#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

UPDATE:SATURDAY 27 FEBRUARY 2021



TUKIO LA PILI; SAFARI YA KIKAZI MWEZI MEI 2012


…….inaebdelea


Akiwa antokea kukagua na kuchukua data za matetemeko ya Ardhi, baada ya gari kuharibika pale Dakawa Morogoro na kuonyesha dalili za kutokutengemaa katika ndani ya muda muafaka wa safari hiyo, aliamua kushuka na kuchukua usafiri mwingine hadi Morogoro mjini. Safari yake siku hiyo ilikuwa ni ya Dar es Salaam na ndani ya siku hiyo lakni alilazimika kuishia Morogoro na kulala pale kwa sababu wakati anaingia Mrogoro tayari jua lilikuwa limezama, na hakuwa na mpango wa tena wa kusafiri usiku. Vinginevyo kama gari ya mwanzo isingepata matatizo, alikuwa anatakiwa kuwasili Dar es Salaam ndani ya siku hiyo kwenye mida ya kama saa kumi jioni. Gari hiyo ilipata breakdown mara mbili, ya kwanza wakafanikiwa ku-ifix ndani ya muda muafaka halafu ile ya pili pale dakawa ndiyo ikabidi ichukue muda mrefu zaidi

Details nyingine za safari hii na ambazo aliwahi kuzitoa kwa “SPECIALST” hawezi kuziongelea humu, hazitoi nafasi ya kufanya hivyo

Hata hivyo, mambo mawili yafuatayo yanatoa nafasi ya kutolewa maelezo kidogo humu jukwaani. Mambo haya yanahusiana na tiketi aliyokuwa anasafiria ambayo ilipotea siku hiyo hiyo na jingine, linamhusus mama yake wa kiroho

  • Siku alliyolala Morogoro, akiwa chumbani alianza kukagua vitu vyake na kukuta ticket ya safari yake haipo tena ndani ya begi lake alimokuwa ameiweka
  • Begi hilo muda wote lilikuwa kwenye carrier ndani ya gari allilokuwa akisafiria
  • Kama kuna kipindi pengine ticket hiyo iliweza kuchukulliwa na mtu mwingine ndani ya begi hilo, basi itakuwa ni wakati huo huo alipokuwa kwenye eneo hilo ambapo gari iliharibikia.
  • Kuna kipindi aliwahi kutoka ndani ya gari hilo na kwenda umbali kidogo na kukaa huko kwa takribani dakika 30, gari likiwa linaendelea na matengenezo
  • Akiwa huko mbali kidogo na gari lilipokuwa, alikuwa anapiga stori na jamaa zake watatu waliopanda kwenye gari hilo na kumkuta akiwa yeye tayari ameshapanda na kukaa kwenye siti yake
  • Watu hawa watatu wote walikuwa ni staff-mates wa mhusika, mmojawapo akiwa pia ni jamaa yake wanayefahamiana kwa karibu kiasi na mhusika
  • Watu hawa alikuwa amesafri pamoja nao kutoka Dodoma na aliachana nao mahali pale ambapo gari lilipata hitilafu
Vinginevyo tiketi hiyo atakuwa aliidondosha chini wakati alipokuwa anajaribu kuiweka ndani ya begi, akadhani kuwa aliiweka humo kumbe hapana

Vile vile akiwa yupo chumbani kwake Morogoro, allijaribu kuwasilaian na mama wa kiroho na kumweleza kilichokuwa kumejiri kwa siku hiyo., kwa sababu hata hapo kabla, mama huyu walikuwa wamewasiliana na aliyekuwa ameanzisha mawasiliano ni yeye, yaani mama wa kirohoo. Siku hiyo, mama huyu aliongea kwa muda na mhusika halafu baadaye tena akawa hapokei simu wala kujibu sms



MWISHO WA TUKIO HILI. DETAILS ZINGINE MUHIMU ZA TUKIO HILI HAZIRUHUSU KUWEKWA HUMU JUKWAANI



HITIMISHO


Baada ya safari, hii mhusika hakubahatika tena kupangiwa safari nyingine ya kikazi hadi mnamo Novemba 2012 alipopangiwa safari nyingie nje ya nchi, nchi jirani, ndani ya Afrika. Hata hivyo, safari hiyo nayo pia hakuweza kuifanya kutokana na sababu ambazo asingependa sana azitolee maelezo ya kina humu jukwaani

  • Safari hii ilihusiana na Mkutano wa Kimataifa kwa ajili ya kuchakata Data za Matetemeko ya Ardhi
  • Kwenye booking ya safari hiyo, alikuwa anatakiwa kuunganisha ndege mbili kupitia nchi nyingine tena jirani, na kuwasili nchi aliyokuwa anakwenda kwenye mida ya kuanzia saa tano usiku
Safari hiyo hakufanikiwa kuifanya na badala yake alikwenda mtu mwingine na tangia pale hadi leo, hajaweza tena kufanya safari yoyote ya kikazi

Mpaka hapa, msomaji inabidi akumbuke pia kuwa, hadi muda huo anasitisha safari hiyo ya nje, alikuwa pia tayari ameshasitisha safari za binafsi tangu Novemba 2010. Kwa hiyo kitendo cha kusitisha tena safari za kiofisi kilipelekea sasa asiweze kusafiri tena tangu pale hadi leo.

Hata hivyo, swala la kusitisha safari za kiofisi lilikuwa nje ya mamlaka yake na hivyo ilibidi aandike barua kuziomba mamlaka za juu kazini kwake kumruhusu asifanye safari hizo, ndani na nje ya nchi.

Zaidi mhusika aliziomba malaka hizo zimlinde kwa namna zinavyoweza kumlinda kutokana na hatari aliyokuwa anaiona katika baadhi ya matukio aliyokuwa amekumbana nayo pindi alipokuwa yuko safarini. Kwa hiyo aliziomba mamlaka hizi zimlinde kwenye mazingira ya ofisini pia

Kwa hiyo, kuanzia pale mpaka leo hii, mhusika akawa ameweka rekodi ya kwamba, mara ya mwisho alifanikiwa kusafiri ilikuwa ni May 2012; na tangia pale hajawahi kusafri tena hadi leo



KWA HIYO REKODI YA SAFARI ZA MHUSIKA KUANZIA PALE HADI LEO IKAWA KAMA ILIVYOONYESHWA HAPA CHINI

MWAKA 2013


Mhusika hakufanya safari yoyote ile nje ya Dar es salaam, ya binafsi wala ya kikazi



MWAKA 2014

Mhusika hakufanya safari yoyote ile nje ya Dar es salaam, ya binafsi wala ya kikazi



MWAKA 2015

Mhusika hakufanya safari yoyote ile nje ya Dar es salaam, ya binafsi wala ya kikazi



