hivyo.

Mara ya kwanza kwa yeye kuwasilisha taarifa hizi ilikuwa Februari 2016, na tukio la kwanza alilowahi kulibaini kwa mara ya kwanza PAPO KWA PAPO lilitokea Novemba 2010 akiwa safarini kusini mwa Tanzania. Hii inamaanisha kuwa kuna matukio mengine alikuja kuyabaini lakini yakiwa yameshapita, yaani alikuja kuyajua baadaye tayari yakiwa yamepita. Mfano mzuri wa matukio ya aina hii ni kama lile la MR Y, ambalo alitakiwa akafanye kazi kusini mwa tanzania lakini hatimaye kazi hiyo iliota mbawa na katika mazingira yasiyoeleweka, kwa hiyo akawa ameshindwa kwenda kufanya kazi hiyo

Matukio haya anayaleta mbele ya umma katika ile hali ya kujaribu kutafuta mtizamo kutoka jicho la pili kutoka kwa watu wengine ambao ni public. Nia hasa ya kuleta matukio haya mbele ya umma ni katika kujaribu kuupa umma nao, nafasi ya kuweza ku-judge kama tuhuma dhidi ya mhusika kuelekea kuwa na kichaa zilikuwa ni sahihi ama la

Na mpaka hapa, wasomaji wa uzi huu inabidi wakubaliane na mwandishi kuwa anayeandika taarifa hizi na mhusika, ni watu wawili toafuti. Hii ni kwa wale wanaodai kuwa anayeandika ndiyo mhusika mwenyewe. Hiki kitu hakiwezekani kwa sababu mtu ambaye amewahi hata kule kutuhumiwa tu kuwa ana uwezekano wa kuugua kichaa, hata kama kweli hicho kichaa hana, bado hawezi kuandika taarifa za namna hii na katika mtindo huu, haiwezekani

Kwa hiyo hapa wasomaji inabidi wakubaliane na mwandishi kuwa anayenadika na anayesimuliwa, ni watu wawili tofauti, japo si lazima kwamba kila msomaji inabidi achukue msimamo huu, ni ushauri tu

Stay tuned

MUBARIKIWE TENE NA BWANA
Mi bado naona kama mhusika na msimuliaji ni mtu mmoja!
Ugonjwa wa akili tunaosema kuwa anao mhusika haumzuii yeye kusimulia matukio haya!
 
UPDATE: 03 MARCH 2021: DOKEZO MUHIMU SANA:

DOKEZO MUHIMU SANA KUHUSIANA NA TUKIO LA JANA TAREHE 02 MARCH 2021, NDANI YA JENGO


Ni kwamba umeme ulikatika jana tangu asubuhi na hadi mwandishi anaondoka ofisini baada ya saa 10, ulikuwa bado haujarudi. Kuna stori kubwa nyuma ya tukio hili la kukatika umeme siku nzima, ambayo itafuata baadaye.

Kwa kifupi tu ni kwamba mhusika hakumbuki ni lini mara ya mwisho, umeme ulikatika kwa kipindi kirefu kama ilivyokuwa jana, labda mwaka juzi 2019. Hii ni kutokana na ukweli kuwa kwa mwaka jana 2020, siku ambayo umeme ulikatika angalau kwa masaa mengi kidogo, ilikuwa nI tarehe 12/07/2020 siku ambayo Mh. Rais wa SMZ alikuwa anapitishwa kuwa mgombea kwa tiketi ya CCM

Kuna stori nzuri tu itafuata baadaye kuhusiana na umeme huo kukatika jana. Zaidi ni kuwa bado "strangers" wanaingia ndani ya jengo ila sasa hivi wamehamishia masikani yao kwenye maabara moja ambayo ipo chini ya Mr X.

Hii maabara imekaa kwenye sehemu ambayo ina tabia moja kwamba

  • Mlango wake uko kulia baada ya pale ngazi za kupandisha ghorofa ya kwanza zinapoishia, na mlangoni juu yake tena ndiyo kuna camera inayotazama kwenye korido; kamera hiyo ikiwa imetazama uelekeo wa ushoto.
  • Maabara hiyo yenyewe iko uelekeo wa kulia kiasi kwamba wote wanaotokea chini na kupandisha ngazi na hatimaye kuingia ndani ya maabara hiyo, hawawezi kuonekana na camera hiyo.
  • Mtu pekee anayeingia ndani ya jengo na kupandisha juu ghrorofa ya kwanza akiwa anatokea chini, na anayeweza kuonekana na kamera hiyo, ni yule tu atakayepitiliza na kuelekea kule uliko uelekeo wa kamera hiyo, yaani atakayepinda kushoto mara tu baada ya kuwa amefika mahali ulipo mlango wa maabara au hiyo.
  • Kwa yule anayetokea chini akipandisha juu ghorofa ya kwanza na hatimaye kuingia ndani ya maabara hiyo, kamera hiyo haiwezi kumuona
Kwa hali hiyo basi, ni kwamba mtu anaweza akapandisha ghorofa ya kwanza na hatimaye kuiingia ndani ya maabara hiyo bila kuonekana na Kamera.

Kwa hiyo kilichofanyika jana ni kuwa “kuna strangers” walifika na kukaa humo kwa muda ule waliohitaji kuwemo humo, na na possibly pasipo kuonekana na camera, na waliingia ndani ya jengo kabla ya saa 4 asubuhi na kabla ya umeme kuwa umekatika



Baadaye sasa ndiyo umeme ulikatika muda mrefu tangu asubuhi mida ya saa 4. Kitendo hicho sasa NADHANI kikapeleka ile backup battery ya camera inayomulika kwenye korido, kuishiwa chaji Baada ya hapo sasa, ndiyo watu hawa nao wakaanza kuonekana tena sehemu zingine ambazo kamera hiyo ingeweza kuwaona kama ingekuwa inafanya kazi.

Mhusika yeye anadhani kuwa kwa sababu umeme ulikatika muda mrefu, kamera hiyo itakuwa ilipoteza uwezo wa kuona na hivyo watu hao walikuwa hawaonekani tena na kamera hiyo. Wangeweza kuonekana iwapo tu camera hiyo ingekuwa inafanya kazi. Ni tekniki fulani ambayo inaendeshwa kwa utaalamu wa sayansi ya hali ya juu kidogo. Hicho ndiyo kilichofanyika jana.

Maelezo ya kina kuhusiana na tukio hili, yatafuata baadaye, mara tu baada ya maelezo yamayomhusu SENIOR MSTAAFU WA KIUME, ambayo kawaida yalitakiwa yawajie jana, assuming umeme usingekatika moja kwa moja siku nzima

Mhusika mkuu kwenye tukio hili safari hii siyo yeye tena SENIOR MSTAAFU WA KIUME bali ni MKUU WA IDARA ALIYEPITA. Na mhusika anashangaa kidogo sijui huyu mtu atakuwa amefanya kitu gani, kingine cha ziada kwa sababu anahangaika mno siku hizi! Na kama atakuwa yuko na Mungu, lazima atafanikiwa kutatua kile kinachoendelea kumhangaisha, ila kama hayuko na Mungu,……………



MUBARIKIWE TENA NA BWANA

UP NEXT:


Tukio la Septemba 2016 lililotokea baada ya tetemeko la Kagera na kumhusisha SENIOR MSTAAFU WA KIUME na mtu mwingine mgeni mwenye uhusiano naye na ambaye alikuwa ametoka nje ya Idara.
 
Mi bado naona kama mhusika na msimuliaji ni kitu kimoja!
Ugonjwa wa akili tunaosema kuwa anao mhusika haumzuii yeye kusimulia matukio haya!
Ni vizuri kama umelitambua hilo, hawa wote itabidi wapatiwe msaada unaostahili
 
UPDATE: 03 MARCH 2021

TUKIO LA NNE NDANI YA JENGO SEPTEMBA 2016
LILOMHUSISHA SENIOR MSTAAFU WA KIUME NA MTU MWINGINE MGENI MWENYE UHUSIANO NAYE NA AMBAYE ALIKUWA AMETOKA NJE YA IDARA.

