#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

HITIMISHO:

Mwanzoni mwa mwaka 2021, kuanzia January hadi March 2021, tuliwahi kupoteza viongozi wa ngazi juu kabisa wa Taifa na katika namna ambayo rekodi ya kupoteza viongozi kwa namna hii haitakuja kutokea tena katika historia ya Taifa letu, NA MHUSIKA ANAOMBA ISITOKEE TENA MILELE KATIKA JINA LA YESU

Pamoja na kupoteza viongozi hawa na kwa kiwango cha ajabu mno, bado mhusika hakuwahi na wala hajawahi hata siku moja kumsikia KM-A akiguswa na swala hili kiasi cha kuitisha maombi ya kuwaombea kinga viongozi wa Taifa letu na Taifa letu kwa ujumla

KM-A hajawahi hata kupata tu yale maono ya kuitisha maombi kwa ajili ya kuwakinga viongozi waliopo madarakani ili janga la aina hiyo lisije likajirudia tena ndani ya nchi yetu

Walio na bahati sana katika upumbavu huu unaoendelea kufanywa na KM-A madhabahuni, ni viongozi wa ngazi za juu wa Kanisa hili ambalo KM-A anatumika. Wana bahati sana kwa sababu mhusika hana mamalaka ya kufanya chochote juu yao

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
PATTERN NYINGINE MUHIMU SANA AMBAYO IMESHAJITOKEZA TENA WAKATI HUU HAPO “KANISA A” TANGU IBADA ZIHAMIE KWENYE KANISA JIPYA

Ibada zote lazima zimalizie kwa maombi, huku Kiongozi wa Ibada (mnenaji wa neno la siku hiyo) akiwa juu madhabahuni anaomba maombi huku wakati mwingine akiwa ANANENA KWA LUGHA.

Wamesharudisha tena ule mtindo waliokuwa wanautmia zamani wa SECRET CODES, maneno ya lugha fulani yanayotumika kwa ajili ya kushambulia madhabahu ili ikae sawia kama wanayotaka ikae wao wenyewe
 
Kingine kikubwa zaidi ni kuwa J2 iliyopita KM-A aliwaita mbele watu wageni waliokuwa wanahitaji kuokoka. Wakati anawaombea, aliwaombea akisema kuwa YESU ALIFANYIKA LAANA KWA AJILI YAO. Uzuri sasa hivi kila kitu kipo kwenye mtandao na hivyo hakuna haja ya watu kukaa wanaendelea kubishana
Haya maneno YESU KUFANYIKA DHAMBI AU LAANA, mara zote huwa anayatumia kama SECRET CODE ya kushambulia madhabahu. Anazo SECRET CODES zake ambazo huwa anatumia, na nyingi tu siyo hizi tu
Zingine zimo kwenye lugha ya KUNENA KWA LUGHA, ....................utamsikia anasema BAKULYANDA!
 
UPDATE: WEDNESDAY 8TH JUNE 2022

TANGAZO JINGINE MOJA (LA KWANZA KABISA) MUHIMU ALILOTOA KIONGOZI MKUU WA KANISA A (KM-A) J2 YA TAREHE 05/06/2022 NA AMBALO LILIKUWA HALIHUSIANI NA MAOMBI


Kwa kiasi fulani, tangazo hilo linaonekana kushahibiana sana na tangazo alilowahi kuliongelea mhusika kwenye post hii hapa #844

Tangazo hili lilitolewa J2 ya tarehe 12 Desemba 2021 (mwaka jana). Kwa jicho la pili, matangazo haya mawili yanaonyesha mfanano wa kipekee sana, ila tofauti yake kubwa na ambayo ni moja tu ni zile SABABU ZILIZOPELEKEA KILA MOJAWAPO YA MATANGAZO MAWILI HAYA KUTOLEWA

MASWALI KADHAA YA MSINGI SANA KUHUSIANA NA TANGAZO HILO

  • Kwa nini waumini wa Kanisa A wasishirikishwe kwa kutoa sadaka halafu watoto hao wahitaji wakanunuliwa nguo mpya kutoka madukani?
  • Kwa nini wao wawe wanapelekewa kukuu tu zilizovaliwa majumbani mwa watu?
  • Je waumini wa Kanisa-A wamewahi kushirikishwa kuhusiana na swala la kuwawezesha watoto hao kwa mahitaji mapya ya kununuliwa moja kwa moja kutoka dukani na wakasema kuwa hawana uwezo huo?
  • Waumini ambao wameweza kujenga Kanisa la mabillion ya pesa hadi likakamilika, je wanaweza kushindwa kununua kaptula sketi na na mashati meupe ya watoto wa shule ya msingi; na ambao ni wahitaji, wanaoishi kwenye mazingira magumu?.
  • Kwa nini watoto hawa wasinunuliwe nguo mpya kutoka dukani na kupelekewa, ukizingatia idadi yao kuwa ni wachache sana?
Mhusika anaamini kabisa kuwa, waumini wa Kanisa-A wana uwezo wa kuwavalisha watoto hao wahitaji kwa nguo mpya za kutoka dukani moja kwa moja hata kama idadi yao ingekuwa elfu moja (1000)

Pia kwenye matangazo hayo, KM-A alienda mbele zaidi akataja na mapazia (of couse haya inabidi yanunuliwe dukani), na katika kutaja mapazia hayo, nadhani akaona kwamba mwishowe anazidi kwenda ndani moja, alisistisha akasema hayo ayaache. Hapo KM-A alikuwa anasoma orodha ya mahitaji ya watoto hao wahitaji kama ambavyo imeshawasilishwa kwake na walimu wa watoto hao wahitaji, na ambao wanaishi mazingira jirani kabisa na pale lilipo Kanisa -A

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
NYONGEZA MUHIMU KUHUSIANA NA KILICHOPELEKEA KM-A KUITISHA MAOMBI YA SIKU TATU

Kitu kingine kinachovutia zaidi kwenye tukio hili la hivi karibuni la ulawiti wa watoto na ambalo lililopelekea KM-A kuitisha maombi ya siku tatu; ni kwamba kuna mama mmoja ambaye ameonekana kwenye vyombo vya habari akitoa ushuhuda wa watoto kutendewa mambo hayo ya ajabu, huku akiwa amejifunika khanga gubigubi, kuficha sura yake. Sasa hapa kwa mtu ambaye ni layman kama mimi unajiuliza maswali kwamba; mtu ambaye siyo mtuhumiwa, unatoaje taarifa huku ukiwa umejifunika nguo gubigubi, ilhali yule anayetuhumiwa yeye yuko easy tu na wala hafanyi jithada zozote za kuficha sura yake?

Kwa sababu mtu ambaye ni shahidi wa tukio la aina hii, lazima kuna uwezekano siku moja akatakiwa kuonekana mahakamani, na kawaida mashahdi wanapokuwa mahakamani huwa hawafuniki nyuso zao. Je, huyu aliyekuwa anaficha sura, alikuwa anamaanisha nini?

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE: THURSDAY 09/06/2022

NYONGEZA MUHIMU KUHUSIANA NA YALE YANAYOENDELEA HIVI SASA KANISA-A UKIYAHUSIANISHA NA KIONGOZI MKUU WA KANISA A (KM-A)


KM-A ana makundi kadhaa ya waumini ambao idadi yao si kubwa sana, na mojawapo ya kundi muhimu sana kwake na ambalo ni active sana, ni la watu ambao wanaongea lugha moja ya kuzaliwa na mhusika

Bahati nzuri tu ni kwamba mhusika na KM-A hawaongei lugha moja ya kuzaliwa, ila kama ingekuwa ni hivyo basi kuna uwezekano mhusika angeweza kumtuhumu KM-A kwa swala la ukabila

Mmojawapo wa watu walioko kwenye kundi hilo na ambao mhusika alishawathibitisha siku nyingi na pasipo shaka yoyote ile, ni kiongozi yule aliyetajwa na KM-A kuwa muumini aliyefunguliwa J2 iliyopita anatoka kwenye eneo lake. Kiongozi huyu wanaongea lugha moja ya kuzaliwa na mhusika

Kwa hali hiyo basi, mhusika anapendekeza kama kuna mamlaka ambayo itahitaji kupata taarifa za nyongeza kuhusiana na haya ambayo yameandikwa hapa, basi mamlaka hiyo inaakiwa isilisahau pia kundi hilo alilolitaja hapo juu. Ni kati ya makundi ambayo yanaweza kuwa na taarifa za maana na muhimu sana

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE: FRIDAY 10TH JUNE 2022

MATUKIO MAWILI MUHIMU SANA NA YANAYOSHAHIBIANA AMBAYO MHUSIKA ALIWAHI KUKUMBANA NAYO NA KUKWEPA MITEGO ILIYOKUWEMO KWENYE MATUKIO HAYO

TUKIO LA KWANZA
: UKARIBISHO WA KWENDA KIGAMBONI ULIOKUWA UMEAMBATANA NA MOTISHA ILIYOJIFICHA DESEMBA 2010

Tukio la kwanza lilitokea mwishoni mwa Desemba 2010 au mwanzoni kabisa mwa mwaka 2011 (kabla ya May 2011)

Tukio hili lilihusiana na mwaliko kwa mhusika, uliomhitaji aende KIGAMBONI kuwatembelea ndugu zake ambao ndiyo walikuwa wamehamia huko muda siyo mrefu. Mwaliko huu kwa kificho fulani, ulikuwa pia umeambatana na motisha fulani (HIDDEN MOTIVE) ambayo mhusika asingependa sana kuiongelea humu kwa sasa.

Ikumbukwe kuwa kwa kipindi hicho mhusika:

  • Alikuwa bado hajaanza kwenda Kanisani
  • Alikuwa ndiyo tayari ameshaibiwa injini ya gari lake, takribani miezi mitatu hivi nyuma
  • Alikuwa tayari ameshafanya safari yake ya kusini, aliyoifanya mwezi Novemba 2010 akiwa yuko likizo, ambapo alikumbana na vitimbi nya hatari njiani na hatimaye kwenda kuripoti Kituo Cha Polisi Mafinga na kupata msaada pale
  • Alikuwa ndiyo kwa mara yake ya kwanza katika kipindi chake cha utumishi tangu aajiriwe kwenye taasisi anayofanyia kazi, kubaini kuwa mahali fulani kuna kundi la watu ambao siyo wazuri na wanaofuatilia maisha yake
  • Alikuwa huko nyuma, tayari ameshafanya safari kadhaa za kikazi wakiwa pamoja na Boss X, mojawapo zikiwa ni zile Ketumbeine, Engaresero, Kondoa, Kibaya, n.k. ambazo maelezo ya kina ya safari hizi tayari alishawahi kuyaleta humu jukwaani kupitia uzi huu
  • Alikuwau tayari ameshafanya review ya safari zote walizowahi kufanya na Boss X na kugundua mapungufu kadhaa ambayo tayari ailishayaainisha humu jukwaani wakati alipokuwa anaotoa maelezo yanayohusiana na safari hizo
Kosa pekee alilofanya mhusika kwa kipidi hicho, ni taarifa hizi kuzi-share na mtu ambaye siku kadhaa baadaye, alikuja kuwa mama yake wa kiroho (ikumbukwe kuwa wakati huo mhusika alikuwa bado hajaanza kwenda kanisani isipokuwa mtu huyu (aliyekuja kuwa mama wa kiroho) walikuwa tayari wanafahamiana ikiwa ni pamoja na kuwa na ukaribu ambao ulipelekea akamwamini na hivyo kuweza ku-share naye baadhi ya maswala muhimu

Kilichopelekea mhusika kushare taarifa zake na mama huyu ni kuwa kipindi hicho alikuwa hajagundua kuwa mama wa kiroho na Boss X walikuwa na mawasiliano

Baada ya kushare taarifa zake na mama, siku chache mbele mhusika katika kujaribu kuufuatilia mwenendo wa Boss X, mhusika alijiridhisha pasipo shaka kuwa kwa kificho sana, Boss X alikuwa katika taharuki ya namna ambayo alionekana kuwa tayari ameshapata taarifa fulani zinazoashiria kuwa mhusika ameshajua baadhi ya mambo ambayo Boss X alidhani kuwa mhusika asingeweza kuyajua

KILE KILICHOPELEKEA MHUSIKA AJUE KUWA BOSS X AMESHAJUA YALE AMBAYO ALIDHANI KUWA MHUSIKA ASINGEWEZA KUYAJUA

Ilikuwa ni siku moja mhusika alikuwa na safari ya kwenda mjini kwa kutumia gari la ofisi wakiwa pamoja na dereva.