TUKIO LA TATU: JANUARY 2016:

TUKIO LA KWANZA NDANI YA JENGO IILIMO OFISI YAKE, LAMTOKEA MHUSIKA ILA LIKIWA NI TUKIO LA PILI KUTOKEA NDANI YA JENGO, AMBAPO LA KWANZA LILIKUWA TAYARI LIMESHATTOKEA KIPINDI KIFUPI NYUMA NA KUMHIUSISHA MTU MWINGINE AMBAYE ALIKUWA NI MKUU WA IDARA WA KIPINDI HICHO

.........MAELEZO YA UTANGULIZI WA TUKIO LENYEWE



………………..inaendelea
 
TUKIO LA TATU: JANUARY 2016:

TUKIO LA KWANZA NDANI YA JENGO IILIMO OFISI YAKE, LAMTOKEA MHUSIKA ILA LIKIWA NI TUKIO LA PILI KUTOKEA NDANI YA JENGO, AMBAPO LA KWANZA LILIKUWA TAYARI LIMESHATTOKEA KIPINDI KIFUPI NYUMA NA KUMHIUSISHA MTU MWINGINE AMBAYE ALIKUWA NI MKUU WA IDARA WA KIPINDI HICHO



MAELEZO YA UTANGULIZI WA TUKIO LENYEWE


Hapa anachojaribu kuueleza umma mhusika ni kwa, kwamba kuna matukio mawili ambayo yalitukia ndani ya muda mfupi na ndani ya jengo ilimo ofisi ya mhusika, ambapo tukio la kwanza lilimhusisha mtu mwingine ambaye siyo yeye, na la pili likamhusisha yeye mwenyewe, yaani mhusika



TUKIO LA KWANZA NDANI YA JENGO: LILIMHUSISHA MKUU WA IDARA WA KIPINDI HICHO MNAMO OKTOBA/NOVEMBA 2015

Tukio hili la kwanza lilimhusisha Mkuu wa Idara wa kipindi hicho


  • Llilitukia kati ya Oktoba/ Novemba 2015
  • Wakati linatokea, Mkuu wa Idara huyu alikuwa bado ni mpya kabisa kwenye nafasi hiyo kwa sababu alianza kutumika kwenye nafasi hiyo mnano Julai 2015
  • Lilitukia katika kipindi ambacho wanafunzi walikuwa bado wako likizo
Kwa kifupi ni kwamba kuna mtu wa ajabu alitokea ndani ya jengo siku ya J2 na kumshambulia Mkuu wa Idara, almanusura amuue

  • Mtu huyo alikuwa anajaribu kuiba Kompyuta aina ya Mac, na ambayo japo ilikuwa ni ya gharama kubwa kidogo, lakini si watu wengi wanaojua kuzitumia au wanapenda kuzitumia, hali inayopelekea kuutokuwa na soko zuri sana hapa nchini kwetu
  • Siku huiska, hapakuwa na mtu mwingine ndani ya jengo. Mkuu huyu alikuwa peke yake
  • Inakadriwa kuwa ilikuwa ni mchana, kwenye mida ya takribani saba hivi
  • Mkuu Ilibidi aruke kutoka ghorofa ya kwanza hadi chini ili kuokoa miasha yake
Tukio hili la kwanza ndani ya jengo, ndiyo lilikuja baadaye tena, lika-trigger tukio jingine la pili ndani ya jengo hilo hilo, ambalo LENYEWE (TUKIO LA PILI) HALIKUMHUSISHA TENA MKUU WA IDARA, BALI MHUSIKA.

Kwa hiyo tukio la kwanza lililowahi kumpata Mkuu wa Idara, Oktoba/ Novemba 2015, ndiyo hilo hilo lilikuja baadaye tena kupelekea mhusika naye kupatwa na tukio jingine ndani ya jengo hilo hilo

Maelezo ya kina kuhusiana na matukio haya mawili, yatafuata mufa mfupi ujao



TUKIO LA PILI NDANI YA JENGO: LILIMHUSU MHUSIKA MWENYEWE: JANUARY 2016

  • Mtu yule yule wa ajabu aliyewahi kumshambulia Mkuu wa Idara alirudi tena ndani ya jengo
  • Safari hii alirudi kama mgeni wa kawaida tu, ndani ya ofisi ya Mkuu wa Idara, kitendo kilichopelekea Mkuu kufanikiwa kumtambua mtu huyu kwa sura na kwa umbile lake pia
  • Siku hiyo, mhusika aliingia ofisini kwa Mkuu na baada ya muda kitambo mtu huyo naye akawa amefika ofisini humo
  • Mkuu wa Idara ambaye ndiye aliwahi kushambuliwa na mtu huyo, akamtambua hasimu wake huyo na hapo hapo akatoa amri kuwa watu wote waliokuwa humo ndani ya ofisini yake wasitoke nje
  • Mhusika naye pia alikuwa mmojawapo wa watu hao waliokuwemo humo ndani. Na hakuwa na hata zaidi ya dakika mbili tangu aingie ofisini humo
Baada ya hapo, badala ya Mkuu wa Idara kupiga simu Polisi ili Polisi waje wamchkue mshukiwa wake, Mkuu huyo alitoa amri akimwambia mhusika pamoja na dereva wake Mkuu, na Mkuu mwenyewe, kwamba watatu hawa kwa ujmla wao wamchukue mtu huyo na kumpeleka Kituo cha Polisi.

Hata hivyo, mhusika siyo Polisi na hajawahi kuwa Polisi, na wala utaratibu wa kukamata mshukiwa huwa hauendi hivyo. Mkuu wa Idara alitakiwa apige simu Polisi kisisrisiri na kuwaomba waje wamkamate mtuhumiwa huyo



………………..inaendelea
 
TUKIO LA TATU LA MHUSIKA: JANUARY 2016:



……………….inaendelea



MAELEZO YA KINA KUHUSIANA NA MATUKIO YOTE MAWILI YALIYOWAHI KUTOKEA NDANI YA JENGO
, YAANI LILE LILOMHUSU WA MKUU WA IDARA NA JINGINE LILILOMHUSU MHUSIKA



TUKIO LA KWANZA NDANI YA JENGO: LILIMHUSISHA MKUU WA IDARA WA KIPINDI HICHO MNAMO OKTOBA/NOVEMBA 2015

Hili lilitokea siku ya J2 ambapo ndani ya jengo hapakuwa na mtu yeyote isipokuwa Mkuu wa Idara (MWI) mwenyewe