Tukio hili lilitokea ndani ya wiki ya kuanzia tarehe 12/09/2016 (J3) hadi 16/09/2016 (IJUMAA)

  • Jumamosi ya wiki kabla ya J3 tajwa hapo juu, ndiyo siku ambayo lilikuwa limetokea tetemeko la Kagera
  • J3 tajwa mhusika alifika ofisini asubuhi na kukuta kuna gari moja au mbili (za ma-office mates wake ndani ya jengo hilo), zimepaki kwenye parking
  • Gate la kuingilia ndani ya jengo lilikuwa wazi, kuonyesha kuwa kulikuwa na angalau watu ndani ya jengo hilo
  • Mhusika aliingia ofisini na kukuta hakuna mtu hata mmoja, kwenye ghorofa ilimo ofisi yake. Ofisi zote zilikuwa zimefungwa na hapakuwa na mtu hata mmoja anayemiliki ofisi kwenye floor hiyo aliyekuwa tayari ameshafika ofisini muda huo
Mpaka hapa, mhusika akakumbuka pia kuwa kwenye siku za Alhamis na Ijumaa wiki iliyopita nyuma yake, hapakuwa na mtu yeyote kwenye floor hiyo. Siku hizo mbili alikuwa mwenyewe peke yake kwenye floor nzima.

Kwa siku hizo mbili za wiki iliyokuwa imepita, kwenye floor inayofuata, walikuwa wamebaki Katibu Mhutasi (KMH) wa MWI pamoja na mtu mmoja mwingine, tumwite XX_2. Sehemu zingine zote za jengo hapakuwa na mtu na kuna baadhi ya wenye ofisi hizo ambao walikuwa wamesafiri. Kwa mfano, Mr X pampja na MAMA SENIOR AMBAYE HAJASTAAFU (MSH), walikuwa wamesafiri kikazi kwenda Kyerwa, Kagera

Kwa hiyo kuanzia Alhamis ya tarehe 08/09/2016 na kuendelea, jengo zima lilikuwa limebaki na watu watatu tu ambao ni XX_2, KMH pamoja na mhusika. Taarifa hizi za uwepo wa watu wachache hivi ndani ya jengo, mhusika alizipata siku hiyo ya J3 ya tarehe 12/09/2016. Hapo kabla hakujua hilo



Baada ya mhusika kufika ofisini na kukuta floor nzima haina watu kwa siku ya tatu mfululizo, aliamua kupandisha juu ofisini kwa MWI. Huko alimkuta Katibu Mhutasi (KMH) wa MWI akiwa peke yake. Hapakuwa hapakuwa na mtu mwingine tena zaidi ya huyo ndani ya jengo kwa muda huo, japo kwenye parking palionyesha kuwa kuna mtu mwingine wa tatu ameshawasili maeneo ya ofixsini ambaye ni XX_2 kwa sababu gari yake ilikuwepo kwenye parking.

Hata hivyo, kwa wakati huo, XX_2 hakuwemo ndani ya jengo, ila alikuwa bado yupo amekaa ndani ya gari lake lililokuwa kwenye parking

Mhusika katika kujaribu kuongea na KMH, mama huyu alisema kuwa amekuta geti kuu la jengo la ofisi hizo likiwa wazi, na amekuta gari ya XX_2 ikiwa imepaki. Kwa hiyo mpaka hapa ikaonekana kuwa XX_2 ndiye aliyefungua geti, lakini kumbe hapana, hata XX_2 naye pia hakuwa amefungua geti hilo kwa sababu alivyofika na kupaki na akaendelea kubaki ndani ya gari, hakuwa ameshuka kwenye gari.

Hata hivyo, mpaka hapa, mambo kadhaa yakawa yamejidhihirsha hapa kwamba:

  • XX_2 alifika ofisini akakuta geti la lango kuu liko wazi
  • Kwa wakati huo, XX_2 alikuwa ameachiwa kukaimu Ukuu wa Idara, na alijua kuwa amebaki na watu wengine wawili tu ndani ya jengo hilo ambao ni KMH na mhusika, na wengine wote hawakuwepo
Kwa hiyo, kitendo cha XX_2 kufika ofisini na kubaki ndani ya gari kwenye parking kilimuwezesha kuweza kufahamu yafuatayo

  • Geti la lango kuu lilikuwa wazi
  • Alifika ofisini kabla ya wenzake wawili ambao ni KMH na mhusika
Na kwa sababu watu aliokuwa amebaki nao walikuwa wawili tu na hapo hapo yeye alikuwa amefika akiwa ni wa kwanza na kukuta geti liko wazi, ilhali wale wenzake wawili kwa wakati huo walikuwa bado hawajafika, kuanzia hapa sasa yeye XX_2 kama KAIMU MWI kwa wakti huo, alitakiwa apate swali kichwani kwamba:

SIYO MIMI (YAANI XX_2) NILIYEFUNGUA GETI LA LANGO KUU NA WALA SI KMH AU MHUSIKA, JE NANI ATAKUWA AMEFUNGUA GETI HILI?

Hii ni kutokana na ukweli kuwa:

  • Hata XX_2 naye hakuwa amefungua geti hilo, na wala hakuwa ameingia ndani ya jengo hilo asubuhi hiyo bali alikuwa yupo amebaki kwenye gari yake iliyokuwa ipo kwenye parking,
  • Wote wawili KMH pamoja na mhusika waliikuta gari ya XX_2 ikiwa ipo kwenye parking, na wakati huo geti likiwa wazi
  • Kwa hiyo, KMH wakati anafika ofisini na kukuta geti la lango kuu liko wazi, alijua kuwa XX_2 ndiyo alifungua geti hilo
  • Vile vile, mhusika naye pia alipofika ofisini na kukuta hali hiyo, akajua kuwa mmoja wao kati ya KMH na XX_2 ndio walifungua geti hilo
Kumbe hapana, haikuwa hivyo. Wote hawa watatu hawakuwa wamefungua geti hilo siku hiyo, japo wote walikuwa mazingira ya ofisini. Ni kwa sababu XX_2 alifika ofisini na kubaki ndani ya gari lake , hakuingia ndani ya jengo, wakati KMH yeye alifika na kuingia ndani ya jengo geti likiwa wazi

Ilionyesha kuwa XX_2 alifika ofisini wa kwanza na kukuta geti liko wazi, ila hakustuka kuona hivyo

  • Baadaye tena ndiyo akaja KMH na kukuta geti liko wazi, akaingia ndani ya jengo, huku XX_2 akiwa yupo ndani ya gari lake na akimuona KMH
  • Baadaye tena mhusika naye alifika na kuingia ndani ya jengo, XX_2 akiwa yupo ndani ya gari lake na akimuona mhuiska vilevile


MAELEZO KWA UFUPI SANA KUHUSIANA NA XX_2

Ni mfanyakazi ambaye ana wajina wake ndani ya idara, YAANI NI MMOJAWAPO WA WATU WAWILI TU NDANI YA IDARA AMBAO MAJINA YAO YA UBINI YAMEFANANA, yaani SURNAME zao zinafanana. Kwa hiyo kuna mwingine tuseme anaitwa XX_1 ambayo jina lake la ubini limefanana na la XX_2



…………………..inaendelea
 
MASAHIHISHO MUHIMU SANA KWENYE MAELEZO HAYO HAPO JUU

Jengo lilikuwa lilibaki na watu wanne (4), na siyo watatu (3); na pia XX_2 hakuwa Kaimu Mkuu wa Idara kwa wiki hiyo

  • Aliyekuwa anakaimu ni mtu mwingine, mtaalamu wa mambo ya matetemeko
  • Kwenye hii siku husika ambayo maelezo yake yametolewa hapo juu, Kaimu huyo hakuwa amewahi kufika ofisini siku hiyo
  • Aliyekuwa amewahi na kufika ofisini wa kwanza siku hiyo alikuwa ni huyo XX_2 na maelezo mengine yote yaliyotolewa hapo juu yanabaki kama yalivyo, ila sahihisho kubwa tu ni kwamba XX_2 hakuwa kaimu MWI.
 
