#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

MAELEZO YA KINA KUHUSINA NA YALE YALIYOJIRI SIKU YA ALHAMISI TAJWA KUANZIA ASUBUHI AKIWA BADO YUKO NYUMBANI HADI ALIPOFIKA OFISINI NA HATIMAYE KUTOKA OFISINI NA KURUDI TENA NYUMBANI

Aliondoka nyumbani akaacha umeme ukiwa umekatika, akafika ofisini na kukuta nako pia umekatika

Baadaye alilazimika kutoka ofisini na kurudi nyumbani baada ya saa 8 za mchana, akiacha umeme ukiwa bado haujarudi, na alipofika nyumbani akakuta umeme umesharudi

Kwa hiyo kwa kifupi, alitoka nyumbani umeme ukiwa umekatika, akafika ofisini na kukuta nako pia umekatika, akatoka ofisini akaacha bado umekatika, ila alipofika nyumbani akakuta kwenye umesharudi

MAELEZO YA KINA KUHUSINA NA YALE YALIYOJIRI SIKU YA ALHAMISI (YA WIKI JANA) YATAREHE 10/06/2021
  • Aliondoka nyumbani akaacha umeme ukiwa umekatika; alifika ofisni akauta vile vile umeme vileukiwa umekatika, na aliondoka ofisini akaacha umeme ukiwa umekatika; ila alirudi nyumbani akakuta umeme ukiwa umesharudi
  • Alirudi nyumbani mida ya baada ya saa 8 mchana
Na kwa sababu aliondoka nyumbani akaacha umeme ukiwa umekatika, akafika ofisini nako akakuta pia umekatika na hadi anaondoka ofisini umeme ulikuwa haujarudi; ktuokana na hali hii, wakati anaondoka ofisini plan yake ilikuwa kama ifuatavyo;
  • Akifika nyumbani baadaye itabidi aende mtaani kutafuta bites kwa ajili ya chakula cha jioni
  • Huwa anakula mara moja tu kwa siku, bajeti yake kwa sasa hairuhusu kumuwezesha kula mchana na jioni.
  • LABDA KAMA IKITOKEA AKALIPWA STAHIKI ZAKE PAMOJA NA MALIMBIKIZO YA PESA AMBAZO AMEKUWA AKIZIDAI KWA MUDA MREFU SASA, BASI KUNA UWEZEKANO AKAANZA KUWA NA RATIBA YA KULA MCHANA PIA
  • Hela hivyo hela anayopata inamruhusu kula mchana na usiku
Maeneo aliyokuwa amepanga kwenda kuchukua bites ni yale yale ambayo angeweza kwenda usiku wa saa moja ya Jumanne ya tarehe 01/06/2021, kwa ajili ya kwenda kumtumia hela binti ndugu yake ambaye alihitaji kwenda kwenye msiba uliokuwa umetokea ghafla kijijini kwao siku hiyo (Post #655)

Kwa hiyo, pamoja na kukuta umeme ukiwa umerudi nyumbani siku hiyo, bado mhusika aliamua kwenda kununua bites kutokana na sababu kuu mbili zifuatazo
  • Aliondoka nyumbani umeme ukiwa umekatika, na alitoka ofisini umeme ukiwa umekatika. Kwa hiyo psychologically alikuwa ameji-set katika hali ya kukuta umeme haupo nyumbani pia
  • Na kwa sababu sikolojia yake ilikuwa imejijenga katika mazingira ya kukuta hakuna umeme nyumbani, saikolojia hiyo hiyo pia ilikuwa imem-set katika hali ya kula chakula cha jioni tofauti na kile alichokuwa nacho nyumbani kwake
Kwa hiyo kwa kuzingatia sababu hizi mbili, pamoja na kukuta nyumbani umeme upo ukiwa umerudii, bado aliamua kwenda mtaani kutafuta chakula hicho cha jioni, na hapo ndipo shambulio kwenye gari lake lilipotokea
  • Shambulio hilo lilitokea mara tu baada ya kuwa amemaliza pilika pilika zake mtaani na hatimaye kuamua kuwasha gari ili arudi nyumbani
  • Wakati anageuza uelekeo wa gari ili aanze kurudi nyumbani, ndipo kipindii alipobaini kutokea kwa kasoro ya ghafla kwenye gari yake
Details za kasoro hiyo ambazo zilipelekea hadi asiweze kuhudhuria hafla muhimu sana KANISANI J2 Iiliyopita, anazi-withhold

MTIZAMO WA MHUSIKA KUHUSINA NA JIRANI WAKE WA ZAMANAI NA YULE WA SASA, AKIWAHUSIANISHA NA MATUKIO HAYA YA HUJUMA KWENYE GARI LAKE

Kwa mtizamo wake yeye anaona KAMA watu hawa wamekuwa wakishirikiana katika kuratibu matukio haya, kuanzia lile la la kwanza mwaka 2019 hadi haya mengine mawili ya hivi karibuni:

  • .Inaonyesha KAMA irani wa sasa huwa anatekeleza matukio hayo usiku kwa vitendo halafu huyu wa zamani yeye huwa anatengeneza maigizo siku moja kabla ya tukio ili hujuma zitazofanyika zipelekee mhusika adhani kuwa si hujuma bali ni mashambulio la kiroho
  • Kwa hiyo dhana aliyonayo mhusika kwenye matukio haya yote ni kwamba hayana uhusiano wowote wa masmabulio ya kiroho bali ni hujuma za kawaida au kwa lugha nyingine watu huwa wanasema “ordinary organized crime”
MAMBO KADHAA MUHIMU ALIYOYAONA MHUSIKA KUTOKA KWA BAADHI YA WAFANYAKAZI WENZAKE PINDI ALIPOKUWA BADO YUPO MAZINGIRA YA OFISINI ALHAMISI HIYO AMBAYO UMEME ULIKUWA UMEKATIKA

Kuna wafanyakazi wenzake na mhusika (watatu) ambao waliwahi kutoa details au comments zilizoonyesha inconsistency ya wazi kuhusiana na tukio la kukatika umeme huo ofisini na hivyo kupelekea mhusika kuanza kupata picha ya kama kulikuwa na kitu kingine cha nyongeza ndani ya tukio hilo, japo hakuwa na uhakika sana na hilo. Wafanyakazi hawa ni
  • Wa kwanza: aliyekuwa ni msimamiszi wa ukarabati wa hivi karibuni wa jengo
  • Wa pili ni yule ambaye aliwahi kukaimu ukuu wa Idara Januari 2021 , halafu akatokea (katika kipindi hicho) kwamba barua za madai ya stahiki za mhusika alizokuwa akiandika kwenda mamlaka za juu, kuwa zinarudishwa (kwa kutokupitishwa) na hivyo kupelekea mhusika kutofanikiwa kupata stahiki hizo hadi leo hii
  • Wa tatu ni aliyewahi kuomba lift kwenye gari la mhusika, kurudi nyumbani kutokea mjini, siku mhusika alipokuwa amehudhuria mkutanoo wa kimataifa ukumbi wa Mwalimu Nyerere mwaka 2017 ; mkutano uliokuwa umeandaliwa na MR Y
…………………..inaendelea
 