  • Siku hiyo alifika ofisini akitaka kufanya kazi, ofisini kwa MWI
  • Alipofika ofisini akagundua kuwa kulikuwa na mtu ndani ya ofisi hiyo ya MWI
  • Mtu huyo alikuwa amepita vipi kwenye geti la lango kuu haikujulikana isipokuwa ilionekana aliingia ndani ya ofisi ya MWI kwa kunyofoa grill kutoka ukutani na hatimaye kutumia kitu kama master key kufungua mlango wa ofisi hiyo
  • Motive ya mtu huyu ilikuwa kuiba kompyuta aina ya Mac, yenye thanmani ya takriban TZS 2,000,000/=
  • Ilikuwa siku ya J2 mchana kweupe
Kilichotokea baada ya watu hawa kufumaniana kwa wizi, ni confrontation iliyopelekea kuanza kupigana. Na kwa sababu mwizi huyu alikuwa pande la mtu, MWI hatimaye alizidiwa na kujisalimisha kwa kuruka kutoka juu ghorofa ya kwanza na kutua chini kwenye sakafu

  • MWI huyu aliumia mkono, hasa kwenye kiwiko kwa sababu J3 iliyofuata alionekana akiwa amefunga POP
  • Ilisemekana kuwa alitua chini kwa kiwiko na hivyo aliumia kiwiko
Hata hivyo mhusika alipata shida kidogo katika kuelewa namna utuaji huu kwa kiwiko ulivyotokea kwa sababu, mtu akianguka kutoka juu na akatua chini kwa kutumia kiwiko, ataumia zaidi begani kuliko hata kiwiko chenyewe. Ni kweli kiwiko lazima nacho kitaumia lakini hakiwezi kuumia peke yake isipokuwa na bega nalo vile vile ltaumia pia, tena zaidi kuliko hata kiwiko.

MWI alikuwa ameumia kiwiko, bega lilikuwa liko sawsawa kabisa halijaguswa na chochote

Baada ya tukio hili kuwa limempata mtu huyu na taarifa zake kuwa zimesambaa kwa kasi sana ndani ya taaasisi nzima

  • Huku nyuma Idarani hapakuwa na briefing yoyote official kuhusiana na tukio hili kwa watu wote waliokuwa ofisi zao zilikuwa ndani ya jengo jengo hilo
  • Kilichokuwa kimertokea baada ya tukio hilo ni taarifa tu kusambaa kwa haraka sana kupitia kwenye mailing list ya wafanyakazi wote wa taasisi nzima, email iliyomjulisha kila mfanyakazi uwa kuna tukio la hatari limetokea ndani ya jengo fulani ambapo MWI wa jengo hilo amenusurika kuuawa na mtu wa ajabu aliyekuwa ameingia ndani ya jengo kwa ajili ya kuiba kompyuta
  • Zaidi ni kuwa watu wote wa idarani hawakuweza hata kufanya kikao kifupi cha kujadili kuhusiana na tukio hilo ili waweze kuona ni kwa namna gani sasa watajikinga na matukio mengine yanayofanana na hili mbele ya safari, kama yatakuwepo
  • Kilichotokea tu ni kwamba kuliwekwa karatasi ya michango wa fedha pale idarani ofisini kwa MW,I ikiwaomba watu wote idarani kumsaidia MWI pesa kiasi kama mchango kwa ajili ya matibabu ya mkono aliokuwa ameumia ghafla
Kwa hiyo kitu pekee kilichofanywa na watu pale idarani baada ya tukio hilo kutokea ni kutoa michango ya fedha tu basi, hakuna kingine



…………….inaendelea
 
TUKIO LA TATU LA MHUSIKA: JANUARY 2016:



……………….inaendelea



MAELEZO YA KINA KUHUSIANA NA MATUKIO YOTE MAWILI YALIYOWAHI KUTOKEA NDANI YA JENGO
, YAANI LILE LILOMHUSU WA MKUU WA IDARA NA JINGINE LILILOMHUSU MHUSIKA



TUKIO LA KWANZA NDANI YA JENGO: LILIMHUSISHA MKUU WA IDARA WA KIPINDI HICHO MNAMO OKTOBA/NOVEMBA 2015

………….inaendelea

Baada ya tukio hilo kuwa limepita, MWI alichukua miezi kadhaa akiwa nje ya ofisi akiuguza majeraha ya mkono uliokuwa umeumia, na hatimaye aliweza tena kurejea ofisini. Ikumbukwe kuwa mtu huyu aliingia kwenye ofisi hii ya MWI kwa mara ya kwamnza mnamo Julai 2015. Miezi kadhaa mbele ndiyo akapata tatizo la kushambuliwa na hadi inafika January 2016, ndiyo alikuwa anakaribia kutimiza nusu mwaka akiwa ofisini kama MWI



TUKIO LA PILI NDANI YA JENGO LATOKEA TENA NA KUMHUSISHA MHUSIKA

  • Hili lilitokea mnamo Februari 2016
  • Safari hii, tukio hili lilimhusu mhusika
  • Wakati huo, MWI aliyekuwa amejeruhiwa kwenye tukio la kwanza naye tayari wakati huu alikuwa amesharudi ofisini


MAELEZO YA UTANGULIZI YA TUKIO LA PILI NDANI YA JENGO



…………………inaendelea
 
…………….inaendelea

TUKIO LA PILI NDANI YA JENGO LILILOTOKEA NA KUMHUSISHA MHUSIKA

MAELEZO YA UTANGULIZI YA TUKIO LA PILI NDANI YA JENGO


Siku moja kwenye mida kama ya saa 8-9 hivi, mhusika akiwa ofisini kwake aliamua kupandisha ghorofa ya juu ilipo ofisi ya MWI. Alikuwa anaelekea washroom lakini huwa ana kawaida ya kupitia ofisini kwa MWI akiwa anatokea huko kwa ajili ya kuangalia kama kunaweza kukawa na ujumbe mpya kwenye pigeon hole yake

Kabla hajapandisha juu, jirani na ofisi ya mhusika, aliwaacha watu wawili wakiwa kwenye chumba kingine cha maabara ambacho kimetenganishwa na ofisi ya mhusika kwa kutumia partition za vioo kwa juu, halafu chini zikiwa ni mbao. Hivyo mtu akiwa kwenye maabara hiyo, huwa anaweza kumuona mhusika akiwa ofisini kwake, na mhusika pia vile vile huwa ana uwezo wa kuona watu walioko kwenye chumba hicho kilicho jirani na ofisi yake

Kwa hiyo kwenye chumba jirani na ofisi ya mhusika, kulikuwa na watu wawili

  • Mmoja wao watu hawa alikuwa mwanamme mgeni kwa wakati huo, japo aliwahi kuwa mwenyeji ndani ya jengo hilo kwa sababu alikuwa na siku kadhaa (takriban mwaka na ushee) tangu astaafu kama mmoja wa waliokuwa wafanyakazi wa idara hiyo
  • Yaani mtu huyo alikuwa MSTAAFU kutokea idara hiyo isipokuwa siku hiyo alikuwa amekuja kwa kazi maalumu tu ambayo alikuwa ameitwa kuja kuifanya idarani hapo, ndani ya chumba hicho cha maabara kilicho jirani na ofisi ya mhusika
Siku hiyo, ilikuwa ni mara ya kwanza kwa mhusika kumuona mtu huyu idarani hapo, tangu astaafu. Vile vile ilikuwa ni mara ya kwanza kwa mhusika kuonana tena na mtu huyu tangia kipindi alipostaafu na kuondoka kwenye mazingira hayo ya ofisini.

