#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

UPDATE: 21 AUGUST 2020

WASIFU WA MHUSIKA KWA KIFUPI SANA

Inaendelea……………….




12 WASIFU WA KIROHO WA MHUSIKA KABLA HAJANZA KUABUDU KANISA A

  • Mara ya kwanza anaona LIVE watu wakijaribu kutoa pepo Kanisani ilikuwa mwaka 2011., hapo hapo Kanisa A.
  • Hapo kabla, alikuwa anaona kwenye TV tu na alikuwa anadhani kuwa ni maigizo, yaani makubaliano kati ya watumishi wa Mungu na waumini wao makanisani
  • Alikuwa hajui kama mapepo wapo, na pia alikuwa hajui maana ya pepo
  • Uwepo wa shetani yeye alikuwa anaona ni dhana tu au falsafa, isipokuwa alikuwa anaamini uwepo wa Mungu kwa concrete evidence ambazo details zake hawezi kuzitoa hapa
  • Mara ya kwanza kwake kuhakikisha kuwa kuna ulimwengu wa roho ilikuwa pia mwaka 2011, baada ya kusoma kitabu kilichaondikwa na Mtumishi maarufu wa Mungu hapa Tanzania, Mwalimu Christopher Mwakasge
  • Kitabu hicho alikinunua Makao Makuu ya KKKT (Luther House, mjini kule City Centre)
  • Mara ya kwanza kwake ku-detect pattern isiyo ya kawaida katika maisha yake na hatimaye kung’amua kuwa pattern hiyo haikuwa inaitokana na nguvu za kawaida zinazoonekana kwa macho, ilikuwa mwaka 2010
  • Hisia za uwepo wa ulimwengu wa roho, kwake zilianza mwaka 2010. Kabla ya hapo, kila tukio lililokuwa likimtokea, alikuwa analiona na kulifanyia kazi katika tafakuri ya ulimwengu wa macho ya nyama tu basi
Kwa hiyo kabla ya 2010, alikuwa hajui chocote kuhusiana na ulimwengu wa roho na alikuwa hajui kama ulimwengu huu upo. Kilichomtoa huko kote nyuma akiwa mzima tangu akiwa mdogo hadi kumfikisha mwaka 2010, ni imani thabiti tu kuwa Mungu yupo. Tangu akiwa mdogo, amekuwa na strong faith ya kwamba Mungu yupo, na pengine tuseme hicho ndiyo pekee alichokuwa anakijua kwenye ulimwengu wa roho, kwamba Mungu yupo, hilo tu basi!



MUBARIKIWE TENA NA BWANA

MwiH
elly obedy
 
In the war between FALSEHOOD and TRUTH (GOD), falsehood wins the first battle and TRUTH, the last"

Yohana 14:6
Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
 
UPDATE: MONDAY, 24 AUGUST 2020

WASIFU WA MHUSIKA KWA KIFUPI SANA

Inaendelea……………….



NYONGEZA MUHIMU


1 WASIFU WA KIMWILI:

  • Aliwahi kudhulumika gari mpya kutoka Japan, haikuwa na zaidi ya miaka miwili tangu iwasili kutoka japan
  • Hakuibiwa bali alinyang’anywa. Ilikuwaje?
  • Alipata ajli ajali pale Super Star kwa kupigwa pasi ubavuni upande wa dereva, yeye akiwa anatokea Ubungo kuelekea Mwenge
  • Gari aliyogangana nayo ilikuwa inatokea Sinza kuelekea Mwenge, na ilikuwa inatokea Barabara ndogo ya Sinza kuingia barabara kuu ya kuelekea Mwenge
  • Yeye alikuwa barabara kuu akiwa amenyoosha
  • Baada ya ajali, alipeleka gari lake Garage kwa ajili ya kunyoosha bodi, jirani na mahali anapoishi
  • Garage hiyo inasemekena kuwa ni ya staff-mate wake
  • Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kupeleka gari pale
  • Garage walivyomaliza kunyoosha bodi, na gharama zote akiwa nimelipia, wakawa wamebadilisha injini na kuweka nyingine kuukuu, ila aina ile ile kama ile ya mwanzo
  • Injini yake yeye ilikuwa almost mpya na ilikuwa nzuri sana
  • Ailipogundua kuwa wamebadilisha injini, aikawarudishia gari na kuwaomba warudishe injini mpya ya gari lake
  • Wakaja juu Garage nzima, wakataka kumpiga
  • Akawaambia wakigoma kurudsha injini ya gari lake, atawachia gari lote
  • Wakagoma kumrudishia, akatoka hapo na hajawahi kurudi hapo tena mpaka leo. Walifikiri alikuwa anawatania
  • Hiyo ilikuwa ni Septemba 2010
Gari hilo aliwaachia, hakuwapa, kwa sababu zifiatazo