Mwenye Summary ya hii naomba..., inawezekana mkasa ni mzuri ila in this day an age ya mambo mengi na muda mchache summary inapendeza zaidi (Yaani toa dondoo alafu mwenye kutaka kujua zaidi mpatie gazeti lako)
 
Mwenye Summary ya hii naomba..., inawezekana mkasa ni mzuri ila in this day an age ya mambo mengi na muda mchache summary inapendeza zaidi (Yaani toa dondoo alafu mwenye kutaka kujua zaidi mpatie gazeti lako)
Mkuu unahitaj jitihada binafsi kuyaelewa yaliyofichwa kwenye mkasa huu. Kuna code nyingi ila ukizichambua vzr kunamaana kubwa kwenye maisha ya taifa...
 
…………………..inaendelea

MAMBO KADHAA MUHIMU ALIYOYAONA MHUSIKA KUTOKA KWA BAADHI YA WAFANYAKAZI WENZAKE ALHAMIS HIYO

KUTOKA KWA ALIYEWAHI KUKAIMU UKUU WA IDARA JANUARY 2021


Yeye huyu baada ya kuwa wesalimiana na mhuiska asubuhi ya siku hiyo, alamua kumuaga mhusika kuwa anarudi nyumbani kwa sababu aliona dalili kuwa umeme hautarudi
  • Muda huo ilikuwa muda wa saa nne kasoro
  • Haikuwa mara ya kwanza kwa umeme kukatika asubuhi, ya namna ile na kulikuwa na masaa kadhaa mbele yenye kuashiria kuwa umeme ungerudi, na mara nyingi tu umeme umekuwa ukikatika asubuhi ya namna hiyo na hatimaye kuruid tena baada ya muda mfupi au ndani ya masaa kadhaa; ilhalii matukio la kukatika umeme na hatimaye kutorudi kabisa au kurudi baada ya muda mrefu sana, huwa ni ya ndra zaidi ukilinganisha nay ale ya kawaida, yaani yako SOMEHOW VERY RARE
  • Kwa kuzingati a hoja hii hapa juu, yeye huyu Kaimu MWI alijuaje kwamba tukio la kukatika kwa umeme Alhamis hiyo lilikuwa mojawapo ya yale ambayo ni rare na si kati ya yale ambayo ni ya kawaida; wakati hapakuwa pametolewa tangazo lolote lile kuhusiana na kukatika kwa umeme huo?
ALIYEWAHI KUOMBA LIFT KWENYE GARI LA MHUSIKA MWAKA 2017
  • Huyu yeye alidiriki kumweleza mhusika, huku akiwa ana-peruzi kwenye smartphone yake, kuwa kuna tangazo lioko kwenye mtandao limetolewa na PRO likisema kuwa umeme utarudi kuanzia saa tisa
  • Wakati huo ilikuwa mida ya saa nne kamili au na dakika kadhaa, chache
  • Mhusika alitaka kuhakikisha uthabiti wa taarifa za tangazo hilo lakini la kwenye mtandao lakini mwenye smartphne alionekana kutokuwa tayari kumshirikisha kusoma tangazo hilo
  • Baada ya hapo, mhusika aliamua kupandisha juu utawala kwenda kuangalia matangazo ya notice board ambayo huwa yanabandikwa huko kwa sababu kawaida PRO akishatoa tangazo lazima pia huwa linakuwa limebandikwa kwenye notice nboard ya utawala
Mhusika alipandisha juu hadi kwenye notice board na kukuta tangazo ni “HOLAAAAA! Hapakuwa na tangazo lolote la aina hiyo

III ALIYEKUWA MSIMAMIZI WA JENGO
  • Huyu yeye alianza kwa kuwasha jenereta jipya la umeme ambalo ameshaweka kama standby generator, halafu baada muda wa kama dakika tano hivi akalizima tena
  • Baada ya takribani dakika 30-40 tangu alipozima jenerata hilo, alifika ofisini kwa mhusika na kumuuliza swlali “vipi kwako taa haziwaki”
  • Mhusika naye alimjibu kuwa umeme umeshakatika
  • Msimamizi wa ujenzi alijibu kwa kusema kuwa nimewasha jenerta na pale kwangu taa zinawaka
Kilikuwani kituko cha karne kwa sababu jenerata lenyewe lilikuwa kimya na wala hapakuwa na taa yoyote iliyokuwa ikiwaka ndaniya jengo

Actually yalikuwa ni maongezi ambayo ni ridiculous na wakati mwingine taarifa za namna hii zinaweza kupelekea unayeziandika kushukiwa kuwa una matatizo ya akili. Kwa hiyo mwandishi wa taarifa hizi anapendelea aishie hapa kwa hili

Wakati maongezi haya yakiendelea, yule mwingine ambaye aliwahi kuomba lift kwenye gari la mhusika, naye pia alikuwepo ofisini kwa mhusika. Hawa wawili wao ni office-mates, wanashare ofisi moja



MUBARIKIWE TENE NA BWANA
 
Mkuu unahitaj jitihada binafsi kuyaelewa yaliyofichwa kwenye mkasa huu. Kuna code nyingi ila ukizichambua vzr kunamaana kubwa kwenye maisha ya taifa...
Wala hakuna code ila ni vifupisho tu vya maneno ya kawaida kwa ajlii ya ku-save muda wa mwandishi. Kwa mfano anapoandika KM-MWI anamaanisha Katibu Muhtasi wa Mkuu wa Idara, neno ambalo anakuwa ameshali-define kwanza huko nyuma, kabla ya kuanza kutumia kifupi chake kwenye maelezo mengine yote yanayofuata mbele
 
Wala hakuna code ila ni vifupisho tu vya maneno ya kawaida kwa ajlii ya ku-save muda wa mwandishi. Kwa mfano anapoandika KM-MWI anamaanisha Katibu Muhtasi wa Mkuu wa Idara, neno ambalo anakuwa ameshali-define kwanza huko nyuma, kabla ya kuanza kutumia kifupi chake kwenye maelezo mengine yote yanayofuata mbele
Mkuu think big and big.. you will see the message between the lines.. the huge powerful massage...
 