Mtu wa pili aliyekuwa ameambatana na mwanaume huyu mstaafu kwenye chumba hicho, ni mama ambaye kwa sasa ni SENIOR AMBAYE HAJASTAAFU (tumwite MSH), kwa maana kwamba katika wale wote waliopo idarani kwa sasa, hayupo mwanamke ambaye bado hajastaafu, na ambaye ni senior kumzidi mama huyu

Kwa hiyo wakati mhusika anapadisha juu, aliwaacha watu hawa wawili wakiwa chumba hicho jirani na ofisi ya mhusika, wakiwa wanafanya kazi zao humo



MAELEZO MENGINE MAFUPI YA NYONGEZA KUHUSIANA NA HUYU MAMA SENIOR AMBAYE HAJASTAAFU (MSH),

Kabla mhusika hajaendelea mbele, angependa kumrudisha nyuma kidogo msomaji kwenye tukio moja la nyuma kidogo lakini la hivi karibuni, ambalo mama huyu aliwahi kuhusika pia. Hapo awali, mhusika alikuwa ameacha kuliongelea tukio hili kwa makusudi kwa sababu alikuwa amelitunza ili kuja kuliunganisha na hili la zamani ambalo analiongelea hapa muda huu sasa

Ni kwamba kwenye tukio la mwaka jana LILILOHUSIANA NA KIKAO CHA KUMJULISHA MHUISIKA KUWA ATALIPWA MASLAHI YAKE, na ambacho kilimhusisha mwanamme mwingine MSTAAFU kutoka nje ya idara, na ambaye alikuja akiwa ameleta taarifa za malipo hayo, MAMA HUYU (MSH)

  • Ndiye alianza kwa kumpa taarifa mhusika kuwa mstaafu huyo mwenye taarifa njema za “mshiko” angekuja mazingira ya idarani, yaani ofisini, siku moja kabla ya ujio wa mtu huyo
  • Baada ya MSH kumpa mhusika taarifa hizo, kesho yake kweli mstaafu huyu aliwasili idarani hapo
  • Mstaafu huyu alipowasili maeneo ya ofisini siku hiyo, alifikia ofisini kwa MSH kwanza ambayo iko ground floor
  • Baada ya hapo sasa ndiyo Mr X naye tena akafika ofisini kwa mhusika kumjulisha kuwa mstaafu aliyesemekana anakuja kwa ajili ya maongezi yanayohusiana na “mshiko”, ameshawasili maeneo ya ofisini kwa ajili ya maongezi hayo
  • Baada ya hapo mhusika alitoka ofisini na kuelekea kwenye chumba cha mkutano ambacho nacho pia kilikuwa ground floor, ila upande mwingie wa jengo hilo
Mhusika alipoingia ndani ya ukumbi wa mkutano, hakumuona mstaafu aliyetajwa kuwa amekuja isipokuwa baada ya muda kitambo mstaafu huyo aliingia akiwa wameambatana na MSH

  • Ilionyesha kama mstaafu alikuwa anasubiria kuona response ya mhusika kwanza itakuwaje
  • Kwa hiyo ilibidi afikie ofisini kwa MSH kwanza
  • Pengie kama mhusika asinge-respond, possibly hata mstaafu naye angeishia ofisini humo kwa MSH na kurudi kule alikotoka
Zaidi ni kuwa ilikuwa ni mara ya kwanza mhusika kumuona mstaafu huyu akiwa amevaa kofia, na yaliwahi kujiri kwenye kikao hicho tayari mhusika alishayatolea ufafanuzi humu jukwaani

  • Kikao hiki kilifanyika muda ikiwa ni muda mfupi tangu wanafunzi wafunge na kuondoka maeneo hayo ya ofisini
  • Baada ya mkutano huo kuisha, MSH na mstaafu waliendelea kubaki kwa muda ndani ya ukumbi huo wa mkutano, na wengine waliondoka kurudi maofisini mwao akiwemo mhusika mwenyewe
Kwa hiyo huyu mtu aliyekuwa na MSH kipindi kile cha tukio la mwaka 2016 alikuwa ni mstaafu, na huyu wa juzi aliyekuja kwenye kikao kilichohusiana na mambo ya “kuwajaza watu mapesa”, naye pia alikua ni mstaafu, NA WOTE HAWA WAMEKUWA WAKIAIMABATANA NA HUYU MSH





……………….inaendelea
 
TUKIO LA PILI NDANI YA JENGO LILILOTOKEA NA KUMHUSISHA MHUSIKA

MAELEZO YA UTANGULIZI YA TUKIO LA PILI NDANI YA JENGO



…………….inaendelea


Kwa hiyo mhusika alipandisha juu akawaacha watu wawili jirani na chumba chake, MSH pamoja na mgeni mwanamme ambaye alikuwa ni mstaafu. Na wakati huo ilikuwa ni January 2016

Baada ya kuwa ametoka washroom na hatimaye kupitia ofisini kwa Mkuu wa Idara

  • Ndani ya ofisi hiyo aliwakuta watu wawili
  • Mmoja alikuwa Katibu Mhutasi wa MWI wa kipindi hicho
  • Mwingine wa pili alikuwa ni mfanyakazi ambaye kama mhusika kumbukumbu zake hazimtuni vibaya, alikuja akastaafu baadaye mnamo February 2017
  • Baada ya muda siyo mrefu, aliingia tena kijana mgeni, mrefu hivi akiwa ameambatana na msichana
  • Baada ya hao kuwa wameingia, muda mfupi tena aliingia mwenye ofisi, yaani MWI mwenyewe
Kwa hiyo mpaka hapa ndani ya ofisi kukawa na idadi ya watu Sita kwa ujumla, kwamba:

  • Mhusika aliingia kakakuta kuna watu wawili
  • Hatimaye wakaongezeka wageni wawili
  • Na mwisho akaingia MWI mwenyewe
YALIYOJIRI BAADA YA MKUU WA IDARA KUINGIA OFISINI HAPO