  • Mtu unaibiwa kitu pale unapopotelewa na kitu hicho pasipo kumfahamu yule aliyekichukua,
  • Na mtu unanyang’anywa kitu pale inapotokea aliyechukua kitu chako unamjua, na anapenda umjue!
  • Mwizi ni mwoga, huwa hapendi afahamike na mtu aliyemwibia
  • Mnyang’anyi huwa anapenda sana umfahamu na huwa ana kitu kingine cha ziada mbele, kizito zaidi kuzidi kile cha kwanza
  • Yeye kukunyang’anya tu huwa haitoshi kwake
  • Kawaida huwa anafanya hivyo akiwa anatafuta ziada nyingine kwako na ndiyo maana huwa ananyang’anya, na huwa anapenda umfahamu, hajifichi!
 
TUKIO JINGINE TENA (LA TATU) MANEO YA SAVEI

Inaonyesha KAMA siku hizi catchment area ya mahasimu wake imehamia Savei pia. Jumamosi iliyopita (22-08-2020), majira ya kati ya saa 2 na saa 3 asubuhi, alipatwa na tukio jingine tena pale Savei, linalofanana kabisa na mawili ya mwanzo aliyowahi kuyalezea hapo awali, ila set-up yake tu ndiyo ilikuwa tofauti. Alikuwepo mtu pale akiwa amejiandaa ili apande kwenye gari lake. Mhusika anaona hana haja ya kutoa details za tukio hilo kwa sababu, tofauti na mengine yaliyopita, hili la juzi lilishuhudiwa na umati wa kutosha wa PUBLIC, baada ya plan ya mtu aliyehitaji kupanda kwenye gari la mhusika, kuwa ime-abort. Walikuwepo watu wa kutosha kuweza kuthibitsiha uwepo wa tukio hilo na pia hata mamlalka za Serikali nazo baadaye ziliwasili eneo hilo. Audience hii inatosha kabisa kulihakiki tukio hili kama lilikuwa la kwaida ama la. Hana haja ya kutoa details za tukio lenyewe kwa sababu watu wengi walikuwepo na walilishuhudia. Lilitokea pale Savei darajani
 
Huyu mtu aliyekuwa ametumwa ku-engineer tukio la namna hi lililotjwa hapo juu, alitaka aingie ndani ya gari la mhusika, kwa kuvunga kuwa anataka apewe rushwa or somrething similar.
 
In the war between FALSEHOOD and TRUTH (GOD), falsehood wins the first battle and TRUTH, the last"

Yohana 14:6
Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
 
Halafu ndio yeye huyo huyo,unawezaje kumkremu mtu mpaka nukta?
Makanyaga
How do you manage to tell someone's story without any nukta? In anyway, whether the story is yours or not the nuktas must be around your entire text.
Unless the story is a fabrication, you are being urged to focus mainly on the content, and not on the story teller
 
Malaki 3:5
Nami nitawakaribieni ili kuhukumu; nami nitakuwa shahidi mwepesi juu ya wachawi, na juu ya wazinzi, na juu yao waapao kwa uongo; na juu yao wamwoneao mwenye kuajiriwa, kwa ajili ya mshahara wake, wamwoneao mjane na yatima, na kumpotosha mgeni asipate haki yake, wala hawaniogopi mimi, asema Bwana wa majeshi.
 