UPDATE: WEDNESDAY 16 JUNE 2021

KUHUSIANA NA KIFAA KILICHOKUWA KIMEHARIBIKA KWENYE GARI LA MHUSIKA


Kwa macho yake ya ki-layman, mhuiska yeye alikiona kifaa hicho kikiwa kama kimeungua kama vile kimepigwa na shoti ya umeme
  • Kiliungua na kusababisha kukatika kwa steering wheel belt na hivyo kupelekea usukani kuwa mgumu sana wakati wa kuendesha gari
  • Kilikuwa kinapata joto kubwa sana ndani ya sekunde kadhaa tu baada ya kuwa kimezungusha mkanda wa usukani (steering wheel belt)
Kwa lugha yake ya ki-layman, mhusika anaweza kukiita kifaa hiki kwa jina la steering wheel belt ROLLER


NEXT:

HISTORIA YA MATUKIO YA FUNGUO:

MATUKIO YA FUNGUO YALIKOANZIA NA NAMNA YANAVYOHUSIANA NA MATUKIO YA HIVI KARIBUNI YALIYOTOKEA KATI YA MIEZI YA APRIL 2021 NA JUNE 2021


I FUNGUO ZA GARI ALIZOWAHI KUCHONGEWA MHUSIKA MNAMO AUGUST 2019

Muhimu ni kwamba maelezo ya matukio haya yanatokana na dhana aliyonayo mhusika kwa sasa, baada ya kuwa tayari ameshaona matokeo ya matukio hayo

Historia ya matukio ya funguo inaanzia kwenye funguo za gari alizowahi kuchongewa huko mjini mnamo August 2019 na katika kipindi alipokuwa yuko likizo nyumbani

Mojawapo ya dhana alizonazo mhusika kuhusiana na funguo hizo ni kwamba, baada ya kuwa amechonga funguo hizo kuna mtu mwingine naye alibahatika kufahamu mhusika alienda kuchonga funguo hizo duka gani na baadaye naye kuchukua kopi ya ufunguo wa gari la mhusika na kwenda kuchonga funguo zingine zilizofanana kabisa na zile alizokuwa amechonga mhusika
  • Kwa ujumla, hii ni dhana nzima (kuhusiana na matukio haya ya funguo) inaweza ikawa iko sahihi au isiwe sahihi,
  • Hata hivyo, dhana hii imetokana na utafiti ambao mhusika amekuwa akiufanya katika kipindi chote kuanzia siku ya Ijumaa kuu, tarehe 02 APRIL 2021 hadi siku ya Alhamis ya tarehe 10 JUNI 2021, HUKU AKIWA ANAUNGANISHA NA MATUKIO MENGINE YALIYOKUWA TAYARI YAMESHATOKEA HAPO AWALI
………………………………inaendekea
 
………………………………inaendekea

HISTORIA YA MATUKIO YA FUNGUO:


I KUHUSIANA NA FUNGUO ZA GARI ALIZOWAHI KUCHONGEWA MHUSIKA MNAMO AUGUST 2019

JUMAPILI YA TAREHE 01 MARCH 2020 (MWAKA JANA):

FUNGUO ZA GARI ZAPOKONYWA GHAFLA KANISANI NA KITOTO RAFIKI YAE NA MHUSIKA


Akiwa yuko kwenye Ibada na ukiwa ni wakati wa Ibada ya kusifu na kuabudu, kitoto ambacho ni rafiki yake na mhusika, kilifika alipokuwa amesimama kwenye safu ya viti vya nyuma kabisa pembezoni mwa Kanisa. Wakati huo mhusika alikuwa ameshika funguo hizo mkononi, zikiwa zimeunganika na zingine za nyumbani pia. Ghafla kitoto hicho kilipokonya funguo hizo na kukimbia nazo. Kwa kuhofia kuwa kingeweza kuzipoteza, mhusika alijaribu kukifuatilia, lakini kilikimbia nazo na kikamchenga kwenye magari yaliyokuwa yamepaki karibu karibu na hakufanikiwa kukipata tena

  • Wakati huo Ibada ilikuwa inaendelea na aliamua bora arudi kwenye Ibada, kitoto atakitafuta baadaye
  • Jumapili hiyo ndiyo ile iliyokuwa siku ya Harusi ya mtoto wa Kiongozi Mkuu wa Kanisa A (KM-A) na ulikuwa ni wakati wa Ibada ya kwanza
  • Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa kitoto hicho kufanya kitendo cha aina ile kwa mhusika, na kwa wakati huo kilikuwa tayari kimeshafikia umri wa kuweza kuelewa vizuri nini kitoto hicho kilkuwa kinafanya kulingana na tendo ambalo kililifanya siku hiyo
Baada ya kuwa zimepita takribani dakika 15 hivi, mhusika aliamua kutoka kwenye Ibada na kuanza kukifuatilia tena. Safari hii alibahatika kukipata kikiwa kimeambatana na dada yake. Mhusika alimujulisha dada yake kuwa angependa akichape kofi la miguuni kwanza halafu ndiyo akiachie kwa sababu tayari kimeshakuwa na akili ya kujua nini kinafanya.
  • Baada ya hapo kweli mhusika alikichapa kofi la miguuni,, akiwa tayari ameshakinyang’anya funguo
  • Dada alishuhudia kofi hilo na kwa bahati nzuri, mwalimu wake na mhusika naye kumbe pia alibahatika kuliona tukio hilo
  • Mwalimu wa mhuiska alithibitisha hilo baada ya kuonana na mwanafunzi wake
BAADA YA IBADA KUISHA J2 HIYO

Mhusika alipitia shell kwa ajili ya kufanya service ya gari yake na baada ya service, battery ya gari akiwa anatka kuondoka, battery ya ikawa haiwezi kupiga tena, na hivyo kulazimika kuwapigia simu mafundi wake kuja kushugulikia hali hiyo. Maelezo ya tukio hili tayari alishawahi kuyatolea ufafanuzi hapo awali kwenye post hii hapa #613

DHANA ALIYONAYO MHUSIKA MUDA HUU KUTOKANA NA TUKIO HILO LA KUPOKONYWA FUNGUO NA KITOTO
  • Kitoto hicho kilikuwa kimetumwa makusudi kuja kupokonya funguo hizo, na kilikuwa kimeelekezwa kufanya hivyo baada ya Ibada kuwa imeanza
  • Baada ya kuzipokonya, kilizipeleka kwa mtu aliyekuwa amekituma.
  • Na kama dhana ya kuzipeleka kwa mtu iko sahihi, basi kilizipeleka aidha kwa mzazi (mama) au kwa MR X au kwa mke wa MR X
Baada ya kitoto hicho kuwa kimezifikisha funguo huko, funguo hizo zilibadilishwa, ukatolewa ule aliokuwa nao mhusika siku zote na kuwa replaced na ufunguo mwingine ambao ulikuwa umechongwa na wao, na uliofanana sawsawa kabisa na ule aliokuwa anautumia mhiusika siku zote
  • Kiongozi Mkuu wa Kanisa A (KM-A) alijua kuhusu mpango huu
  • Vile vile, mwalimu wake na mhusika naye pia alijua na ndiyomaana aliweza kuwa makini kufuatilia kila kitu kilichokuwa kinaendelea.Ndiyo maana, baada ya kitoto hicho kuwa kimepokonya funguo hzo, mwalimu wake na mhusika aliweza kuliona hata tukio la kofi wakati waumini wengine wote walikuwa wameconcentrate na Ibadan a hawakuliona tukio hilo
BAADA YA FUNGUO ZA MHUSIKA KUWA ZIMEBADILISHWA

