#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

Ila mhusika huwa ni mtiifu sana linapokuja swala la kanisani,
Kila wito ukitolewa ye huwa anautii

Kidogo kazini huwa ni mbishi...
Hata kazini nako vile vile siyo mbishi. Wewe unawezaje kuamriwa na bosi wako umpeleke mtu Polisi wakati wewe ni raia, si askari; na wale waliokuwa wakimpeleka na wenyewe nao hawakuwa Polisi? Wewe uliye raia unaweza kukamata mtuhumiwa kumpeleka Polisi na wakati huo huo ukiwa huna hata ule uhakika kama kweli ni mtuhumiwa?
 
Hata kazini nako vile vile siyo mbishi. Wewe unawezaje kuamriwa na bosi wako umpeleke mtu Polisi wakati wewe ni raia, si askari; na wale waliokuwa wakimpeleka na wenyewe nao hawakuwa Polisi? Wewe uliye raia unaweza kukamata mtuhumiwa kumpeleka Polisi na wakati huo huo ukiwa huna hata ule uhakika kama kweli ni mtuhumiwa?
Hapana mhusika kazini ni mbishi,
Asingekuwa mbishi angetii maagizo ya kumpeleka mtuhumiwa Polisi, maana hakupewa jukumu hilo peke yake,
Kumbuka ubishi huu huu ndio ulipelekea mhusika hata whatsapp akaacha kutumia wakati inarahisisha mawasiliano na wafanya kazi wenzie hali inayopelekea yeye kuchelewa kupata taarifa muhimu, au kutopata taarifa hizo kabisa!

Mhusika huwa ni mtiifu sana kanisani !
Ingekuwa maagizo hayo hayo ya kumpeleka mtu polisi yametokewa kanisani basi naona kama mhusika angetii agizo hili bila shida[emoji28][emoji28]

Pia mhusika character yake ni mtu mpenda haki, ye hupenda vitu vyote vifanyike kwa ukamilifu na kufuata utaratibu na mtitiriko pasipo kupindisha pindisha, hali hii mwanzoni ilinifanya nimuone mhusika kama mtu mkorofi ila kadri nilivyozidi kumsoma nikaona kuwa yeye sio mkorofi bali ni mpenda haki!!
 
Kumbuka ubishi huu huu ndio ulipelekea mhusika hata whatsapp akaacha kutumia wakati inarahisisha mawasiliano na wafanya kazi wenzie hali inayopelekea yeye kuchelewa kupata taarifa muhimu, au kutopata taarifa hizo kabisa!
Msomaji mzuri ila kuna baadhi ya mambo unachanganya sana. Mhusika aliacha kutumia Whatsup tangu mwaka 2014 wakati hilo tukio lilitokea mwaka 2016 mwanzoni, miaka miwili mbele.

By the way, huyo aliyekuwa anasemekana kuwa ni mtuhumiwa wala hakuwa mtuhumiwa, yalikuwa ni maigizo yaliyokuwa yamelenga kumdhuru mhusika. Dhana aliyonayo mhusika mpaka mtu huu ni kwamba alikuwa ni mtu aliyekuwa amekuja akiwa na silaha kwa ajli ya kumdhuru mhusika na kitendo hicho angekitimiza wakati wakiwa kwenye gari. Mhusika angekaa nyuma kwenye gari na mtuhumiwa, halafu wengine ilikuwa wakae mbele. Nyuma ya gari ilikuwa ni bangallow, yaani hollow, yenye viti vya pembeni kama ambulance!
 
Msomaji mzuri ila kuna baadhi ya mambo unachanganya sana. Mhusika aliacha kutumia Whatsup tangu mwaka 2014 wakati hilo tukio lilitokea mwaka 2016 mwanzoni, miaka miwili mbele.

By the way, huyo aliyekuwa anasemekana kuwa ni mtuhumiwa wala hakuwa mtuhumiwa, yalikuwa ni maigizo yaliyokuwa yamelenga kumdhuru mhusika. Dhana aliyonayo mhusika mpaka mtu huu ni kwamba alikuwa ni mtu aliyekuwa amekuja akiwa na silaha kwa ajli ya kumdhuru mhusika na kitendo hicho angekitimiza wakati wakiwa kwenye gari. Mhusika angekaa nyuma kwenye gari na mtuhumiwa, halafu wengine ilikuwa wakae mbele. Nyuma ya gari ilikuwa ni bangallow, yaani hollow, yenye viti vya pembeni kama ambulance!
Huenda kweli nachanganya huu uzi ni mrefu mnoo kiasi kukumbuka matukio yote kwa ukamilifu sio rahisi

Sasa kesi iliishaje? Au hata polisi hawakufika baada ya mhusika
 
Huenda kweli nachanganya huu uzi ni mrefu mnoo kiasi kukumbuka matukio yote kwa ukamilifu sio rahisi

Sasa kesi iliishaje? Au hata polisi hawakufika baada ya mhusika
Wangeenda Polisi kuna uwezekano wangeweza kwenda kuzalisha kesi nyingine ya pili.. Wala hawakuwa na mpango huo
 
UPDATE:WEDNESDAY; 6th JANUARY 2021

“RARE COINCIDENCE” NYINGINE AMBAYO INAWEZA KUWA IMETOKEA “KANISA A”


Msomaji inabidi azingatie kwa umakini kidogo maelezo ya mhusika kwenye taarifa hii kwamba, coincidence hii:

  • inaweza kuwa imetokea au haijatokea
  • uwepo wake unategemea kile ambacho kinaweza kuwa kimetokea katika uhalisia (if A then B, if not A then not B)


UTANGULIZI


Kuna kipindi kwenye maelezo yake ya nyuma, mhusika aliwahi kugusia swala la kipindi cha Ibada ya maombezi kuvamiwa na watu kutoka nje ya Kanisa A, na ambao walidhihirika kutokuwa na nia njema na kipindi hicho

  • Hiki ni kipindi ambacho huwa kinakuwepo kila Jumapili mara baada ya Ibada ya pili
  • Kawaida huwa kinaanza kwenye mida ya baada ya saa 7, ila kwa mara nyingi kuanza kwake hutegemea sana muda ambao Ibada ya pili ilimalizika
  • Washiriki wake walio wengi, ni waumini ambao huwa wamekuwepo na ambao huwa wameshiriki kwenye Ibada ya pili
Nadhani ilikuwa mwaka 2011 na 2012, ambapo kipindi hiki kilikuwa kinafanyikia kwenye la jengo la ghorofa, na kilikuwa kinafanyikia kwenye ghorofa ya kwanza ya jengio hilo lililo ndani ya uzio wa Kanisa A