Anzisha kitabu sasa uzi wote umejaa maelezo yako tu
 
NEXT: Yale ambayo mhusika alikuja kuyabainisha kuwa Mtumishi wa Mungu Mgeni (MMM) alikuwa ametumwa kuja kuyafanya nyumbani kwa mhusika .....................................
...................................................................................................................

In the war between FALSEHOOD and TRUTH (GOD), falsehood wins the first battle and TRUTH, the last"

Yohana 14:6
Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.

Malaki 3:5

Nami nitawakaribieni ili kuhukumu; nami nitakuwa shahidi mwepesi juu ya wachawi, na juu ya wazinzi, na juu yao waapao kwa uongo; na juu yao wamwoneao mwenye kuajiriwa, kwa ajili ya mshahara wake, wamwoneao mjane na yatima, na kumpotosha mgeni asipate haki yake, wala hawaniogopi mimi, asema Bwana wa majeshi.
 
Muhimu: Uzi huu unawafaa sana hasa wale ambao tu huwa wana muda na wanapenda kuchambua mambo kwa kina, vinginevyio kama wewe siyo mmoja wao, unaweza ukaona kana unapoteza muda wako kuufuatilia

Nilipoona onyo hili nilipuuza, ona sasa kilichonikuta. Sijaelewa kitu
Hahahaha Bora kabla cjasoma nimekutana na hii comment....[emoji38][emoji38][emoji38]
 
Hahahaha Bora kabla cjasoma nimekutana na hii comment....[emoji38][emoji38][emoji38]
Umenikumbusha kitu kuna siku mwalimu aliingia darasani kwenye kipindi cha somo la IT (Profesa Mjema, Mkuu wa Chuo CBE)., wakati anaendelea kufundisha (Decision Support Sytems-DSS) akauliza swali "How do you people normally think"? Kabla watu hawajajibu swali, akasisitiza tena akasema "how" , not "what".
Ni kwa sababu aliona dalili za kisaikolojia kuwa watu walikuwa wanataka kujibu swali la "what" badala lile la "how" alilokuwa ameuliza
 
In the war between FALSEHOOD and TRUTH (GOD), falsehood wins the first battle and TRUTH, the last"
 
Yohana 14:6
Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.

Malaki 3:5

Nami nitawakaribieni ili kuhukumu; nami nitakuwa shahidi mwepesi juu ya wachawi, na juu ya wazinzi, na juu yao waapao kwa uongo; na juu yao wamwoneao mwenye kuajiriwa, kwa ajili ya mshahara wake, wamwoneao mjane na yatima, na kumpotosha mgeni asipate haki yake, wala hawaniogopi mimi, asema Bwana wa majeshi.

WAEBRANIA 6:4-6 SUV
Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu, na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo, wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu kwa mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.
 
UPDATE: MONDAY 31 AUGUST 2020

NYONGEZA MUHIMU KUHUSIANA NA BAADHI MATUKIO AMBAYO TAYARI MHUSIKA AMESHAYAONGELEA


  • KUHUSIANA NA SWALA LA MTUMISHI KUSIMAMA MADHABAHUNI KWA AJILI YA KUFUNDISHA MAANDIKO MATAKATIFU NA KUANZA KUFUNDISHA MANENO HAYO BILA KUOMBA
Hili swala halihusiani na watumishi ambao:

  • Kabla ya kuanza kufundishwa Maandiko Matakatifu muda mfupi unaofuata, mtumishi huyo anakuwa ndiye aliyepanda juu madhabahuni kwa ajili ya kuhitimisha kwa sala, huduma hiyo ya Ibada ya Kusifu na Kuabudu
  • Baada ya hapo, mtumishi huyo huyo ndiyo tena anakuwa ndiyo yule yule ambaye ni mhudumu au mwalimu kwa ajili ya neno la siku hiyo
Mtumishi wa aina hii, kulingana na uelewa wa mhusika, halazimiki tena kutoa sala kwa ajili ya kuombea neno atakaloenda kulifundisha, kwa sababu ndiyo yule yule ambaye ni mwalimu wa neno la siku huyo na wakati huo huo anakuwa ndiye yule yule aliyetoa sala ya kuhitimisha Ibada ya kusifu na kuabudu

Katika hili, mtizamo wa mhusika ni kuwa swala la kuombea maneno matakatifu yanayotakiwa kufundishwa siku hiyo linamhusus mtumishi yule ambaye:

  • Wakati wa kuhitimisha Ibada ya kusifu na kuabudu, hakuwepo madhabahuni na hivyo anakuwa si yeye aliyehusika kutoa sala ya kufunga Ibada ya Kusifu na kuabudu, kabla ya kuanza Ibada ya mafundisho ya neno la Mungu
  • Huwa anapanda madhabahuni kwa ukaribisho kutoka kwa mtumishi mwingine na hivyo inakuwa ni mara yake ya kwanza/ au mara yake nyingine tena mpya ya kupanda kwenye madhabahu ndani ya siku hiyo ya Ibada husika
Kwa hiyo mtumishi huyu kawaida anakuwa ni yule ambaye huwa anapanda madhabahuni kwa ukaribisho kutoka kwa mtumishi mwingine; na hasa pale inapotokea kuwa kuna Ibada moja au zaidi ya moja, na kila ukaribisho ukiwa unahusisha Ibada nyingine tofauti na nyingine iliyopita/ zilizopita

Hivyo basi, mhusika hapa yeye ambacho huwa anakiona kwenda kinyume ni pale tu mtumishi aliyekaribishwa anapopanda madhabahuni kwa ajili ya kufundisha neno siku hiyo, na kuanza kufundisha maandiko matakatifu bila kuwa ameyaombea, au ameomba mtumishi mwingine ayaombee kwa niaba yake, baada ya (mtumishi huyo) kuwa amepanda madhabahuni.

Kwa hali hiyo, katika toleo lake lililopita juu ya swala hili, mhusika hakuwa anamaanisha mtumishi ambaye anakuwa tayari yupo madhabahuni kabla ya neno kuanza na ambaye huwa amehusika pia kutoa sala kuu ya kuhitimisha Ibada ya Kusifu na Kuabudu; na wakati huo huo ndiyo yeye yule yule tena ambaye anakuwa ni mwalimu wa neno la siku hiyo. Mtumishi aliyehitimisha kwa sala Ibada ya kusifu na kuabudu, huyu yeye halazimiki kuomba tena kwa ajili ya neno iwapo tu atakuwa ndiyo yule yule anayetakiwa kufundisha neno la siku hiyo. Anaweza akafanya hivyo kwa kupenda ,,,,,, “ombeni bila kukoma”!

Hata hivyo huu ni uelewa wa mhusika na hana uhakika sana kama yuko sahihi kwa hii scenerio ya pili ila uhakika alionao ni ule wa scenario ya kwanza, kwamba:

  • Kama wewe ni mtumishi umekaribishwa madhabaguni kwa jalili ya kufundisha neno, hata kama itakuwa ni kwa mara nyingine ya pili au ya tatu ndani ya siku hiyo, kawaida unatakiwa uombe kwa ajili ya neno hilo unalokwenda kulifundisha, au umuombe mtumishi mwingine aombe kwa niaba yako, kwa ajili ya neno hilo.
Hii ndiyo kawaida na ndivyo inavyotakiwa kuwa siku zote


Yohana 14:6

Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.