Baada ya zoezi hilo la ku-swap funguo kuwa limefanyika, mhusika hakuweza kubaini kuwa ufunguo huo uliwahi kubadilishwa na hivyo kuendelea kuutumia akijua kuwa ni ule ule aliokuwa nao tangu mwanzo
  • Kwa hiyo mhusika alitoka Kanisani J2 hiyo akaelekea shell kwa ajili ya service ya gari akiwa hajui kile kilichokuwa kimefanyika kwenye ufunguo huo
  • Baada ya service, battery ya gari ikagoma kupiga hali iliyopelekea kuwaita mafundi wake wakaja kurekebisha hali hiyo
Still, tangu siku ya service ya gari hadi siku kadhaa mbele, mhusika bado alikuwa hajaweza kubaini kama ufunguo huo ulikuwa umeshaanza kuwa na tabia tofauti na zile za awali

Hata hivyo kadri siku zilivyoenda, baadaye ndiyo alikuja kuustukia ufunguo huo kuwa umekuwa na tabia tofauti na uivyokuwa awali, na ulianza kuonnyesha tendency ya kuwa una-affect Voltage ya battery, mshale wa battery ulianza kuwa unashuka au kucheza cheza

Mbali na hayo, mhusika alibaini pia mienendo isiyokuwa ya kwaida kutoka kwa MR X na hata mke wake pia, na kwamba mienendo hiyo ilikuwa ina uhusiaano na funguo hiuo wa gari; kwamba mara kadhaa MR X alikuwa anajaribu kutengeneza mazingira yasiyokuwa ya lazima ya mhusika kuwasha gari lake katika uwepo wake ila pasipokuwa na sababu za ulazima wowote wa yeye kuwepo katika hayo pindi mhusika anapokuwa anawasha gari lake

  • MR X alikuwa anatengeneza mazingira ya namna hiyo hasa pindi mhusika alipokuwa yupo katika mazingira ya Kanisani
  • Vile vile, kuna siku nyingine tena MR X aliwahi kufanya hivyo hivyo ila katika mazingira ya ofisini, safari hii wakiwa wawili na mke wake
Maelezo kamili mazingiranya ofisini mhusika tayari alishawahi kuyatoa katika post hii hapa #146 isipokuwa tu tofauti ni kwamba kwa wakati huo, mhusika alikuwa hajazibaini bado sababu hizi za nyongeza zilizowahi kupelekea MR X na mke wake, wafanye hivyo

…………………inaendelea
 
………………………………inaendekea

HISTORIA YA MATUKIO YANAYOHUSIANA NA FUNGUO:


I KUHUSIANA NA FUNGUO ZA GARI ALIZOWAHI KUCHONGEWA MHUSIKA MNAMO AUGUST 2019

Baada ya mhusika kuwa amepata hints kadhaa kutokana na matendo ya MRX na ambayo yalimthibitishia pasipo shaka kuwa ufunguo aliokuwa anautumia ulikuwa na matatizo
  • Mhusika alaiamua kuaacha kuutumia ufunguo huo na kuchukua ufunguo mwingine (kopi ya pili) kwa kwa sababu alikuwa amechongewa kopi tatu
  • Kwa hiyo alichukua kpoi ya pili na kuanza kutumia hiyo
KOPI HIYO YA PILI ameitumia bila matatizo yoyote hadi J2 YA TAREHE 11/04/2021 alipoamua kuibadilisha na kuanza kutumia tena KOPI YA TATU

MOTIVE
hasa iliyopelekea aache kutumia KOPI YA PILI na ku-switch kwenda kwenye KOPI YA TATU, ni UTAFITI. Kwa ieleweke kuwa kopi hiyo ya pili, yenyewe haikuwahi kumletea matatizo yoyote yale isipokuwa aliamua kuacha kuitumia kwa ajili ya utafiti tu na si vinginevyo

Kwa hiyo kopi hii ya ya tatu alianza kuitumia J3 ya tarehe 12 APRIL 2021

NEXT:

SABABU ZILIZOPELEKEA MHUSIKA KUFANYA UTAFITI KWA KU-SWITCH KUTOKA UFUNGUO WA KOPI YA PILI KWENDA KOPI YA TATU


Ni kwamba kulionekana mazingira kama wahuska waliowahi ku-swap funguo za mhusika mwezi March 2020 (mwaka jana) muda ambaoi kitoto kilipokonya funguo za mhusika, walikuwa wameshajua kuwa mhusika ameshaubadilisha ufunguo huo na kuanza kutumia kopi nyingine. Kutokana na hali hiyo mhusika naye alitamani pia kujua kama kweli walikuwa wameshajua hilo, na hivyo kupelekea J3 ya tarehe 12 APRIL 2021 mhusika kuubadilisha tena ufunguo huo na kuanza kutumia kopi nyingine ya tatu


………………….inaendelea
 
………………………………inaendekea

HISTORIA YA MATUKIO YANAYOHUSIANA NA FUNGUO:

SABABU HASA ZILIZOPELEKEA MHUSIKA KUANZA KUTUMIA KOPI YA TATU KWA AJILI YA UTAFITI


Siku ya Ijumaa kuu, yaani tarehe 02/04/2021 mhusika alifika Kanisani na kukuta hakuna Ibada, kulikuwa na tatizo lilikuwa limetokea na kwa bahati mbaya hakuwa amepata taarifa za awali
  • Taarifa hizi alizipata kutoka kwa swahiba wake, askari yule ambaye aliwahi kumfukuza mhusika J2 moja Kanisani na hivyo kupelekea mhusika kuanzisha kwa uzi huu
  • Ijumaa hiyo, Askari huyu alikuwa kwenye parking akiwa na muumini mwingine wa kike
  • Askari alikuwa anamsaidia muumini huyu kufungua mlango wa gari lake kwa kutumia ufunguo, baada ya mlango huo kuwa umeleta shida ya kufumguka
Askari huyu alifanikiwa kuufungua mlango wa garihilo na hatimaye kuukabidhi ufunguo kwa mmiliki wa gari mbele ya mhusika
  • Ndani ya siku chache sana, hili lilikuwa tukio la pili kwa mhusika kuona ufunguo wa chombo cha moto cha mtu mwingine na katika mazingira ambayo yeye aliyaona kama alitakiwa auone ufunguo huo
  • Vile vile, kabla ya Ijumaa hiyo, J2 iliyokuwa imepita nyuma yake, yaani ile ya tarehe 28/03/2021, mhusika alikuwa amebahatika kuona pia ufunguo mwingine ila wenyewe ulikuwa si wa gari bali wa pikipiki
  • Ufunguo huo hakuonyeshwa as such isipokuwa aliuona tu kwa bahati; japo katika mazingira yaliyopelekea adhani kuwa pengine alikuwa anaonyeshwa
  • Mbali na matukio haya mawili, J2 ya tarehe 11/04/2021 mhusika alibahatika pia kuona ufunguo wa gari wa muumini mwingine waliyekuwa wamekaa karibu, napia katika mazingira ambayo alidhani hapakuwa na ulazima sana wa yeye kuuona ufunguo huo
Baada ya kuwa ameyaona matukio yote haya matatu na kumtia shaka kama yanaweza kuwa ni coincidences za kawaida tu, ndiyo hapo sasa kuanzia J3 ya tarehe 12/04/2021 akaamua kuingia kwenye utafiti kwa kuacha kutumia kopi ya pili na kuanza kutumia kopi ya tatu. Motive yake hasa ikiwa ni kutaka kuona kitakatokea nini mara baada kuwa ameacha kutumia kopi ya pili na kuanza kutumia kopi ya tau