Dereva aliyekuwa naye siku hiyo, ndiyo yule waliyekuwa wanafanya naye safari zote za nyuma ambazo mhusika na Boss X waliwahi kuzifanya

Siku hiyo, mhusika alikuwa anaelekea Samora kwenye duka moja linalouza vifaa vya IT. Alikuwa anenda kununua vifaa fulani vinaitwa RJ-45 (Rgistered Jack 45). Hivi ni vichwa vya zamani vya waya za internet ambavyo hufungwa kila upande wa waya za internet halafu kichwa kimoja kinaingia kwenye computa na kingine kinaingia ukutani au kwenye switch/ router

Siku hiyo, dereva na mhusika wakiwa nje wanataka kuanza safari ya kuelekea mjini, dereva akamjulisha mhusika kuwa Boss X naye amesema ana safari ya kwenda mjini

Aliposikia hivyo, mhusika ikabidi apishe kiti cha mbele kwenye gari akaakaa nyuma

Boss X akaja wakamchukua na hatimaye kuanza safari ya kuelekea mjini

Kabla hawajafika mbali sana, nadhani hata Mwenge walikuwa hawajapita Boss X akaanzisha mazungumzo na kumuuliza mhsika “FULANI, GARI LAKO LINAHITAJI SHILLINGI NGAPI’?

Hapa Boss X alikuwa na-refer gari la mhusika lilikouwa limeibiwa injini na mwenyewe kulietelekeza. Mpaka hapa, mhusika aliomuna Boss X kama mtu ambaye alikuwa anataka kumchezea akili kwa sababu:

  • Kwanza, naturally hana moyo huo
  • Pili, miezi kadhaa ilikuwa tayari imeshapita; huku yeye Boss X akiwa anajua fika ni nini kilikuwa kimetokea kuhusiana na gari hilo; muda wote huo alikuwa wapi?
Mhusika aliamua “kumpotezea” vijana wa mjini huwa wanasema, na bada ya siku hiyo Boss X hakuwahi kuliongelea tena gari hilo. Zaidi ni kuwa mhusika akishatendewa jambo baya kwa makusudi, huwa na yeye anachukua uamuzi ambao huwa hawezi kuubadilisha; MSIMAMO: Hata MZEE WA UPAKO anapenda sana msimamo, na alishawahi kufundisha na kusisitiza waumini wake kuwa na MSIMAMO

Baada ya hapo, kitu pekee alichokiona mhusika kikiwa kinaendelea ni mtu mmoja kuwa anamvizia mhusika kwa baadhi ya safari, pindi anapokuwa anelekea washroom; na akishamkuta humo mtu huanzisha naye mazungumzo ya kuanza kumshawishi alinunue gari lake (mhusika) mazungumzo hayo yakiwa strictly yanafanyikia humo humo washroom tu.

Mtu huyu ni yule ambaye siku za hivi karibuni walishirikiana “tribal mate” wake wakamtuma bibi muuza vitabu ofisini kwa mhusika wakati mhusika alishamweleza bibi huyo kuwa hawezi tena kununua vitabu

TUKIO LA KWANZA: HITIMISHO

Kwa hiyo mbele ya haya yote yaliyoelezwa hapa, baada ya kuwa yalishatokea huko nyuma, mengine yakiwa yalitokea zamani na mengine kwa siku za usoni za wakati huo, ndiyo mhusika akapata sasa mwaliko huo wa kwenda Kigamboni, ukiwa umeambatana na motisha nyingine kubwa iliyokuwa imejificha chini ya mwavuli wa mwaliko huo

KILICHOTOKEA ABAADA YA MWALIKO HUO WA TUKIO LA KWANZA

Mhusika hakuhudhuria mwaliko huo na na kuanzia pale akakta kabisa safari za kwenda Kigamaboni na hadi leo hajawahi tena kwenda Kigamboni; na mara yamwisho mhusika alikuwa Kigamboni ilikuwa ni mwishoni mwaka 2004 siyo 2014, ni 2004), na ilikuwa ni kwenye tkuio la dharura; msiba. Hilo tukio la kwanza likapita

TUKIO LA PILI:

SAFARI NYINGINE NA YA KWANZA KABISA YA KIKAZI YA KWENDA
KIGAMBONI SEPTEMBA 2017

Hii ilipangwa na Boss X; Ilikuwa ni kwenye siku mojawapo wakati wa Mkutano wa Kimataifa wa Kuchakata Data za Matetemeko ya Ardhi ambao ulifanyikia kwenye taasisi anayofanyia kazi mhusika, na Boss X ndiyo alikuwa anau-host mkutano kwa niaba ya Taasisi

………………….inaendelea
 
………………….inaendelea

MKUTANO WA KIMATAIFA WA KUCHAKATA DATA ZA MATETEMEKO YA ARDHI SEPTEMBA 2017 NA SAFARI YA PILI YA KWENDA KIGAMBONI


Mkutano huu ambao ulikuwa ni wa siku saba (7), ulihusisha nchi karibia zote zinazopakana na Tanzania, ukiondoa nchi tatu tu ambazo ni DRC, Rwanda na Burundi

Zaidi ulihusisha pia nchi zingine mbili ambazo hazipakani na Tanzania na zilizoko kwenye pembe ya Afrika na ambazo aidha hazipakani pia na Kenya

BAADHI TU YA MATUKIO MUHIMU AMBAYO YALIKUWA TAYARI YAMESHATOKEA HADI KUFIKIA TAREHE YA MKUTANO HUO WA SEPTEMBA 2017

Yaliyokuwa tayari yameshajiri hadi kufikia tarehe ya mkutano huo ni pamoja na yale yote ambayo mhusika ameshayataja kwenye kipengele hicho cha maelezo ya SAFARI YA KWANZA YA KIGAMBONI, ukiongezea na MENGINE yafuatayo hapa chini, ambayo nayo ni baadhi tu ya matukio yale ambayo ni muhimu

  • Kuanzia Desemba 2010, mhusika alipokumbana na matatizo safarini na hatimaye kwenda kuishia Kituo cha Polisi, mhusika aliamua kuanzia pale kusitisha safari zote za binafsi, ikiwa ni pamoja na zile za likizo, akaamua kubakiza tu zile ambazo ni za kiofisi
  • Mnamo Mei 2012 , takribani miaka miwili baadaye; mhusika akiwa yupo njiani kwenye safari ya kikazi ya kukagua vituo vya Matetemeko ya Ardhi pamoja na kukusanya data za vituo hivyo kwa ajili ya kuja kuzichakata ofisini, wakati wa kurudi akiwa anatokea Dodoma ambako alitoka saa 5:00 asubuhi; alilazimika kulala Mororgoro badala ya kuja moja kwa moja hadi Dar es Salaam, baada ya ya kubaini kwa mara nyingine tena, mambo kadhaa yasiyokuwa ya kawaida kuhusiana na usalama wake, kwenye safari hiyo. Hivyo mhusika aliamua kusitisha safari hiyo na kuishia Morogoro, halafu akaendelea na safari hiyo kesho yake asubuhi. Zaidi ni kuwa alipokuwa Morogoro kwenye nyumba ya kulala wageni, alimpigia simu mama wa kiroho kumjulisha hali hiyo
Mnamo Desemba 2012, mhusika alipangiwa tena na Boss X safari nyingine ya kikazi nje ya nchi, ndani ya Afrika. Safari hii nayo ilikuwa pia ni kwa ajili ya Mkutano mwingine wa Kimataifa wa kuchakata Data za Matetemeko ya Ardhi

  • Safari hii ya Desemba 2012 ilifuatana na ile ya ndani ambayo mhusika aliwahi kuifanya Mei 2012; ambayo maelezo yake tayari ameshayatoa hapo juu. Kwa hali hiyo hapo katikati hapakuwahi kuwa na safari nyingine yoyote ile ya kikazi kwa mhusika aidha ya ndani au ya nje ya nchi na hivyo baada ya Mei 2012, safari nyingine iliyofuatana na hiyo ilikuwa ni hii ya Desemba 2012
  • Ukizingatia pia kwa wakati huo mhusika alikuwa tayari ameshasitisha safari zake zile za binafsi; utaona kuwa tangu Mei 2012 hadi kufikia muda huo, mhusika alikuwa hajawahi kusafiri tena kwenda mahali pengine popote pale nje ya Dar es Salaam, hadi kufikia wakati huo wa safari hiyo nyingine ya Desemba 2012
Kwenye safari hii ya sasa, ilikuwa aondoke hapa nchini na ndege ya usiku, na ambayo ilikuwa inapitia nchi nyingine jirani na hatimaye kuelekea kwenye destination yake ambayo ilikuwa nchi nyingie tena jirani, ambako ilikuwa iko scheduled kuwasili saa 5:00 kamili usiku

  • Kwa bahati mbaya mhusika hakufanikiwa kuifanya safari hii, kitu ambacho kilipelekea kuwepo kwa mgogoro wa kiofisi na Boss X
  • Mgogoro huo haukutokea papo kwa papo, bali ulikuja kujitokeza baadaye baada ya miezi kadhaa kuwa imepita mnamo March 2013
  • Baada ya mgogoro huo, mhusika alimuomba Mkuu wa Idara wa wakati huo, kwamba “allegations” zake kutoka kwa Boss X, ziwekwe kwenye maandishi halafu yeye atazijibu
  • Mkuu wa Idara wa wakati huo alikuwa ndiyo yule ambaye hapo awali, alikuwa ame-faclitate zoezi la mhusika kushushwa cheo (February 2014) na hatimaye kukatwa mshahara (kuanzia June 2012 hadi leo) na tangu kipindi hicho mhusika hajawahi kupanda cheo hadi leo hii
Hadi kufikia Mei 2013, allegations hizo za maandishi mhusika alikuwa hajapewa

Baada ya hapo, hiyo Mei 2013 mhusika aliamua kwa mara ya kwanza, kuuandkia uongozi wa juu wa taasisi akiujulisha kuwa ana wasiwasi na usalama wake hasa anapokuwa yupo safarini na hivyo kuuomba uongozi huo umsaidie kwa kumlinda katika ule uwezo ambao taasisi kama taasisi inao, ikiwa ni pamoja na kumruhusu asifanye safari zozote za kikazi; ndani na nje ya nchi