Mhusika pamoja na wageni wawili wakati huo walikuwa wamesimama nje ya kaunta ya mapokezi, na hawa wengine watatu walikuwa wapo ndani ya kaunta ya mapokezi ya ofisi hiyo ya MWI. Mhusika alikuta watu wawili ndani ya ofisi hiyo, wakiwa sehemu ya ndani ya kaunta ya mapokezi. MWI naye alipowasili, naye akaingia tena sehemu ya ndani ya kaunta ya mapokezi na alikuwa yuko njiani kuelekea ndani ofisini kwakei

Baada ya MWI kutupa jicho ofisini kwa mgeni aliyekuwa amesimama nje ya kaunta ya mapokezi, akamtambua kuwa ndiye aliyewahi kushambuliwa naye mtu huyo miezi kadhaa iliyopita. Hapo hapo tena mama Katibu Muhtasi wa MWI, naye akaanza kudaa kuwa kijana huyo ni mwanaye wa kumzaa yeye na ambaye amekuja pale kwa ajli ya kumuona yeye ambaye ni mama yake. Kuanzia pale yakazuka sasa mabishano yasiyokuwa na mwisho kwa dakika kadhaa, MWI na katibu Muhtasi wake wanabishana, kila mmoja nakimbishia mwenzake.

  • MWI akiwa anasisitiza m
  • kuuwa mtu aliyewahi kushambuliwa naye ndiyo huyo amemfahamu
  • Katibu Muhtasi naye akiwa anaendelea kushikilia kuwa hawezi kuwa huyo kwa sababu huyo ni mwanae wa kumzaa yeye, na hivyo MWI atakuwa amemfananisha tu
Mabishano haya hayakufikia muafaka, na mwishowe yalikuja kupigiliwa msumari na mtu huyu mwingine aliyekuwemo humo ndani ofisini, huyu aliyekuja kustaafu Febrruari 2017

  • Huyu mwenyewe alisema kuwa kisheria, ni kawaida na inaruhusiwa kwa mtu kumshuku mtu mwingine
  • Baada ya hapo sasa MWI alipata nguvu nyingine mpya tena na kuamua kumchkua mtu huyu ili kumpeleka kituo cha Polisi
  • Hapo hapo akamchagua mhusika waambatane naye kwa kumepleka mtu huyo Polisi
  • MWI hakumchagua yule aliyesema kuwa kumshuku mtu inaruhusiwa kisherai
Baadaye MWI aliondoka na kijana huyo pamoja na mama yake wakaenda kumpandisha kwenye gari la idara lililokuwa tayari lina dereva ndani yake, wakaondoka naye na kumpeleka Polisi. Mhusika hakuweza kufuatana nao kwenye safari hiyo kwa sababu yeye hana mamlaka ya kukamata mtu.

Tangu mhusika kuingia ofisini kwa MWI na matukio haya yote kutokea na hadi kufikia watu hawa kuamua kupelekana Polisi, ilichukua muda wa takribani dakika tano tu hivi na is zaidi ya hapo



Kitu cha muhimu ambacho wasomaji inabdi wakikumbuke hapa ni kuwa MWI huyu alitawala katika kipindi kifupi tu cha miezi kadhaa, (Julai 2015 mpaka February 2016) na baada ya hapo alihamishwa na kupelekwa sehemu nyingine

Baada ya kuwa amehamishwa, Mr X alitengeneza bango na kulibandika nje ya jengo, likionyesha wakuu wa Idara waliowahi kutawala katika vipindi tofauti tofauti, huku bango hilo likimwonyesha MWI huyo kuwa aliwahi kutawala kuanzia Julai 2013 hadi 2016, kama kumbukumbu zake mhusika ziko sahihi, kitu ambacho siyo sahihi

Kitendo hiki kinaonyesha kama ulikuwa ni mkakati wa kujaribu kuleta confusion kwa wasio na taarifa kamili za idara hiyo, kuwa ni MWI yupi alihusika na maswala yaliyokuwa yakiendelea kumpata mhusika katika vipindi tofauti tofauti idarani hapo. Hata hivyo bango hilo lipo ndani ya jengo hadi hii leo



MUBARIKIWE TENA NA BWANA




………………itaendelea
 
Code ya kwanza tata nimeshaitambua ingawa nashindwa kuifungua hapa maana itakuwa name calling...

Mzee umekwepa mishale mingi
 
Code ya kwanza tata nimeshaitambua ingawa nashindwa kuifungua hapa maana itakuwa name calling...

Mzee umekwepa mishale mingi
Mzee unatumia Programming language gani?
Katika mazingira ya namna hii, mishale huwa huikwepi mwenyewe, huwa inakwepeshwa na Mungu kwa sababu yeye ndiyo huwa anakuwa ame-set mazingira hayo ili wewe ukabiliane nayo, na kwa kusudi lake maalum. Matukio haya perce yanaonyesha kuwa Mungu yuko kazini, na huyu mtu, aidha kwa kujua au kutokujua, pasipo shaka yoyote, atakuwa amebebeshwa mission ya Mungu . Kumbuka kuwa baadhi ya matukio yametukia akiwa hana hata ile sense ya kwamba yuko katika mazingira ya hatari, ila akaja akagundua hivyo siku nyingi mbele, matukio hayo yakiwa tayari yalishapita.
 
UPDATE: 01 MARCH 2021

DOKEZO LA ZIADA KUHUSIANA NA “DALILI ZA KUUGUA KICHAA” ALIZOKUWA AKITUHUMIWA MHUSIKA KWA MAANDISHI


Hapa tuchukulie sasa kuwa wewe msomaji wa taarifa hizi:

  • Ni boss uliyekabidhiwa mamlaka makubwa kwenye taasisi kubwa na muhimu sana ya Umma, na yenye wafanyakazi wasiopungua elfu tatu
  • Tuseme kwenye taasisi hiyo alishajitokeza siku nyingi nyuma,kabla hata wewe hujaingia madarakani, mfanyakazi mmoja tu ambaye huwa anadai kuwa ana matatizo ya kiusalama na hivyo anahitaji kukuona ili akueleze matatizo hayo
  • Baada ya hapo, ukaamua ku-delegate kazi hiyo kwa mtu mwingine muhimu ndani ya taasisi yako
  • Baada ya hapo, mtu huyu amewasilisha maelezo yake hayo kwa mtu husika uliyemwelekeza kwake, (na kama ambavyo yamewasilishwa humu jukaani pia), lakin hata baada ya maelezo hayo kuwa yamepokelewa na huyu delegate wako, bado mtu huyu ameendelea kulalamika kuwa hali yake ya ki-usalama ndiyo inazidi kuwa tete zaidi kuzidi hata hapo awali kabla hajawasilisha maelezo yake
  • Yaani hali imekuwa tete zaidi, especially baada ya kuwa mthumiwa wa ukichaa, amewasilisha maelezo hayo kwa mtu ambaye wewe bosi wake uliwahi kumwelekeza
Msomaji, katika mazingira ya namna hii kama yalivyoainishwa kwenye maelezo haya mafupi,