UPDATE: 03 MARCH 2021

TUKIO LA NNE NDANI YA JENGO SEPTEMBA 2016
LILOMHUSISHA SENIOR MSTAAFU WA KIUME NA MTU MWINGINE MGENI MWENYE UHUSIANO NAYE NA AMBAYE ALIKUWA AMETOKA NJE YA IDARA.



…………………..inaendelea

Kwa hiyo by elimination or induction; kitendo cha XX_2 kubaki ndani ya gari lake likiwa kwenye parking na hatimaye kuwaona wenzake wawili pekee aliokuwa amebaki nao wakiingia ndani ya jengo, geti la lango kuu likiwa wazi, ilikuwa ni bahati na dalili ya pekee kabisa ya kumfanya ajue kuwa geti la lango kuu siku hiyo lilikuwa limefunguliwa na mtu mwingine ambaye si mmoja wa watu wa Idara hiyo



MHUSIKA AOMBA KUKAA NA KUFANYIA KAZI OFISINI KWA MKUU WA IDARA KWA MUDA, KUANZIA SIKU HIYO


Baada ya mhusika kukuta hakuna watu kwenye floor yake na hatimaye kupandisha juu na kumkuta KMH ofisini kwake, akaunganisha na mazingira mengine tatanishi aliyoyakuta ofisini siku hiyo, ambayo baadhi yake tu atayagusia kwa kifupi sana humu, mhusika aliamua kuhama ofisini kwake na kuhamia ofisini kwa MWI

  • Kuanzia pale, akawa anafanya kazi akiwa amekaa humo, wakiwa pamoja na KMH wa MWI
  • Baada ya kuhamia ofisini kwa MWI, ndiyo sasa hayo yote aliyoyaeleza hapo juu yakajulikana kama alivyoyaeleza humu jukwaani
Kilichokuwa kimetokea ni kwamba siku hiyo hata hakudiriki kufungua mlango wa ofisi yake bali alifika tu akachungulia kidogo halafu akapandisha juu ofisini kwa MWI na kwenda kukaa huko

  • Wiki yote nzima aliitumia ofisini kwa MWI
  • Asubuhi wakati anahamia huko, XX_2 alikuwa bdo yupo kwenye patrking, akiwa amekaa ndani ya gari lake
  • Ilikadiriwa kuwa XX_2 alitumia muda usiopungua angalau saa nzima akiwa ndani ya gari lake hilo
XX_2 baada ya kuwa amekaa hapo kwenye parking, hatimaye aliondoka mazingira ya ofisini na mhusika hakufanikiwa kuonana naye tena siku hiyo



BAADA YA MHUSIKA KUWA AMEHAMIA OFISINI KWA MKUU WA IDARA

  • Baadaye ndiyo alifika ofisini hapo SENIOR MSAAFU WA KIUME (SMME)
  • Muda mfupi baadaye (au possibly muda huo huo, hakumbuki vizuri) alionekana tena rafiki yake na SMME
  • Kaimu Mkuu wa Idara naye pia akawa ameshawasili ofisini muda huo
  • Muda huo huo alionekana tena MR Y (huyu ni yule ambaye aliwahi kumtafutia mhusika kazi ya kwenda kufanya kusini, halafu baadaye kazi hiyo ikayeyuka ghafla)
  • Alionekana pia MWI mstaafu aliyewahi kutawala kipindi cha kuanzia 2006-2012 ambaye yeye wiki moja kabla, aikuwa anasemekana kuwa hakuwa anafika ofisini kwa sababu tayari alikuwa amesafiri. Huyu yeye ndiye alikuwa amepotea kwa kitambo kidogo ukilinganisha na wale wengine


MBADILIKO YA NAFASI YA KAIMU MKUU WA IDARA YATOKEA SIKU HIYO


Kutokana na ukweli kwamba aliyekuwa Kaimu MWI ni mtalaamu wa mateteko na ukizingatia kuwa Jumammosi ya wiki iliyokuwa imepita nyuma yake, lilikuwa limetokea tetemeko Kagera. Mkuu huyu , alilazimika kusafiri ghafla kwenda Kagera akimwachia nafasi hiyo MR Y; yule ambaye aliwahi kumpa mhusika safari ya kwenda kufanya kazi kusini lakini ikashindwa kuiva . Kwa hiyo, kwa wiki yote hiyo nzima MR Y ndiyo akawa anakaimu Ukuu wa Idara



SENIOR MSAAFU WA KIUME (SMME)

SMME AANZA MAANDALIZI KWA AJILI YA SAFARI YA CHINA SIKU HIYO


Asubuhi siku hiyo hiyo, SMME aliingia ofisini kwa MWI akiwa na nyaraka kwa ajili ya safari ya kwenda China, na akiwa anahitaji msaada wa kutolewa nakala za nyaraka hizo na KMH wa MWI.

  • Pilika plika hizi zilimpelekea aingine na kutoka ofisini hapo mara kwa mara siku hiyo
  • zilikuwa nyingi kiasi, na zote zilihusiana na safari yake hiyo
  • Kitu kama hadi siku mbili mbele, pilika pilika za SMME kuingia na kutoka ofisini hapo zilikuwa zinaendelea, zikienda zinapungua kadri muda wa safari yake ulivyokuwa unasogea mbele
  • Safari hiyo ya SMME ilikuwa ni ya Ijumaa ya tarehe 16/09/2016, reporting time Airport ikiwa ni saa 8 kamili mchana
SIKU YA SAFARI YA SSME KUELEKEA CHINA YAWADIA, YAANI IJUMAA YA TAREHE 16/09/2016

Mpaka hapa, msomaji inabidi akumbuke kuwa jengo lilikuwa limebaki na watu watatu kwa sababu hata wale walioonekana siku ya kwanza, nao walikuwa wamepotea tena. Anachokumbuka mhusika ni kuwa mpaka muda huo, walikuwa tena wamebaki watu watatu ndani ya jengo hilo ambao ni mhusika mwenyewe, KMH pamoja na Kaimu MWI ambaye alikuwa ni MR Y

Ilipofika siku hii ya Ijumaa ambayo ndiyo ilikuwa siku ya safari ya SMME

  • KMH wa MWI akawa amepata udhuru wa kutoka kwenda kuonana na “SPECILAST”
  • “SPECILAST huyu si mwingine bali ni yule ambaye mhusika alielekezwa na mamlaka za juu kwenda kumuona na kuanza kufanya naye mazungumzo
Kwa hiyo mhusika siku hiyo akawa amebaki ofisni kwa MWI peke yake, na hata kaimu MWI naye alikuwa hakai ofisini muda wote, kwa hiyo naye pia kwa muda, hakuwepo muda huo



DEREVA WA SMME AWASILI NDANI YA JENGO KWA AJLI YA KUMCHUKUA NA KUMPELEKA AIRPORT

KMH wa MWI akiwa ameshaondoka tayari, kwenye mida kama ya saa saba na dakika 20 hivi, alikuja mtu akiwa na gari lenye namba za Serikali na kujitambulisha kuwa yeye ni Dereva wake na SMME na hivyo amekuja kumchukua ili ampeleke Airport

Mhusika alimkaribisha mtu huyu na kumpa kiti akakaa, ndani ya ofisi ya MWI, ila nje ya kaunta. Reporting time ya Airport ilikuwa ni saa 8 kamili mchana, lakini mpaka inafika saa 8 kasoro dakika 10, aliyekuwa anatakiwa kupelekwa airport alikuwa bado hajaonekana maeneo hayo ya ofisini, na wala hakuonekana kabisa, na hatimaye dereva huyu aliwasha gari akaondoka bila msafiri aliyekuwa amekuja kumchukua kwa ajili ya kumpeleka Airport

Mhusika alikaa hapo ofisini wakiwa na mtu, akiwa amebanwa haja ndogo ambayo alikaa nayo kwa zaidi ya nusu saa akiwa ameibana, hakuwa katika nafasi ya kumfukuza mtu huyu ndani ya ofisi ili akajisaidie halafu arudi na kumkaribisha tena ndani, lakini vile vile hakuwa pia katika nafasi ya kumwamini na kumwachia mtu huyu ofisini akiwa peke yake



HITIMISHO

Hatimaye KMH alirudi baadaye akiwa anatokea kwa “SPECIALIST” na kukuta mtu huyu tayari ameshaondoka. KMH huyu alihamishiwa idarani baada ya kuwa amehamishwa yule mwingine aliyewahi kuingia kwenye mgogoro na MWI alyewahi kuruka kutoka juu ghorofa ya kwanza hadi chini.