Kwa hiyo alichofanya, baada ya kuwa ametoka Kanisani J2 ya tarehe 11/04/2021, aliamua kuchukua kopi ya tatu na kuirudisha kopi ya pili pale ilipokuwa kopi ya tatu

A: MATUKIO KADHAA YA MUHIMU YALIYOJIRI BAADA YA MHUSIKA KUANZA KUTUMIA KOPI YA TATU

Baaada ya kuanza kutumia kopi ya tatu, mambo kadhaa yafuatayo yalitokea
  • Jumapili ya tarehe 18/04/2021 ikawa ni siku ya kwanza ambayo aliingia Kanisani kwenye Ibada akiwa anatumia ufunguo kopi ya tatu
  • Jumapili nyingine iliyofuata ya tarehe 25/04/2021 ikawa ni siku ya pili ambayo aliingia Kanisani kwenye Ibada akiwa anatumia ufunguo kopi ya tatu
YALIYOJIRI JUMAPILI HIYO YA TAREHE 25/04/2021 NA BAADA YA HAPO

Akiwa yupo Kanisani J2 hiyo, inasemekana jirani aliyesababishwa uuharibifu kwenye bamba la gari la mhsika, alifika na kugonga mlangoni kwa mhusika.

Kitoto cha mtu ambaye baadaye alikuja kuhusika na uharibifu wa gari la mhusika, kilikuwa kimekaa standy by J2 hiyo kumpa mhusikaJ taarifa za kugongewa na baba yake, mhusika alipowasili J2 hiyo akiwa anatokea kanisani

iIkumbukwe kuwa mpaka muda huu mtu huyu alikuwa bado hajafanya uharibu wowote kwenye gari la mhusika, isipokuwa alikuwa bado yupo katika maandalizi tu.. Uharibifu hasa alikuja kuufanya baadaye usiku wa J5 kuamkia Alhamis ya tarehe 29/04/2021 halafu ndiyo akau-backdate kwenda siku ya Ijumaa ya wiki iliyokuwa imepita nyuma yake, yaani Ijumaa ya tarehe 23/04/2021 ili uweze kuendana na taarifa za kitoto chake kwa mhusika; zile za J2 ya tarehe 25/04/2021 mhusika alipokuwa amewasili nyumbani akiwa anatolea kanisani
  • J2 hiyo hiyo, huko Kanisani nako kulitokea gari ikaja ikamziba sehemu alipokuwa ameegesha garo lake katika namna ambayo alishindwa kutoka baada ya muda wa Ibada kuisha, ilhali parking zilikuwepo za kutosha na hapakuwa na haja ya waumini kupaki kwa kuzibana
  • J3 ya tarehe 26/04/2021 Iilikuwa Siikukuu ya Muungano, hapakuwa na kazi
  • J4 ya tarehe 27/04/2021 maonyesho ya utafiti ofisini kwake mhusika yalianza na kuziba parking zote za karibu na jengo ilimo ofisi ya mhusika. Kawaida, maonyesho haya huwa yanafanyika baada ya kuwa kumetolewa public notice lakini safari hapakuwa na notice yoyote
  • J5 ya tarehe 28/04/2021 mfanyakazi mwenzake na mhusika alifika ofisini na kumpa ofa ya muda wa kipindi kimoja cha Alhamis tarehe 28/04/2021 ambacho mhusika alikikubali
  • J5 hiyo hiyo ya tarehe 28/04/2021, msimamizi wa ukarabati wa jengo alifika ofisini kwa mhusika na kumjulisha kuwa kesho yake Alhamis chumba chake inabidi kipakwe rangi. Schedule ya kupaka rangi vyumba ilikuwa tayari imeshatoka kipindi kirefu nyuma kabla ya siku hiyo lakini chumba cha mhusika hakikuwa kimewekwa kwenye schedule hiyo
  • Usiku wa J5 kuamkia Alhamis ya tarehe 29/04/2021 gari la mhuiska lilidaiwa kupata ajali likiwa sehemu peke yake kwenye parking mahali anapoishi na mhusika wa uharibifu huo kubainika kuwa ni jirani yake na mhusika
Kwa hiyo jirani wa mhusika alitekeleza azma ya uharibifu kwenye gari la mhusika usiku wa J5 kuamkia Alhamis ya tarehe 29/04/2021