Malaki 3:5
Nami nitawakaribieni ili kuhukumu; nami nitakuwa shahidi mwepesi juu ya wachawi, na juu ya wazinzi, na juu yao waapao kwa uongo; na juu yao wamwoneao mwenye kuajiriwa, kwa ajili ya mshahara wake, wamwoneao mjane na yatima, na kumpotosha mgeni asipate haki yake, wala hawaniogopi mimi, asema Bwana wa majeshi.

WAEBRANIA 6:4-6 SUV
Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu, na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo, wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu kwa mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.

MwiH
elly obedy



……….Inaendelea
 
UPDATE: MONDAY 31 AUGUST 2020

NYONGEZA MUHIMU KUHUSIANA NA BAADHI MATUKIO AMBAYO TAYARI MHUSIKA AMESHAYAONGELEA



Inaendelea……….


  • KUHUSIANA NA MAKATO YA DHULUMA AMBAYO YAMEKUWA YAKIFANYIKA KWENYE MSHAHARA WA MHUSIKA
Kwaida ukikuta mtu ni MUUMINI WA MUNGU halafu kuna matukio yasiyokuwa ya kawaida yanaendelea kwake, ujue kuwa kuna mambo mawili tu makubwa:

  • MOJA: Ni yeye anakuwa anayasababisha mambo hayo kwa sababu anakuwa hajasimama vizuri na Mungu wake
  • PILI: Kama amesimama vizuri na Mungu wake, basi ni matukio ambayo yanakuwa engineered kwake na watu wengine kutokea kwenye ulimwengu wa roho
  • Hayupo mtu mwingine anayeweza ku-engineer matukio ya muumini kutoka kwenye ulimwengu wa roho, zaidi ya muumini mwingine ambaye ana hadhi inayolingana na ya kwake
Na pale inapotokea kuwa uhalisia wa mambo yanayomtokea mtu husika katika ulimwengu wa mwili kweli yanatokana na sababu iliyotajwa kama namba mbili hapo juu, basi matukio hayo lazima yaanzie Kanisani ambako ndiyo base yake ya kiroho iliko. Kwa hiyo shambulio lolote llie ambalo atalipata katika ulimwengu wa mwili, iwe ni dhuluma ya mali yake au kitu kingine chochote kile, lazima liwe limeanzia kwenye ulimwengu war oho, na lazima chanzo chake kiwe ni Kanisani.

Kwa mfano makato yote batili kwenye mshahara wa mtu au chain ya matukio ya mtu kutakiwa afukuzwe kazi, yote lazima yaanzie Kanisani kule iliko base yake ya kiroho halafu ndiyo baadaye yawe manifested kwenye ulimwengu wa mwili, iwapo tu mtu huyo ni muumini wa Mungu

KITU AMBACHO HUWA KINATOKEA MASHAMBULIZI YA KIROHO YANAPOELEKEZWA KWENYE TARGET AMBAYO SI SAHIHI

Pale inapotokea kuwa target inayoelekezewa mashambulizi siyo sahihi

  • Mashambulizi hayo MARA ZOTE huwa yana kawaida ya ku-fireback na kuwarudia washambuliaji
  • Kwa wauumini waliopo Kanisa A, watakubaliana na mhusika kuwa inaonyesha kama mashambulizi waliyokuwa wakiya-engieer viongozi wa Kanisa A, wameanza kuuona uwezekano mkubwa kuwa yanaweza kuwarudia wao wenyewe
  • Hii inathibitishwa na maneno ambayo wamekuwa wakiyatamka pindi waanapokuwa wamesimama madhabahuni wakati wa Ibada za J2, kwa takribani kana wiki kama tatu mfululizo sasa
  • Kwa hiyo mkuki ni kwa nguruwe, kwa binadamu uchungu
Kutokana na hali hiyo mhusika anaomba kuwakumbusha (unamkumbusha mtu kitu ambacho anachokijua tayari na si lazima awe amekisahau, ila ni kama tahadhari tu) waumini wote wa Kanisa A kuwa, pamoja na kwamba kipindi fulani huko nyuma kulifikia hadi hatua ya mabango kuwa yanabandikwa mbele ya madhabahuni ya Bwana, kuonyesha kama kuna mtu anamiliki Kanisa hilo