Vilevile, MWI ambaye alikuwa amesafiri na kuwaachia hawa wengine wakiwa wanakaimu, ni huyu wa juzi ambaye amekuwa akishughulikia maslahi ya mhusika katika namna ambayo mhusika mweyewe ilimchnanganaya



TUKIO LA TANO NDANI YA JENGO: FIRE EXTINGUSHER ILIYOWAHI KULETWA NA MR X NDANI YA JENGO NA KUWEKWA KWENYE CORRIDOR

  • Maelezo ya tukio hili yenyewe tayari yapo mwanzoni kabisa mwa uzi huu, ukurasa ule wa kwanza
  • Kwa kukumbushia tu ni kwamba Fire Extingusisher (FE) hii ilikuwa ni ya maji
  • Wakatihuo kulikuwepo na MWI mstaafu, na ambaye aliwahi kutawala kipindi cha kuanzia 2006-2012, amabye alimfuata mhusika kuona kama anajua kuitumia FE hiyo ili wakazime moto kwenye transformer nyuma ya jengo la ofisi yao, lililokuwa linawaka moto baada ya kupata shoti ya umeme,
  • Wakati huo, umeme wa TANESCO ulikuwa haujazimwa na mmojawapo wa waliokuwa taarifa hizi muhimu za umeme kutokuwa umezimwa, alikuwa ni MR X


MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
Ila mhusika nae ana ukaidi flani hivi[emoji23][emoji23]
Sasa kwanini alikataa kumsindikiza boss wake polisi ?

Pia nimewamiss sana viongozi wa kanisa A
 
UPDATE: 03 MARCH 2021

KULE KANISA B NAKO: JUMAPILI YA TAREHE 11/09/2016


Ikumbukwe kuwa kwa wakati huu, mhusika alikuwa yuko Kanida B

  • Kwa hiyo J2 ya tarehe 11/09/2021 aliabudu Ibada akiwa Kanisa B
  • Siku hiyo, Mzee Kiongozi wa Kanisa B (MZK-B) hakutoa matangazo yeye mwenyewe kama ilivyo kawaida yake, bali alituma mzee mwingine wa chini yake ambaye alimwagiza kutoa moja tu
Tangazo hilo lilisema hivi: LEO TUNA TANGAZO MOJA TU. NI SIKU YA MABOMU YA MAREKANI

  • Kwa uchanga wake wa kiroho mhusika kwa kipindi hicho, hakuweza kujua kwa nini tangazo hilo liltolewa Kanisani kwa sababu halikuwa na uhusiano wowote na mambo ya Kanisani
  • Baadaye siku zilivyokwenda, alikuja akajua maana yake.
  • Neno hilo lilikuwa ni SECRET CODE ya kurusha pepo kwenye madhabahu pale lilipotamkiwa
  • Pepo huyo aliyeriushwa siku hiyo, ni yule ambaye anahusika na mambo ya milipuko ya mabomu au inayofanana na hiyo
  • Ni yule anayeweza kusababisha mlipuko mahali fulani, na kwa mlengwa fulani
  • Kwa hiyo code hiyo ilikuwa inarusha pepo atakayefanya kazi ya kulipua mahali fulani na kwa mlengwa wa pepo hilo
Kadri siku zilivyopita na hatimaye kuwa amepata piccha halisi ya tangazo hili, ndiyo sasa kuanzia pale akaanza kuhitilafiana na Kiongozi Mkuu wa Kanisa B (KM-B) kwa kudhani kuwa ndiye aliyehusika na mpango wa tangazo hilo, kumbe hapana



Hapa sasa uzi unaanza sasa kuchukua uelekeo wa kurudi KANISA B ambako utamwongelea zaidi MZK-B pamoja na mshiriki (MSHK-B), yule aliyewahi kuwa Mkuu wa Shule mahali ambapo mhusika aliwahi kwenda kuomba ajira.

Na kwa uelewa wake mhusika kwa sasa, huyu MSHK-B ndiye aliyemleta kanisani hapo, David Belela (DB)

  • Mhusika yeye kwa kipindi hicho, alidhani kuwa DB aliletwa na KM-B, kumbe hapana
  • Mhusika yeye anachojua kwa sasa ni kuwa KM-B alimkaribisha DB, ila baada ya kuwa ameletwa (au kutambulishwa, kama walikuwa hajawahi kufahamiana kabla) kwake na MSHK-B,
  • Na kama kweli DB aliletwa na KM-B, basi KM-B mwenyewe kwa sababu yupo, atathibitisha hilo
Zaidi ni kuwa mhusika huwa hapendelei sana matangazo ya yeye kutambulishwa kwenye umati wa watu, unless iwe ni lazima sana. Kwa hiyo siku hiyo KM-B alikiuka makubaliano hayo, lakini baadaye mhusika alikuja kubaini kuwa hata utambulisho huo alioufanya KM-B, nao pia alikuwa ameshauriwa na MZK-B kwa sababu MZK-B alikuwa tayari amesha-set target yake aliyokuwa anataka kui-meet, huku KM-B akiwa hajui chochote kuhusiana na target hiyo. Ndiyo maana MZK-B alituma mtu madhabahuni kwenda kutoa tangazo la moja tu na lililohusiana na Marekani

Siku hiyo kulikuwa pia na wageni wengi wa kutoka nje ya Kanisa, na kulikuwa na Mkutano wa Injili uliokuwa umekuwa scheduled kuendelea kwa wiki nzima, ukihusisha watu wengine wengi kutoka nje ya Kanisa hilo. Mhusika alitambulishwa mbele ya umati huo wa wageni, na kwa kitu ambacho hakikuwa lazima, wakati makubaliano yao na KM-B yalikuwa ni kwamba mhusika huwa hapendi kutambulishwa mbele ya Kanisa, iwe kuna wageni au hakuna wageni



……………..itaendelea
 
Ila mhusika nae ana ukaidi flani hivi[emoji23][emoji23]
Sasa kwanini alikataa kumsindikiza boss wake polisi ?

Pia nimewamiss sana viongozi wa kanisa A
Viongozi wa Kanisa A unawajua? Juzi juzi walisimama madhabahuni wakiwa wamebeba hivi vitoto vidogo walikuwa wanaviweka wakfu,,,,,, yaani walivyopendeza na vitoto hivyo mbele ya madhabahu, acha tu. Nikawa natamani rohoni Mungu ashuke physically muda huo awageuze kabisa waache kufanya upumbavu Kanisani. Walikuwa wamependeza muno wakati wanaviombea vitoto hivyo wakiwa wamevipakata mikononi mwao
 
UPDATE: THURSDAY, 04 MARCH 2021

NYONGEZA MUHIMU KUHUSIANA NA TUKIO LINALOMHUSU SENIOR MSTAAFU WA KIUME


  • Ni tukio la mwisho lililowahi kuwakutanisha mhusika na “SPECIALIST” kwa ajili ya maongezi
  • Baada ya hapo, wawili hawa walikuja kukutana mwanzoni mwa mwaka 2018, mhusika alipoenda kutoa shukrani zake kwa “SPECIALIST” kutokana na yale waliyokuwa waliwahi kuyafanya kwa pamoja
Zaidi ni kuwa safari hii ya China ya SMME ilionekana ilikuwa ni ya siku chache tu kwa sababu wiki iliyofuata siku aidha ya J4 au J5, mtu huyu alionekana tena mazingira ya ofisini





MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
Viongozi wa Kanisa A unawajua? Juzi juzi walisimama madhabahuni wakiwa wamebeba hivi vitoto vidogo walikuwa wanaviweka wakfu,,,,,, yaani walivyopendeza na vitoto hivyo mbele ya madhabahu, acha tu. Nikawa natamani rohoni Mungu ashuke physically muda huo awageuze kabisa waache kufanya upumbavu Kanisani. Walikuwa wamependeza muno wakati wanaviombea vitoto hivyo wakiwa wamevipakata mikononi mwao
Ifike mahali hili swala la hawa viongozi wa kanisa A ligundulike kwa waumini wote kuwa kuna kitu cha ziada huwa kinaendelea kanisani hapo!