B: MAMBO KADHAA YA MSINGI ALIYOYABAINI MHUSIKA BAADA YA KUANZA KUTUMIA KOPI YA TATU

…………………..itaendelea
 
UPDATE: THURSDAY 17 JUNE 2021

B MAMBO KADHAA YA MSINGI ALIYOYABAINI MHUSIKA BAADA YA KUANZA KUTUMIA KOPI YA TATU

Dhana aliyonayo kuhuisiana na KOPI YA TAU YA UFUNGUO


Kwenye kipindi cha pilika pilika za mhusika kuwa anakumbana na mazingira yaliyoonyesha kama watu wanafanya makusudi ya kumuonyesha funguo za magari ukiwemo mmoja wa pikipiki
  • Mpaka muda huo, kuna mtu alikuwa tayari ameshaingia nyumbani kwa mhusika kukiwa hapana mtu ndani na kubadilisha ufunguo ule wa kopi ya tatu
  • Ufunguo huo nao ukawa sasa umebadilishwa mithili ya ule wa kopi ya kwanza uliohusisha kitoto kilichopokonya funguo za mhusika wakati wa Ibada Kanisani
  • Mpaka muda huu mtanndao ukawa tayari umefanikiwa kubadilisha funguo mbili, wakabakiza mmoja, yaani ile kopi ya pili ile aliyokuwa mhusika anaendelea kutumia
Baada ya kopi hizo mbili kufanikiwa kubadilishwa, mkakati sasa ukaanza wa kuutafuta ule wa tatu na kilichoendelea baada ya hapo ndiyo hicho ambacho mhusika ameshakielezea hapo juu; yaani ulianza mtindo wa kumuonyesha funguo mhusika ili angalau apate mawazo ya kuubadilisha ufunguo huo, na kwa bahati nzuri kweli aliamua kufanya hivyo
  • Kwa hiyo kipindi mhusika ana-swap funguo hizo kwa kuchukua kopi ya tatu na kuirudisha ile ya pili, kopi aliyochukua ilikuwa nayo tayari imeshabadilishwa na hivyo kupekekea kuwa na tabia kama za kopi ya kwanza aliyowahi kubadilishiwa katika mazingira ya Kanisani
  • Mpaka muda huu, kopi ya pili pekee ndiyo ile iliyokuwa imebaki iko salama
KOSA LA MSINGI ALILOFANYA MHUSIKA WAKATI ANABADILISHA FUNGUO KUTOKA KOPI YA PILI KWENDA YA TATU

Baada ya mhusika kuwa amepata mawazo ya kubadilisha kopi ya pili ili aanze kutumia kopi ya tatu, kosa la msingi alilofanya ni kuirudisha kopi ya pili mahali pale pale ambapo muda wote ilikuwa inakaa kopi ile ya

Baada ya kuwa amefanya mabadiliko hayo, na hatimaye mtandao husika nao kujiridhisha pasipo shaka kabisa kuwa tayari alikuwa ameshafanya hivyo::
  • Mtaalamu ambaye huwa anaingia ndani nyumbani kwa mhusika panapokuwa hapana mtu yeyote ndani, akaingia tena ndani na kuubadilisha ufunguo wa tatu
  • Mpaka hapa sasa wakawa wamefanikiwa kubadilisha funguo zote tatu
Mhusika alikuja kulibaini hili baada ya kuamua kuurudisha tena ufunguo ule wa tatu ili arudi tena kwenye matumizi ya ule wa plii. Baada ya kuwa amefanya hivyo, alibaini kuwa ufunguo huu wa pili nao ulionekana kuwa na tabia zile zile kama za ule wa kwanza na za ule wa wa tatu
  • Kosa la msingi alilofanya mhusika hapa ni kile kitendo chake cha kutokubadilisha mahali au sehemu ambayo funguo hizo amekuwa akizitunza muda wote
  • Pamoja na ukweli kwamba funguo hizi amekuwa akiziweka sehemu iliyofichika sana lakini bado alitakiwa kuwa na tahadhari ya kuwa anabadilisha badilisha mahali zinapokaa kwa sababu inaonekana mtu ambaye huwa anaingia ndani ni mtaalamu sana wa ku-search na anaweza akawaizidi hata watu ambao ni professional
Mhusika anaamini kuwa mtu huyu ambaye amekuwa na tabia za kuingia ndani nyumbani kwa mhusika panapokuwa hapana mtu yeyote ndani, hawezi kuwa mtu wa mbali bali mmojwapo wa majirani zake wanaoishi karibu na nyumba hiyo

Vile vile kitoto cha jirani huyu kilichowahi kumpa ujumbe mhusika kuwa baba yake (kitoto hicho) aliwahi kugonga J2 moja nyumbani kwa mhusika katika muda ambao mhusika alikuwa yupo Kanisani , kwa upande mwingine ujumbe huo unatoa taswira kuwa mtu huyu anaweza kuwa ndiye haswa ambaye mara zote huwa anaingia ndani kwa mhusika panapokuwa hapan mtu ndani.

Hii ni kutokana na ukweli kuwa:
  • Muda ambao mtu huyu alisemekana kugonga nyumbani kwa mhusika, ilikuwa ni J2 na katika muda ambao mhusika alikuwa tayari ameshaenda Kanisani na gari lake halikuwepo nje kwenye parking
  • Kwa hiyo inaonekana kama jirani huyu bado alilazimika kugonga ili kuhakikisha hakuna mtu mwingine ndani, na kuna uwezekano aliingia ndani J2 hiyo akikiacha kitoto kikiwa kinaangalia hali ya hewa nje, na baada ya hapo akakielekeza kuja kumpa ujumbe mhusika ule kilioweza kumpa
KITU UNIQUE SANA KUHUSINA NA MUONEKANO WA JIRANI HUYU

Kwa muonekano wake wa nje, anaonekana yuko tofauti sana na watu walio wengi wa kawaida, yaani anaonekana kama mtu anayeweza kufanya chochote na katika mazingira ya kawaida sana
  • Kwan je anaonekana anaweza kumu-incite mtu halafu akafanya chochote kile anachoona kinafaa
  • Kwa ndani sasa hilo ni swala jingine mhusika hawezi kujua, hamjui sana kwa sababu ni mpya kabisa katika mazingira ya makazi yao
Kwa hakika jirani huyu yuko tofauti sana na watu wote ambao mhusika ameshawahi kuishi nao mahali pale,hadi sasa kwa muda wa takriban miaka 17.Na mhusika akishafikia hali ya kusema kuwa mtu yuko tofauti, yuko tofauti kweli. The man appears as being capable of anything

HITIMISHO:

Assuming dhana ya mhusika ipo sahihi, uhakika wake ni kuwa watu kadhaa wafuatao wanahusika moja kwa moja kwenye set-up ya matukio haya, kulingana na ameneo kama yalivyotajwa hapa chini

KUTOKA MAZINGIRA YA KANISANI


KUTOKA MAZINGIRA YA FISINI


KUTOKA N MAZINGIRA YA YUMBANI MAHALI MHUSIKA ANAPOISHI



…………….inaendelea
 
HITIMISHO:

Assuming dhana ya mhusika ipo sahihi, uhakika wake ni kuwa watu kadhaa wafuatao wanahusika moja kwa moja kwenye set-up ya matukio haya, kulingana na ameneo kama yalivyotajwa hapa chini

KUTOKA MAZINGIRA YA KANISANI

I KIONGOZI MKUU KANISA A (KM-A)


Yale mambo kama “TANO ZA JUU”, “WANGAPI WANA BIBLIA”, n.k. yalikuwa yanasababiswhwa na FUNGUO alizokuwa

II MWALIMU WAKE NA MHIUSIKA

  • Huyu ndiyo huwa ni confidant mkubwa kabisa wa KM-A kwa mambo yote yakiwemo yale ya kipumbavu na kijinga kijinga
  • Mhusika kwa sasa ameanza kuona pengine kuna haja ya siku moja kuja na topiki maalaum kwa ajili ya mtu huyu, ameshaanza kujisahau sana sasa hivi. Nadhani ni baada ya mhusika kuwa amemhifadhi mno na kwa kipindi kirefu sana
III BINTI ALIYEWAHI KULAZIMISHA KUPIGA “TANO ZA JUU” NA MHUSIKA J2 YA TANGAZO LA UCHUMBA WAKE