  • Baadaye kipindi hicho kilihamishwa na kuwa kinafanyikia kwenye banda ambalo ni Kanisa kwa ajili ya Ibada ya watoto wadogo kabisa wale wa rika la mwanzo kanisani hapo
  • Banda hili ndiyo lile ambalo mhusika hivi karibuni alililamika kuwa linawekewa makreti ya soda pembezoni kwa ajili ya watoto kukanyaga juu yake, kukwepa kukanyaga maji ya mvua ambayo huwa yanajitenga pembezoni mwa banda hilo
  • Baada ya Ibada ya maombezi kuhamishiwa kwenye nyumba hiyo ya Ibada ya watoto wadogo, mamluki wa kuvamia Ibada hii ya maombezi, walianza kuonekana kwenye Ibada hiyo
Ni kwa sababu banda hilo liko karibu na geti la kuingilia Kanisani hapo hivyo ilikuwa ni rahisi zaidi kwa wao kuingia haraka haraka ndani na kujiunga na watu waliokuwa wanakuwa kwenye Ibada hiyo ya maombezi

  • Kule ghrorofani ambako Ibada hiyo mwanzoni ilikuwa inafanyikia, haikuwa rahisi sana kwa wavamizi hawa kufika sehemu hiyo. Ingekuwa rahisi sana kwa wao kustukiwa kwa sababu walikuwa wanakuja kutokea nje, wakati maombezi hayo washiriki wake wote huwa ni watu ambao wengi wao ni wale ambao wanakuwa wamehudhuria Ibada ya pili
  • Na kwa sababu ghorofa liko umbali wa kutosha kutoka getini, haikuwa rahisi kwa mtu mgeni na mwenye sura ngeni, kutembea kote kutoka getini hadi lilipo ghorofa hilo, na hatimaye kupandisha juu ghorofani kujiunga na maombi hayo
Ni katika wakati huu tu ambapo kipindi hiki kilihamia karibu na getini, ndiyo watu hawa nao walianza kuonekana kwenye Ibada hiyo

Kwenye mojawapo ya pilika pilika zao wavamizi hawa wa Ibada, kuna siku walionekana kuwasili wakiwa wamekodi tax, na mhusika kubahatika kuwaona kwa macho yake wakipokelewa na binti mmoja mwenyeji wa kanisani hapo, ambaye pia ni mmojawapo wa washiriki mahiri wa Ibada ya Kusifu na Kuabudu Kanisani hapo



MAELEZO YA TUKIO LENYEWE

Binti huyu ambaye ametajwa hapo juu, ni mshiriki mzuri sana na pia kiongozi mzuri sana wa Ibada ya kusifu na kuabudu na ni mara chache sana kwake kutokuonekana Kanisani. Hata hivyo kuna kipindi fulani aliwahi kupotea madhabahuni kwa muga mrefuu kiasi, na kwa sababu ambazo ni za msingi sana, na ambazo mhusika asingependa kuziongelea hapa

  • Baada ya kuwa amepotea kwa kipindi kirefu, hatimaye alirudi tena na akaendelea kushiriki kama kawaida
  • Hata hivyo, safari hii alirudi akawa mara zote anaimba kama mshiriki tu wa kikundi hicho, yaani mwimbaji wa kawaida na si kama kiongozi mwimbishaji
  • Baada ya binti huyu kuwa amerudi tena, kama kuna Ibada ya kusifu na kuabudu ambayo aliwahi kuiongoza kwa kuimbisha, basi atakuwa alifanya hivyo kwa kipande tu huku akishirikiana na mtu mwingine, ila si kwa Ibada nzima
Hata hivyo, hatimaye ilitokea Jumapili ya tarehe 26 Julai 2020 ambapo alibahatika kuongoza Ibada nzima ya kusifu na kuabdudu, mwenyewe peke yake, huku wenzake wote kwenye kundi hilo wakiwa ni waitikiaji tu

  • Tangia aache kuongoza Ibada hiyo, hadi Jumapili ya hiyo ya tarehe 26 Julai 2020, alikuwa amepitisha takribani mwaka mzima
  • Hii ni kutokana na ukweli kuwa hapo kabla, alikuwa pia ameacha kuonekana madhabahuni kwa udhuru uliotokana na sababu za msingi


HITIMISHO

Hata hivyo, tangu Jumapili hiyo tajwa, hajawahi tena kuongoza (kuimbisha) Ibada nzima ya kusifu na kuabudu yeye mwenyewe peke yake na kama amewahi, basi itakuwa ni katika mojawapo ya Jumapili zipatazo tatu zilizotokea mbele ya mwezi huo wa Julai 2020 ambazo mhuiska hakubatika kuwepo kwenye Ibada za Jumapili hizo

  • Hii inamanisha kuwa hadi leo hii January 2021, mhusika hajawahi kumuona tena binti huyu akiongoza Ibada hiyo kama alivyoongoza kwa mara ya mwisho tarehe 26 Julai 2020
  • Kipindi hiki urefu wake unaeleleka miezi sita sasa, au nusu mwaka
  • Vile vile, kabla ya tarehe hiyo tajwa, alikuwa pia amepitisha takriban mwaka mzima bila kuongoza Ibada hiyo
  • Kwa hiyo rekodi aliyonayo mhuiska kuhusiana na binti huyu hadi siku ya leo, inaonyesha kama tarehe 26 Julai 2020 aliongoza Ibada yote ya kusifu na kuabudu yeye peke yake bila kushirikiana na mtu mwingine, kwa mara ya mwisho
Wasomaji wa siku zote wa uzi huu watakumbuka kuwa tarehe hiyo tajwa ndiyo siku ambayo usiku wake mdogo wake na mhusika alipoteza maisha kule nyumbani kwao Mwanza

Unless binti huyu amewahi kuongoza Ibada zingine katika mojawapo ya Jumapili hizo tatu alizozitaja hapo juu, ambazo mhusika hakuwahi kuzishirirki; ila kama sivyo, kwamba hata Ibada hizo binti huyu hakubahatika kuwa kiongozi wake, basi tukio la binti huyu kusimama madhabahuni siku pekee ambayo mdogo wake na mhusika alipoteza maisha, ilhali hakuwa amefanya hivyo kabla ya siku hiyo kipindi kirefu nyuma, na hajawahi tena kufanya hivyo baada ya siku hiyo kipindi kirefu mbele, linaweza kumpelekea mtu yeyote yule mwenye akili timamu kuliita kama RARE COINCIDENCE

Hata hivyo, tukio hili haliwezi kuwa rare coincidence kama binti huyu amewahi kuongoza Ibada zingine kwenye Jumapili hizi tatu zilizojitokeza mbele ya Julai 2020 ambazo mhusika hakubatika kuwepo kwenye Ibada hizo

Siku hiyo pia alihudumu mtumishi wa Mungu kutoka nje ya nyumba ya Ibada ya Kanisa A, na mahubiri yake yalijikita zaidi kwenye utoaji, hali ambayo imepelekea mhusika kwa sasa, kulega lega zaidi kwenye swala la utaoji. Ni kwamba alikuwa tayari ameshalegea, ila kuanzia siku hiyo alilegea zaidi


elly obedy
MUBARIKIWE TENA NA BWANA
Baadhi ta scerios ambazo zimeelezewa katika tukio hili, zimeshajirudia tayari
Post #317
 