Hivi yule kiongozi mwingine anaetaka kukutana na mhusika private ili amtamkie mibaraka, ameacha kutoa huu wito au bado anaendelea??
 
Ifike mahali hili swala la hawa viongozi wa kanisa A ligundulike kwa waumini wote kuwa kuna kitu cha ziada huwa kinaendelea kanisani hapo!

Hivi yule kiongozi mwingine anaetaka kukutana na mhusika private ili amtamkie mibaraka, ameacha kutoa huu wito au bado anaendelea??
Alikuwa.
 
UPDATE: 05 MARCH 2021: DOKEZO MUHIMU SANA:

KUHUSIANA NA TUKIO LA JUMANNE TAREHE 02 MARCH 2021, NDANI YA JENGO


Ni kwamba umeme ulikatika jana tangu asubuhi na hadi mwandishi anaondoka ofisini baada ya saa 10, ulikuwa bado haujarudi. Kuna stori kubwa nyuma ya tukio hili la kukatika umeme siku nzima, ambayo itafuata baadaye.

Kwa kifupi tu ni kwamba mhusika hakumbuki ni lini mara ya mwisho, umeme ulikatika kwa kipindi kirefu kama ilivyokuwa jana, labda mwaka juzi 2019. Hii ni kutokana na ukweli kuwa kwa mwaka jana 2020, siku ambayo umeme ulikatika angalau kwa masaa mengi kidogo, ilikuwa nI tarehe 12/07/2020 siku ambayo Mh. Rais wa SMZ alikuwa anapitishwa kuwa mgombea kwa tiketi ya CCM

Kuna stori nzuri tu itafuata baadaye kuhusiana na umeme huo kukatika jana. Zaidi ni kuwa bado "strangers" wanaingia ndani ya jengo ila sasa hivi wamehamishia masikani yao kwenye maabara moja ambayo ipo chini ya Mr X.

Hii maabara imekaa kwenye sehemu ambayo ina tabia moja kwamba


  • Mlango wake uko kulia baada ya pale ngazi za kupandisha ghorofa ya kwanza zinapoishia, na mlangoni juu yake tena ndiyo kuna camera inayotazama kwenye korido; kamera hiyo ikiwa imetazama uelekeo wa ushoto.
  • Maabara hiyo yenyewe iko uelekeo wa kulia kiasi kwamba wote wanaotokea chini na kupandisha ngazi na hatimaye kuingia ndani ya maabara hiyo, hawawezi kuonekana na camera hiyo.
  • Mtu pekee anayeingia ndani ya jengo na kupandisha juu ghrorofa ya kwanza akiwa anatokea chini, na anayeweza kuonekana na kamera hiyo, ni yule tu atakayepitiliza na kuelekea kule uliko uelekeo wa kamera hiyo, yaani atakayepinda kushoto mara tu baada ya kuwa amefika mahali ulipo mlango wa maabara au hiyo.
  • Kwa yule anayetokea chini akipandisha juu ghorofa ya kwanza na hatimaye kuingia ndani ya maabara hiyo, kamera hiyo haiwezi kumuona
Kwa hali hiyo basi, ni kwamba mtu anaweza akapandisha ghorofa ya kwanza na hatimaye kuiingia ndani ya maabara hiyo bila kuonekana na Kamera.

Kwa hiyo kilichofanyika jana ni kuwa “kuna strangers” walifika na kukaa humo kwa muda ule waliohitaji kuwemo humo, na na possibly pasipo kuonekana na camera, na waliingia ndani ya jengo kabla ya saa 4 asubuhi na kabla ya umeme kuwa umekatika



Baadaye sasa ndiyo umeme ulikatika muda mrefu tangu asubuhi mida ya saa 4. Kitendo hicho sasa NADHANI kikapeleka ile backup battery ya camera inayomulika kwenye korido, kuishiwa chaji Baada ya hapo sasa, ndiyo watu hawa nao wakaanza kuonekana tena sehemu zingine ambazo kamera hiyo ingeweza kuwaona kama ingekuwa inafanya kazi.

Mhusika yeye anadhani kuwa kwa sababu umeme ulikatika muda mrefu, kamera hiyo itakuwa ilipoteza uwezo wa kuona na hivyo watu hao walikuwa hawaonekani tena na kamera hiyo. Wangeweza kuonekana iwapo tu camera hiyo ingekuwa inafanya kazi. Ni tekniki fulani ambayo inaendeshwa kwa utaalamu wa sayansi ya hali ya juu kidogo. Hicho ndiyo kilichofanyika jana.

Maelezo ya kina kuhusiana na tukio hili, yatafuata baadaye, mara tu baada ya maelezo yamayomhusu SENIOR MSTAAFU WA KIUME, ambayo kawaida yalitakiwa yawajie jana, assuming umeme usingekatika moja kwa moja siku nzima

Mhusika mkuu kwenye tukio hili safari hii siyo yeye tena SENIOR MSTAAFU WA KIUME bali ni MKUU WA IDARA ALIYEPITA. Na mhusika anashangaa kidogo sijui huyu mtu atakuwa amefanya kitu gani, kingine cha ziada kwa sababu anahangaika mno siku hizi! Na kama atakuwa yuko na Mungu, lazima atafanikiwa kutatua kile kinachoendelea kumhangaisha, ila kama hayuko na Mungu,……………


MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
Stay tuned, maelezo ya nyongeza kuhusiana na tukio hilo hap juu yanafuata muda siyo mrefu
 
UPDATE: FRIDAY 05 MARCH 2021: MAELEZO YA NYONGEZA KUHUSIANA NA TUKIO LA WATU “STRANGERS” KUONEKANA NDANI YA JENGO JUMANNE YA TARERE 02 MARCH 2021

  • Siku hiyo umeme ulikatika siku nzima
  • Kama ilivyoelezwa hapo awali, ilionekana “strangers’ hawa walifika mapema asubuhi na kukaa kwenye maabara hadi umeme ulipokatika, na hatimaye baadaye tena ndiyo wakajitokeza sehemu zingine ndani ya jengo, umeme ukiwa bado haujarudi
Siku hiyo, mhusika aliwaona watu hao wakiwa wamesimama kwenye mlango wa maabara hiyo, ambayo iko chini ya MR X

Kabla ya kuendelea mbele, mhusika anaomba awarudishe nyuma kidogo wasomaji kwa kuwaletea taarifa hizi mpya, ila zinazohusiana na taarifa zilizowahi kuwepo humu muda siyo mrefu nyuma



JANA ALHAMIS TAREHE 04 MARCH 2021. MUHUSIKA AFUATILIA BARUA YAKE ALIYOIANDIKA KWENDA MAMLAKA ZA JUU NA KUKUTA HAIKUFIKA HUKO

Barua hii ni ile aliiandika na kuiwasilisha Idarani siku ya Alhamis ya tarehe 21 JANUARY 2021. NI BARUA ILIYOKUWA IKUMBUSHIA MAMBO MAKUU MATATU, ambayo hata hapo kabla, amekuwa akiandika barua kadhaa kuyakumbushiwa