  • Hadi kufikia Novemba 2013, mhusika alikuwa bado hajapata majibu ya ombi lake, kitu kilichopelekea akumbushie tena mwezi huo
  • Ilipofika Mei 2014, mhusika akaandikiwa barua ya kuitwa kwenye kiako cha nidhamu, akituhumiwa kukatili maagizo ya kazi kutoka kwa wakuu wake wa kazi
  • Mhusika alitakiwa kuijibu kwanza barua ndani ya siku 14, halafu kikao kingefuata baada ya majibu ya barua yake
  • Mhusika aliijibu barua hiyo ndani ya muda na baada ya pale kukawa kimya tena
  • Ilipofika tena Septemba 2014, mhusika akaandikiwa barua nyingine tena akiitwa kwenye kiako cha nidhamu kilichokuwa kinafanyika siku kadhaa mbele
Mhusika alijiandaa kwa ajili ya kikao hicho na siku ilipofika, akiwa anaelekea kwenye kikao, Katibu Muhtasi wa Mkuu wa Idara wa wakati huo, alimfuata mhusika akiwa anashuka kwenye ngazi akielekea kwenye kikao na kumtaarifu kuwa kikao hicho kilikuwa kimeahirishwa

…………………..inaendelea
 
………………….inaendelea

BAADHI YA YALIYOKUWA TAYARI YAMESHATOKEA HADI KUFIKIA SEPTEMBA 2017


Mhusika alifuatilia kuhusiana na taarifa hizo za kikao kuahirishwa kwa sababu alikuwa amezipata kutoka kwa mtu ambaye, mpaka muda huu anakiri kuwa hayupo mtu mwingine ambaye hajawahi kutokumwamini kama ambavyo aliwahi kutokumwamamini Katibu Mhutasi huyo

Na kweli sensor zake mhusika zilikuwa sahihi. Alipofuatilia kuhusiana na kikao hicho, alienda akapewa taarifa kuwa kikao hakikuwa kimeahirishwa kilikuwepo; isipokuwa swala lake yeye ndiyo lilikuwa limeahirishwa; na hivyo kuambiwa asubiri atajulishwa tarehe nyingine mbadala ya kikao hicho

Ilipofika Julai 2015, Mkuu wa Idara aliyekuwepo akahamishwa, akaja mwingine huyu ambaye baadaye alikuja kuanguka kutoka ghrorofa ya kwanza na kuumia kiwiko

Vile vile, hiyo hiyo Julai 2015, mhusika akapigiwa simu na “SPECIALIST”, na wakati huo Mkuu wa Idara mpya akiwa tayari alishaanguka kutoka ghorofani

“SPECIALIST” alimuuliza mhusika kama wanaweza kuongea kuhusiana na maswala yake; huku “SPECIALIST” akimjulisha mhusika kuwa amekuwa akipewa kila nakala ya barua zake ambazo amekuwa akiuandikia uongozi wa juu wa taasisi

Mhusika alikubali kuwa hilo halina shida, isipokuwa akatoa angalizo kwamba angependa zaidi kwa wakati huo, aongee na uongozi wa juu wa Taasisi kwa sababu tayari alikuwa na tuhuma kwenye file lake ambazo zilikuwa bado hazijawa resolved. Kwa kuongea naye “SPECIALIST” peke yake pasipo kuwepo wale walio juu yake, yeye kama yeye angeweza kuzi-resolve vipi tuhuma hizo peke yake na wakati si yeye aliyezitoa? Mhusika alimuuliza “SPECIALIST” swali hilo

Kwa siku hiyo, mhusika na “SPECIALIST” waliishia hapo, wakabadilishana mawasiliano ya simu na hatimaye kuachana

Ilipofika Jumapili Oktoba 25, 2015, siku ya kupiga kura kwa ajli ya Uchaguzi Mkuu; mhusika akakoswakoswa na tukio la hatari siku hiyo maeneo ya ofisini sehemu ambayo ndiyo kilikuwepo kituo chake cha kupigia kura.

Siku hiyo ya uchaguzi mkuu, nadhani ili wahusika wa tukio waweze kumu-identify kirahisi mhusika, alijikuta ameambatanishwa na mtoto wa mojawapo wa wagombea uraisi; na hivyo mtu huyo na mhusika walienda na pamoja kwenye sehemu ya kupigia kura, wakapiga kura wakiwa pamoja; na wakati mtu huyu anataja majina yake kwa wasimamizi wa uchaguzi, alitaja majina yake ya ubini yakiwa yanawaiana sawia kabisa na majina ya mmojwawapo wa wagombea uraisi yaliyokuwa yameandikwa kwenye karatasi za kupigia kura ya uraisi

Zaidi ni kuwa mhusika na mtu huyu wanafanamiana siku nyingi nyuma; ni mwanafunzi wake aliwahi kumfundisha Makongo Sekondari mwaka 1999. Details zaidi za tukio hili mhusika anaziwithhold

Vile vile ilipofika February 2016, mhusika aliletewa barua ya kufutiwa tuhuma zilizokuwa zikimkabili tangu Mei 2014; kutoka uongozi wa juu wa taasisi

Tofauti na ilivyo kwa barua zingine zote ambazo huwa analetewa na kuzikuta zikiwa zimewekwa kwenye pigeon hole yake, hii ya wakati huo ilikabidhiwa kwake na Mkuu wa Idara; ambaye tayari alikuwa ana siku kadhaa ofisini tangu arudi ofisini baada ya kutokuwepo kwa kipindi kirefu cha zaidi ya miezi mitatu; alipokuwa yupo anauguza jeraha lile la kudondoka kutoka ghorofa ya kwanza

Barua hiyo ilikuwa pia imemwelekeza mhusika aende akamuone “SPECIALIST” na kwa sababu iliyokuwa imetajwa kuwa ni “medical treatment”. Barua ilikuwa imeelekeza, haikuwa imeshauri

Katika kuishangaa barua hiyo ambayo yeye aliiona ikiwa imebeba mambo makubwa mawili kwa wakati mmoja, moja likiwa sahihi kama anavyolifahamu yeye na lingine likiwa siyo:

  • Mhusika alimjulisha Mkuu wa Idara aliyemkabidhi barua kuwa angependa kuijibu kwanza barua hiyo ili aulize kuwa hiyo “medical treatment” ni ya ugonjwa gani; ukizingatia kuwa mhusika huwa akiugua sana ni kichwa tu cha panadol au koo linalotokana na mashambulio ya kutokea kule kanisani kwake
  • Mkuu wa Idara alimshauri mhusika kuwa hakuna haja ya kuijibu barua hiyo; na alisisitiza sana kuwa mhusika asiijibu barua hiyo
  • Mhusika naye baada ya kuona kuwa swala kubwa tayari limeshakuwa resolved kwenye barua hiyo, ambazo zilikuwa ni tuhuma, aliamua kui-ignore hiyo discrepancy; akajua pengie labda ni ilikuwa ni mojawapo tu ya code ambazo wakati mwingine, wakubwa huwa wanazitumia kwa surbodinates wao
  • Baada ya siku hiyo kupita, mhatimaye mhusika alirudi tena kwa “SPECIALIST” na kuanzia pale wakaanza kufanya mazungumzo na “SPECIALIST” kuhusiana na yale maswala ambayo zaidi ya nusu mwaka uliopita, “SPECIALIST” aliwahi kumuita mhusika ili wayaongee
Baada tu ya maongezi hayo kuanza, Mkuu wa Idara aliyemkabidhi mhusika barua alihamishwa idarani na kupelekwa utawala ambako ndiko aliko mpaka muda huu

KUHUSIANA NA NENO “MEDICAL TREATMENT” LILILOKUWA KWENYE BARUA ILIYOFUTA TUHUMA ZA MHUSIKA

Kwa dhana aliyonayo sasa hivi mhusika, inaonekana kama waliokuwa wanamuona mhusika akiwa anafanya maongezi na “SPECIALIST”, walikuwa wanajulishwa kuwa mtu huyo ana matatizo ya kisaikolojia na hivyo anafanyiwa counseling na “SPECIALIST”. Hii iliwekwa hivi ili watu wengine wasiweze kujua ni nini hasa kilichokuwa kinaendelea kati ya mhusika na “SPECIALIST”

Mbali na hilo, kwenye kipindi hicho hicho cha maongezi yao, kuna siku moja mhusika aliwahi kukumbatana na kitu kingine pia kutoka kwa “SPECIALIST”. Wakiwa pale katikati wakati wanaendelea na mazungumzo yao

  • Kuna siku “SPECIALIST” aliwahi kumpigia simu mhusika na kumuomba mhusika amtumie hela “SPECIALIST” haraka kwa njia ya simu; alikuwa mahali fulani mbali safarini na gari lake lilikuwa limepata hitilafu.
  • Kwa bahati mbaya mhusika akawa hana hela kwenye simu kwa wakati huo na alimshauri “SPECIALIST” kama angeweza kusubiria kidogo mhusika aende Benki kwanza akachukue ili amtumie
Baada ya pale mawasiliano kati yake na “SPECIALIST” yaliadimika na hivyo siku hiyo wakawa wameishia pale. Mhusika alijilaumu sana kwa nini hakuwa na hela kwenye simu siku hiyo

Hata hivyo, baada ya siku hiyo, ilipofika mwaka 2018 huku maongezi yao yakiwa tayari walishafikia tamati tangu Septemba 2016, siku moja mhusika aliamua kupita ofisini kwa “SPECIALIST” na kumpatia hela laki tatu kwa jumla, kama shukrani tu kwamba waliwahi kufanya naye mazungunumzo muhinu. Alipita mara ya kwanza akamwachia laki mbili cash, halafu tena baada ya siku kadhaa, akapita na kumwachia laki moja; cash

Kumbe kitendo hiki cha mhusika ndiyo sasa kwa wakati huo, kika-cement issue ya kwamba mhusika aliwahi kufanyiwa counseling na hivyo hela hizo alizompelekea “SPECIALIST” yalikuwa ni malipo kwa ajili ya huduma ya counseling ambayo mhusika aliwahi kufanyiwa na “SPECIALIST” siku za nyuma

………………….inaendelea
 
………………….inaendelea

BAADHI YA YALIYOKUWA TAYARI YAMESHATOKEA HADI KUFIKIA SEPTEMBA 2017


Kwa hiyo, February 2015 Mkuu wa Idara aliyekuwepo kwa wakati huo alihamishwa na nafasi hiyo kuchukuliwa na mwingine ambaye alikaa hadi mwaka 2020 na hatimaye naye kumpisha mkuu mwingine ambaye ndiyo yupo mpaka muda huu

Mbali na hayo Jumamosi ya tarehe 10/09/2016 lilitokea tetemeko la Kagera

  • Kesho yake J3 karibia watu wote hawakuwepo ofisini; baadhi walikuwa tayari walishaenda likizo na wengine field, na wengine kama wawili hivi walielekea Kagera kwa ajili ya kupima uharibifu wa kijiolojia uliokuwa umesababishwa na tetemeko hilo
  • Mhusika alikuwa amebaki ofisini na baadhi tu ya wafanyakazi wachache sana akiwemo Katibu Muhtasi wa wakati huo, wa Mkuu wa Idara.
  • Mhusika alikoswa koswa na tukio jingine la hatari safari hili KWA MARA YA KWANZA, LIKIWA LIMEKUWA ADMINISTERED NDANI YA JENGO LA OFISI. Details za tukio hilo tayari alishawahi kuzileta humu jukwaani siku za nyuma
Kwa kifupi tu ni kwamba, kila anachojaribu kukielezea kwenye post ya siku hii ya leo, tayari alishawahi kukitolea maelezo ya kina huko nyuma, isipokuwa tu kwa sasa anajaribu kuyarudia maelezo yake kwa kifupi, AKIYAHUSIANAISHA NA SAFARI YA KIOFISI YA KIGAMBONI AMBAYO ALITAKIWA AIFANYE MNAMO SEPTEMBA 2017