  • Je, huwezi angalau bosi husika ukapata hata nafasi ya siku moja ukamwita mtu huyu na kujaribu kumhoji ili na wewe ujiridhishe kuwa tuhuma anazokabiliwa nazo za kuhusiana na kuugua ugonjwa wa akili, anazo kweli au hana?
  • Unawezaje kukaa muda wote, unamwandikia barua tu za kumtuhumu kuugua ugonjwa wa akili huku ukisambaza nakala kwa wakuu wake wengine wa kazi, na ukiendelea kum-refer kwa mtu yule yule wa mwanzo?
  • Kwa nini angalau kama kweli huna muda wa kumsikiliza, usibadilishe angalau hata huyu mtu wa kumsikiliza, assuming assuming nafasi yako wewe kuonana naye physically haipo?
Kwa mara ya kwanza, mhusika aliwasilisha taarifa zake kama hizi hizi anazozileta humu jukwani, Februari 2016 na kuanzia pale, akawa anatuhumiwa kutaka kuugua ugonjwa wa akili, hadi leo. Mara ya mwisho alipata barua ya kumtuhumu kuwa anaelekea kuwa na matatizo ya akili ilikuwa ni Septemba 2019, na mapka sasa yeye mhusika uelewa wake kuhusu bosi wake huyo ni kulingana na baraua hoyo ya mwisho aliyowahi kuipata kutoka kwa mkuu wake huyo wa kazi

Kwa kifupi ni kuwa mazingira ya usalama wa mhusika, yalianza kuwa mabaya sana na tete zaidi kuliko hata yalivyokuwa hapo awali, muda mfupi tu baada ya kuwa amewasilisha taarifa zake hizo kwa mtu husika ambaye alielekezwa awasilishe taarifa hizo kwake.



MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
TAARIFA MUHIMU YA NYONGEZA KUHUSIANA NA “MUDA WA UTAWALA” WA MKUU WA IDARA (MWI) ALIYEWAHI KUANGUKA KUTOKA GHOROFA YA KWANZA NA KUUMIA KIWIKO CHA MKONO

Ni kwamba huyu mtu alitawala kuanzia Julai 2015 na kuishia Februari 2016, ila baada ya hapo, Mr X alichukua jukumu la kutengeneza bango linaloonyesha kuwa MWI huyo aliwahi kutawala kuanzia “2014 to date” ndivyo bango hilo linavyosomeka mpaka leo hii mwaka 2021.

Utaalamu aliotumia Mr X ni kama ambavyo umefafanuliwa hapa chini.

Ni kwamba bango hilo linaonyesha wakuu wa Idara waliowahi kutawala katika vipindi mbalimbali na tofauti tofauti, ambapo hapa mhusika angependa kuongelea zaidi wale waliowahi kutawala kuanzia 2004 mpaka hiyo “2014 to date” iliyotajwa hapo juu, na kama ambavyo wameonyeshwa kwenye bango hilo

  • Kuna yule ambaye ameonyeshwa kwenye bango hilo kuwa, aliwahi kutawala kuanzia 2004 mpaka 2006, huyo pekee ndiye muda wake uko sahihi kwenye bango hilo, hauna tatizo lolote
  • Mwingine anayefuatia kwenye bango hilo, aliwahi kutawala kuanzia 2006 mpaka Julai 2012, na kwa jumla ya miaka sita. Huyu ndiyo mtu wa kwanza ambaye muda wake hauko sahihi kwa sababu bango hilo linamuonyesha kuwa alitawala kuanzia 2006 mpaka 2010, kitu ambacho siyo sahihi. Bango hilo linaonyesha utawala wa mtu huyu wa pili kwa pungufu ya miaka miwili kamili
  • Anayefuatia tena kwenye bango hilo, aliwahi kutawala kuanzia Julai 2012 mpaka Julai 2015, kwa jumla ya miaka mitatu. Huyu naye muda wake hauko sahihi kwenye bango hilo kwa sababu linamuonyesha kuwa alitawala kuanzia 2010-2014
Na wa mwisho kabisa kwenye bango hilo, ndiyo huyu aliyewahi kuanguka kutoka juu ghorofani aliyetawala kuanzia hiyo Julai 2015 mpaka Februari 2016 na baada ya hapo, ndiyo alifuatia sasa huyu ambaye amekuwa akifanya pilikapilia za kushughulikia maslahi ya malimbikizo ya mhusika kwa njia ambazo mhusika mwenyewe zilimchanganya kidogo hadi ikapelekea taarifa zake azilete humu jukwaani



MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
TUKIO LA TATU LA MHUSIKA: JANUARY 2016:

NDANI YA JENGO LA OFISI

……………….inaendelea


Taarifa hizi ziliwajia wasomaji na kuishia pale ambapo MWI na Katibu Muhtasi (KMH) walishindwa kuafikiana juu ya swala la mgeni aliyekuwa amefika ofisini hapo ambaye MWI aliendelea kumtuhumu kuwa ndiye aliyewahi kumshambulia ndani ya jengo, huku KMH akidai kuwa huyo ni mwanaye wa kumzaa yeye

  • Halii hii ilipelekea kijana huyu kuchukuliwa na watu hawa wawili na kwenda kupandishwa kwenye gari la Idarani akipelekwa Polisi
  • Mhusika naye ilikuwa awe mmoja wao, lakini alikataa kwa sababu yeye hata ile nguvu tu ya kukamata mtuhumiwa huwa hana, achilia mbali mamlaka hayo


MUDA MFUPI BAADA YA TUKIO HILO, KUPITA: MHUSIKA APOKEA BARUA YA KUFUTIWA TUHUMA ZILIZOKUWA ZIKIMKABILI TANGU MWEZI MEI 2014

Tangia mwezi mei 2014, mtuhumiwa alikuwa akikabiliwa na tuhuma za kukaidi maagizo ya kazi ya mwajiri wake, na tuhuma hizi zilidumu hadi Februari 2016. Tuhuma hzi zilisababishwa na mhusika mwenyewe, baada ya kuiandika barua mamlaka ya juu akiIomba aondolewa kwenye kazi za kiofisi zile zinazohitaji mfanyakazi kusafiri nje ya Dar es Salaam na hata nje ya nchi. Barua hii aliiandika March 2013, na hatimaye kuja kukumbushia tena juu ya majibu yake, Novemba 2013 . Hii ilitokana na barua yake ya kwanza kutokuwa imejibiwa hadi muda huo