SIFA ZA J2 AMBAZO HUWA ZINAONYESHA VIASHIRIA KUWA HUKO MBELE KUTAKUWA NA TUKIO LISILO JEMA

Mara nyingi
(si mara zote, tuchukulie labda kama asilimia 90% hivi) huwa ni J2 ambazo:
  • wiki hiyo ndani ya siku za wiki, kulikuwa na maombi ya angalau siku 2 au zaidi au hata wiki nzima
  • wiki hiyo ndani ya siku za wiki, kulikuwa na kundi maalum la watu Kanisani kwa kazi maalum, na baada ya hapo kukafuatia na semina ya angalau siku tatu
  • Wiki hiyo ndani ya siku za wiki, kulikuwa na maombi ya siku 2 pamoja na Semina ya siku tatu (3)
  • Kulikuwa na mtumishi mgeni kutika nje ya Kanisa
Hii huwa inafanyika hivi kwa lengo moja tu la kuwaepusha maveterani (akiwemo Kiongozi Mkuu, na maswali ya wao kujibu iwapo kama J3 inaayofuatana na J2 husika, kunaweza kukawa na tukio la ajabu

Maelezo ya nyongeza zaidi yako hapa:

Post #187

 
UPDATE: MONDAY 22 MARCH 2021

SHAMBULIO JINGINE LA KOO ALILOLIBAINI ASUBUHI YA SIKU YA JUMAMOSI YA TAREHE 20.03.2021 LILILOTOKANA NA MAJI ALIYOTUMIA ASUBUHI WAKATI AKIPIGA MSWAKI


Shambulio hili alilibaini siku ya Jumamosi lakini maandalizi yake yalifanyika siku ya Ijumaa akiwa ofisini
  • SAFARI HII, MR X ANAONEKANA KUTOKUHUSIKA WENYE TUKIO HILI
  • Hakuna ushahidi wowote au dalili zozote zinazoashiria kuhusika kwake, isipokuwa ossibly kuna mtu mwingine ambaye ameshajitokeza na ambaye alikuwa anataka ku-take advantage ya kumchafua tena MR X kwa kitu ambacho hajafanya
  • Chances kubwa ni kwamba shambulio hli lilikuwa launched wakati wa jioni kipindi mhusika alipokuwa anatoka nje ya jengo kwenye lango kuu la gate la ofisini, kuelekea nyumbani
  • Hata hivyo “main ingredient” ya shamabulio hilo inaonekana kuwa ni maji aliyotumia asubuhi ya siku hiyo alipomaliza kupiga mswaki
  • Kwa hiyo kwa kipindi kingine chote alipokuwa yupo ofisini siku hiyo, hapakuwa na chochote cha ajabu, isipokuwa wakati anatoka nje pale getini kwenye lango la jengo ndipo pale shambulizi linapoweza kuwa liltokea
  • Hata hivyo ni shambulio la pekee ambalo mhusika amelipata na ambalo linaonekana kama kutomhusisha kabisa MR X
  • KWA HIYO KWA SAFARI HII, MR X ANAWEZA KUWA HAHUSIKI KABISA NA SAMBULIO HII

Vilivyohusika ni maji aliyotumia mhusika kusukutua mdomoni wakati wa asubuhi siku ya Ijumaa, baada ya kuwa amepiga mswaki, ukiunganisha na mtu mwingine mtaalamu aliyekuwa maeneo ya ofisini, ambaye kwa sasa mhusika bado hajamfahamu vizuri mtu huyu. Aliyehusika moja kwa moja ni mtu mmoja au wawili na si zaidi ya hapo

MAELEZO YA NYONGEZA JKUHUSIANA NA SHAMBULIO HILI

Shambulio hili safari hii linaonekana kuhusisha MAJI ALIYOTUMIA MUSIKA KUSUKUTUA MDOMONI BAADA YA KUWA AMEPIGA MSWAKI SIKU HIYO YA IJUMAA

MAELEZO YA ZIADA KUHUSIANA NA MAJI HAYO ALIYOTUMIA MHUSIKA SIKU YA IJUMAA ASUBUHI


Ikumbukwe kuwa nyumbani kwa mhusika hapana maji tangu Novemba 2018. Kwa hiyo mara zote mhusika huwa anachota maji kutoka kwenye bomba lililoko nje, ambalo hata majirani zake wengine nao wakati mwingine nao pia huwa wanalitumia

Hata hivyo, kuna siku moja usiku mhusika alisikia bomba hili likiwa limefunguliwa na linamwaga maji kwa nguvu kubwa sana pale nje, akaamua kwenda kulifunga.
  • Muda huo ulikuwa ni majira kama ya baada ya saa tatu za usiku
  • Pale nje hapakuwa na mtu yeyote isipokuwa baada ya kufunga bomba, mhusika alimuona mlinzi naye anaingia pale nyumbani kwa ajili ya kazi zake
  • Baada ya kurudi ndani, mhusika akapata wazo la kuchota angalau maji kidogo kwa ajlil ya usafi wa asubuhi
  • Kwa usafi wa kinywa pamoja na kunywa, mhusika amekuwa siku zote na kawaida ya kuchota maji kutokea bombani moja kwa moja
  • Kuna njia mbili za kuchota naji hayo, moja ikiwa ni kwa kutumia mpira mrefu ambao hufungwa kwenye koki ya bomba, na nyingine ya kuchota moja kwa moja kutokea kwenye koki ya bomba hilo
SABABU ZILIZOPELEKEA ACHOTE MAJI HAYO USIKU HUO

Kwa siku za hivi karibuni
, maji ambayo huwa anatumia kwa matumizi mengine kama kuoga, mara nyingi, kwa kipindi cha hivi karibuni, amekuwa akiyapndisha juu kwa kutumia mpira
  • Hata hivyo, yale ya kunywa pamoja na usafi wa asubuhi huwa anayachota moja kwa moja bombani pasipo kutumia mpira
  • Ni kwa sababu mpira huo wakati mwingine huwa unatumika na akina mama wanaofua nguo na unakuwa siyo msafi
  • Mdomo wa mpira huo wakati mwingine huwa unalowekwa kwenye nguo chafu zinazofuliwa na hivyo mtu hawezi kuchota maji ya kunywa kwa kutumia mpira huo
Kwa hiyo hizi ndiyo sababu zilizomfanya mhusika achote maji hayo ya usafi wakati huo wa usiku

Siku hiyo, mhusika alichota maji hayo na kuyaingiza ndani nyumbani kwake na akayaweka juu ya mojawapo ya madumu yake mengine ya kuhifadhia maji yaliyoko sebuleni kwake, madumu hayo yakiwa hayako mbal sana kutoka mlango wa kuingilia ndani nyumbani kwa mhusika
  • Baada ya mhusika kuwa amechota maji hayo, yaliendelea kukaa pale pasipo kuwa ameanza kuyatumia, kwa zaidi ya wiki moja au mbili
  • Ni kwa sababu kule bafuni alikuwa bado anayo maji kwa ajili ya usafi huo
  • Hadi kufikia Alhamis tarehe 18/03/2021 maji aliyokuwa mhusika anatumia awali yakawa yameisha, na hivyo akalazimika sasa kuyachukua haya mengine yaliyokuwa sebuleni ( aliyowahi kuyachota usiku siku kadhaa nyuma) na kuyapeleka bafuni, ila siku hiyo nayo pia hakuyatmia maji hayo, alikuwa bado anamalizia yale ya mwanzo
  • Kwa hiyo ilipofika Ijumaa ya tarehe 19/03/2021 alilazimika kutumia sasa haya maji mapya ambayo aliyaingiza bafuni siku ya Alhamis, ambayo yamekuwa sebuleni kwa zaidi ya wiki moja au mbili hivi
CHA PEKEE ALICHOKIONA MHUISIKA MAZINGIRA YA OFISINI KWA SIKU ZA ALHMAIS NA IJUMAA