  • La kwanza lilihusu kuiomba mamlaka husika kumrudishia cheo chake alichowahi kukipata Julai 2012 na hatimaye kunyang’anya tena cheo hicho ilipofika Februari 2014
  • La pili lilihusu malipo ya malimbikizo ya mshahara wake yatakayotokana na marekebisho hayo ikiwa ni pamoja na malimbikizo mengine ambayo yamewahi kujitokeza baada ya hapo
  • La tatu lilihusu kurudishiwa makatto yaliyowahi kuanzishwa kwenye mshahara wake pasipo yeye kuwa ameyaidhinisha, mojawapo yakiwa ni ya mfuko wa Bima ya Afya ambao yeye si mwanachana, na hivyo hajawahi kujiunga


Barua hii haikufika kule ilikotarajiwa kufika, baada ya Katibu Muhtasi (KMH) wa Mkuu wa Idara (MWI) kumshauri mhusika kufanya mabadiliko kwenye barua hiyo, kuhusiana na mkondo wa namna barua hiyo ilivyotakiwa kutoka idarani na kumfikia kiongozi wa juu ilikokuwa inatakiwa kwenda, ambayo mhusika mwenyewe pia aliyakubali na kuyaona kuwa yako sahihi

Hata hivyo, si kwamba mabadiliko hayo mhusika alikuwa hayajui, hapana. Alikuwa isipokuwa tu uelewa wake yeye mpaka wakati huo, ulikuwa tofauti kidogo na wa KMH na maelezo yake kuhusu uelewa huo wa mhusika, yatafuata baadaye kidogo hapa chini



MAELEZO YA UTANGULIZI YA KILICHOTOKEA BAADA YA MUHUSIKA KUWA AMEANDIKA BARUA HIYO

Baada ya kuwa amekamilisha kuiandika barua hiyo, mhusika aliiwasilisha kwa KMH wa MWI kama ilivyo kawaida

  • KMH alipoisoma akamjulisha kuwa amekosea namna ya kui-address
  • KMH alisema kwamba, mhusika alikuwa amekosea mkondo wa namna barua hiyo ilivyotakiwa iende na kumfikia mkuu wa mwisho
  • Mkubwa aliyekuwa anayefuata JUU YA IDARA ambaye barua hiyo ilihitajika ipitie kwake kwanza, aipitishe na baada hapo ndiyo iende mamlaka za juu na kumfikia mkuu wa juu kabisa na wa mwisho, hakuwa sahihi kwenye barua hiyo
  • KMH alimjulisha mhusika kuwa mabadiliko ya mkondo huo wa mawasiliano kutokea hapo idarani kwenda juu, unatokana na mabadiliko ya hivi karibuni kwenye muundo wa taasisi (change of organization structure)
  • Kwa hiyo KMH alimshauri mhusika abadilishe mkondo wa mawasiliano aliokuwa ameutumia kwenye barua hiyo, ambao ni ule wa zamani, halafu aingize mkondo mpya wa sasa ambao KMH aliushauri.
  • Mhusika alikubali kuingiza mabadiliko hayo na baada ya hapo, alimpa KMH soft copy ya barua hiyo
  • KMH alifanya mabadiliko hayo na baada ya hapo mhusika alienda akaisaini na baadaye tena akaiwasilisha kwa KMH wa MWI
Mabadiliko hayo yalikuwa ni rahisi muno kuyafanya kwa sababu yalihusu sehemu ndogo tu ya ule ukurasa wa kwanza



………..inaendelea
 
MAELEZO YA NYONGEZA KUHUSIANA NA TUKIO LA WATU “STRANGERS” KUONEKANA NDANI YA JENGO JUMANNE YA TARERE 02 MARCH 2021

………………..inaendelea

MABADILIKO YALIYOTOKEA KWENYE MUUNDO WA TAASISI MAMA (CHANGE OF ORGANISATION STRUCTURE)


Ni kwamba kuna mabadiliko yamefanyika kwenye taasisi mama anayofanyia kazi mhusika, na ambayo yamepelekea muundo wa taasisi hiyo kubabdilika. Kwa hiyo, mara tu baada ya mabadiliko hayo kufanyika, kuna taarifa za mabadiliko hayo ambazo zilitolewa kwa ajili ya umma wa watanzania pamoja na wadau wote popote pale walipo duniani, kuweza kufahamu juu ya mabadiliko hayo

Hata hivyo, kuna taarifa zingine bado ziko ndani na ambazo bado hazijawekwa public, na mojawapo ya taarifa hizo ni zile ambazo mhusika hakuwa amezitumia kwenye barua yake lakini hatimaye alilazimika kuzitumia baada ya kuwa ameshauriwa na KMH



Kwa hiyo kutokana na mabadiliko hayo, mpaka muda huu, kuna taarifa za mabadiliko ya muundo wa taasisi za aina mbili, kwamba kuna zile ambazo:

  • UMMA WA WATANZANIA UMESHAJULISHWA, IKIWA NI PAMOJA NA WADAU WOTE POPOTE PALE WALIPO DUNIANI
  • UMMA BADO HAUJAJULISHWA
Sehemu ya taarifa zinazoangukia kwenye kundi la zile ambazo umma bado haujajulishwa, ndiyo zile ambazo:

  • Mhusika alishauriwana KMH kuzitumia kwenye barua yake aliyoiandika tarehe 21 JANUARY 2021 na ambayo haikufika kule ilikokusudiwa kufika
  • Mpaka jana tarehe 04 March 2021, barua hiyo ilikuwa haipo kwenye ofisi husika ambako mhusika alikuwa amei-address


HIVI KARIBUNI MHUSIKA ALIWAHI KUPOKEA BARUA KUTOKA MAMLAKA ZA JUU IKIWA IMEPITIA MKONDO ULE WA ZAMANI

Hivi karibuni, mhusika aliwahi kupokea barua iliyotoka mamlaka za juu ambayo nayo pia iliandikwa tarehe hiyo hiyo ya 21 JANUARY 2021

  • Barua hii aliipata siku ya J5 tarehe 27 January 2021, wakati huo yeye akiwa tayari alishaandika ile ya kweke, kuelekea kwenye ofisi ile kule ilikokuwa imetoka hii aliyoipokea yeye kwenye tarehe hiyo tajwa
  • Kwa hiyo ofisi ilikokuwa imetoka barua hiyo, ndiyo ofisi hiyo hiyo ambayo mhusika ali-address barua yake ya tarehe 21 JANUARY 2021, na ambayo jana ilibainika kuwa haijawahi kufika huko
  • Kwa ile aliyoipokea mhusika, alifanikiwa kuijibu hiyo ndani ya muda muafaka
  • Barua hii ilimfikia mhusika ikiwa imepitia mkondo wa mawasiliano ule ule wa zamani, (yaani kabla ya mabadiliko ya muundo wa taasisi) na aliijibu kwa kutumia mkondo huo wa mawasiliano wa zamani.
  • Barua ya majibu ya mhusika kuelekea ngazi za juu (kupitia kwenye mkondo ule ule wa zamani na ambao ulitumika na barua aliyotakiwa kuijibu) aliikuta kwenye rekodi za ofisi hiyo ikiwa tayari ilishafika huko
  • Kwa kumbukumbu zake, barua hiyo ya majibu (ambayo alikuta imeshafika ofisini huko), aliiwasilisha ofisini kwa MWI tarehe 03 Februari 2021
Kwa hiyo, barua ile ya mwanzo aliyoiandika mhusika haikuweza kuonekana kwenye rekodi za ofisi hiyo, licha ya kuwa ilitafutwa kwa muda usiopungua dakika 10.