  • Kanisa hilo ni mali ya Taasisi, na hakuna mtu binafsi mwenye hatimiliki na Kanisa hilo, awe ni mtumishi wa Mungu au muumini wa kawaida
  • Kanisa hilo halitasambaratika kutokana na maneno ya mtumishi yeyote yule anayesimama madhabahuni akilalamika, possibly kwa sababu labda pengine UWINGI WA ZAKA NA SADAKA kwa sasa hauendani na kiwango kilichokuwa kimezoeleka kuwepo hapo awali
  • Taasisi inayomiliki Kanisa hilo ndiyo pekee yenye mamlaka ya kuamua Kanisa hilo lisambatratika ama la na nina uhakika kuwa itachukua hatua za kuhakikisha kuwa kitu hicho hakitokei.
Mhusika ana uhakika kabisa kuwa watumishi hawa lazima watadhibitiwa kikamilifu na Tasisi husika ili wasije wakasababisha taharuki nyingine tena ndani ya nyumba hiyo ya Ibada


Yohana 14:6
Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.

Malaki 3:5
Nami nitawakaribieni ili kuhukumu; nami nitakuwa shahidi mwepesi juu ya wachawi, na juu ya wazinzi, na juu yao waapao kwa uongo; na juu yao wamwoneao mwenye kuajiriwa, kwa ajili ya mshahara wake, wamwoneao mjane na yatima, na kumpotosha mgeni asipate haki yake, wala hawaniogopi mimi, asema Bwana wa majeshi.

WAEBRANIA 6:4-6 SUV
Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu, na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo, wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu kwa mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.

MwiH
elly obedy


………inaendelea
 
UPDATE: MONDAY 31 AUGUST 2020

NYONGEZA MUHIMU KUHUSIANA NA BAADHI MATUKIO AMBAYO TAYARI MHUSIKA AMESHAYAONGELEA



Inaendelea……….


  • KUHUSIANA NA SWALA LA KUNENA KWA LIGHA KAMA ISHARA YA UJAZO WA ROHO MTAKATIFU
Mhusika anapenda kuongelea maswala kadhaa ya msingi kuhusiana na swala hili la kunena.

Mambo haya ni kama yaifuatayo.

Kunena kwa lugha:

  • Ni ishara ya nje ya ujazo wa Roho Mtakatifu (RM) na si ya ndani
  • SI KILA ANAYENENA kwa lugha ANAO ujazo wa RM
  • SI KILA ASIYENENA kwa lugha HANA ujazo wa RM
  • Maana yake ni kwamba ni kweli kabisa kuwa kunena kwa lugha ni ishara ya ujazo wa RM lakini pia si dalili pekee ya kukuhakikishia kuwa mtu husika anao ujazo wa RM
  • Si kila anayeonekana kwa nje akinena kwa lugha, ana ujazo wa RM, wengine huwa wana mapepo
Kabla sijaendelea zaidi, nambatanisha clip hiyo hapo ya mtumishi wa Mungu alipokuwa akihudumu kwenye Semina hapo Kanisa A mwaka 2012. Kwa waliokuwepo kwenye Semina hiyo, najaribu tu kuwakumbusha maneno kile alichosema khuus kunena kwa lugha na kunavyohusiana na karama ya kupambanua roho ili kuweza kujua kama mnenaji mhusika nanena kwa kutmuia Roho wa Mungu ama la



……………….inaendelea
 

Attachments

KUNENA KWA LUGHA



Inaendelea……….