Katika siku zote hizo mbili, mara zote amekuwa akitoka ofisini na kukuta kundi la watu wakiwa mesimama nje ya gate la lango la jengo, kama vile wanasubiria mtu fulani. Watu hao wamekuwa wakibadilikabadilika kwa siku hizo mbili isipokuwa wawili wao ndiyo walikuwa ni wale wale kwa siku zote mbili.
  • Mmojawapo wa wawili hao ni staff msimamizi wa ukarabati unaoendelea kwenye jengo hilo na ambaye taarifa zake ziliwahi kuwajia humu wakati ukarabati huo ulipokuwa unaanza
  • Wa pill ni yule fundi anayehusika na ukarabati huo, ambaye mwanzoni, naye pia taarifa zake ziliwahi kuwajia humu jukwaani wakati ukarabati huo ulipokuwa unaanza
Ukarabati huo bado upo unaendelea mpaka leo

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE: TUESDAY 23 MARCH 2021

PONGEZI NYINGI SANA KWA KIONGOZI MKUU KANISA A KWA FUNDISHO FUPI LA JANA JUMAPILI YA TAREHE 22 MARCH 2021


Jumapili ya tarehe 22/03/2021 KM-A alifundisha somo kwa kifupi sana, lakini vizuri muno, na sijui kama yeye aligundua hilo

Kikubwa sana alichoongea ni kwamba, wale wote waliomkabidhi Yesu maisha yao kuwa Bwana na Mwokozi wao, wanao uwezo wa kuwaombea wengine pia ambao hawamjui, na kupelekea roho za watu hao kupokea uzima wa milele, yaani hata wale ambao hawamjui Yesu kabisa. Wanachotakiwa kufanya cha kwanza kabisa ni kuwaombea rehema ndugu zao, au jamaa zao, au wazazi kwa sababu binadamu wote tu wakosaji, hakuna aliye mkamilifu. Baada ya hapo wanatakiwa sasa kufanya kazi ya kuzikabidhi roho zao hao wanaowaombea, kwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo na hiki kitu inabidi kifanyike kipindi cha uhai wao, yaani muda kabla hawajatwaliwa na Bwana

Kwa hiyo mtu ukimuombea rehema halafu tena ukaikabidhi roho yake kwa Bwana Yesu, roho hiyo inapata uzima wa milele, ijapokuwa unaweza ukaja hatimaye kumpoteza kimwili, lakini kiroho uatakuwa umemponya, anakuwa amepokelewa na Bwana Yesu na kuwa mrithi wa uzima wa milele

Neno hili la KM-A lilifanyika faraja sana kwa mhusika J2 ya jana. Ni kwa sababu yeye amekuwa na tatizo kubwa tangu siku nyingi nyuma, kwamba kuna baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki zake anaowapenda lakini hawamjui kabisa Yesu. Sasa alikuwa anakaa anajiuliza maswali, kwamba je, hakuna namna ambayo yule anayemjua Yesu anaweza akafanyika njia na kupelekea uponyaji kwa mtu mwingine yule ambaye hamjui kabisa Yesu, na pasipo mtu huyo (mpokea uponyaji) kuwa amesikia habari za Yesu? Kwamba je mtu mwingine hawezi kupokea uponyaji wa damu ya Yesu pasipo kuwa ameshiriki wala kuujua mchakato wa uponyaji huo?

Maana sasa alikuwa anaona kumjua Yesu kunakuwa na mipaka na yenye manufaa zaidi kwa yule tu aliyempokea na si kwa wengine ambao hawajawahi kumpokea na possibly wala kumjua kuwa Yesu yupo

Mhusika aliyapenda muno maneno machache yaliyotolewa na KM-A kwenye Ibada ya J2 jana, na anampongeza sana KM kwa fundisho hilo, Mungu azidi kumbariki sana

Mhusika anashauri kama KM anaweza akapata tena muda wa kulirudia somo hilo kwenye J2 moja nyingine huko mbele, iatependeza sana

KWA HIYO, YESU NI WETU SOTE, TUNAOMJUA NA WASIOMJUA PIA. WASIOMJUA WANAO UWEZO WA KUPOKEA UPONYAJI WA KIROHO KUPITIA KWAKO WEWE UNAYEMJUA

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE: FRIDAY 26 MARCH 2021

UHUSIANO WA MAKINIKIA NA TETEMEKO LA KAGERA LA SEPTEMBA 2016

  • Makinikia ulikuwa ni mpango uliobuniwa ili ku-divert attention ya watu kutoka kwnye tetemeko la Kagera
  • Mbali na hivyo, kulijitokeza baadhi ya wanasiasa waliodai kuwa makainikia siyo mali yetu ili kuwa –attract viongozi wa kisiasa washughulike na swala hilo zaidi
Pia, inaonyesha kama matokeo ya utafiti uliofanywa na kuonyesha kiasi cha madini kilichokuwemo kwenye makinikia hayo haukuwa sahihi,na wale waliokuwa wakipinga matokeo hayo ndiyo wanaweza kuwa walikuwa sahihi kwa kiasi fulani

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE: SATURDAY 27 MARCH 2021

MAELEZO YA UFAFANUZI KWA WAUMINI WA KANISA A

DHANA (HPOTHESIS)
ALIYONAYO MHUSIKA KWA SASA KUHUSINA NA SWALA LA YEYE KUZUSHIWA KUWA ANAELEKEA “KUUGUA KICHAA”


Kwa wasomaji wa siku zote wa uzi huu, watakumbuka kuwa kuna matukio yaliwahi kutokea Kanisa A na hatimaye kupelekea mhusika kuwa na ratiba tofauti kidogo na waumini wengine Kanisani hapo, lengo lake likiwa ni kuhakikisha kuwa analinda usalama wake na kwa wakati huo huo anaendelea kushiriki Ibada kwa kiwango anachokihitaji, pale ambapo muda wake unakuwa unaruhusu kufanya hivyo

Matukio yaliyopelekea mhusika kuchukua hatua hii, kwa kiasi kikubwa, yalichangiwa na KIONGOZI MKUU KANISA A(KM-A), KIONGOZI-X na MR X, kama ambavyo amewahi kutoa maelezo yake humu jukwaani hapo awali. Hawa ndiyo walikuwa vinara wa kupanga matukio ya hatari kwake pindi mhusika alipokuwa anakuwa yupo mazingira ya Kanisani nyakati za usiku na katika muda ambao ulikuwa ni baada ya saa 12:00 jioni