Matukio haya yote yakiwa sasa tayari yameshatokea, ikiwa ni pamoja na mengine mengi ambayo mhusika hajayaelezea humu; ndiyo sasa ulifuata ule Mkutano wa Kimataifa wa Septemba 2017 ambao uliambatana na safari ya field ya siku moja maeneo ya Kigamboni

Ikumbukwe kuwa hadi kufikia muda huo, mhusika alikuwa hajawahi tena kule kusafiri hata nje tu ya Dar es Salaam; na alikuwa miaka zaidi ya miaka mitano (5) bila kuwa amesafiri

BAADHI TU (MENGINE) YA MUHIMU YALIYOJIRI WAKATI WA MKUTANO HUO

Wakiwa kwenye mkutano huo ambao ulikuwa unafanyikia kwenye jengo la Idara nyingine (haukufanyikia kwenye jingo la idara ambayo Boss X na mhusika wanafanya kazi)

  • Kwenye mojawapo ya siku Boss X aliwahi kum-prompt mhusika kwa kumuomba afanye kitu kwenye chumba walichokuwa wanatumia na ambacho kilimtia mashaka makubwa; tena alimuomba mbele ya washiriki wote wa mkutano huo
  • Boss X alimuomba mhusika kufanya hivyo kwa sababu ulikuwa ni wakati wa lunch, na yeye mhusika kawaida huwa siku hali mchana; huwa anakula jioni
  • Kitu alichomuomba Boss X mhusika afanye, hakikuwa na kasoro isipokuwa kilikuwa redundant na ambacho katika hali ya kawaida, mtu mwenye akili timamu hawezi kufakinya namna hiyo
  • Mbali na hivyo, assuming mhusika angeamua kukifanya, kilikuwa kinapelekea abaki peke yake ndani ya chumba hicho cha mkutano
  • Kabla ya siku hiyo, huko nyuma tayari kulikuwa kumeshafanyika attempts kadhaa za baadhi ya watu ofisini, kum-trick mhusika ili abaki peke yake kwenye ofisi ambazo yeye ni mgeni
  • Trick hizi zilikuwa zinafanyika pindi mhusika alipokuwa ametokea kupeleka shida au hitaji msaada kwenye ofisi nyingine ambayo si yake
  • Baada ya kuona hivyo, mhusika alianza kuwa extra-ordinary sensitive pindi alipokuwa anainbia kwenye ofisi za watu wengine tofaut na ile ya kwake
  • Boss X alitumia trick hii kwa kujua kuwa ingweza kum-excite mhusika na kumuweka katika hali ya kuzila, ili asiende lunch na wageni, na vile vile pia asiendelee kubaki pale ofisini, na badala yake akakae kule idarani kwake ofisi yake ilipo, akiwasubiri wageni warudi kutoka lunch
Katika kujaribu kujibu hoja ya Boss X, mhusika alisema kuwa kwa siku hiyo na yeye alikuwa anapendelea kwenda lunch ili kuwapa kampani wageni na kweli alienda lunch

Hata hivyo, mtego haukuwa kwenye chumba hicho walichokuwa wanatumia wakati wa mkutano

Boss X alikuwa ametarajia kuwa kwa kumuomba mhusika kubaki ndani ya chumba hicho

  • Atapata wasiwasi wa kubaki kwenye chumba hicho peke yake, na hivyo kuamua kwenda kwenye chumba kingine, most probably, ofisini kwake idarani ambako mkutano ulikuwa haufanyikii
  • Hii ni kwa sababu mhusika huwa hali mchana.
  • Kwa hiyo uwezekano mkubwa wa uamuzi wake pengine ungekuwa ni kuamua kutoka kwenye chumba hicho cha mkutano na kurudi kwa muda Idarani ofisini kwake akisubiria washiriki wa mkutano watoke lunch halafu na yeye ndiyo akawa-join tena
Kwa hiyo siku hiyo, set-up ilikuwa imewekwa ofisini kwake, kule Idarani ambako mkutano haukuwa unafanyikia.

Na ndiyo maana huu ulikuwa ndiyo mkutano pekee kati ya mikutano yote iliyowahhi kuwa hosted kweye taasisi hii husika, ambao uliwahi kufanyikia kwenye idara nyingine ambayo si ile wanayofanyayia kazi mhusika na Boss X

Hata hivyo kwenye idara hiyo ambako mkutano huo ulifanyikia, kuna mtu ambaye ni very qualified kwenye haya mambo ya electronics na ndiye ambaye huwa anahusika na ku-service vifaa vyote vya matetemeko. Kabla ya wiki ya mkutano huo, mtu huyu alikuwa ameutumia muda wote wa weekend siku zote mbili za Jumamosi na Jumapili za wiki iliyokuwa imepita nyuma ya wiki ya mkutano huo, akifanya kazi akiwa ofisini kwa mhusika, funguo za ofisi akiwa amepewa na Boss X ambaye naye pia huwa ana kopi ya ufunguo wa ofisi hiyo

MSHIRIKI MMOJA MGENI AMBAYE ALIKUWA ANAONEKAMA KAMA AMEHUDHURIA MKUTANO HUO KIMAKOSA

Katika washiriki wote waliokuwepo kwenye mkutano huo, kuna mmoja ambaye alikuwa ametoka nchi jirani, na ambaye alikuwa anaonekana kuwa na wasiwasi kama vile amehudhuria mkutano huo kimakosa. Wakati wa break kama vile chai, mara kadhaa alikuwa anaonekana kuteta na Boss X as if anatafuta ushauri fulani

Baadhi ya sifa za mshiriki huyu zilikuwa kama ifyuatavyo

  • Alikuwa mrefu,body well built
  • Umri kati ya miaka 32-36
  • Alikuwa kabisa hajui chochote kilichokuwa kinafanyika mwenye mkutano huo
  • Kutokana na hali hiyo, alikuwa mara nyingi anatumia smart phone kupiga picha screen ya mtu aliyefanya kazi kwenye software ambayo washiriki wa mkutano huo walikuwa wanatumia, halafu na yeye ndiyo anarudi tena kwenye kompyuta yake na kwenda kuanza kujaza kwenye software aliyoifungua, kwa kutizamia kile alichokuwa amepiga picha na ambacho alikuwa ameshajua kuwa kilikuwa sahihi
Kwa ujumla tu kuna mambo mengi sana yaliwahi kutokea kwenye mkutano huo, hali iliyopelekea baada ya mkutano huo kumalizika, mhusika kuomba kuongea na Mkuu wa Idara

  • Bahati mbaya Mkuu wa Idara alikuwa amesafiri, na alikuwa hajarudi kutoka safari
  • Kwa wakati huo, kulikuwa na mwingine ambaye alikuwa ameachiwa ku-act, (wa kwanza) ambaye naye pia alikuja kusafiri na kumwachia acting mwingine tena (wa pili)
  • Siku safari ya Kigamboni inafanyika, kulikuwa na acting yule wa kwanza
Acting huyu wa kwanza ni mmojawapo wa wale wachache ambao walikuwepo idarani kwa wakati huo, waliowahi kusomea matetemeko ya ardhi, kama alivyo Boss X

……………………..itaendelea
 
UPDATE: MONDAY 13TH JUNE 2022

By the way
: SAHIHISHO MUHIMU KWENYE TAARIFA ILIYOKO HAPO JUU


Vitendo vya mhusika kushushwa cheo na hatimaye kukatwa mshahara vilifanyika mwaka 2014 na si 2012

BAADHI TU YA YALE AMBAYO YALIYOKUWA TAYARI YAMESHATOKEA HADI KUFIKIA SEPTEMBA 2017; KABLA YA KUWADIA SIKU YA SAFARI YA KIKAZI YA KWENDA KIGAMBONI

………………….inaendelea
 
SIKU YA SAFARI FIELD YA KIGAMBONI

Siku hiyo lilipowadia, Boss X aliwajulisha wageni kutoka nje ya nchi kwamba ilikuwa ni siku nzuri pia ya wao kwenda kuliona daraja la Kigamboni. Ikumbukwe kuwa wakati mhusika anakwepa kwenda Kigamboni mwaka 2010 kwa safari binafsi, daraja la Kigamboni lilikuwa bado halijajengwa na hivyo halikuwepo

Siku hii ya safari ya field ya kikazi ilipowadia, mhusika alienda akamuona Kaimu Mkuu wa Idara na kumuomba amruhusu yeye asiende Kigamboni mkuu huyo hakuona tatizo aliridhia, na hivyo mhusika hakwenda Kigamboni siku hiyo

Ikumbukuwe pia kuwa tangu March 2013, mhusika alikuwa ameshauandikia uongozi wa juu wa taasisi akiuomba umruhusu kutokusafiri nje ya Dar es Salaam, na hivyo nje ya nchi pia. Hata hivyo, safari hii ya Kigamboni ilikuwa ni ya ndani ya Dar es Salaam na hivyo ilihitaji ridhaa ya mkuu wa kazi wa mhusika kuridhia kwa yeye (mhusika) kutokwenda Kigambon siku hiyoi

MENGINE KADHAA YA MUHIMU YALIYOJIRI WAKATI WA MKUTANO HUO WA KIMATAIFA, UKIONDOA LILE LA MSHIRIKI ALIYEKUWA ANAFANYA KAZI KWA KUPIGA PICHA SCREEN ZA COMPUTER


Kuna mambo mengine kadhaa ya muhimu yaliwahi kujiri wakati wa mkutano huo, na ambayo yalihusisha set-up ya Boss X pia kwa maana kwamba yalitokea baada ya yeye kuwa amenuia yatokee kama yalivyotokea

MAELEZO YA UTANGULIZI

MAELEZO MUHIMU KUHUSIANA NA MTOTO (BINTI) RAFIKI YAKE NA MHUSIKA ALIYEKUWA ANAFANYA KAZI KWENYE JENGO ILIMO OFISI YA MHUSIKA KIPINDI HICHO


Huyu binti alikuwa ni mtoto wa miaka inayozidi kidogo 20, kwa kipindi hicho

  • Alikuwa ni mfanyakazi wa kampuni ya usafi iliyokuwa inafanya kazi kwenye jengo ilimo ofisi ya mhusika
  • Alipofika idarani kwa mara ya kwanza, mojawapo ya ofisi alizokuwa anahudumia ni ile ya mhusika
  • Kutokana na hali hiyo, mhusika na binti huyu walitokea kuzoeana sana na hatimaye kuwa marafiki, huku wakiitana babu na mjukuu
Zaidi ni kuwa binti huyu anatokea kanda ile maalumu ambako mhusika aliwahi kuishi kwa mwaka mmoja akiwa JKT, na hatimaye kuondoka huko akiwa ametengeneza marafiki kadhaa ambao huwa anakuwakumbuka hadi leo, hajawasahau. Kwa hiyo naturally, mhusika huwa mara nyingi anapenda kutengenesza urafiki na watu wanaotoka mkoa anaotokea huyu binti