  • Wakati barua hiyo inafika idarani, ilimkuta MWI aliyewahi kujeruhiwa akiwa bado yupo ofisini
  • Ndiyo barua ya kwanza ambayo iliambatana na kipengele tata kilichotanhibisha wazi kuwa mtizamo wa kule ilikokuwa imetoka, yaani mamlaka za juu, ni kwamba mhusika anaweza kuwa ameanza kuonyesha matatizo ya akili
  • Vile vile, tofauti na ilivyo kawaida kwa barua zingine zote ambazo mhusika huwa anapata, ambazo kawaida zenyewe huwa zinawekwa kwenye pigeon hole yake na hatimaye yeye kuzichukua humo; hii ya kipindi hiki yenyewe aliitwa ofisini kwa MWI na barua hiyo kukabidhiwa na MWI wakiwa wawili ofisini humo
  • Zaidi ni kuwa MWI alimshauri mhusika asikifuatilie kwa kuandika barua, kipengele tata kilichokuwa kimeainishwa kwenye barua hiyo, kilichohusiana na swala la yeye kuanza kuonekana kwa mamlaka za juu kuwa anaweza kuwa hayuko kawaida kiakili
Mda mfupi tu baada ya barua hiyo kuwasili na kukabidhiwa kwa mhusika, hatimaye mhusika alisikia taarifa kuwa MWI huyo amehamishwa na nafasi yake kuanzia pale ilichukuliwa na huyu mwingine ambaye kwa kipindi cha hivi karibuni amekuwa katika pilikapilka za kushughulikia maslahi au malimbikizo ya mhusika kwa namna ambayo ilijaribu kumchanganya mhusika



KILICHOKUWA KIMEJIRI MUDA MFUPI KABLA YA MWI HUYU KUHAMISHWA

Ni kwamba mwezi Septemba 2015, mhusIka akiwa ofisini kwake, alipokea simu kutoka kwa mtu wanayefahamiana, mfanyakazi mwenzake. Hapo awali kwenye maelezo haya ya humu jukwaani, amemuongelea kidogo mtu huyu na kumtaja au kumpa jina kama “SPECIALIST”

  • “SPECIALIST” huyu alimhitaji mhusika afike ofisini kwake ili waweze kufanya mazungumzo
  • Mhusika aliitikia wito huo na alipofika ofisini kwake, “SPECIALIST”alimjulisha mhusika kuwa barua zake zote ambazo huwa anaiandikia mamlaka za juu kuhusiana na matatizo yake aliyonayo, yeye naye (“SPECIALIST”) huwa anapewa kopi zake na kuzisoma
Kwa hiyo “SPECIALIST” huyu alimuomba mhusika kama wanaweza kukaa chini na kuzungumza ili naye (“SPECIALIST”) aweze kujua nini kilichokuwa kikiendelea upande wake mhusika. Mhusika alikubali kufanya mazungumzo hayo ila akatoa maangalizo kadhaa kama ifuatavyo:

Kwamba pengine kwa wakati huo, “SPECIALIST” huyo asingeweza kuyatatua kwa usahihi matatizo yaliyokuwa yakimkabili mhusika hata kama mhusika atampa maelezo ya kina “SPECIALIST” huyo kwa sababu

  • Mpaka muda huo, ndani ya faili lake, mhusika alikuwa ana barua za tuhuma kutoka ngazi za juu zinazomtuhumu kukaidi maagizo ya kazi ya wakuu wake wa kazi
  • Vile vile, mpaka muda huo, mamlaka za juu zilikuwa hazijawahi kumsikiliza matatizo yake pamoja na kuwa amekuwa akiziandikia barua mara kadhaa akiziomba zifanye hivyo.
  • Badala ya mamlaka za juu kumsikiliza, ziliamua kumuandikia barua ya kumtuhumu, kitu ambacho kimepelekea tuhuma hizo kuwepo ndani ya faili lake mpaka muda huo (muda alipokuwa akifanya maongezi hayo na “SPECIALIST)
Baada ya mhusika kuwa ameainisha mambo haya yote, alimalizia kwa kumuomba “SPECIALIST wasifanye naye mazungumzo kwanza kwa muda huo, na badala yake “SPECIALIST” aijulishe mamlaka ya juu kwamba mhusika anaomba sana kuonana na kuongea na mamlaka hiyo kabla ya mtu mwingine yeyote.

Zaidi mhusika alimuuliza “SPECIALIST” swali kuwa japo amepewa mandate na mamlaka za juu kumsikiliza mhusika, je atawezaje kuya-resolve matatizo ya mhusika katika kipindi hiki ambacho mhusika bado ana tuhuma ndani ya faili lake, mamlaka hizo hizo zikiwa zimemtuhumu?

Hadi kufikia hapa “SPECIALIST” aliona haja ya kusitisha kwanza maongezi na mteja wake kwa sababu ilikuwa obvious kwamba tuhuma zilizokuwa zinamkabili mhuska, zilihitaji lazima mamlaka ya juu izishugulikie kwanza na siyo yeye “SPECIALIST”

Kwa hiyo kwa awamu ya kwanza, mhusika na “SPECIALIST” waliishia hapa

Baada ya hapo, ndiyo sasa ikaja ile barua ya mwezi Februari 2016, iliyokuwa ikifuta tuhuma za mhusika na ikiwa ina kipengele kilichokuwa kinamwelekeza (haukuwa ushauri, yalikuwa maelekezo) mhusika kwenda kumuona tena “SPECIALIST” na huu ndiyo ukawa mwanzo wa mhusika kutoa taarifa zake zote alizokuwa nazo kwa mtu huyu “SPECIALIST” na ambazo mwanzoni, alihitaji kuzitoa kwa mamlaka za juu

Kwa hiyo kuanzia Februari 2016 mhusika akaanza kufanya mazungumzo na “SPECIALIST” na mara ya mwisho wawili hawa walikuatana na kuongea, ilikuwa mwezi Septemba 2016 baada ya tukio lile la tetemeko la Kagera. Sessions zote za mazungumzo haya zilikuwa zikifanyikiaofisini kwa “SPECIALIST”

Hata hivyo wakati wanaanza kufanya mazungumzo hayo hiyo Februari 2016, MWI aliyewahi kuanguka kutoka juu ghorofani akawa tayari ameshahamishwa na akaingia huyu mwingine ambaye taarifa zake zimekuwa humu jukwani tangu mwanzo



…………inaendelea

UP NEXT………
KWA KIFUPI SANA: RATIBA YA MATUKIO KAMA AMBAVYO IMEKUWA IKIJIONYESHA KUHUSIANA NA MATUKIO AMBAYO AMEKUWA AKIKUMBANA NAYO MHUSIKA
 