Mhusika tayari alishatoa maaelezo kamili kuhusiana na binti huyu kwenye post za siku za nyuma wakati tukio hilo linatokea

KUTOKA MAZINGIRA YA OFISINI

MR X na watu wengine wote waliokuwa wakijihusisha na pilika pilika za maswala ya funguo akiwemo Mkuu wa Idara

KUTOKA MAZINGIRA YA NYUMBANI MAHALI ANAPOISHI MHUSIKA

Mhusika mkubwa hapa ni jirani ambaye hivi karibuni ameamua kuchukua hatua ya kukata usiku bampa la gari la mhusika na kusingizia kuwa ilikuwa ni ajlali

Kitu muhimu ambacho msomaji inabidi akifahamu hapa ni kwamba gari la mhusika huwa linapaki peke yake na kwenye parking kubwa kabisa, likiwa mbali kabisa na magari mengine (takribani mita 15 au zaidi) na kunakuwa hakuna gari nyingine yoyote kulia wala kushoto kwake. Hata kama kweli ni kuligonga kwa ajali ya kawaida, si rahisi hata kama mtu atakayekuwa anaendesha gari ni leaner wa siku moja

Maelezo mengine ya nyongeza au ziada yatafuata baadaye

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
Hii akili kubwa Sana... Mwanza nlikuwa na dhana watu wenye akili hum ni wawil tu lkn nmekupata... Ur talented broo... Hi kitu ukisonga nayo vzr ntajua vitu Ving mno ambavyo mwanzo ckuwa na vijua.... Keep in touched..
 
UPDATE: FRIDAY 17 JUNE 2021

MAELEZO YA NYONGEZA: ALICHOKIBAINI MHUSIKA KUHUSIANA NA FUNGUO ZA KITASA KIPYA ALIZOKABIDHIWA NA MKUU WA IDARA (MWI) HIVI KARIBUKI


Funguo hizo alizokabidhiwa mhusika na MWI, zimefanana na funguo za kitasa kingine cha lango kuu la Maabara iliyo chini ya usimamizi wa MR X, na hivyo kitasa kilichowekwa kwenye maabara iliyo chini ya usimamaizi wa mhusika, kinafanana na kitasa hicho kilichoko kwenye maabara ya MR X isipokuwa tofauti ni rangi tu, kimoja kina rangi ya gold na kingine kina rangi ya silver. Mhusika alifanikiwa kugundua kitu hiki jana baada ya mambo kadhaa kujitokeza kama atakavyoyaainisha baadaye kidogo hapa chini

Na iwapo kama kuna chochote cha msingi kilichokuwa kinaendelea kutokana na mfanano wa vitasa na funguo zake kwenye maabara hizi mbili, basi kuna uwezekano pia kuwa vitasa vya aina hiyo vinaweza kuwepo pia
  • Nyumbani kwake na MR X, kwenye nyumba anayoishi
  • Kanisa A, possibly kwenye ofisi ya Kiongozi Mkuu wa Kanisa A, kwenye “JENGO JIPYA” au mahali pengine popote pale ndani ya nyumba hiyo ya Ibada.
Hii ni kutokana na ukweli kuwa MR X ni mmojawapo wa waumini waaminfu sana kwenye maswala ya fedha na hivyo ilipelekea awe mmojawapo wa waumini walio kwenye Kamati ya Ujenzi Kanisani hapo. Kitasa hiki kipya kilichoko kwenye maabara ya MR X kimewekwa hivi karibuni baada ya maabara hiyo kuwa imefanyiwa ukarabati mkubwa

Vile vile, mhusika anadhani kuwa vitasa vya aina hiyo vinaweza kuwepo pia kwenye baadhi ya nyumba za waumini walio karibu na MR X na ambao huwa wako pamoja na MR X katika kutengeneza matukio haya kutokea Kainsani

UP NEXT:

YALIYOJIRI JANA OFISINI ALHAMISI YA TAREHE 17/04/2021 KWENYE MAONGEZI YA MHUSIKA NA MR X, BAADA YA MR X KUTEMBELEA KWA MUDA MFUPI OFISINI KWA MHUSIKA
 
…………………………inaendelea

YALIYOJIRI JANA OFISINI ALHAMISI YA TAREHE 17/04/2021 KWENYE MAONGEZI YA MHUSIKA NA MR X, BAADA YA MR X KUTEMBELEA KWA MUDA MFUPI OFISINI KWA MHUSIKA


Jana Alhamis MR X alifika ofisni kwa mhusika na kuongea na mhusika kwa muda mfupi sana mambo kadhaa. MR X hakuingia ndani bali alifungua mlango kidogo tu halafu akawa amechungulia ndani ofisini kwa mhusika na kuanza kumweleza mambo yafuatayo, kwamba MR X alikuwa amejisahau kidogo kumjulisha mhusika taarifa zilizokuwa zimepeklekea awepo ofini kwa mhusika muda huo

MR X alianza kumjulisha mhusika kuwa kwenye saa 5:00 kamili asubuhi hiyo, Mkuu wa Taasisi atakuja kukagua maendeleo ya ukarabati wa jengo na hivyo anaweza akapendelea pia kukagua baadhi ya maeneo ikiwemo kwenye maabara. Hivyo MR X alikuwa anamjulisha mhusika ili asiwe mbali, muda wote awepo mazingira ya ofisini.

Mpaka hapa mhusika akawa anataka kujua muda hasa wa ujio wa Mkuu huyu, kama ni saa tano au muda mwingine.
  • MR X alimjibu mhusika kwa kumweleza kuwa Mkuu alikuwa na ratiba ya kuanzia kwenye majengo mengine pia ambayo yamekuwemo kwenye ratiba hii ya ukarabati na hivyo muda wa kuwasili kwake idarani hapo ulikuwa haujulikani vizuri ila itakuwa kuanzia saa tano
  • Baada ya maongezi haya, MR X na mhusika walikubaliana kwamba mhusika atakuwa standby pindi Mkuu atakapokuwa amefika kwenye maabara ya MRX, mhusika naye ataungana nao kuanzia pale kwa sababu muda wote anapokuwa amekaa ofisini kwake, huwa anaweza kuona vizuri kila kinachokuwa kikiendekea kwenye lango la kuingilia ndani ya Maabara ya MR X
  • Hii ilitokana na ukweli kuwa muda wa MKuu kuingia ndani ya jengo ulikuwa unajulikana itu kuwa ni kuanzia saa 5 kamili na si vinginevyo
Maongezi ya wawili hawa yaliishia hapa na baada ya muda kuwa umepita, tuseme nusu saa au dakika 45, walikuja watu kama watatu au wanne hivi, wakawa wamesimama kwa kipindi kirefu sana kwenye korido ambayo huwa inamuwezesha mhusika kuona kwa urahisi kinachokuwa kikiendelea kwenye lango la kuingia kwenye maabara ya MR X. Kati ya wale waliokuwa wamesimama kwenye Korido hilo, mmojawapo anadhani alikuwa ni aliyewahi kuhudumu kama Mkuu wa Idara kwenye kipindi cha kuanzia Julai 2006 hadi Juni 2012, aliona sura hiyo na kuitambua, na wengine wote waliobaki walikuwa wagni machoni pake