Katika hali hii basi, mhusika alilazimika kusitisha baadhi ya ibada kulingana na muda wa Ibada hizo (zile zilizokuwa zinaisha usiku baada ya saa 12:00 jioni) na pia akabuni utartibu wake binafsi wa ratiba ya Ibada zingine binafsi kulingana na muda wake ulivyokuwa unaruhusu

Hata hivyo, mhusika bado aliendeea kufuata kama kawaida, ratiba ya Ibada zingine zote ambazo muda wake ulikuwa hauendi zaidi ya saa 12:30 jioni

Kutokana na maelezo hayo hapo juu, kuanzia Sepemba 2017 (alirudi Kanisa-A April 2017) hadi kufikia April 2020, ratiba ya mhusika Kanisani hapo ilikuwa kama ifuatavyo hapa chini

KWA IBADA ZOTE ZA SIKU ZA JUMAPILI:
  • Alikuwa anaanza na Ibada ya asubuhi kabisa ya Morning Glory, saa 12:00 asubuhi, na hatimaye Ibada ya kwanza saa 1:00 asubuhi , na hatimaye tena baada ya hapo, alikuwa anashiriki kipindi cha somo la uanafunzi na maandiko, ambacho ndicho kilikuwa kinahitimisha Ibada ya kwanza kwenye mida ya saa 4:00 au saa 4:30 asubuhi
  • Baada ya hapo, mhusika alikuwa anashiriki tena sehemu ya kwanza ya Ibada ya pili ya kipindi cha kusifu na kuabudu, iliyokuwa inaanza saa 4:30 au saa 5:00 asubuhi na kuendelea mbele kwa takriban dakika 40 au 45
Baada ya kipindi hiki cha Kusifu na Kuabudu wakati wa Ibada ya pili, mhusika ndiyo alikuwa naye anaondoka Kanisani na kurudi nyumbani

Wakati huo watu wote ambao walikuwa wameshirki Ibada ya kwanza, anakuwa wameshaondoka Kanisani. Wote wanakuwa wameishia kwenye sehemu ile inayohitimisha Ibada ya kwanza, yaani sehemu ya Somo la Uanafunzi na Maandiko wakati mhusika yeye alikuwa anaongeza kipindi kimoja zaidi, kufidia muda ule ambao alikuwa hawezi kuendelea kuwepo maeneo ya Kanisani KWA IBADA ZILE ZA SIKU ZA KATIKATI YA WIKI, kutokana na matatizo ya usalama wake mahali pale

KWA IBADA ZOTE ZA SIKU ZA KATIKATI YA WIKI
:

Ibada hizi zilikuwa ni zile zilizokuwa zikifanyika kuanzia saa 10:30 jioni mpaka saa 12:00 jioni kwa siku za Jumatano ya kila wiki na pia kuanzia saa 12:30 jioni mpaka saa 2:00 usiku kwa siku za Ijumaa kila wiki
  • Ibada zile za Jumatano kuanzia 10:30 jioni mpaka saa 12:00 jioni alikuwa anahudhuria kama kawaida na kwenye muda huo kama ulivyopangwa
  • Hata hivyo, Ibada zingine zile za Ijumaa kuanzia 12:30 jioni mpaka saa 2:00 usiku ndiyo zile ziliwahi kumletea matatizo ya kiusalama wakati wa usiku akiwa anajiandaa kutaka kutoka Kanisani hapo, au njiani wakati akiwa tayari ameshatoka katika mazingira ya Kanisani
  • Kwa siku hizi za Ijumaa, mhusika alikuwa vile vile anafika Kanisani kuanzia kuanzia 10:30 jioni na kuondoka saa 12:00 au saa 12:30 jioni
Kwa hiyo kwenye Ijumaa hizi, alikuwa anafika Kanisani kwa ajili ya kufanya maombi binafsi pamoja na kujifunza maandiko matakatifu katika muda ambao ulikuwa unakuwa tofauti na waumini wengine kanisani hapo

Kwa hali hiyo basi, kwenye siku hizi za Ijumaa kila wiki, ilikuwa kila waumini wakifika kwa ajli ya kuanza Ibada ya pamoja saa 12:00 jioni, yeye alikuwa anapishana nao kwa sababu ndiyo ulikuwa muda wake muafka wa kuondoka Kanisani pale. Muda mwingine zaidi ya masaa hayo ulikuwa si salama kwake kuendelea kuwepo Kanisani hapo

Kwenye wiki ambazo kulikuwa kunakuwa maombi ya siku mbili, J3 na J4 halafu yanauatiwa tuseme na Semina ya kuanzia J5 mpaka Ijumaa, MARA ZOTE mhusika alikuwa anakosa Ibada zote hizi kwa sababu MARA ZOTE ratiba yake ilikuwa ni kuanzia saa 12:00 jioni mpaka saa 2:00 usiku. Hata hivyo mhusika alikuwana ratiba yake binafsi iliyomuwezesha kuwa anafika Kanisani siku za J5 na Ijumaa na alikuwa anaondoka saa 12:00 au saa 12:30 jioni, muda ambao waumini wenzake ndiyo walikuwa wanaanza Ibada

HITIMISHO:
Ukiangalia ratiba ya mhusika namna ilivyokuwa imekaa, na ukiunganisha na tukio la J2 ya tarehe 26 April 2020 ambapo kuliitishwa mkutano wa ghafula wa wanaume na KM-A, kitendo kilichopelekea MR X kuja kukaa karibu kabisa na mhusika; muunganiko wa matukio haya yote unaonyesha kuwa:
  • Kuna taarifa zilikuwa zimeshasambazwa na viongozi Kanisani hapo wakishirikian na MR X kuwa huyu mtu siku hizi akili yake haiko kawaida ina hitilafu
  • MR X atakuwa ndiyo alikuwa anawahakikishia kwa sababu wako pamoja ofisini na ambako nako pia tayari alishatuhumiwa tena kwa maandishi, kuwa katika hali ya kutokuwa na akili isiyo kawaida
  • Huku Kanisani nako alionekana kuendesha baadhi ya Ibada akiwa peke yake kwa kufauata ratiba yake tu kiasi kwamba kwa baadhi ya siku za Ibada, wenzake wakiwa wanaondoka yeye ndiyo anaingia au anaendelea na Ibada na hatimaye kusitisha Ibada hiyo kwa muda wake peke yake
IBADA YA KUSIFU NA KUABUDU YA IBADA YA PILI

Ikumbukwe kuwa mhusika alikuwa anashiriki Ibada ya kwanza huku akiongezea na sehemu nyingine ya Ibada ya pili ambayo ni Kusifu na Kuabudu