KILICHOTOKEA PINDI MKUTANO HUU WA KIMATATIFA ULIPOKUWA UNAENDELEA. BINTI HUYU AKIWA MMOJAWAPO WA WAHUDUMU WA BITES ZA CHAI YA SAA 4;00 ASUBUHI NA SAA 10:00 JIONI

Asubuhi moja kwenye mojawapo ya siku za mkutano huo, binti huyu na wenzake walifika wakiwa wamebeba bites, asubuhi saa mbili kabla hata ya mkutano kuanza

  • Siku hiyo, ilikuwa ni siku ya tatu au ya nne tangu siku ya kwanza ya kuanza kwa mkutano huo
  • Bites hizi waliziwahisha na kuzihifadhi sehemu muhimu ya karibu ili wakati wa chai utakapofika, waweze kuzihudumu kutokea pale karibu badala ya kutokea kule ambako zilikuwa zinanaandaliwa,; na mhusika alibahatika kuziona bites hizo (kwenye malaji husika huwa hapitwi na kitu na hilo ndiyo tatizo lake la siku zote)
  • Mojawapo ya bites hizo vilikuwa ni VITUMBUA; na mara zote mhusika anapenda vitumbua.
  • Pasipo yeye kuwa anajua, kumbe kuna baadhi ya watu wengine nao ambao nao pia walishajua kuwa mhusika huwa anapenda vitumbua
Muda wa chai ya saa 4:00 ulipofika, washiriki walizikuta bites na chai vikiwa tayari vimeshaandlaiwa mezani, huku wahudumu wa mlo huo wakiwa hawapo, walikuwa tayari wameshaondoka

  • Ilikuwa ni kawaida yao siku zote kuandaa mlo huo kwa mtindo huo
  • Hata hivyo, haikuwa kawaida yao kuzitanguliza bites hizo asubuhi sehemu ya ukumbi ambapo mkutano ulikuwa unafanyikia
  • Siku wanazitanguliza bites, ilikuwa ni mara ya kwanza kwa wao kufanya hivyo na ndiyo maana mhusika aliziona
Washiriki wa mkutano walipoanza kunywa chai, mhusika aligundua kuwa VITUMBUA havikuwepo tena na alishangaa

  • Baada ya kuvikosa VITUMBUA, ikabdi mhusika ampigie simu rafiki yake kumuuliza VITUMBUA vilienda wapi
  • Binti rafiki alimjibu mhusika kuwa vitumbua vilikuwa ni kwa ajili ya chai ya saa 10:00 na ndiyo maana hawakuviandaa kwa chai ya muda huo
Maongezi ya mhusika na rafiki yake yakaishia hapo; ila kikubwa kilichofanyika hapa ni kwamba mhusika alimpigia simu binti, kwa mara ya kwanza ndani ya wiki hiyo ya mkutano

MHUSIKA ALAZIMIKA KUMPIGIA TENA SIMU BINTI KWA MARA NYINGIE YA PILI


Mhusika hakumbuki vizuri ila anadhani ilikuwa ni kwenye siku iliyofuata; ambapo kuna mazingira mengine yalijitokeza tena na hivyo kuepelekea mhusika ampigie tena simu binti, kwa mara ya pili sasa

Hii ilikuwa ni baada ya Boss X kumuomba mhusika amweleze binti huyo apeleke funguo za ukumbi wa mkutano alizokuwa amezichukua; kwa Boss X ili Boss X aweze kufungua ukumbi huo

Binti huyu alizichukua funguo hizi baada ya chai ya saa, baada ya umeme kuktaika wakati wa chai ya saa 4

Wakati binti anakuja kukusanya vifaa vyake vilivyokuwa vimetukika kwa ajili ya chai ya saa 4 ili akavifanyie usafi, washiriki wote wa mkutano walikuwa wametoka nje ya ukumbi na hivyo wakati anatoka hapo ukumbini, ilibidi afunge ukumbi na pia kuondoka na funguo za ukumbi huo. Kitendio hicho cha binti kuondoka na funguo, ndicho baadaye kilipelekea Boss X amuombe mhusika ampe ujumbe binti uliohusiana na funguo za ukumbi huo

KILICHOPELEKEA BOSS X KUMUOMBA MHUSIKA AMPATIE UJUMBE BINTI

Mkutano ukiwa unaendelea siku hiyo, wakati wa chai ya saa 4:00 umeme ulikatika, na HAPAKUWA NA STANDBY GENERATOR kwenye jengo hilo ambalo ukumbi wake ulikuwa unatumika na mkutano huo

Kwenye harakati za kujaribu ukumbi mwingine ambao ulikuwa una STANDBY GENERATOR, mhusika na Boss X wakashauriana na kuamua waende kwenye kitengo cha mambo ya ICT kilichopo kwenye taasisi hiyo, ambacho muda jengo huwa linakuwa na umeme.

Meanwhile, as a precaution, Boss X naye akaamua aende pia kwenye kitengo kingine kinachhusika na mambo ya walimu, akaangalie ukumbi mwingine huko

Wawili hawa wakatawanyika, mhusika akaenda kule ICT, na huko alienda akapata ukumbi mara moja pasipo tatizo lolote

Baada ya kupata ukumbi, mhusika akampigia simu Boss X kumweleza kuwa ukumbi umepatikana

Baada ya mashauriano dakika kadhaa, huku simu ya Boss X ikipatikana kwa kukatika katika, Boss X alimjulisha mhusika kuwa kuna ukumbi mwingine tena jengo jirani,(directly opposite, upande wa pili wa barabara) ambao ulikuwa umepatikana

Ukumbi huo alioupata Boss X, ulikuwa ukumbi mwingine wa pili kwenye Idara ile ile ambayo mkutano huo ulikuwa unafanyikia

Baada ya hapo, mhusika alirudi na alipofika kwenye ukumbi wa awali ambapo alikutana tena na Boss X, hapo ndipo set-up nyingine ya pili iliyosababisha mhusika ampigie simu binti, ilipoanzia. Wakati huo umeme ulikuwa bado haujarudi

WALICHOONGEA BOSS X NA MHUSIKA WALIPOKUTANA PALE NJE YA UKUMBI WA AWALI AMBAO HAUKUWA NA STANDBY GENERATOR

………………….inaendelea
 
………………….inaendelea

WALICHOONGEA BOSS X NA MHUSIKA BAADA YA KUKUTANA PALE NJE YA UKUMBI WA AWALI AMBAO HAUKUWA NA STANDBY GENERATOR


Walipokutana nje ya ukumbi huo, mhusika akiwa anatokea kwenye harakati za kutafuta ukumbi kwenye kitengo cha ICT, Boss X alimuuliza mhusika kuwa kwa muda huo alikuwa anataka kuelekea wapi

  • Mhusika alimjulisha Boss X kuwa anaelekea idarani kwa muda, akisubiria matayarisho ya ukumbi mpya uliokuwa umepatikana jengo jirani
  • Boss X alimuomba mhusika huko idarani akamjulishe binti rafiki kuwa funguo za ukumbi zinahitajika na hivyo azilete kwake Boss X kwa sababu ni yeye (binti) aliyekuwa amefunga ukumbi na kuondoka na funguo hizo
  • Mhusika aliipokea taarifa hiyo na kuanza kuelekea idarani
  • Alipofika idarani, mhusika hakumkuta binti, hakuwepo idarani
  • Taarifa zikasema kuwa alikuwa ameenda jengo jingine jirani, almost opposite na jengo la idara ila upande wa pili ng’ambo ya barabara
MHUSIKA AAMUA KUMPIGIA TENA BINTI SIMU; (KWA MARA YA PILI SASA NDANI YA WIKI HIYO MOJA)

Mpaka hapa sasa mhusika akaanza kujaribu kumtafuta binti kwa simu lakini aidha simu ilikuwa haipatikana au ilikuwa haina majibu, hakumbuki vizuri kuhusu hili. Still, funguo hizi zilikuwa bado zinahitajika kwa sababu vifaa vya washiriki wote vilikuwa bado vimo kwenye ukumbi ule wa awali, na ilibidi wahame navyo kwenda kwenye ukumbi ule mwingine uliokuwa umepatikana jengo jirani

BAADA YA MHUSIKA KUSHINDWA KUMPATA BINTI KWA NJIA YA SIMU

Mhusika aliamua kwenda kwenye jengo lile ambalo alielekezwa kuwa binti alikuwa ameelekea, haikuwa mbali, ilikuwa ni ng’ambo ya pili tu ya barabara

Mhusika akiwa yupo nje anataka aelekee kwenye jengo hilo, alimuona SENIOR STAFF MMOJA MWANAUME ALIYEKUWA AMESIMAMA NDANI YA OFISI USAWA WA DIRISHA LILLILOKUWA LIKO WAZI KWENYE GHOROFA YA KWANZA YA JENGO HILO

  • Kwa sababu jengo haliko mbali sana, badala ya mhusika kukatiza barabara na kwenda kwenye jengo hilo, aliamua kuongea na staff huyu akimuuliza kama huyo binti mhitajika alikuwepo kwenye jengo hilo
  • Staff huyu alijibu kuwa ni kweli binti huyo alikuwepo muda siyo mrefu ndani ya jengo hilo, ila kwa wakati huo alikuwa tayari ameshaondoka tena na kurudi kule kwenye ukumbi wa mkutano
Mpaka hapa mhusika akaamua kumpigia tena simu Boss X akimweleza kuwa binti alikuwa tayari amesharudi huko kwenye ukumbi lakini Boss X alijibu kuwa hakuwepo huko na hivyo ukumbi ulikuwa bado umefungwa

Baada ya hapo, mhusika aliamua kumpigia tena binti rafiki

  • Safari hii binti rafiki alipatikana kwenye simu
  • Zaidi binti rafiki alijibu kuwa ni kweli hakuwepo kwenye ukumbi wa mkutano ila alikuwepo jengo la KEMIA, ambalo ni jengo jingine jirani kabisa na lile lenye ukumbi ule mpya ambao ulikuwa umepatikana
Baada ya hapo washiriki walihamisha vifaa vyao na mkutano kuanza kuendelea kwenye ukumbi mwingine hadi siku ya mwisho ulipomalizika

TUKIO JINGINE MUHIMU LILILOTOKEA SIKU HIYO HIYO; SIKU AMBAYO MHUSIKA ALIKUWA AKIPIGA SIMU ZA MARA KWA MARA ZIKIELEKEA KWA BINTI RAFIKI

Kwenye siku hii, ndiyo ile pia ambayo Boss X aliamua kumuomba mhusika abaki kwenye ukumbi huo, na afanye kitu ambacho hakikuwa cha lazima sana

Boss X alimuomba mhusika afanye hivyo wakati wa lunch break, washiriki wengine wote watakapokuwa wameenda lunch.