Hiyo ndiyo ile aliyoshauriwa na KMH kubadilisha mkondo wa mawasiliano na akafanya hivyo

Kwa hiyok kilichojitokeza kwenye barua hizi mbili ni kwamba

  • Ile ambayo mhusika alikuja kuiandika baadaye na kutumia mawasiliano yale ya zamani ILIFIKA kule ilikotakiwa kufika
  • Ile ambayo ALIIANDIKA KABLA kwa kutumia mawasilano ya KMH, yenyewe HAIKUFIKA kule ilikotakiwa kufika


UP NEXT

A: TAARIFA ZA MABADILIKO YA MUUNDO WA TAASISI AMBAZO UMMA WA WATANZANIA UMESHAJULISHWA, IKIWA NI PAMOJA NA WADAU WOTE POPOTE PALE WALIPO DUNIANI

B: TAARIFA ZA MABADILIKO YA MUUNDO WA TAASISI AMBAZO UMMA BADO HAUJAJULISHWA



……………..inaendelea
 
TAARIFA ZA MABADILIKO YA MUUNDO WA TAASISI AMBAZO UMMA WA WATANZANIA UMESHAJULISHWA, IKIWA NI PAMOJA NA WADAU WOTE POPOTE PALE WALIPO DUNIANI

Ni kwamba hapo awali, Idara ya mhusika ilikuwa ndani

Ni kwamba hapo awali, Idara ya mhusika ilikuwa ni unit moja (tuiite UNIT-A) ikiwa ndani ya unit nyingine kubwa (tuiite MAJOR UNIT-A) isipokuwa tarehe 02 Novemba 2020, tangazo kwa umama lilitoka kuwa UNIT-A itakuwa ndani ya unit nyingine ambayo ni MAJOR UNIT-B

  • Kwa hiyo kuanzia pale UNIT-A ikawa haipo tena kwa jina hilo
  • Vile vile UNIT-A ikawa si sehemu tena ya MAJOR UNIT-A bali ikawa sehemu ya unit nyingine mpya ambayo ni MAJOR UNIT-B
Mbali na hayo, taarifa hiyo kwa umma ilibainisha kuwa

  • Aliyekuwa mkuu wa Idara wa UNIT-A ndiye mkuu wa unit mpya ambayo ni MAJOR UNIT-B
  • UNIT-A imehama kutoka MAJOR UNIT-A na kwenda MAJOR UNIT-B na si kwamba imebadilika na kuwa MAJOR UNIT-B
Kwa hiyo mpaka hapa, ni kwamba UNIT-A haijabadilika na kuwa MAJOR UNIT-B, isipokuwa imehamia kwenye unit mpya kubwa ambayo ni MAJOR UNIT-B



MAELEZO KWA KIFUPI KUHISANA NA MKUU WA UNIT MPYA, YAANI MAJOR UNIT-B

Mkuu wa huyu wa MAJOR UNIT-B ndiye alikuwa MWI wa mhusika

  • Ndiye yule amekuwa akishughulikia maslahi ya mhusika katika namna ambayo mhusika ilimchanganya
  • Mkuu huyu bado hajapata ofisi kama Mkuu wa MAJOR UNIT-B, isipokuwa anayo tu ile ofisi yake ya kawaida
  • Ile aliyokuwa anatumia mwanzo, hawezi tena kuitumia muda huu kwa sababu yeye siyo MWI tena
  • Kwa hiyo kwa sasa kuna Kaimu MWI mwingine ambaye taarifa za yeye kukaimu nafasi, umma bado haujajulishwa
Hivyo basi, kile kilichotokea mpaka muda huu ni kwamba Kaimu MWI (au UNIT-A kwa sasa) anayo ofisi wakati Mkuu wa MAJOR UNIT-B, yeye hana ofisi.

Hizi MAJOR UNIT kama ambavyo mhusika anajaribu kuzitolea maelezo yake humu, ni unit kubwa ambazo kawaida huwa zinakuwa na idara kadhaa chini yake



Hata hivyo, taarifa kwa umma kuhusiana na nani ambaye kwa sasa anakaimu nafasi ya Mkuu wa Idara wa UNIT-A, bado hazijatolewa isipokuwa yupo/wapo anayekaimu/wanaokaimu



MABADILIKO MENGINE YANAYOHUSU MUUNDO WA TAASISI NA AMBAYO UMMA WA WATANZANIA UMESHAJULISHWA PIA


Ni kwamba Taasisi mama, imefaniikiwa kujipanua na kufikia kwenye uwezo wa kuzi-asili na taaisi zingine mbili zilizoko Dodoma na Nzega, na hivyo kuwa ni sehemu yake. Taasisi hizi sasa tuziite UNIT-G na UNIT-H

Baada ya hapa turudi sasa kwenye mabadiliko ambayo bado yanasikika midomoni mwa watu tu ila hakuna taarifa zozote ambazo zimeshatolewa kwa umma





UPNEXT

B: TAARIFA ZA MABADILIKO YA MUUNDO WA TAASISI AMBAZO UMMA BADO HAUJAJULISHWA

  • Ni taarifa ambazo kwa sasa mhusika anazisikia masikioni mwa watu tu kwenye mazingira ya ofisini
  • Zinaweza kuwa ziko sahihi au haziko, ila zitathibitishwa pale tu mamlaka za juu zitakapokuwa zimetoa tangazo husika kwa umma


……………………….inaendelea
 
……………………….inaendelea

TAARIFA ZA MABADILIKO YA MUUNDO WA TAASISI AMBAZO UMMA BADO HAUJAJULISHWA


Mambo kadhaa yafuatayo bado hayajulikani

  • Anayekaimu ukuu wa Idara wa UNIT-A kwa sasa anajulikana Idarani tu isipokuwa hakuna taarifa rasmi kwa umma iliyotolewa kuonyesha kuwa huyo ndiyo Kaimu MWI
  • Mbali na hilo, kwa taarifa zilizopo wanazoendelea kubadilishana watu kwa sasa kwenye mazingira ya ofisini, ni kwamba kuna unit zngine kadhaa zilizo ndani ya mazingira ya Taasisi mama (tuziite kwa ujumla wake UNIT-B) ambazo baadaye zitakuja kuungana na UNIT-A, pamoja na UNIT-G na UNIT-H zilizoko Dodoma na Nzega
  • Baada ya hapo unit zote hizi kwa ujumla wake ndiyo zitaunda MAJOR UNIT-B, iliyopelekea UNIT-A kuhama kutoka MAJOR UNIT-A ilikokuwa zamani
Hizi units zote zilizotajwa hapa zipo na zote ni sehemu muafaka kabisa ya Taasisi mama. Kitu pekee ambacho mpaka muda huu bado hakijasemwa ni huo muunganiko ambao watu wa ngazi za chini wanaendelea kuuongelea huku mamlaka za juu zikiwa bado hazitamka lolote

Kwa hiyo yote yaliyotajwa hapo bado hayajawa rasmi mpaka pale mamlaka husika zitakapokuwa zimechukua hatua ya kuujulisha umma kuwa zimeamua kufanya hivyo



TURUDI SASA KWENYE BARUA TATU ZA MHUSIKA TUKIZIHUSIANISHA NA MABADILIKO HAYA YA MUUNDO WA TAASISI MAMA

Kati ya barua hizi tatu ambazo mhusika ameshaziongelea leo:

  • Mbili aliziandika yeye zikielekea mamlaka za juu, wakati moja aliipata ikiwa imetoka mamlaka za juu kuja kwake
  • Kati ya zile mbili alizoandika, moja ililfika na nyingine haikufika

MKONDO WA MAWASILIANO WA BARUA ZA MHUSIKA KWENDA NGAZI ZA JUU, NDANI YA TAASISI MAMA

A: MKONDO KAMA ULIVYOKUWA ZAMANI


Mkondo wa zamani wa mawasilIano ya barua za mhusika kwenda ngazi za juu ulikuwa kama ifuatavyo

UNIT-A⟹⟹MAJOR UNIT-A⟹⟹NGAZI ZA JUU

Kwa hiyo barua zake zote zilikuwa zinapitia kwenye MAJOR UNIT-A kabla ya kuwa zimepokelewa na ofisi husika ngazi za juu