…………inaendelea

MHUSIKA NA “SPECIALIST”:

MHUSIKA ARUDI TENA OFISINI KWA “SPECIALIST” KWA AJILI YA KUMSHUKURU


Siku kadhaa baada ya mhusika na “SPECIALIST” kuhitimisha mazungumzo yao, lakini hali ya kiusalama ya mhusika ikiendelea kuwa tete siku hadi siku:

  • Mhusika alirudi tena ofisini kwa “SPECIALIST” kumshukuru kwa ajili ya mazungumzo waliyowahi kufanya huko nyuma
  • Hadi muda huo, ulikuwa tayari umeshapita mwaka mmoja na ushee, au hata miwili
Hapo kabla, mara tu baada ya kuwa wamehitimisha mazungumzo yao, mhusika alikuwa anaogopa kuonekana akiwa katika mazingira ya pamoja tena na “SPECIALIST” kwa kuhofia kuwa angeonekana kama anafanya lobbying ya taarifa alizowahi kumpatia “SPECIALIST”, zifanyiwe kazi zikiwa zinapendelea upande wake yeye mhusika. Kwa hiyo ilibidi mhusika asubirie mpaka muda mrefu wa kutosha ulivyopita, ndiyo akarudi tena ofisini kwa “SPECIALIST”, kwa ajili ya kumshukuru

Kwa hali hiyo basi, matukio yote ambayo mhusika amekuwa akiyaeleza humu ambayo yaliwahi kumkumba akiwa ndani na hata nje ya nchi, ukianzia kabisa na lile la MR Y (safari ya kikazi kuelekea mikoa ya kusini, safari iliyowahi kuyeyuka ghafla na akashindwa kwenda, mnamo August 2008); taarifa za matukio yote haya aliwahi kuziwasilisha kwa “SPECIALIST” ili zifanyiwe kazi



MUBARIKIWE TENA NA BWANA



UP NEXT………

RATIBA TA MATUKIO AMBAYO MHUSIKA AMEKUWA AKIKUMBANA NAYO KWA UFUPI:

KWA KIFUPI SANA
 
Nini hiki jamani au mm ndo sielewi?
Ni msomaji wa uzi huu siku zote au ndiyo umeanza leo? Kama umeanza leo, itakuchukua muda mrefu kuelewa maudhui ya uzi huu. Nakushauri bora uachane nao uwaachie wale ambao tu unawahusu
 
Ni msomaji wa uzi huu siku zote au ndiyo umeanza leo? Kama umeanza leo, itakuchukua muda mrefu kuelewa maudhui ya uzi huu. Nakushauri bora uachane nao uwaachie wale ambao tu unawahusu
Sawa baba
 
KWA KIFUPI SANA: RATIBA YA MATUKIO KAMA AMBAVYO IMEKUWA IKIJIONYESHA KUHUSIANA NA MATUKIO AMBAYO AMEKUWA AKIKUMBANA NAYO MHUSIKA

Orodha ya safari hizi, si safari zote ambazo mhusika alishawahi kuzifanya isipokuwa ni baadhi tu ya zile ambazo aliwahi kuzifanya na hatimaye kuona kitu kisichokuwa cha kawaida kwenye safari hizo

Kitu cha pekee ambacho msomaji ataweza kukiona hapa ni kuwa


  • Kipindi kabla mhusika hajasitisha safari za nje ya Dar es salaam, mtu huyu hakuwahi kutokewa na tukio lolote lile akiwa ndani ya jengo ilimo ofisi yake
  • Kwa hali hiyo basi, matukio yote yaliyowahi kumtokea mhusika akiwa ndani ya jengo, yalianza kutokea tu baada ya kuwa amesitisha kufanya safari za nje ya Dar es salaam
Hii inamanisha kuwa kipindi mhusika akiwa bado anafanya safari za nje ya Dar es salaam kama kawaida, HAKUWAHI KUSHUHUDIA HATA TUKIO MOJA TU, LLILILOJITOKEZA KWAKE AKIWA NDANI YA JENGO



MLOLONGO WA MATUKIO YENYEWE KWA KUFATANA MUDA YALIPOJITOKEZA

July 2008 na August 2008
: Safari mbili za kikazi kwenye mikoa ya Arusha, Manyara, Dodoma na Singida


  • Hakuwa peke yake, alikuwa na wenzake wawili
  • Safari hizi hajawahi kuzitolea maelezo yake humu lakini nazo pia zinaangukia kwenye kundi hili la matukio yasiyo ya kawaida aliyowahi kukumbana nayo akiwa yupo safarini
August 2008: Safari ya kikazi kusini; ambayo hakufanikiwa kwenda, iliyeyuka ghafla



Novemba 2010: Safari ya binafsi ya Sumbawanga akiwa likizo. Alirudia njiani akiwa amefika Tunduma



August 2012: Safari ya kikazi kwenye mikoa ya Arusha, Manyara, Dodoma na Singida


  • Ni safari ya mwisho aliyowahi kufanya
  • Safari hii ilifuatiwa na nyingine mwezi Novemba 2012; safari ambayo ilikuwa asafiri kikazi kwenda nje ya nchi lakini hakufanikiwa
Baada ya hapo, ilipofika mwezi March 2013 mhusika aliandika barua kazini ya kuomba kuruhusiwa kutosafiri kikazi, ndani na nje ya nchi. Hata hivyo matukio hayakuishia hapo



BAADA YA KUACHA KUSAFIRI, MATUKIO YAANZA KUMSAKAMA NDANI YA JENGO AKIWA OFISINI

Baadhi ya matukio haya ni kama vile


  • Lile lililomhusiha MWI aliyeruka ghorofani (Septemba/ Oktoba 20115) la January 2016
  • Tukio la Septemba 2016 baada ya tetemeko la Kagera. Tukio hili lilimhusisha SENIOR MSTAAFU WA KIUME na mtu mwingine mgeni kutoka nje ya Idara. Tukio hili hajwahi kuliongelea humu na ataliongelea kama TUKIO LA NNE kwenye mlolongo wa matukio anayoendelea kuyaongelea kipindi hiki
  • Tukio jingine lililowahi kumhusisha MAMA SENIRO MSTAAFU, mwaka 2017. Tukio hili alishawahi kuliongelea. Ni lile ambalo liliwahi kuhusisha hadi baadhi ya wafanyakazi wa Benki A


UP NEXT:

Tukio la Septemba 2016 lililotokea baada ya tetemeko la Kagera na kumhusisha SENIOR MSTAAFU WA KIUME na mtu mwingine mgeni mwenye uhusiano naye na ambaye alikuwa ametoka nje ya Idara.
 
Back
Top Bottom