  • KUHUSIANA NA SWALA LA KUNENA KWA LIGHA KAMA ISHARA YA UJAZO WA ROHO MTAKATIFU


UZOEFU ALIOUPATA MHUSIKA KUHUSIANA YA DHANA YA KUNENA KWA LUGHA, PINDI ALIPOKUWA UHAMISHONII KANISA B

Mhusika aliwahi kukaa uhamishoni Kanisa B kwa takribani miaka mitatu (3). Katika kipindi chote alipokuwa huko alikutana na mambo kadhaa yafuatayo ambayo hakuwa amewahi kuyaona kabla, na ambayo baadhi yake (mengi) hajawahi kuyaona tena tangu aondoke Kanisa B

  • Hakuwahi kumuona mtu akinena kwa lugha kwenye maombi yoyote yale.
  • Ukiondoa hili la kutokumuona muumini yeyote akinena kwa lugha , yafuatayo hapa chini hajawahi kuyaona tena tangu aondoke huko.
  • Aliwahi kuwa aanwaona baadhi ya waumini (wa kike wawili na baadhi ya wachungaji akiwemo Mchungaji Kiongozi (wa kiume)) wakiendesha maombi huku wakiongea maneno kutoka kwenye maandiko matakatifu kwa mfululizo kwa muda hata wa taktibani saa nzima bila kupumzika au kukatiza
  • Lugha walizokuwa wanatumia ni Kiswahili na Kiingereza tu basi
  • Walikuwa wanaendesha maombi kwa lugha hizo, katika namna ambayo mtu anaweza akadhani kuwa ndiyo lugha ambazo walizaliwa wakiwa wanaongea
  • Iwe ni kwa Kiingereza au kwa Kiswahili, wachungaji hawa au waumini hawa wa kawaida, wataendesha maombi kwa takribani saa nzima, wanaongea Biblia tupu bila kupumzika hata sekunde moja na kwa mojawapo ya lugha hizo mbili, yaani Kiswahili au Kiingereza
Hiki kitu kwa Kanisa A, mhusika hajawahi kukiona hata mara moja kikifanyika kwenye maombi yoyote yale, kwa muda wote wa takribani miaka 7 ambayo amekuwepo Kanisa A.

Hawa watu wanaofanya maombi kwa jinsi hii, je ni kweli kwamba wao hawana RM kwa sababu hawaneni kwa lugha ngeni? Hawa kabisa walikuwa hawaneni kwa lugha ngeni lakini wana uwezo wa kuendesha maombi kwa takribani saa nzima bila kupumzika, wakitamka maneno kutoka kwenye Maandiko MJatakatifu utafikiri kuna Biblia ya Kiingereza au ya Kiswahili imefichwa mahali fulani ambapo hapaonekani na macho ya wengine, halafu wao wanasoma mfululizo baadhi ya mafungu hayo, randomly kutoka kwenye Biblia hiyo bila kupumzika, kwa lugha hizo. Je ni kweli hawa wao hawana RM kwa sababu hawaneni kwa lugha ngeni?

Hata hivyo, mhusika yeye katika swala hili la RM, mpaka muda huu anaamini kuwa mtu akikosa RM lazima afe, kwa sababu mtu yeyote yule awe ni muumini ama la. hawezi akaendelea kuwa hai wakati hana RM kabisa. Yeye anaamini kuwa kila mtu aliye hai ana RM isipokuwa tu kwa wale waliopo Kanisani, RM wao yuko activated zaidi kuzidi wale ambao huwa hawaendi. Ndiyo maana mtu anaweza akaongozwa sala ya Toba leo na akajazwa RM hapo hapo. Hii ina maana kuwa mtu huyu alikuwa naye RM tangu mwanzo isipokuwa tu alikuwa hawezi kumtumia katika kiwango kilichokuwa kinatakiwa. Mtu yeyote akikosa kabisa RM lazima afe kwa sababu RM ndiye anayemlinda kila mwanadamu, bila kujali binadamu huyo ni muumini wa Mungu ama la!