B: MKONDO KAMA ULIVYO SASA

UNIT-A⟹⟹MAJOR UNIT-B⟹⟹NGAZI ZA JUU

Mpaka hapa, msomaji inabidi arejee mambo kdahaayafuatayo

  • Barua aliyoipata mhusika tarehe 27 JANUARY 2021, ikiwa imetoka mamlaka za juu, na iliyoandikwa tarehe 21 JANUARY 2021, ilitumia MKONDO WA ZAMANI
  • Mhusika naye pia aliijibu barua hiyo kwa kutumia MKONDO HUO HUO WA ZAMANI, na barua hiyo ya majibu ilifika kule ilikokuwa imekusudiwa
  • Vile vile, barua aliyoandika mhusika tarehe 21 JANUARY 2021, ikiwa inaelekea mamlaka za juu, mwanzoni aliiandika AKIWA MEKUSUDIA ITUMIE MKONDO WA ZAMANI
  • Hata hivyo, baadaye alishauriwa na KMH kuwa inabidi atumie mkondo mpya na alifanya hivyo
Baada ya kuwa ametumia MKONDO MPYA kwa mawasiliano na kama alivyoshauriwa na KMH, barua hii ya mhusika haikuweza tena kufika ngazi za juu kule ilikokuwa imekusudiwa kufika



BARUA NYINGINE ALIYOIANDIKA MHUSIKA BAADA YA TAREHE 27 JANUARY 2021 KWA KUPITIAMKONDO WA ZAMANI


Baada ya kupata barua kutoka mamlaka za juu ikiwa imepitia kwenye mkondo wa zamani, mhusika alibadilisha mawazo na kudhani kuwa pengine ushaurri wa KMH kwa barua yake ile ya mwanzo haukuwa sahihi

  • Mhusika aliamua kutoa nakala barua nyingine, sawa na ile ya tarehe 21/01/2021 na kuiwasilisha idarani ili iende ngazi za juu, kwa kupitia MKONDO WA ZAMANI
  • Hata hivyo, barua hiyo ilirudishwa na Mkuu wa MAJOR UNIT-A (hii ni unit kule ambako UNIT-A wamehama) ikiwa na ki-note cha kikimshauri MHUSIKA APITISHIE BARUA ZAKE KWENYE MKONDO MPYA
Ikumbukwe kuwa mpaka hapa, mhusika alikuwa tayari ameshapata barua kwa kutumia mkondo wa zamani, na hatimaye naye kuijibu kwa kutmia mkondo huohuo

Baada ya hali hii kujitokeza, mhusika hatimaye aliitwa na Kaimu MWI mwingine mpya (Kaimu wa siku zote yule ambaye bado hajatangazwa, alikuwa safarini) ofisini kwa MWI kujadili swala hilo na baada ya maongezi yao, hatimaye mhusika aliamua apumzike kwanza na swala la barua hizi. Hiyo sasa ilikuwa ni J3 ya tarehe 07 Februari 2021 na kweli kuanzia pale alipumzika

  • Ni kwa sababu barua hizo alikuwa akiziandika na hatimaye zingine kuwapa nakala baadhi ya wakuu wengine ndani ya taasisi hiyo
  • Mhusika alihofia kuwa nakala za barua hizo hatimaye zingeweza kuwachanganya, na possibly kupelekea kumuona yeye kama mtu aliyechanganyikiwa
Hata hivyo, kwa wakati huo, jibu lililokuwa amelipata kwa ki-note kutoka kwa Mkuu wa MAJOR UNIT-A, baada ya kutokuipitisha barua yake, lilimthibitishia kuwa mkondo ule alioutumia kwa barua yake ya kwanza ya tarehe 21/01/2021 na kwa ushauri wa KMH, ulikuwa sahihi na hivyo akawa ana imani kua barua hiyo ya kwanza kabisa itakuwa ilishapokelewa na mamlaka husika



HITIMISHO

Baada ya mkanganyiko huu kujitokeza, mhusika aliamua kusitisha kwanza zoezi la barua hizi, na ndipo J2 ya wiki hii tarehe 02 MARCH 2021 ziilipoanza kujitokeza “movements” zilizosababisha kumuweka kwenye tahadhari kubwa

Baada ya hapo jana Alhamis tarehe 04 MARCH 2021 aliamua afuatilie kwenye ofisi husika alikokuwa ameelekeza barua yake ili kuona kama kuna kitu tayari kinaendelea ndiyo akautana na situation ya HOLAAAAA, vijana wa mtaani huwa wanasema. Baruahiyo haikufika huko

Kwa hiyo mpaka muda huu, situation ya mawasiliano ya barua za mhusika ni kwamba

  • Akiandika barua kupitia mkondo wa zamani, barua hizo zinarudishwa kwake
  • Aakiandika barua kupitia mkondo huu wa sasa, barua hizo hazifiki kule zinakotakiwa kwenda, nadhani zinapotelea njiani
Na kwa sasa hivi, huyu Kaimu MWI wa siku zote (ambaye hajatangazwa) hayupo, yuko safarini.
Vile vile wakati ule wa pilikapilka ukiwemo ushauri wa barua kubadilishwa mkondo wa mawasiliano, na hatimaye zingine kuwa zinakwenda na kurudi, napo pia vile vile hakuwepo

Actually, barua zilizowahi kurudishwa na Mkuu wa MAJOR UNIT-A ni mbili, isipokuwa mwandishi hakuona mantiki ya kuziongelea zote mbili. kwa sababu moja tu ilikuwa inatosha kama sample

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE: SATURDAY 06 MARCH 2021

BAADA YA BARUA ZA MHUSIKA KUPITIA MKONDO WA ZAMANI KUWA ZINARUDI: WALICHOONGEA MHUSIKA NA KAIMU MKUU WA IDARA (K-MWI) OFISINI KWA MKUU HUYO


Mpaka hapa, msomaji wa taarifa hizi inabidi akumbuke kuwa:

  • Mhusika aliandika barua yake ya kwanza kuelekea mamlaka za juu tarehe 21/01/2021
  • Barua hiyo alikuwa ameiandika ikiwa inaonyesha kuwa inatakiwa kupitia MKONDO WA ZAMANI WA MAWASILIANO KUELEKEA NGAZI ZA JUU
  • Baada ya kuiwasilisha idarani, KMH akamshauri mhusika abadilishe mkondo wa mawasiliano, atumie huu mpya wa sasa
  • Hapo kabla, mhusika alikuwa hajawahi kutumia mkondo huu mpya wa mawasiliano
  • Vile vile, mhusika hakuwa amewahi kuona barua nyingine yoyote ile ambayo ilikuwa imetumia mkondo huo wa mawasiliano
Baada ya ushauri wa KMH, mhusika alikubaliana na ushauri huo, lakini hadi kufikia Alhmais ya tarehe 04/03/2021, ilikuja kubainika kuwa barua ilikuwa haijazifikia ngazi hizo za juu,yaani kule alikokuwa ameielekeza

Hata hivyo mhusika akiwa tayari ameshaandika barua yake ya kwanza, amewahi kupokea barua nyingine ikitoka ngazi hizo za juu na ikiwa imepitia kwenye mkondo wa mawasilano wa zamani, na akaijibu kupitia mkondo huo huo. Hiyo yenyewe aliikuta tayari imeshafika kule alikoielekeza

Mbali na hayo, baada ya barua hii tajwa hapa juu kuwa ameijibu, mhusika naye pia alichukua hatua za kubadilisha mkondo wa mawasiliano na kurudi kwenye ule wa zamani. Mhusika aliandika barua mbili kwa kutumia mkondo huo wa mawasiliano lakini zilirudishwa kwake zikiwa na ki-note kilichokuwa kikionyesha kuwa anatakiwa atumie mkondo mpya wa mawasiano na si ule wa zamani



………………..inaendelea
 
Back
Top Bottom