Baadaye kidogo, mhusika aliona kundi la watu likiwa linaanza kutoka kwenye maabara ya MR X, na hivyo kuamua kulifuata kundi hilo.
  • Kundi hilo hakuwa ameliona wakati linaingia kwenye maabara hiyo
  • Kumbe kutokuliona kundi hilo kulisababishwa na watu waliokuwa wamesimama muda kitambo kwenye korido, japo hapo awali alidhani kuwa angeweza kuwa makini sana ili kundi hilo lisiweze kumzuia kuona chochote kitakachokuwa kikiendelea kwenye maabara hiyo especially watu watakaokuwa wanaingia na kutoka kwenye maabara hiyo
Baada ya kuona kundi linatoka, mhuiska alijaribu kuliwahi na kukuta tayari limeshatokomea, isipokuwa alibahatika kuona na MR X muda huo huo naye akiwa tayari ameshachana na kundi hilo

  • Kundi hilo likwa tayari limeshaondoka, MR X alimjulisha mhusika kuwa Mkuu wa Taasisi hakuwa anapendelea kukagua sehemu nyingine yoyote ile isipokuwa ukarabati ule uliofanyika kwenye maabara yake tu (MR X)
  • Kwa hiyo MR X alimjulisha mhusika kuwa MKUU hakuwa na nia ya kupita sehemu nyingine yoyote ile tofauti na hiyo, na hivyo maabara ya mhusika ilikuwa haihusiki na ugeni huo
Maongezi ya mhusika na MR X yaliishia hapo, halafu baada ya masaa kadhaa kupita, akakumbana na watu wawili waliokuwa ground floor wakitaniana, mmoja mwanafunzi wa ngazi za juu na mwingine mfanyakazi ambaye anahusika na maabara ambayo iko jirani na ile ambayo ni ya mhuiska

…………………….inaendelea
 
………….inaendelea

UTANI KATI YA MWANAFUNZI WA NGAZI ZA JUU NA MFANYAKAZI


Utani kati ya waili hawa ulikuwa unahusiana na ugeni uliokuwa umefika idarani asubuhi hiyo

Mwanafunzi alikuwa anamtania mfanyakazi akisema maneno kama “ kitambi kilipungua” au kitu kama “kitambi kiliingia ndani

Mpaka hapa mhusika akawa amevutiwa na utani huo, ikabidi aulize swali “nini ujio wa Mkuu?”. Halafu mfanyakazi akajibu “ndiyo”. Baada ya mhusika kupewa jibu hilo, akauliza swali jingine tena “vipi kwani alipita huku chini?”. Mfanyakazi akajibu akasema, hapana alipitiliza kwenda juu

Still, mhusika akawa hajaliamini sana jibu hilo. Mpaka hapo akawaacha wawili hao wanaendelea na utani wao, akapandisha juu. Baadaye tena akapata wazo la kwenda kumuona MR X ili amuulize kama kweli taarifa alizompa awali kuwa MKUU hakuwa na mpango wa kupitia sehemeu nyingie yoyote ile, lilikuwa ni sahihi ama la
  • Mhusika alifika ofisini kwa MR X na kukuta mlango umefungwa
  • Akadhani pengine atakuwa yumo ndani kwenye maabara. Aliingia ndani kwenye maabara, mlango ulikuwa wazi lakini hapakuwa na mtu yeyote ndani
  • Mhusika hakufanikiwa kumuona tena MR X hadi muda wa jioni saa 12 kasoro dakika chache alipokuwa anaondoka ofisini kurudi nyumbani, alikuwa hajafanikiwa kuonana naye
Mhusika akiwa anafungua mlango wa mabara hiyo ya MR X ili atoke nje, ndiyo pale alipobaini kuwa aina ya kitasa kile ambacho hivi karibuni kimewekwa kwenye lango ya maabara yake, ndiyo aina hiyo hiyo ya kitasa ambacho kipo kwenye lango kuu la maabara ya MR X; kile cha maabara ya MR X kikiwa kimetangulia kuwekwa (miezi kadhaa iliyopita, possibly mwaka jana mwishoni) wakati hiki cha mhusika ndiyo kimewekwa ndani ya mwezi huu wa Juni 2021, a week past or so

HITIMISHO

Mhusika ameamua kuleta kwenu maelezo haya kwa sababu MR X IS A PROFESSIONAL kwenye maswala haya ya propaganda

Anaweza kuwa PENGINE alikuwa amepewa maelekezo ya kwamba mhusika anatakiwa awepo mahali akiwa anasubiri ujio wa MKUU muda fulani, lakini yeye akapeleka taarifa kuwa NILIMWELEZA LAKINI AKAKATAA, AKASEMA HAWEZI KUACHA KAZI ZAKE


Na kwa watu ambao wana jumbe ambazo ni malicious, mara nyingi huwa wanafika ofisini kwa mhusika na kuongea naye katika muda ambao anakuwa amewasha AC yake. Ana AC anatumia zile za zamani ina muungurumo nusu ya ile generator ndogo ya umeme

MR X aiifanya timing hiyo wakati “nusu generator” hilo likiwa limewasha na linaunguruma

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
NYONGEZA KUHIMU KUHUSIANA NA HAYA AMBAYO YAMEKUWA YAKIENDELEA

Engineering yote ya mambo yote haya mara zote huwa iko chini ya SENIOR MSTAAFU WA KIUME
  • Ajapokuwa yeye anaweza kuwa katika baadhi ya haya yuko msafi kisheia, lakini ukweli ni kuwan kama watu wangekuwa wanaweza kusema ukweli wa kilichoko ndani ya roho zao, ukimuliza swali yeye mwenyewe angeweza kukiri hilo pasipo shaka yoyote ile
  • Kwenye haya maswala, SENIOR MSTAAFU WA KIUME is as professional as is MR X and the vice versa is true
Inasikitisha kiasi na hadi wakati mwingine mtu anaweza kuona huruma, kwamba mtu ulikuwa unaongoza taasisi ya watu zaidi ya elf tatu (>3,000), umestaafu na kulazimisha kuongoza kisehemu cha tasisi chenye wafanyakazi wanaozidi thelathini (>30) tu, tena kwenye mambo yaliyo kinyume kabisa

MUBARIKIWE TENE NA BWANA
 
Back
Top Bottom