JE, KUNA UWEZEKANO KUWA HUWA KUNA PEPO LA UTAMBUZI WA LUGHA NGENI WANAZONENA WATAKATIFU WA MUNGU

Bila kuficha ukweli ulivyo, ukizingatia hali tete ya kiroho iliyopo Kanisa A kwa sasa na kwamba kuna mapepo yanendelea kurushwa, kwa muumini halisi kabisa aliyejazwa RM kunena kwa lugha kunaweza kukawa na risk kubwa iwapo tu kunaweza kukawa na uwezekano wa mapepo ya utambuzi wa lugha wanazoweza kunena watakatifu wa Mungu

Pepo linaweza kurushwa halafu likawa linatafsiri kila wanachonena waumini halafu linakifuta kwenye ulimwengu wa roho na kuzuia maombi yao kwenye ulimwengu wa roho, kama ilivyowahi kutokea kwa Daniel. Vile vile inaweza ikatokea scenario kama iliyomtokea mhusika ambayo ameshailelezea hapo nyuma. Unafuta ulichonena kwa lugha kama alivyokuwa akifuta yeye mhusika alipokuwa anasoma Zaburi yote ya 119 pale tu alipokuwa anaufikia na kuusoma mstari wa Zabuti 119:130. Pindi alipokuwa anaufikia, mstari huu ulikuwa unafuta kila kitu alichokuwa anasoma mhusika, juu na chini ya mstari huo. Hali kadhalika alivyokuwa akisoma Wakolosai 3:1-17, kuna kigingi kiliwekwa kwenye mstari wa 16, ambacho ilikuwa kila akiufikia na kuusoma mstari huo, ulikuwa unafuta mafungu yote juu ya mstari huo, na vile vile fungu moja la 17 lililokuwa chini ya mstari huo

Kama pepo anaweza kumfutia muumini alichosoma kutoka kwenye maandiko matakatifu, je atashindwa kufuta kila nachoweza kukinena kwa lugha ngeni?

Mhusika mpaka muda huu anamini kuwa pepo la utambuzi wa lugha likirushwa na likafanikiwa kuwepo ndani ya nyumba ya Ibada, wanenao kwa lugha wote wana uwezekano wa kupoteza kila kitu kwenye maombi yao.

Mhusika anashuri kuwa kama mtu anao ujazo huo, bora akautumie zaidi akiwa kwenye maombi ya faragaha, kuliko akiwa Kanisa A



HITIMISHO:

Kwa hiyo katika miaka yote mitatu ambayo mhusika alifanikiwa kuwepo Kanisa B, hakuwahi hata siku moja kusikia mtu ananena kwa lugha wakati wa maombi, lakini msisitizo uliopo Kanisa A kwa sasa juu ya unenaji kwa lugha umekuwa ni wa kiwango cha juu muno, kiasi kwamba mantiki iliyopo Kanisa A kwa sasa ni kuwa wale wote wasionena kwa lugha hawana RM. Je hiki kitu ni kweli?

Hii kwa upande mwingine inamaanisha kuwa kule alilkowahi kuwepo mhusika, yaani Kanisa B, AIDHA hakuna hata mtu mmoja kwenye nyumba hiyo ya Ibada aliye na ujazo wa RM AU wapo waliojazwa na ambao wanao uwezo wa kunena kwa lugha ila kwa bahati mbaya MAOMBI YAO NI YA KIWANGO CHA CHINI SANA kwa sababu huwa wanaomba si kwa kunena kwa lugha, japo wanao uwezo huo wa kunena kwa lugha ngeni



MUBARIKIWE TENA NA BWANA

Yohana 14:6
Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.

Malaki 3:5
Nami nitawakaribieni ili kuhukumu; nami nitakuwa shahidi mwepesi juu ya wachawi, na juu ya wazinzi, na juu yao waapao kwa uongo; na juu yao wamwoneao mwenye kuajiriwa, kwa ajili ya mshahara wake, wamwoneao mjane na yatima, na kumpotosha mgeni asipate haki yake, wala hawaniogopi mimi, asema Bwana wa majeshi.

WAEBRANIA 6:4-6 SUV
Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu, na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo, wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu kwa mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.

MwiH
elly obedy
 
Back
Top Bottom