Hii ni kutokana na ukweli kuwa Boss X alijua kuwa mhusika huwa haendi lunch

  • Mhusika kwa kuzingatia mlolongo wa matukio yaliyokuwa yametokea asubuhi siku hiyo, alilazimika na yeye kuwa-join wageni kwa ajili ya lunch; hakuwa tayari kubaki peke yake kwenye ukumbi huo siku hiyo
  • IHakuwa tena na nerve za kumuwezesha kubaki kwenye chumba hicho kipya akiwa yuko peke yake; na wala hakuwa tayari kurudi idarani ofisini kwake na kwenda kukaa humo akiwasubiria washiriki wenzake warudi kutoka lunch
Kwa siku zote zilizokuwa zimepita nyuma, ilikuwa kila wenzake wakienda lunch, yaye alikuwa anarudi ofisini kwake idarani na kuanza kufanya kitu kingine. Baada ya lunch, nndiyo alikuwa anarudi tena ukumbini kwenda kujiunga na washiriki wenzake na kuendelea na mkutano

HITIMISHO

Taarifa zaidi kuhusiana na ombi hili la Boss X kwa mhusika siku hiyo; (kwenye muda wa lunch) tayari mhusika alishalitolea maelezo yake kwenye siku ya kwanza kabisa alipokuwa anaanza kutoa taarifa hizi zinazohusiana na SAFARI MBILI ZA KUELEKEA KIGAMBONI

Mojawapo ya sababu nyingine kubwa iliyopelekea asiende kukaa idarani ofisini kwake siku hiyo (tofauti na ilivyokuwa kawaida yake kwa siku zingine zote za mkutano zilizokuwa zimepita nyuma ya siku husika) na badala yake kuamua kwenda luch, alikuwa ni yule mfanyakazi mtaalamu wa electronics, ambaye alikuwa amefanya kazi ndani ya ofisi ya mhusika kwa siku mbili za weekend kufuatia J3 ya wiki ya mkutano huo

Mbali na hilo, ukumbi huu mwingine wa pili uliokuwa umepatikana baada ya umeme kukatika, ulikuwa upo kwenye jengo moja japo sakafu tofauti, na ilimo ofisi ya mfanyakazi huyu mtaalamu wa electronics,

Simu za mara kwa mara za mhusika kwenda kwa binti rafiki, ilikuwa zitumike kama ushahidi kuwa mhusika na binti hawakuwa marafiki wa kawaida tu, bali wapenzi pia

PICHA ILIYOKUWA IMEKUSUDIWA KUONEKANA KATI YA MHUSIKA NA BINTI RAFIKI


Alichokuja kuiona dhahiri baadaye kuwa kilikuwa kimepangwa na Boss X, ni kwamba kuna tukio baya lilitakiwa kumpata mhusika siku hiyo, na baada ya hapo binti rafiki alitakiwa sasa kuja kuwa shahidi wa tukio hilo baya.

Binti rafiki angekuja kutoa ushahidi kuwa yeye na mhusika walikuwa si marafiki tu wa kawaida bali wapenzi pia. Binti rafiki angeenda pia mbele zaidi kwa kuongeza kuwa ndani ya siku za hivi karibuni kuna mahali fulani wametokea kuhitilafiana na hivyo binti rafiki kuamua kusitisha mapenzi na mhusika, na baada ya hapo mhusika sasa naye kuamua kuchuka maamuzi ambayo matokeo yake yangekuwa ndiyo hayo ambayo binti rafiki wa mhusika angekuwa anatumika kushuhudia

“Mfanyakazi mtaalamu wa electronics hapa angekuwa ameshakamilisha set-up yake na Boss X wakishirikiana na binti rafiki wa mhusika”

Mpaka sasa hivi, binti huyu bado ni rafiki yake na mhusika na huwa (binti) anamtembelea mhusika ofisini kwake pindi inapotokea amepata muda wa kufika ofisini. Binti rafiki alishaacha kazi kipindi kirefu nyuma; baada ya kuwa amejiunga na masomo ya Elimu ya juu mwaka 2018 ambapo mpaka muda huu; tayari alishahitimu masomo yake ya shahada ya kwanza

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE: TUESDAY 14TH JUNE 2022

KWA UTAFITI WAKE MHUSIKA (WA MIAKA KADHAA SASA)

KILE KINACHOFANYIKA BAADA YA MADHABAHU KUWA IMESHAMBULIWA KWA NJIA YA “MTUMISHI KUTAMKA MANENO MACHAFU AKIWA AMESIMAMA MBELE/ MADHABAHUNI’

MAELEZO YA UTANGULIZI


Kwa wasomaji wa siku zote, wanaombwa warejee baadhi tu ya taarifa kwenye baadhi tu ya post kama vile hizi hapa: #91 , #196, #639 , #845

NAMNA AMBAVYO MADHABAHU HUWA INABADILIKA NA KUWA; BAADA YA KUWA IMESHAMBULIWA

  • Madhabahu ikishashambuliwa, huwa inabadilika kiasi kwamba kila neno linalotamkwa kutokea kwenye madhabahu hiyo huwa linageuka na kuwa AIDHA NI SHAMBULIZI KAMILI AU NUIO LA MASHAMBULIZI kwa muumini yeyote yule anayesikia neno hilo
  • Na kwa sababu neno hilo linakuwa ni SHAMBULIZI KAMILI AU NUIO LA MASHAMBULIZI; neno hilo linaweza sasa kuanzia pale, kumshambulia muumini au kutokumshambulia, kutegemea na jinsi alivyosimama kiimani au kulingana na alivyokomaa kiimani.
Chances kubwa ni kwamba walio wachanga kiimani na wale ambao wanakuwa hawajasimama vizuri kiimani, manuio kama hayo lazima yanakuwa na madhara makubwa sana kwao na mara nyingi wanakuwa ndiyo wahanga wa mashambulio ya aina hiyo

Kwa kifupi tu ni kwamba, madhabahu ikishashambuliwa, inaanza kutumika kama source ya kurusha mapepo kwa kila kitu ambacho neno linalohusu kitu hicho, linakuwa limetamkwa kutokea madhabahu hiyo

Hapa kitu cha kukumbuka ni kuwa mechanism hii ya urushaji mapepo kutokea madhabahuni, huwa inawezekana tu pale ambapo madhabahu inakuwa imeshashambuliwa kwanza

Kwa hiyo madhabahu ikishashambuliwa kwanza, hata Maandiko Matakatifu yanayotamkwa kutokea madhabahu hiyo yanageuka na kuwa mashambulizi kwa waumini.

Mbali na hivyo, kila jina la kitu chochote kile ambacho kinaweza kutamkwa kutokea madhabahuni, kitu hicho lazima kivamiwe na pepo, iwapo tu hakikuwa kimewahi kuwekwa wakfu kwa Bwana hapo awali. Kwa mfano, KANISA JIPYA LA KANISA A a.k.a “JENGO JIPYA” HALIJAWAHI KUWEKWA WAKFU KWA BWANA

Hivyo basi, madhabahu inapokuwa tyari imeshashambuliwa; mtumishi wa Mungu akisimama kwenye madhabahu hiyo halafu akataja tuseme kwa mfano:

  • Kalamu, lazima kalamu zote ambazo hazijawekwa wakfu zichukue mapepo;
  • Ipad/ Tablet lazima Ipad/ Tablet zote ambazo hazijawahi kuwekwa wakfu zichukue mapepo, n.k
  • Na orodha ni ndefu na vingine tu labda kwa ufafanuzi zaidi ni kama vifuatavyo
  • Miwani ya macho ya kusomea…………………..
  • Sketi za bluu za watoto wa shule ya msingi……..
  • Kaptula za bluu za watoto wa shule……………..
  • Mashati meupe ya watoto wa shule za msingi……………………….
  • Mapazia (hayo tuyaache…..) (alisema hivyo KM-A J2 ya terehe 05/06/2022 baada ya kuwa ametamka mapazia, yalifuatiwa na neno “hayo tuyaache”
  • Vijiko vya kulia chakula…………………………..
  • Sahani……………………………….
  • Vikombe……………………………..
  • Sabuni za kuogea………………………………
  • Mafuta ya mgando ya kupaka…………………
  • Mafungu au maneno ya kwenye Biblia kwa mfano:
  • Kufafanusha maneno yako kwatia nuru na kumfahamisha mjinga (Zaburi 119:130)
  • …..Yesu alifanyika dhambi
  • …Yesu alifanyika laana
  • …Yesu anamwambia Petro kuwa yeye (Yesu) ni mwamba ambapo atalijenga Kanisa lake

Mhusika hana uhakika sana lakini anadhani kuwa neno hili lilirudiwa tena na mhubiri wa J2 iliyofuata ya tarehe 05/06/2022 wakati anafundisha somo wakati wa Ibada kuu. Uhakika zaidi katika hili hana, ila anadhani kuwa alisikia neno hilo likitamkwa. Mhusika atarudisha baadaye mrejesho kuhusiana na neno hili, bado analifanyia kazi jambo hili

Vinginevyo kuna maneno mengine ambayo aliyasikia yakitamkwa na yaliyokuwa yakiendana na fungu la Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanawe wa pekee…….. halafu kuna utani ulifuata ukiwa unasema ‘ili tupate magari, majumba…….n.k.

Katika kusikiliza mkanda, maneno hayo hajaweza kuyapata isipokuwa amepata maneno mengine tu ambayo hayana utani huo ila yanafanana kiasi na hayo na yako kwenye muda kuanzia 1:06:56 na kuendelea mbele kidogo. Kwenye hili nalo pia la mhusika kuyakosa maneno haya wakati aanakiri kuwa aliyasikia, atarudisha mrejesho

Unless kama ni yeye tu mhusika aliyesikia utani huo, ila KAMA KUNA MUUMINI MWINGINE AMBAYE ANAWEZA KUSHUHUDIA KUWA NAYE PIA ALIUSIKIA UTANI HUO, BASI MANENO HAYO YATAKUWA YALITAMKWA!

Na illikuwa ni mara ya pili sasa kwa mhusika kumsikia KM-A akiusema utani huo akiwa anafundisha neno la Mungu; hapo awali alishawahi kuyatamka tena maneno hayo

………………..inaendelea
 
KUHUSIANA NA MAOMBI YA MFUNGO WA “MAJI TU” AMBAO UMEKUWA POPULAR SANA KWA MIAKA TAKRIBANI MITATU SASA

Kama ilivyoelezwa hapo juu; maji yanapotajwa kupitia madhabahu iliyochakachuliwa, maana yake ni kwamba maji hayo yanarushiwa pepo na kumchukua pepo huyo


Mbali na hilo, kuna urahisi zaidi wa kurusha pepo kwenye maji kuliko kwenye chai au chakula kingine chochote kwa sababu “source” ya maji ni ardhi na huwa hayahitaji kuwekewa kiungo kingine chochote kile na mtumiaji baada ya kuwa ameyapata. Mtumiaji yeyote wa maji, huwa anayapokea kama yalivyo na hivyo kuyatumia kama yalivyo pia; na kama kuna chochote kingine anachoweza kuyaongezea, basi ni kuyarekebisha tu joto kidogo kwa kuyaweka kwenye friji au kuyachemsha kwenye jiko

Kwa upande mwingine, chai yenyewe huwa haiko hivyo; yenyewe inatofatiana sana kutoka mlaji mmoja kwenda mwingine na aina ya chai huwa iantegemea pia kipato cha mtu

Kwa hiyo, “uniformity” kutoka mtumiaji mmoja kwenda mwingine ndiyo inayosababisha urahisi wa pepo kurushwa kwenye maji na hatimaye, pepo hilo kum-affect kila muumini aliyefunga na kuamua kutumia maji peke yake kwenye siku husika

Njia mbili kuu ambazo mpaka muda huu, mhusika ameshazibaini kuwa zinatumika zaidi (popular) kurusha pepo ni kama zifuatazo hapa chini