Sehemu hii ya Ibada ya Kusifu na Kuabudu aliyokuwa anashiriki kwenye Ibada ya pili kila siku za J2, ambayo waumini wengine waliokuwa wameshiriki pamoja naye Ibada ya kwanza walikuwa hawashiriki, alikuwa anafanya hivyo kufidia Ibada zile za katikati ya wiki zilizokuwa zikifanyika muda wa lala salama na ambazo yeye alikuwa hawezi kushiriki. Hizi ni Ibada zile zote zilizokuwa zinaanza saa 12:30 jioni na kuisha saa 2:00 usiku

MUBATIKIWE TENA NA BWANA
 
CHIMBUKO LA DHANA HII YA MHUSIKA ALIYOIELEZEA HAPO JUU

Dhana hiyo aliyoielezea hapo juu ambayo ndiyo anayo mhusika kwa sasa inatokana na ukweli kuwa
  • Siku ya mkutano wa dharura wa wanaume Kanisani, MR X alitokea ghafula na kuja kukaa karibu kabisa na mhusika
  • Kitendo hiki kilikuwa ni tahadhari aliyochukua MR X siku hiyo kwa ajili ya kuhakikisha kuwa anakuwa karibu na mtu huyu mwenye viashiria vya matatizo ya akili, just in case angeamua ku-react tofauti na matarajio ya wengine
  • Hatua hiyo pia Ilikusudiwa kumuonyesha MR X kama alikuwa anachukua tahadhari ya kukwepa lawama kutoka kwa waumini kwamba “sasa wewe kwa sababu unamjua kuwa ana matatizo ya akili, kwa nini hukuchukua hatua ya kwenda kukaa karibu naye, wewe kama staff mate wako?’
  • Kwa hiyo MR X alikuja kukaa karibu na mhusika kwa ajili ya kumdhibiti, in case angeamua kufanya kuchangia chochote kile siku hiyo. Wangeanzisha fujo ambazo chanzo chake kingetengenezwa na kuonekana ni mhusika aliyepelekea ziwepo
Mbali na hayo, ofisini nako tayari alikuwa tayari ameshatuhumiwa (kwa swala hilo hilo la uelekeo wa kuwa na matatizo ya akili), mara mbili na kwa njia ya maandishi

Kwa hiyo siku hiyo ya mkutano, kama wangefanikiwa kuanzisha fujo waliyokuwa wamepanga, baadaye wangekuja kutoa maelezo kuwa mhusika ndiye aliyesababisha fujo hizo kutokana na kuwa na matatizo ya akili

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
Je, huu uzi unazungumzia nini hasa?
Nimeusoma mpaka basi, sijaelewa unazungumza kuhusu nini? Kwa ufupi kidogo tafadhali 🤔
 
Je, huu uzi unazungumzia nini hasa?
Nimeusoma mpaka basi, sijaelewa unazungumza kuhusu nini? Kwa ufupi kidogo tafadhali 🤔
Ni mambo ya umbe umbea tu hivi. Kama huna muda wa kutosha achana nao
 
UPDATE: FRIDAY 02 APRIL 2021

SHOTI ZA UMEME
KWENYE BAADHI YA VIFAA VYA UMEME VIKIWEMO VIFAA VYA MHUSIKA MWENYEWE

DHANA ALIYOMAYO MHUSIKA MPAKA MUDA HUU KUHIUSIANA NA MATUKIO YA SHOTI ZA UMEME KWENYE BAADHI YA VIFAA VYA UMEME AMBAYO YANAONYESHA KAMA MR X ALIHUSIKA



TUKIO LA KWANZA:

KUUNGUA KWA TRANSFOMA KWA SHOTI YA UMEME MAENEO YA OFISINI KWA MHUSIKA


Wasomaji wa siku zote wa uzi huu watakumbuka kuwa, hapo awali mhusika aliwahi kuongea kuhusiana na swala la transfoma lililowahi kuungua nje jirani kabisa na ofisi ya mhusika. Transforma hilo liliungua siku kadhaa baada ya MR X kuwa ameleta “Fire Extingusher” ndani ya jengo na kuliweka kwenye korido ya ghorofa ya kwanza

Tukio hili la kuungua kwa transforma, ukiongezea na matukio mengine matatu ya kuungua kwa shoti za umeme, battery tatu za gari la mhusika, ndani ya muda usiozidi miaka minane, mpaka muda huu, matukio haya yote kwa ujumla wake yameshapelekea mhusika kuwa na dhana kuwa:

  • Kwenye ulimwengu wa roho, MR X anao utaalamu wa ku-shoti vifaa vya umeme
  • Transforma lililowahi kuungua, halikuungua kwa shoti ya umeme wa kawaida, bali kuungua huko kulitokana na nguvu zilizo nje ya ulimwengu wa mwili
  • Ukizingatia maneno aliyowahi kuongea MR X siku hiyo, ilionekana wazi kuwa kiasi kikubwa alikuwa amelitarajia tukio la kuungua transforma hiyo
  • Vile vile, siku mhusika alipopata tatizo kwa mara ya pili la betri ya pili ya gari kupata shoti ya umeme, MR X akiwa anaongea na mhusika siku hiyo, alionyesha pia kuwa alilitarajia tukio hilo kwenye betri hiyo ya nhusika.
Hat hivyo, details za namna MR X alivyolitarajia tukio hilo kwenye betri ya mhusika, mhusika anaziwithhold!

Zaidi ni kuwa inaonyesha kama MR X huwa natekeleza project yake hii kwa kutumia sadaka ya fedha ya bure kutoka kwenye mikono ya mhusika mwenyewe

Ukiangalia hata kwenye tukio la hivi karibuni la harusi ambayo ilishindikana kufungwa, MR X alikuwa pia mmojawapo wa wanakamati na ndiye ambaye alichukua hatua ya kumhammasisha mhusika kutoa mchango wa harusi hiyo. Kwenye hariusi hii pia inaonyesha kama MR X alikuwa vile vile alikuwa kwenye “similar project”

  • Kwa hiyo MR X alimhamamsisha mhusika kutoa mchango wa harusi hiyo huku yeye (MR X )akiwa anajua kuwa ilikuwa ni sadaka
  • Baada ya tukio hilo la harusi iliyoahirishwa kuwa limeshindikana kuzaa matunda, MR X aliamua kutumia mbinu nyingine ya kumtumia binti yake mkubwa
  • Binti huyo anaonekama kama alitumwa na MR X, amewahi kuoongea na mhusika mara mbili tu na kwa namna fulani ya kificho sana, mazingira ya ndani ya Kanisani kwenye viti na sehemu ambayo huwa wanakaa waumini wakati wa Ibada
  • Mara ya kwanza waliongea mwezi wa pili mwanzoni, na binti huyo kueleza shida yake kuwa anahitaji kwenda kwenye mkutano wa injili
  • Binti alisema kuwa safari ya kwenda kwenye mkutano huo ni mwezi wa tatu
  • Mhusika alimsihi waonane mwezi wa pili mwishoni ili aweze kumpa mchango huo aliouhitaji
Hata hivyo muda ulipofika (mwezi wa pili mwishoni) binti huyo akawa anaonekana kama kumkwepa mhusika, ambapo mhusika naye hakutaka kumfuatilia akisubiri aone kitatokea nini huko mbeleni.