MOJA: Ni kwa kuyatamka “maji” kupitia madhabahu iliyochakachuliwa

Kama hiyo option hiyo ya kwanza haiwezekani; yaani pale ambapo pengine madhabahu inakuwa imegoma kuchakachuliwa; basi pepo hurushwa kwenye ardhi au kwenye udongo;

Baada ya pepo kuwa amerushwa kwenye ardhi, hatimaye huwa anakuwa linked kutokea huko kwenye udongo kuja kwenye maji. Hapa ni kwamba pepo anakuwa hayuko moja kwa moja kwenye maji, ila anakuwa amewekwa kwenye ardhi huku akiwa ana-operate kwenye maji. Pepo wa aina hii huwezi kumtoa kwa kuyatakasa maji; ukifanya hivyo hatoki. Ili uweze kumgtoa, inabidi uitakase ardhi; kule ambako natokea na kuwa linked kwenye maji

MAELEZO YA NYONGEZA KUHUSIANA NA HUU UTARATIBU WA KU-LINK MAPEPO; YANAPOKUWA YAPO SEHEMU A LAKINI YANAFANYA KAZI KWENYE SEHEMU NYINGINE B

MFANO WA KINYESI KILICHOKUWA KIPINDI FULANI KIMEACHWA NA KUWA KINASAMBAZA HARUFU KANISANI WAKATI WA IBADA


Kwa waumini wa Kanisa A watakumbuka kuwa kuna kipindi kulikuwepo na kinyesi ambacho kilikuwa kimeachwa kikiwa kinavuja makusudi kutoka kwenye chemba; na mabacho kwa muda huu, mhusika alishajiridhisha kabisa pasipo shaka kuwa kinyesi hicho kilikuwa kinatumika kama source ya mapepo Kanisani wakati wa Ibada.

Mapepo hao walikuwa wana-operate Kanisani (walikuwa wako linked Kanisani) lakini kutokea kwenye harufu ya kinyesi hicho na hivyo ilikuwa kwa mfano; haiwezekani kuwakemea wakatoka moja kwa moja Kanisani hapo kwa sababu wao walikuwa hawaishi Kanisani bali walikuwa wanaishi kwenye harufu ya kinyesi iliyokuwa ipo Kanisani; wao hawakuwa Kanisani

TUKIRUDI KWENYE SWALA LA URAHISI WA KURUSHA PEO KWENYE MAJI BALI SI KWENYE CHAI

Urahisi wa kurusha pepo kwenye maji unatokana na ukweli kuwa karibia maji yote ambayo huwa yanatumika na binadamu, binadamu huyapata moja kwa moja kutokea sehemu moja tu ambayo ni ardhini. Chakula kingine pia huwa kinatoka ardhini, lakini matumizi yake si ya moja kwa moja kama yalivyo maji. Huu ni utafiti wake mhusika

Kwa hali hiyo, ni maji yaliyokingwa moja kwa moja tu kutoka kwenye mvua inayonyesha yanayoweza kupona kutokana na pepo la aina hii; assuming bati lililotumika kuyapokea na hatimaye kuweza kukingwa kwenye vyombo vya maji, lililkuwa halina pepo au lilikuwa tayarai limeshawekwa wakfu

KILE KINACHOPELEKEA MFUNGO WA MAOMBI “KANISA A” USIWE HATA SIKU MOJA WA CHAI BALI SIKU ZOTE UNAKUWA NI WA MAJI TU

Kinachopelekea hali hiyo ni ugumu wa kurusha pepo kwenye chai kutokana na variety ya ingredients zinazotumika kutengeneza chai; na zinazotofautina kutoka familia moja kwenda nyingine; tofauti na ilivyo kwa maji

  • Kwanza, sukari inayotumika kwenye chai inakuwa imetengenezwa na viwanda tofauti tofauti na inakuwa imetoka sehemu mbali mbali na pengine nyingine inakuwa imetoka hata nje ya nchi
  • Viungo vingine mbali mbali vya ziada vinavyotumika kweye chai kama vile: majani ya chai; kahawa, cocoa, hiriki; tangawizi; mdalasini, n.k.
Kwa hiyo; kwa upande wa chai, inakuwa ni vigumu kurusha pepo kwenye kinywaji hiki kutokana na “heterogeneity” ya ingredients ambazo huwa zinatumika kwenye chai

Kwa hiyo chai inayonyweka na waumini majumbani mwao, inatofautiana sana kutoka nyumba ya muunini moja kwenda ya muumini mwingine, na hivyo kupelelekea ugumu wa kurusha pepo kupitia kinywaji hicho

Kwa upande mwingine, maji yako “homogeneous” na hivyo ukifanikiwa kuwa-restrict waumini wote kunywa maji halafu ukawa umerusha pepo kwenye maji; waumini wote waliokunywa maji pekee kwa siku nzima wanakuwa chini ya influence ya huyo pepo. Na si waumini tu, hata mtu mwingine yeyote yule ambaye kwa bahati mbaya, atatokea kuwa amekunywa maji tu kwa siku hiyo na baada ya hapo, hakubahatika kuweka kitu kingine chochote tumboni zaidi ya maji

Kwa miaka kadhaa sasa, zaidi ya mitatu, maombi yote ya Kanisa A ni lazima yanakuwa na sifa kuu hzi mbili

  • Ya mfungo (hakuna tena maombi ambayo si ya mfungo; hayapo tena siku hizi, waumini walishayasahau siku nyingi)
  • Mfungo wa naji tu
………………..inaendelea
 
KUHUSIANA NA HILI NENO LA YESU KUFANYIKA LAANA/ DHAMBI KWA AJILI YETU

KWA MARA YA TATU MFULULIZO SASA, KM-A NA KIONGOZI MWINGINE KIJANA HUWA WANAJIPANGA KUHUDUMU KWA WIKI MBILI ZINAZOFUATANA MFULULIZO NA KILA MMOJA KUYATUMIA MANENO HAYA


Huyu mwingine; kiongozi junior ambaye alihudumu kwenye Ibada ya pili J2 ya tarehe 12/06/2022; huko nyuma alishawahi hata kuhubiri kwa kutumia kichwa cha somo kilichosema “YESU KUFANYIKA DHAMBI

Kwenye mahubiri ya J2 tarehe 05/06/2022; KM-A aliwaombea watu akiwatamkia kuwa YESU ALIFANYIKA LAANA

Kwenye mahubiri ya J2 iliyofuata ya tarehe 12/06/2022; Kiongozi junior aliyesimama madhabahuni kwa ajili ya kutoa neno J2 hiyo, naye pia alisema kuwa YESU ALIFANYIKA LAANA. Maneno hayo yako kwenye muda wa kuanzia 01:39:00 (saa moja na dakika 39) hadi kufikia muda wa 01:41:00. Muda wa siku ulikuwa ni kati ya saa sita (6) na dakika 16 mchana (12:16PM)

POST YA AWALI YA MHUSIKA KUHUSIANA NA SWALA HILI LA YESU KUFANYIKA DHAMBI/ AU LAANA

Hapo awali mhusika alishawahi kuleta taarifa zinazohusiana na jambo hili humu jukwaani kwamba wawili hawa; huko nyuma walishawahi kujipanga tena kwa mara zipatazo mbili na kila mmoja kutamka maneno yanayoshahibiana na hayo; na kipindi hicho walitumia neno la YESU KUFANYIKA DHAMBI

Mojawapo ya posts ambazo mhusika aliwahi kuongelea swali hili (japo kichwa cha post hakikuwa kinahusiana na hilo) ni kwnye post hizi hapa #608 (post ya tarehe 04/04/2021-mwaka jana) #796 (post ya tarehe 13/10/2021-mwaka jana) ambazo baadhi ya maneno aliyosema mhusika kuhusiana na swala hili ni kama yanavyoonekana hapa chini kwenye italics

POST
#608

  • Na ndiye yule yule ambaye alisimama madhabahuni J2 ya leo akiwa na ujumbe uliokuwa unamwelezea Yesu kuwa ALIFANYIKA DHAMBI
  • Vile vile huko nyuma kwenye mojawapo ya J2 ambazo aliwahi kusimama na baadaye Betri ya Gari la mhusika kupigwa shoti ya umeme, JUNIOR huyu huyu aliwahi pia kusimama akiwa na ujumbe huo huo wa YESU KUFANYIKA DHAMBI, sawa na ule alioukuwa nao leo
Ni kijana ambaye anaibukia kwa kasi sana na anafuata sawia kabisa nyayo za Kiongozi Mkuu, kiasi kwamba anaonekana kuwa atakuja kuwa qualified zaidi kwenye haya maswala ya uchakachuaji, possibly kuwazidi hata hawa wanaomfanyia training hiyo

Mwisho wa ku-quote maneno kwenye post hii #608



POST #796


Kawaida maneno haya huwa anapenda sana kuyatamka mhubiri chipukizi alyesimama madhabahuni kuhudumu J2 hiyo wakati wa Ibada ya Pili, lakini inaonekana kwa kwa bahati mbaya chipukizi huyu ambaye anaandaliwa na anachipuka kwa kasi sana kwenye swala hili la ubabaishaji kupitia MADHABAHU YA BWANA, alisahau kuyatamka maneno hayo J2 hiyo. Huyu chipukizi ndiye ambaye ana kawaida ya kuwa kila akipata nafasi ya kusimama MADHABAHUNI PA BWANA, mara nyingi huwa anatamka maneno hayo

Kwa sababu chipukizi hakufanikiwa kuyatamka siku hiyo, ilibidi sasa KM-A asimame na kuyatamka yeye mwenyewe


Mwisho wa ku-quote maneno kwenye post hii #796

Mara zote neno hili Yesu kufanyika laana, au wakati mwingine Yesu kufanyika dhambi; huwa anaanza analitumia kwanza KM-A J2 hii, halafu J2 nyingine inayofuata, hupanda madhabahuni Kiongozi mwingine junior ambaye naye pia hurudia tena kulitumia neno hilo

…………………..itaendelea
 
BY THE WAY;

NI KWA MARA PILI SASA KILA KM-A ANAPOTANGAZA MAOMBI KANISA-A; ZINAANZA KUTOKEA AJALI MBAYA SANA ZA BARARABANI


Alichowahi kukisema mhusika kwenye post hii hapa #929; kimejirudia tena wiki iliyopita

Kwa kifupi tu ni kwamba; kwenye wiki hiyo iliyotajwa kwenye post hiyo, KM-A alitangaza maombi ya wiki nzima kuanzia J3.