Hatimaye mhusika alikuja kugundua kuwa kumbe binti alikuwa anakwepa watu wasimuone anaongea na mhusika, kitu ambacho pengine kingepelekea baadhi ya waumini waanze kujiuliza maswali ya nini wawili hao huwa wanakaa wanaongea

Hata hivyo, ilipofika mwezi wa tatu mwanzoni, J2 ya tarehe 07 March 2021, ndiyo pale binti huyu alipojitokeza tena kwa kumfuata mhusika mahali alipokuwa amekaa, Ibada ya pili ikiwa imeshaanza na inaendelea.

Wakati huo waumini wengi walikuwa wame-concetrate na Ibadan na inawezekana hakuna mtu hata mmoja ambaye alimuona biti huyo akiwa anaongea na mhuska kwa kumnong’oneza. Vile vile vyombo vya muziki vilikuwa pia navyo vilikuwa na waumini wote walikuwa wakiimba kwa sauti ya juu

Binti yeye alikuwa amehudhuria Ibada ya kwanza, na wakati huo alikuwa anatoka kuelekea nyumbani isipokuwa alikuwa amechelewa kidogo kiasi cha kupelekea Ibada ya pili kuanza kabla hajatoka nje ya uzio wa Kanisa, kitu ambacho huwa ni cha kawaida tu kwa muumini yeyote yule Kanisani hapo

MUDA ALIOWASILI MHUSIKA KANISANI JUMAPILI HIYO

J2 hiyo, mhusika yeye alifka Kanisani akiwa amechelewa kidogo tofauti na ilivyo kawaida yake na hivyo alikuta Ibada ya pili taryari imeshafunguliwa, iko mwanzoni

  • J2 hiyo mhusika alipoingia Kanisani, akienda kukaa kwenye sehemu yake ya siku zote
  • Ibada ikiwa inaendelea na watu wote wakiwa wanaimba mapambio kwa sauti ya juu, binti huyu alionekana akiwa anatokea sehemu za washroom na kwenda moja kwa moja kwa mhusika hadi pale alipokuwa amesimama mhusika na kuongea naye
  • Binti huyu alikumbushia mchango J2 hiyo, ule ambao walikuwa wamekubaliana kuwa wangepeana mwezi wa pili mwishoni
  • Mhusika alimuuliza binti kuwa safari ya kwenda kwenye mkutano wa injili ni lini, binti akasema ni J5 wiki ijayo, yaani tarehe 10/03/2021
  • Mhusika alimjibu binti kwa kumwambia kuwa “nitampatia mchango huo baba yako kesho ofisini”
  • Baada ya hapo binti huyu aliondoka na kuelekea nyumbani
J2 hiyo mhusika alipokuwa anatoka ofisni, alipitia maeneo ya Sinza Super Star na kuweka salio kwenye simu yake. Kesho yake alionana na MR X ofisini na kumweleza kuwa anahitajika kutoa mchango wa mtoto anayeenda kwenye mkutano wa injili na hivyo angependelea kumpa fedha hiyo yeye, yaani MR X

  • MR X alimshauri mhusika aitume moja kwa fedha hiyo moja kwa moja kwenye simu ya binti yake
  • Mhusika alikubali na MR X alitoa namba ya binti huyo na hatimaye mhusika alimtumia binti huyo fedha hiyo kwa ajili ya safari ya kuelekea kwenye mkutano wa injili.
  • Binti huyo aliupokea mchango huo kwenye simu yake nahatimaye alirudisha majibu ya kumshukuru mhusika, kwa ujumbe wa mfupi wa simu
Hiyo sasa ilikuwa ni J3 ya tarehe 08/03 2021



NEXT:

MATUKIO MENGINE: YA KUPIGWA SHOTI YA UMEME BETRI TATU TOFAUTI TOFAUTI ZA GARI LA MHUSIKA, NA KATIKA VIPINDI TOFAUTI TOFAUTI



……………………….inaendelea
 
MATUKIO MENGINE: YA KUPIGWA SHOTI YA UMEME BETRI TATU TOFAUTI TOFAUTI ZA GARI LA MHUSIKA, NA KATIKA VIPINDI TOFAUTI TOFAUTI

……………………….inaendelea

TUKIO LA PILI: KUPIGWA SHOTI YA UMEME NA KUPELEKEA KUHARIBIKA BETRI YA KWANZA YA GARI LA MHUSIKA


Tukio hili lilitokea Septemba 2014

  • Lilitokea siku ya Jumamosi ASUBUHI
  • Betri ilipata shoti ya umeme ghafla na kupelekaea kuharibika
  • Mhusika alilazimika kununua betri nyingine
Kwenye tukio hili la kwanza, hakuna ushahidi wowote wenye mantiki unaoonyesha kuwa MR X alihusika

Usiku huo wa Ijumaa kuamkia Jumamosi, aidha taa za kwenye parking zilikuwa hazifanyi kazi au umeme ulikuwa umekatika, yaani hapakuwa na umeme kwenye parking na kupelekea uwepo wa giza kwenye parking hiyo

Baada ya betri hii kuungua, mhusika alilazimika kununua betri nyingine



TUKIO LA TATU: KUPIGWA SHOTI YA UMEME NA KUPELEKEA KUHARIBIKA BETRI YA PILI YA GARI LA MHUSIKA

Tukio hili lilitokea January /mwanzoni mwa February 2018

Lilitokea siku ya JUMATATU ASUBUHI wakati mhusika alipokuwa akijandaa kuwasha gari ili aelekee ofisini

  • Jana yake ilikuwa J2 ambapo mhusika alikuwa ametokea Kanisani na alipofika nyumbani alipaki gari na hakuligusa tena
  • Gari hilo hakuwahi kulitumia tena baada ya kuwa ametoka Kanisani J2 hiyo mpaka kesho yake J3 alipokuwa anataka kuelekea ofisini
  • Asubuhi hiyo akiwa anawasha gari, betri ya gari hiyo ilipata shoti ya umeme ghafla na kupelekaea kuharibika
  • J2 jana yake kulikuwa na sadaka nyingine ya ziada na MAALUMU Kanisani, mbali na ile sadaka ya kawaida
Usiku huo wa J2 kuamkia J3, aidha taa za kwenye parking zilikuwa hazifanyi kazi au umeme ulikuwa umekatika, yaani hapakuwa na umeme kwenye parking na kupelekea uwepo wa giza kwenye parking hiyo

Baada ya betri hiyo ya pili kuungua, mhusika alilazimika kununua betri nyingine



SADAKA MAALUMU YA JUMAPILI HIYO

Ni kwamba wiki kadhaa nyuma, “Kiongozi X” wa Kanisa A alikuwa ametangaza wito wa waumini wote kutoa sadaka ya shukrani kwa Mungu, kwa kuwavusha kutoka mwaka mmoja na kuingia mwaka mwingine