Ndani ya wiki hiyo hiyo ya maombi, kilichotokea ni kwamba zilianza kufululiza ajali za barabarani; nyingi zikiwa zinahusiana na kufeli breki na ilikuwa ni kwa mara ya kwanza kwa ajali kutokea tangu mwaka huu wa 2022 uanze

  • Tangu mwaka huu wa 2022 uanze, ndiyo ilikuwa ni mara ya kwanza kwa ajali za barabarani kutokea kwa mwaka huu
  • Kabla ya hapo hapakuwa pametokea ajali zozote za barabarani
  • Kama kuna zipo zilizokuwa zimewahi kutokea kabla; basi zitakuwa ni zile ambazo hazikuwahi kutangazwa au kuandikwa kwenye vyombo vya habari
  • Ajali hizo hazikuishia wiki hiyo tu ya maombi bali ziliendelea hadi kwenye wiki nyingine ile ya pili iliyofuata; na possibly ziliendelea hadi kwenye wiki ya tatu kwa sababu zilifululiza kwa kufuatana fuatana kwa siku kadhaa; mhusika hakumbuki vizuri idadi ya siku hizo au wiki zake
Ukiacha hilo, ndani ya wiki iliyoishia J2 ya tarehe 12/06’2022 ambayo KM-A alikuwa ametangaza tena maombi ya kuombea ULAWITI, ajali za barabarani zilirudi tena

Kati ya ajali nne zilizotokea wiki hiyo, tatu zimetokea siku moja, almost kwenye muda MMOJA na kwenye POINT MOJA

  • Lori lilianguka, halafu baada ya hapo ikaja Hiace ikagonga Lori, halafu baada ya ahapo, ikaja tena gari nyingine ya tatu ikavigonga tena vyote viwili, Lori na Hiace
  • Zaidi ya watu 20 wanasemekana kupoteza maisha kwenye ajali hiyo ya kwanza
Ajali ya aina hii si ya kawaida sana kwa akili za binadamu yeyote yule ambaye anamwamini Mungu

Baada ya hapo, ndiyo kuna ajali nyingine tena ya nne iliyokuja kutokea siku nyingine kufuatia hiyo iliyomaliza watu wengi sana

Hoja ya mhusika hapa ni kwamba; hata kama maombi yanayofanyika KANISA A SIYO SPECIFICALLY KWA AJILI YA KUOMBEA AJALI ZA BARABANI lakini kitendo cha kwamba kuna maombi maalumu yanafanyika Kanisani ndani ya wiki hiyo, lazima ajali hizi zingekuwa zinatokea kwenye window nyingine inayokwepana kabisa na wiki za maombi ya Kanisa A

Tofauti na ilivyo kawaida; kwenye wiki zisizokuwa za maombi ndiyo kunakuwa hakuna ajali; halafu kwenye wiki ya maombi ndiyo ajali za bararabani zinaumana na wiki ya maombi!

Hiki kitu ni kama paradox ya aina fulani hivi kwa mtu yeyote anayemwamini Mungu na anayejua MAANA YA MAOMBI YA KUMUOMBA MUNGU NI NINI, bila kujali aina ya maombi hayo kwa Mungu!
 
KILICHOTOKEA KWENYE IBADA YA J2 TAREHE 12/06/2022 WAKATI SOMO LA MAANDIKO MATAKATIFU LINAFUNDISHWA

Kichwa cha somo kilikuwa very unique kwa maana kilibeba maudhui ambayo haijawahi kabisa kufundishwa na Kiongozi yeyote yule wa Kanisa A kwa miaka yote tangu mhusika aanze kuabudu Kanisani hapo mwaka 2011

Mbali na hilo; kichwa cha somo kilibeba pia maudhui ambayo, siku zote mhusika amekuwa mara kwa mara akishauari kwa msisitizo wa hali ya juu sana kwamba inabidi waumini wafundishwe maudhui hiyo mara kwa mara ili waweze kuifahamu vyema

MAUDHUI INAYOSHAHIBIANA NA SOMO LA J2, MARA YA MWISHO ILIWAHI KUFUNDISHWA MWANZONI MWA MWAKA 2013 NA MTUMISHI ALIYEKUWA AMETOKA NJE YA KANISA A

Hata hivyo, maudhui inayofanana na hiyo, iliwahi kufundishwa na mtumishi kutoka nje ya Kanisa A mwanzoni mwa mwaka 2013. Ilikuwa ni kwenye wiki ambayo uongozi wa ngazi za juu wa Kanisa A ulifika Kanisa A na kutumia wiki nzima ukiwa unatoa huduma hapo. Ujumbe unaofanana na wa J2 iliyopita, uliwahi kufundishwa na mtumishi ambaye hata yule aliyekuwa anafundisha somo , alimtaja kwa jina (aliyewahi kuufundisha kabla)

Ukweli ni kuwa kila muumini wa Kanisa A atakiri kuwa ujumbe huu ulikuwa mpya kabisa kuwahi kufumdishwa na mtumishi wa Kanisa A, tangu mwaka huo wa 2013

Kuhusiana na ujumbe huo, mara zote mhusika amekuwa akisisitiza kuwa waumini walio wengi wanakosa kitu muhimu unaotokana na ujumbe kutokufundishwa na hivyo wanahitaji kitu kama kuamshwa hivi ili waweze kujua nafasi yao ni ipi kama Kanisa la Bwana, hasa katika ulimwengu wa roho

Mhusika alishawahi kudokeza humu jukwaani kuwa jumbe zote ambazo huwa zinatolewa Kanisa A, karibia mara zote huwa ni zile ambazo ni negative; yaani zile za kuwafanya waumini wajione kuwa wana mapungufu tu na hawana chochote cha maana; isipokuwa kwenye UTOAJI WA SADAKA TU!

Jumbe zile za kuwa-encourage waumini na kuwafanya waweze kujiona kuwa wana kitu kikubwa na cha maana sana ukiachilia mbali kwamba bado wanayo mapungufu yao kadhaa kama binadamu, hizo huwa hazitolewi kabisa Kanisa A

KUHUSIANA NA HUYU MTUMISHI ALIYESIMAMA MADHABAHUNI J2 YA TEREHE 12/06/2022

Huyu mtumishi aliyesimama kufundisha neno la Mungu J2 ya tarehe 12/06/2022 alikuwa ame-calculate kutokana na haya yaliyotajwa hapa, ukiyahusianisha na kile ambacho KM-A alikifanya kwenye madhabahu J2 ya tarehe 05/06/2022

Kwa hiyo kilichofanywa na mtumishi aliyesimama madhabahuni J2 ya tarehe 12/06/2022 kwa kufundisha somo zuri sana na la kuwafanya wajitambue wao ni nani kwenye ulimwengu wa roho, lilikuwa ni changa la macho. Kilichokuwa kinafanyika hasa ulikuwa ni mwendelezo tu wa uchakachuaji wa madhabahu uliokuwa umefanyika J2 ya wiki iliyokuwa imepita nyuma yake

Kiongozi huyu junior alisimama madhabahuni siku hiyo kwa ajili ya ku-back-kile kilichokuwa kimefanyika J2 iliyokuwa imepita nyuma

Mbali na hilo, katika hali ya kawaida; Kiongozi huyo junior ndiyo alitakiwa kuwa Kiongozi wa zamu kwa wiki hiyo; kulingana na tangazo lililokuwa limetoka madhabahuni J2 ya tarehe 05/06/2022

Hata hivyo inaonekana ndani ya wiki, upepo ulisoma tofauti na ilivyokuwa imetarajiwa hali ilyopelekea zamu hiyo kuchukuliwa na mtu mwingine ili yule aliyetakiwa kuwa zamu aweze kujiandaa kwa ajili ya kusimama madhabahuni J2 inayofuata

Hii ni kutokana na ukweli kuwa si kawaida sana kwa kiongozi wa zamu wa wiki hiyo, kusimama tena madhabahuni J2 kwa ajli ya kufundisha neno la Mungu, japo inawezekana

…………………….inaendelea
 
HITIMISHO

Kwenye utafiti wake, mhusika ameshajiridhisha kabisa kuwa pale madhabahu ya Bwana inapokuwa imechakachuliwa;

  • Mbali na kuwa butu, Maandiko Matakatifu ya Biblia huwa yanageuzwa na kuwa mkuki au silaha ya maangamizi; badala ya kuwa ulinzi kwa waumini
  • Kwa hiyo maneno kama “Yesu kufanyika dhambi au laana” yanapokuwa yametamkwa kutokea madhabahu hiyo, yanakuwa yamebeba negative connotations za ajabu sana kwa waumini na zenye madhara makubwa sana kiroho
“Kila andiko lenye pumzi ya Mungu lafaa kwa mafundisho na kwa kuwaonya watu makosa yao………..”

Hili andiko lenye pumzi ya Mungu ni andiko lililotokana na kinywa cha Mungu au lililotokana na manabii na mitume wake

Kwa hali hiyo; siyo lazima neno hilo liwe positive.
Kwa mfano
  • Yesu akamwambia Petro; “toka nyuma yangu shetani…..”
  • Yesu alifanyika dhambi..........
  • Yesu alifanyika laana...............
Haya yote ni mameno negative lakini yenye pumzi ya Mungu, na yanafundisha; yanaonya

Unless kama kuna muumini anayeweza ku-prove kwamba kwenye phrase tatu zilizotajwa hapo juu; hakuna fundisho wala onyo llilo kwenye phrase hizo

Nabii Hosea aliambiwa aende akaoe mwanamkea aliyewahi kuwa kahaba--- bado kuna fundisho kubwa tu kwenye kitendo (very negative order)

Nabii Hezekia aliongezewa umri wa kuishi miaka 15 (a very positive act)

Simeo aliwahi kuambiwa na Roho Mtakatifu kwamba hatakufa mpaka Yesu atakapokuwa amezaliwa (positive order? Negative order?). Hata hivyo, hili Simeo hii ililkuwa ni negative order kwa sababu; baada ya Yesu kuzaliwa; Simeo alienda akambeba mto Yesu mikononi akamshukuru Mungu huku akimuomba amruhusu na yeye ili aweze kufa.Hapa kuna fundisho moja kubwa kwamba “mtu ambaye ameishi na Mungu siku zote lazima awe positive na kifo; kama ameshatimiza umri ambao uko sahihi

Tofauti na ilivyokuwa kwa Hezekia; fundisho tunalolipata kutoka kwa nabii huyu ni kwamba “mtu ambaye ameishi na Mungu siku zote lazima awe negative na kifo; iwapo tu atakuwa hajatimiza umri ambao uko sahihi



Kwa hali hiyo, halipo neno moja ndani ya Biblia ambalo halina pumzi ya Mungu ISIPOKUWA SI KILA NENO LILILO KWENYE BIBLIA LINAMHUSU MUUNINI WA MUNGU HAPANA; MENGINE YANAMHUSU SHETANI

Shetani anapotaka kumuangamiza muumini wa Mungu; huwa haendi kununua sumu kwenye duka la madawa ya kuua wadudu; bali huwa anaingia kwenye Maandiko Matakatifu. Hata alipokuwa anamjaribu Yesu; alitumia Biblia

Kwa hiyo wanaofanya uchakachuaji kwenye madhabahu ya Bwana, hatimaye sasa inabidi watumie neno la Mungu ili wasijulikane. Wanatumia neno la Mungu wakiwa tayari wameshaliondoa makali yake, wakiwa wamelifanya kuwa butu. Hiki kitu kinawezekana kabisa pale wanapokuwa wamepata mlango wa kuweza kumshirikisha shetani

Na kwa masikitiko makubwa kabisa; watumishi hawa kwa sasa wanaonekana wameshafanikiwa kupata external beck-up kutokana na ujinga wao huu wanaoendeleza; mhusika alishaliona hili siku nyingi sana akaamua kukaa kimya tu

Katika kipindi cha maisha yake yote ya wokovu; ni watumishi hawa wawili tu ambao mhusika amewahi kuwasikia wakiwa wanatumia haya maneno ya Yesu kufanyika dhambi; laana

Haya maneno hajawahi hata mara moja, kuyasikia yakitumiwa na mtumishi wa Mungu mwingine yeyote yule nje ya hawa wawili aliowataja hapa

One of the 48 laws of power has the phrase “seem dumber than your mark….”

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
Back
Top Bottom