  • J2 hiyo ndiyo ilikuwa ile ambayo waumini walitoa sadaka hiyo
  • Mhusika naye pia alitoa sadaka hiyo (TZS 100,000/=) na kuiweka kwenye bahasha maalumu
Baada ya waumini kuwa wametoa sadaka hiyo, alikaribishwa kiongozi mwingine kwa ajli ya kuiombea. Sadaka hiyo iliombewa na kiongozi yule ambaye aliwahi kusema

“ukiona watu wanaanza kulalamika Kanisani, ujue wamekosa kazi ya kufanya”



TUKIO LA NNE: KUPIGWA SHOTI YA UMEME NA KUPELEKEA KUHARIBIKA BETRI YA TATU YA GARI LA MHUSIKA


Tukio hili lilitokea Oktoba 2019

Lilitokea siku ya JUMATATU ASUBUHI wakati mhusika alipokuwa akijandaa kuwasha gari ili aelekee ofisini

  • Jana yake ilikuwa J2 ambapo mhusika alikuwa ametokea Kanisani na alipofika nyumbani alipaki gari na hakuigusa tena
  • Gari hilo hakuwahi kulitumia tena baada ya kuwa ametoka Kanisani J2 hiyo mpaka kesho yake J3 alipokuwa anataka kuelekea ofisini
  • Asubuhi hiyo akiwa anawasha gari, betri ya gari hiyo ilipata shoti ya umeme ghafla na kupelekaea kuharibika
  • J2 jana yake kulikuwa na sadaka nyingine ya ziada ila ya kawaida Kanisani, mbali na ile sadaka ya siku zote
Usiku huo wa J2 kuamkia J3, aidha taa za kwenye parking zilikuwa hazifanyi kazi au umeme ulikuwa umekatika, yaani hapakuwa na umeme kwenye parking na kupelekea uwepo wa giza kwenye parking hiyo

Baada ya betri hiyo ya tatu kuungua, mhusika alilazimika kununua betri nyingine

Kwenye tukio hili la pili, kuna ushahidi uliojitokeza kumuunganisha MR X na tukio hili, baada ya kuwa ametoa ushauri kwa mhusika ulioonyesha kama alikuwa anatarajia tukio hilo kumpata mhusika



HITIMISHO

Kwenye matukio yanayohusiana na kupigwa shoti za umeme betri ya pili na ya tatu za gari la mhusika, msomaji atagundua mfanano wa kipekee wa matukio haya mawiili kwamba yote:

  • Yametokea siku za JUMATATU ASUBUHI wakati mhusika akiwa anajandaa kuwasha gari ili aelekee ofisini
  • Yanaonyesha kuwa jana yake ilikuwa ni J2 ambapo mhusika alikuwa ametokea Kanisani na alipofika nyumbani alipaki gari na hakuligusa tena
  • Kila J2 husika ya jana yake, kulikuwa kunakuwa na sadaka nyingine YA ZIADA KANISANI, MBALI NA ILE SADAKA YA IBADA ZA KAWAIDA
  • Mara zote, kwenye siku za usiku wa J2 kuamkia J3, aidha taa za kwenye parking zilikuwa zinakuwa hazifanyi kazi au umeme ulikuwa umekatika, na kupelekea uwepo wa giza kwenye parking hiyo


WAY FORWARD YA “MR X” KWENYE MATUKIO HAYA YA SHOTI ZA UMEME

Mpaka muda huu MR X bado yupo anaendelea kushughulika na project nyingine ya aina hii, na J2 iliyopita ya tarehe 28/03/20 kulitangazwa ghafla sadaka maalum Kanisani ambayo mhusika hakuitoa

Kawaida sadaka maalumu kwa Kanisa A huwa zinatangazwa wiki kadhaa nyuma kabla ya siku inayotarajiwa sadaka hiyo kutolewa na mara zote huwa zinatangazwa na Kiongozi Mkuu

  • Hii ya J2 iliyopita ilitangazwa na Kiongozi mwingine mwandamizi, the most junior kati ya viongozi karibia wote waliopo Kanisa A
  • Ilitangazwa ghafla J2 hiyo hiyo, yaani hata J2 nyingine iliyokuwa imetangulia kabla ya J2 hiyo, ya tangazo la sadaka hiyo, sadaka hiyo haikuwa imetangazwa kuwa itakuwepo
Hapakuwa na haja ya Kiongozi mwingine Junior kutangaza sadaka hiyo kwa sababu KM-A amwenyewe likuwepo na pia alisimama madhabahuni kutoa matangazo mengine. Hii inaonyesha kuwa KM-A alikuwa amekwepa kutoa tangazo hilo yeye mwenyewe, na hivyo kuamua kuli-delegate kwa kiongozi mwingine, the most junior

Sadaka iliyotangazwa Ilikuwa ni sadaka ya muhimu sana na ambayo si kawaida tangazo lake kutolewa papo kwa papo; ilikuwa ni sadaka kwa ajili ya mjane.

Sadaka ya aina hii mara zote, kawaida huwa inatangazwa na Kiongozi Mkuu wiki kadhaa nyuma na si vinginevto



Zaidi ni kuwa J2 hiyo mhusika hakuweza kutoa sadaka hiyo ya mjane Kanisani kwa sababu, kwenye usiku wa J2 hiyo ya tarehe 28/03/2021 kuamkia J3, hapakuwa na umeme kwenye parking ya gari, kwenye makazi ya mhusika





NEXT:

MHUSIKA AWASHAURI (NI USHAURI, SIYO AGIZO) VIONGOZ WOTE KANISA A


  • Waombe msamaha kwa Mungu, iwapo tu wanaona ndani ya roho na nafsi zao kuwa kuna mahali wamemkosea Mungu katika haya yanayoendelea kuandikwa humu
  • Vile vile wawaombe msamaha waumini wa kanisa A, kila kiongozi mmoja kwa wakati wake
Vinginevyo, wakanushe haya yanayoandikwa humu, mbele ya macho ya waumini wote



Hitaji hili la viongozi hawa kuomba toba na rehema kwa Mungu, halimhusu Kiongozi mmoja tu ambaye amekuwa masomoni katika kipindi chote ambacho mambo haya yaliyopinda panda yamekuwa yakiendela Kanisa A

Mhusika ataleta orodha ya mambo ambayo kwayo viongozi hawa inabidi waombe toba na rehema kwa Mungu, ikiwa ni pamoja na kuomba msamaha mbele ya waumini wa Kanisa A

Ikumbukwe kuwa utakuwa ni ushauri, na si agizo; ushauri ambao wanaweza kuufuata au kutokuufuata



MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
Wakati mhusika anaongea na MR X wakiwa ofisini J3 ya tarehe 08/03/2021. mhusika alijaribu kumuuliza MR X kuwa binti yake anaenda lini kwenye mkutano wa injili. MR X alijibu kuwa ni wiki ijayo, wakati binti mwenyewe alikuwa ameshasema kuwa ni J5 ya wiki hiyo. Hata hivyo kupishana kwao huku ni kwa kawaida sana iwapo tu safari hiyo waliwahi kuiongelea kipindi kirefu huko nyuma na baada ya hapo, hawakuwahi kuiongelea tena

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
Back
Top Bottom